Waraka wa muhimu Kwenu wana CC

ladyfurahia

JF-Expert Member
May 10, 2011
14,699
9,455
Habari wapendwa marafiki zangu,
Leo nimeonelea niongee au nizungumze nanyi habari hii ambayo ni muhimu sana Kwetu sote, wengine hamtafurahia bali wengine watafurahia na kusema kuwa Rafiki umetupendelea leo kutupa waraka huu muhimu kwetu sote. Katika kipindi Hichi tunachokumbuka mateso aliyoyapata Bwana Yesu miaka 2000 iliyopita, ni vyema tunajihoji nafsini mwetu Je maisha yetu tunayoishi yanafanana na maisha Ambayo Yesu Kristo aliishi hapa duniani miaka hiyo iliyopita? Na je maisha yetu yanampendeza Mungu ni vigezo gani ambavyo vinakufanya utambue kuwa wewe ni mtakatifu mbele za Mungu? Je kuwa mpole au mnyenyekevu, kuwa mtu mtoaji sana kwa yatima na wajane na wahitaji, au kuishi kwa amani na watu wote? Ni nini hasa kitakachokufanya uende mbinguni kwa vigezo nilivyotaja hapo juu? Majibu ya Maswali haya unayo wewe mwenyewe rafiki yangu,

Nina jambo ambalo ningependa kukushirikisha rafiki yangu nalo je unaenenda kwa Roho wa Mungu? Jinsi unavyoishi sasa je unampendeza Mungu au unajipendeza nafsi yako na tamaa za mwili wako wa kutaka maendeleo ya shortcut, au maendeleo ya haraka yaani vodafasta? Je unajua hatma ya maisha yako iko wapi? Unajua kwanini siku hizi vijana wanaondoka duniani na wazee wapo wakipeta, sisemi wako wote la hasha nao wanaondoka, ila sio kama vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa. Hivi umeshajiuliza mara kwa mara kwanini uliumbwa ukawepo duniani na kwanini unafanya makosa yaa kumtenda Muumba wako dhambi kiasi hicho na wala huoni kuwa unafanya dhambi wewe waona ni starehe? hujui kuwa shetani ndiye anayekupelekea ummkosee Mungu wako? Hujui kuwa ibilisi yuko nafsini mwako akikunogoneza kuwa fanya hivi na sio dhambi nawe bila hata ya kujijua unafanya lile kusudi na takwa la shetani? Hujatambua kuwa shetani ni baba wa uongo na ndiye chanzo cha wewe kumkosa Mungu wako?
Hivi kwanini unafanya machukizo na kufuata tamaa za mwili huu zikudanganyazo kwa kitambo na mwishowe tukose uzima wa milele. Nitanukuu kidogo katika maandiko matakatifu katika kitabu cha Wagalatia 5:16 inasema ‘Basi nasema enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili………….’ Mwisho wa kunukuu.
Basi marafiki zangu jifungeni nira na dirii ya haki mwenende kama Mungu anavyotaka, na sio kama mtakavyo ninyi, mkatende yaliyo mema na kupendeza Mungu. Kwanini ufanye dhambi ilihali ukijua kuwa dhambi ni chukizo kwa Mungu hamjui yakuwa mshahara wa dhambi ni mauti ya milele? Hamfahamu yakuwa mkitenda dhambi mnatengwa na Mungu na kuukosa uzima wa milele, sasa kwanini unaendelea kufanya dhambi ambazo ni chukizo kwake Mungu,? Hivi mnatambua kwa damu ya Yesu Kristo tunao ukombozi wetu, msamaha wa dhambi sawasawa na wingi wa neema yake? Soma Efeso 1:7-10 na Efeso 2:1-3 nitanukuu kidogo inasema: ‘Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu ambazo mliziendea za imani kwa kufuata kawaida ya ulimwengu huu’
Rafiki yangu mpendwa mpaka hapo utaelewa nini kimenisukuma mpaka nikaamua kuandika waraka huu kwenu, , kama upo tayari kwa kumpokea Yesu aingie moyoni mwako afanyike kuwa Bwana na mtawala wa maisha yako huna budi kufuata sala hii fupi hapa chini
Sema ehee! Yesu nakupokea wewe kuwa Bwana na Mtawala wa maisha yangu, nimechoka kuishi maisha ya dhambi, na usumbufu wa shetani, nakuihitaji uingie moyoni mwangu ufanyike mwokozi wa maisha yangu, Ninatubu maovu yangu yote niliyokutenda na nisiyokutenda pia, futa jina langu katika kitabu cha hukumu, andika jina langu katika kitabu cha uzima wa milele,
Mpendwa rafiki yangu kama utakuwa umefuta sala hii kwa unyenyekevu wote na umakini utakuwa umesamehewa dhambi zako zote na usitende dhambi tena. Kama utapata nafasi basi soma Warumi 10:9-11, Nakushauri nenda katika makanisa ya kiroho utapata mafundisho ya kuukulia wokovu wako . Nakutakia baraka na furaha katika
Nawapenda nyote marafiki zangu.



N:B: Pls mods msifute thread hii. kama mkiona hapa hafai hii post basi pelekeni panapofaa zaidi.
Nawapenda na kuwajali zaidi.

siku njema
 
Ubariikiwe nawe pia kondoo wangu jana sikukuona kanisani ulikwenda wapi kusali best? Au ulikwenda kunyunyiziwa mito, vijito vya uhai wa baraka?

Mbona nilikuwepo, nadhani hukuona kwa sababu ya uwingi wa watu....
 
Ubarikiwe sana my cousin kwa ujumbe mzuri, Mungu akupe nguvu na uwezo uendelee kutangaza jina la Yesu kwa wote waaminio na wasioamini ili tuendane katika njia impendezayo bwana Mungu wetu
 
labda uwingi wa watu mndo mana sikukuona oky kama ulikuwepo ulisikia lile neno alilotoa mwinjilisti naomba ulifanyie kazi na uniambie umefikia wapi
Mbona nilikuwepo, nadhani hukuona kwa sababu ya uwingi wa watu....
 
Ahsante kwa kutujali kwa kiwango hicho na kutupatia neno ambalo ni chakula cha uzima wa roho, hakika ubarikiwe sana mpendwa katika jina la bwana ndg yangu ladyfurahia.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom