msiwe na shaka juu ya hilo maana chadema hawako pale kumuapisha sheikh au askofu..ni darasa kwenda mbele la kujitambua,kujielewa na kujua mustakabali wa nchi..wazanzibar si wajinga kiasi hicho na wengi wao wanaitambua chadema..hayo mengine yatapita kama upepo..subiri uone
Mkuu sana sheiza ni muhimu sana kujifariji ila ni muhimu zaidi kuuona ukweli kuukubali na kuchukua hatua stahili kwa muda stahiki. Ila kuhusu kona hiyo ya dunia mi nna hakika kabisa kuwa ndio tunaanza mwanzo kabisa kuwazindua kutoka usingizi wa pono ni wakati ambao mtu hawezi kutegemea matokeo bora mara hii,ila ni wakati wa kutayarisha shamba. Mimi nilitegemea hayo na zaidi ya hayo sijui mwenzangu hukuijua zanzibar?huijui ccm wewe?achilia mbali udini wapo tayari kuona amani ya nchi ikitokomea ili tu waonekane wameshinda uchaguzi hata wa vichochoroni.
[/HR
]