Waraka wa Kwanza Kwa Ndugu yangu, Comrade, mstahiki, muheshimiwa sana, Mshika Mpini Mshana jr

Mgibeon

JF-Expert Member
Aug 7, 2011
11,139
20,775
U hali gani bosi wangu, shaka sina unaendelea vema kabisa na harakati za ujenzi wa taifa, Naandika waraka huu nikiwa na nia na lengo la kukumbusha tulipotoka ila sio kukukosoa.

Ndugu yangu mshana jr ni dhahil-shahil kwamba katika maisha yako yote hukuwahi kuwaza kukamatia nafasi uliyonayo sasa, yaani kwa kiswahili cha haraka haraka ambacho watu wanaweza kuelewa ni kwamba ulidondokewa na embe chini ya mnazi.

Hata unakumbuka mtu ambaye ilibidi awe hapo ni kiasi gani ameamua kuwa na moyo wa chujio wa kukubali kupoteza kwa maslahi mapana ya amani ya wote waliotaka yeye akalie hicho kiti ulichokalia wewe, ajabu ni kwamba badala ya kuunga mkono yale yanayozungumzwa na ndugu zake ambao umeapa hasirani-abadani kwamba hutaki hata kuwasikia, ndiyo kwanza umekua ukiwakejeli na kuwanyima upenyo kuonekana na kuzungumza.

Imefika mahali unajitapa hadharani kwamba hicho kiti ulikipata kutokana na jitihada zako na wala hakuna yeyote aliyekushauri kwenda kwa seremala kukichongesha! Yaani umewadharau mpaka wale jamaa wawili walioingia msituni, wakatafuta mti mzuri, wakaukata na kuuchana vizuri na kuuleta kwa huyo seremala wako unayejivunia. Huku ni kukosa shukrani sana hasa kwa mtu kama wewe ambaye unapenda sana kuingia kwenye nyumba za ibada na kujifanya wewe ni mpole na huruma sana.

Ulipoanza kukikalia kiti ulikua mnyenyekevu haswa hata ukawaomba wanakijiji wakukumbuke katika dua zao ila sasa inaonekana ushaota mkia na pembe umejiongezea mwenyewe, nikukumbushe tu ndugu yangu mshana jr kua wewe sio wa kwanza kukalia hicho kiti, utakaa na ikiwa mapenzi ya mwenyezi Mungu tunaendelea kua hai basi ishaallah atakalia mwengine wewe utake au usitake.

Hebu mtazame mkalia-kiti aliyepita sasa hivi! Unamuonaje? Anajisikia raha kweli kweli maana kila anapopita watu wanamshangilia na kumsifia ingawa in reality watu walimponda sana wakati akiwa hatamuni, ila kutokana na majigambo na kujiona wewe unakaribia kua Muumba watu wanaona bora yeye kuliko wewe, naam hizo ndio tamaduni na mazoea yetu sisi ngozi nyeusi, tunapenda kulinganisha perfomance.

Hivi bwana mkubwa mshana jr unajua huku kijijini kwa sasa maisha yamekua magumu mnoo, yaani hata ugali umekuja kua anasa kweli? Huku wapi unatupeleka ndugu yangu? Hebu jitafakari mara mbili mbili, inawezekana kuna mahali unakosea au wanaokushauri hawakupi mbinu nzuri, kikubwa braza tunataka unafuu hapa kijijini kwetu.

Najua wale walioleta ule mti uliotengeneza kiti chako kwa sasa wanaonekana wapuuzi tu ila trust me pamoja na uhakika wa mambo ya CHAJE 2020 unashughuli pevu sana, maana matokeo hua hayajipangi, yule mkongwe alipotamka kua "jamani mimi nayasoma kama nilivyoyapokea" sio kweli kwamba hakujua mambo ya Teknohama yalihusika, alijua sana, na mimi binafsi kama Mgibeon naamini kua pale ni zaidi ya pesa ilitumika, mapenzi na upendo ulichochea mtu mzima kupindisha ukweli, Anyway nakutania tu comrade, usichukulie serious kiiiiiiiiiiiiivo! Hivi unajua mimi nimeoa Lembeni pale, kwahiyo wewe ni shemeji yangu, usinune.

Halafu hakuna namna unawezafanya "kisichana cha kizaramo" kikarudi sokoni,? Ni aibu kuweka BAPA/JIBAPA mchana kweupe-pee halafu meza nzima umekaa peke yako! Fanya manuva basi.

Aluta continua.
 
U hali gani bosi wangu, shaka sina unaendelea vema kabisa na harakati za ujenzi wa taifa, Naandika waraka huu nikiwa na nia na lengo la kukumbusha tulipotoka ila sio kukukosoa.

Ndugu yangu mshana jr ni dhahil-shahil kwamba katika maisha yako yote hukuwahi kuwaza kukamatia nafasi uliyonayo sasa, yaani kwa kiswahili cha haraka haraka ambacho watu wanaweza kuelewa ni kwamba ulidondokewa na embe chini ha mnazi.

Hata unakumbuka mtu ambaye ilibidi awe hapo ni kiasi gani ameamua kuwa na moyo wa chujio wa kukubali kupoteza kwa maslahi mapana ya amani ya wote waliotaka yeye akalie hicho kiti ulichokalia wewe, ajabu ni kwamba badala ya kuunga mkono yale yanayozungumzwa na ndugu zake ambao umeapa hasirani-abadani kwamba hutaki hata kuwasikia, ndiyo kwanza umekua ukiwakejeli na kuwanyima upenyo kuonekana na kuzungumza.

Imefika mahali unajitapa hadharani kwamba hicho kiti ulikipata kutokana na jitihada zako na wala hakuna yeyote aliyekushauri kwenda kwa seremala kukichongesha! Yaani umewadharau mpaka wale jamaa wawili walioingia msituni, wakatafuta mti mzuri, wakaukata na kuuchana vizuri na kuuleta kwa huyo seremala wako unayejivunia. Huku ni kukosa shukrani sana hasa kwa mtu kama wewe ambaye unapenda sana kuingia kwenye nyumba za ibada na kujifanya wewe ni mpole na huruma sana.

Ulipoanza kukikalia kiti ulikua mnyenyekevu haswa hata ukawaomba wanakijiji wakukumbuke katika dua zao ila sasa inaonekana ushaota mkia na pembe umejiongezea mwenyewe, nikukumbushe tu ndugu yangu mshana jr kua wewe sio wa kwanza kukalia hicho kiti, utakaa na ikiwa mapenzi ya mwenyezi Mungu tunaendelea kua hai basi ishaallah atakalia mwengine wewe utake au usitake.

Hebu mtazame mkalia-kiti aliyepita sasa hivi! Unamuonaje? Anajisikia raha kweli kweli maana kila anapopita watu wanamshangilia na kumsifia ingawa in reality watu walimponda sana wakati akiwa hatamuni, ila kutokana na majigambo na kujiona wewe unakaribia kua Muumba watu wanaona bora yeye kuliko wewe, naam hizo ndio tamaduni na mazoea yetu sisi ngozi nyeusi, tunapenda kulinganisha perfomance.

Hivi bwana mkubwa mshana jr unajua huku kijijini kwa sasa maisha yamekua magumu mnoo, yaani hata ugali umekuja kua anasa kweli? Huku wapi unatupeleka ndugu yangu? Hebu jitafakari mara mbili mbili, inawezekana kuna mahali unakosea au wanaokushauri hawakupi mbinu nzuri, kikubwa braza tunataka unafuu hapa kijijini kwetu.

Najua wale walioleta ule mti uliotengeneza kiti chako kwa sasa wanaonekana wapuuzi tu ila trust me pamoja na uhakika wa mambo ya CHAJE 2020 unashughuli pevu sana, maana matokeo hua hayajipangi, yule mkongwe alipotamka kua "jamani mimi nayasoma kama nilivyoyapokea" sio kweli kwamba hakujua mambo ya Teknohama yalihusika, alijua sana, na mimi binafsi kama Mgibeon naamini kua pale ni zaidi ya pesa ilituma, mapenzi na upendo ulichochea mtu mzima kupindisha ukweli, Anyway nakutania tu comrade, usichukulie serious kiiiiiiiiiiiiivo! Hivi unajua mimi nimeoa Lembeni pale, kwahiyo wewe ni shemeji yangu, usinune.

Halafu hakuna namna unawezafanya "kisichana cha kizaramo" kikarudi sokoni,? Ni aibu kuweka BAPA/JIBAPA mchana kweupe halafu meza nzima umekaa peke yako! Fanya manuva basi.

Aluta continua.
Mgibeon , ni wachache sana watakuelewa ulichoondika hapa. Ila Mwenye macho na aone, mwenye masikio na asikie. Kama anadhani wale majirani wawili wa kabila lake la siri watamsaidia mshana jr , basi anajidanganya. Maana hata Gwiji wa maunjanja aliyepita, pamoja na mtandao usiomithilika alishindwa kumwachia kiti mtu anayemtaka. Sembuse yeye wa kuja?
 
Mgibeon , ni wachache sana watakuelewa ulichoondika hapa. Ila Mwenye macho na aone, mwenye masikio na asikie. Kama anadhani wale majirani wawili wa kabila lake la siri watamsaidia mshana jr , basi anajidanganya. Maana hata Gwiji wa maunjanja aliyepita, pamoja na mtandao usiomithilika alishindwa kumwachia kiti mtu anayemtaka. Sembuse yeye wa kuja?
Kweli kabisa Mkuu, unless abadilishe KITABU kua ukomo ni kufia.
 
.

Halafu hakuna namna unawezafanya "kisichana cha kizaramo" kikarudi sokoni,? Ni aibu kuweka BAPA/JIBAPA mchana kweupe halafu meza nzima umekaa peke yako! Fanya manuva basi.

Aluta continua.
Kila kitu kimeadimika, why?????

Pesa zote za 'dili' ndogo wanazofanya watanzania wa kawaida mwisho wake nyingi zinarudi serikalini kwa njia ya kodi mbali zinazokatwa kwenye huduma mbalimbali watanzania hawa wanazozitumia siku hadi siku. Sasa kila 'dili' halali wanazofanya watz hawa wa kawaida zisibanwe kwani huko ni kuongeza sintofahamu kwenye mzunguko wetu wa pesa.
Rushwa bado ipo sana tu kwa wafanyakazi mbalimbali wa serikali, japo si ya waziwazi kama awamu zilizopita. Sasa hivi wanajiuliza mara mbili kabla hawajavuta.
 
Mgibeon , ni wachache sana watakuelewa ulichoondika hapa. Ila Mwenye macho na aone, mwenye masikio na asikie. Kama anadhani wale majirani wawili wa kabila lake la siri watamsaidia mshana jr , basi anajidanganya. Maana hata Gwiji wa maunjanja aliyepita, pamoja na mtandao usiomithilika alishindwa kumwachia kiti mtu anayemtaka. Sembuse yeye wa kuja?
Hivi anaundugu na wale vampires wawili? Mmoja mwembambaaaaaaaaaaaaa, mwingine, anasimamishaga Gari porini ili aongee na simu
 
Hivi anaundugu na wale vampires wawili? Mmoja mwembambaaaaaaaaaaaaa, mwingine, anasimamishaga Gari porini ili aongee na simu

Ndiyo washauri wake na wana kaunasaba. Ukiona hata watu wa system wameanza kuhoji uhalali wa uswahiba wa yule tall na Mshana wetu ujue hali ni tete. Kuna msystem mmoja nayeishi Usikochi, ambaye pamoja na Mzee wetu wa Kijiji anayeishi USA waliokuwa wamejitoa akili kumtetea Mshana Jr. sasa wanajuta na ndo hao wameanza kuogopa uhusiono huo wa hao Terrible Twins wa maziwa makuu.
 
Noma sana kila kona mshana jr kila chocho mshana jr
mkuu mshana umetisha sana maana hata mimi nakukubali sana maana kama
hapa umetumika kufikisha ujumbe ambao kule ugweno juu sijui kama watakuelewa
Ujumbe umefika vema pale karibu na ofisi za Bin Slum Tyre
 
Ndiyo washauri wake na wana kaunasaba. Ukiona hata watu wa system wameanza kuhoji uhalali wa uswahiba wa yule tall na Mshana wetu ujue hali ni tete. Kuna msystem mmoja nayeishi Usikochi, ambaye pamoja na Mzee wetu wa Kijiji anayeishi USA waliokuwa wamejitoa akili kumtetea Mshana Jr. sasa wanajuta na ndo hao wameanza kuogopa uhusiono huo wa hao Terrible Twins wa maziwa makuu.
Mzee wetu wa Kijiji amekuwa tofauti na tulivyo mzoea, ngwe kadhaa zilizopita. Ngoja tuone, atanyooka tu, maana siku hizi ndio mtetezi Mkuu wa mshana jr
 
Mgibeon nafukuzana na sembe hapa mashineni ndo nafuu kidogo 1700.pale kwa mangi ni 1900.nimeokoa shilingi 200.sabuni ya unga ya mia mbili 200.. elfu mbili imeisha ,nimepata kilo na sabuni ya unga nyama nusu 3500. mchicha wa 500. du mafuta kumbe hamna ya taa na kupikia .....narudi badae
 
Nimefungua uzi haraka haraka nikajua leo mshana jr anapewa ushauri hasaa ulio makini!

kumbe daaah siyo ila ni ushauri mzuri kwa yule baba mwenye gari siyetaka kuambiwa gari hand break haifanyi kazi maana atasema kwani jiwe hakuna?

ilimradi safari iende! na gari likisimama mtu kushuka tunaweka tu jiwe ili lisiserereke!

ha ha ha haaaa...huyo ndo baba mwenye gari bhnaaa
 
Back
Top Bottom