Waraka wa Kibanda kabla ya kufikishwa mahakamani

Status
Not open for further replies.
chama tawala wagonjwa waende Kenya wajionee uhuru wa waandishi wa habari... sooon CCM yatawatakumba
 
iNGEWAWEKA NDANI WOTE HAWA

WAKISHAMALIZA IHAMIE KWA WAANDISHI WA HABARI USHWARA AMBAO THEY CANT THINK BEYOND YANAYOANDIKWA JF

MEDIA IN TANZANIA IS JUST DISGUSTING....
 
Na Yule Mhariri wa Gazeti la serikali aliyeandika wakati wa uchagu yakwamba kamwe DR SLAA atokuwa RAISI anafikishwa lini mahakamani? na matusi wanayotukana baadhi ya watangaji wa clouds FM kuna hatua zimechuliwa? au hii ni CCM vs CHADEMA waje wazi wazi basi wanajificha nini?

serikali ipi???
 
poor wahariri.....ukiacha mwananchi/citizen wengine wote hamna mnachokifanyia nchi hii...majungu tu, acheni mmalizane wenyewe..

Kibdana ni mtoto wa EL....hii vita haiko inavyodhaniwa
 
poor wahariri.....ukiacha mwananchi/citizen wengine wote hamna mnachokifanyia nchi hii...majungu tu, acheni mmalizane wenyewe..

Kibdana ni mtoto wa EL....hii vita haiko inavyodhaniwa
Kama ni kweli na serikali inataka kumshukia Kibanda ili kuithibiti kasi ya EL, then imechelewa!. Hawatamweza EL, huwezi kuizima cheche ya moto wa nyikani kwa kuipulizia upepo kama kuzimavyo mshumaa au njiti ya kibiriti!.
 
Tayari habari zisizothibitishwa zinataja baadhi ya wahariri walio kwenye orodha ya kukamatwa na kushitakiwa katika mkakati wa serikali kutumia polisi kutisha waandishi wa habari na wakosoaji wengine wa serikali.


Hata kabla ya Jukwaa la Wahariri kutoa tamko lao, vyanzo kadhaa vya habari serikalini vililidokeza gazeti hili kwamba polisi wanatekeleza mpango huu kwa amri ya wakubwa wanaokerwa na ukosoaji unaofanya na baadhi ya waandishi, wanasiasa, wanaharakati na vyombo vya habari.
Wajameni kwa msiojua, huu ni utekelezaji wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976 ambayo ni moja ya sheria kandamizi na imo kwenye ile list ya sheria 40 ambazo Tume ya Nyalali ilishauri zifutwe.

Ninachokiona sasa ni kwa serikali kifanya double standards kwa kuwalenga inaowatafuta na kuwaacha kujivinjari inao wasupport.

Tusimlilie Mwigamba na Kibanda, bali tupaze sauti zetu sheria hii isitishwe kitumika na badala yake sheria mpya ya habari yenye haki ya kupata habari ambayo serikali wameikalia tangu mwaka 2003, sasa iletwe bungeni na kuireplace hiyo Newspapers Act of 1976.

Tena tushukuru Mungu kwa miaka hiyo yote, serikali haikuwahi kuitumia sheria hii ipasavyo kwani kama ingetumika huko nyuma, magazeti kama Mwanahalisi, Raia Mwema and the like yaliyojikita kwenye ukosoaji wa serikali, yangekuwa ni hadhithi tuu kwani yangeshafungiwa zamani!.

Nionavyo mimi, lengo la serikali kwenye hiki kibano kwa Mwigamba na Kibanda tena watamuunganisha na printer, Mwananchi Communications, ni kutuma salamu kwa wahariri wote kuwa very carefull na contents za magazeti yao kwani sheria hiyo bado ipo!.

Kitendo cha kumuunganisha printer kama sheria inavyosema ni kuhakikisha wachapishaji wanakuwa resiponsible na contents hali itakayopelekea kususa kuchapisha baadhi ya magazeti yatakayo leta burning issues!.

Nimesema serikali inafanya double standards ili tuu kutishia nyau uandishi critique!.

Bado sijajua Mwigamba anatetewa na nani, ila wanasheria watetezi wa Kibanda, Nyaronyo Kicheere na Juma Thomas, wote ni wanahabari/wanasheria waliofikia level za editors Nyaronyo akiwa mhariri wa Citizen na Juma Thomas alikuwa mhariri wa the Guardian, natumaini waitumia kesi hii sio tuu kuonyesha jinsi sheria hiyo ilivyo mbaya, bali kumconvince jaji pia atoe order sheria hiyo iwe scrapped off from the books of law!.
 
Wajameni kwa msiojua, huu ni utekelezaji wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976 ambayo ni moja ya sheria kandamizi na imo kwenye ile list ya sheria 40 ambazo Tume ya Nyalali ilishauri zifutwe.

Ninachokiona sasa ni kwa serikali kifanya double standards kwa kuwalenga inaowatafuta na kuwaacha kujivinjari inao wasupport.

Tusimlilie Mwigamba na Kibanda, bali tupaze sauti zetu sheria hii isitishwe kitumika na badala yake sheria mpya ya habari yenye haki ya kupata habari ambayo serikali wameikalia tangu mwaka 2003, sasa iletwe bungeni na kuireplace hiyo Newspapers Act of 1976.

Tena tushukuru Mungu kwa miaka hiyo yote, serikali haikuwahi kuitumia sheria hii ipasavyo kwani kama ingetumika huko nyuma, magazeti kama Mwanahalisi, Raia Mwema and the like yaliyojikita kwenye ukosoaji wa serikali, yangekuwa ni hadhithi tuu kwani yangeshafungiwa zamani!.

Nionavyo mimi, lengo la serikali kwenye hiki kibano kwa Mwigamba na Kibanda tena watamuunganisha na printer, Mwananchi Communications, ni kutuma salamu kwa wahariri wote kuwa very carefull na contents za magazeti yao kwani sheria hiyo bado ipo!.

Kitendo cha kumuunganisha printer kama sheria inavyosema ni kuhakikisha wachapishaji wanakuwa resiponsible na contents hali itakayopelekea kususa kuchapisha baadhi ya magazeti yatakayo leta burning issues!.

Nimesema serikali inafanya double standards ili tuu kutishia nyau uandishi critique!.

Bado sijajua Mwigamba anatetewa na nani, ila wanasheria watetezi wa Kibanda, Nyaronyo Kicheere na Juma Thomas, wote ni wanahabari/wanasheria waliofikia level za editors Nyaronyo akiwa mhariri wa Citizen na Juma Thomas alikuwa mhariri wa the Guardian, natumaini waitumia kesi hii sio tuu kuonyesha jinsi sheria hiyo ilivyo mbaya, bali kumconvince jaji pia atoe order sheria hiyo iwe scrapped off from the books of law!.

Pasco uko sahihi mkuu, hizi ni salam mbaya sana kwa wanataaluma ya habari na wadau wake kwamba sheria mbaya bado zipo, japo zilikua hazitumiki na kwamba kutotumika kwake haina maana kutokuwapo kwake.

Jambo la msingi ni kwamba je, kwa kuwa sheria zipo tuache kuandika? Je, kama tunaandika tuchukue hatua gani? Haya ndio maswali ya kujiuliza na kufanya maamuzi ya pamoja ya kitaaluma na mshikamano hapa ni muhimu.

Kuna tatizo moja baya katika taaluma yetu kwa sasa kwamba bado ule mgawanyiko wa chini kwa chini miongoni mwa wanahabari unawatafuna na mara nyingine busara inashindwa kutawala na pengine kutoaminiana kunachukua nafasi. Katika hili, tusidanganyane HAKUNA ALIYE SALAMA hata waandishi wa UHURU na DAILY NEWS hawako salama kisheria. Tusidanganyane kwamba kosa lililofanywa na serikali itakuwa ndio mwisho, huu ni mwanzo na ni sawa na simba kula nyama ya mtu, atamaliza kijiji chote kwa utamu wake. Nakumbuka na hadi sasa hiyo sheria ipo ya PCCB kifungu cha 37 ambayo inazuia habari
Zozote zinazochunguzwa kuandikwa ama kuzungumzwa hata na wakuu wa PCCB wenyewe, lakini mara tu ilipopitishwa waandishi na wanaharakati waliikiuka na hadi leo hakuna hatua zilizochukuliwa kwani wangechukuliwa hatua wangap? TUTAFAKARI
 
Tatizo kubwa kwa watanzania ni kwamba tunatanguliza ushabiki na kuweka pembeni uzalendo. ombwe la uongozi linaonekana wazi halihitaji degree kuelewa.

Wachangiaji ioneeni huruma inchi hii na vizazi vijavyo. Atakaeumia hapo baadae ni kaka, dada, shangazi, mjomba au aweza kua mjukuu wako.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom