Waraka wa Bernard Membe kwa Askofu Mwamakula: Sitishiki, sitakaa kimya na kamwe sitaabudu mtu wala miungu wengine

Waraka huu lazima umtoe povu yule mshamba na limbukeni. Lazima atafyatuka tu.

Utangulizi wa kachero mbobezi nimeupenda sana pia, ameanza kwa maneno 2 tu "NIGUSE NINUKE".

Nami namuonya limbukeni, asithubutu kumgusa kachero mbobezi.

Patamu hapo
 
"Tusipotokea wachache wa kuyasema na kuyakemea mabaya Baba Askofu, nchi hii itaingia kwenye matatizo makubwa zaidi ya haya tunayoyaona!"

"Lakini leo sisi tunaonekana ni maadui wa Serikali na hakuna jema lililofanywa na awamu zilizopita"

"Pamoja na makosa yote yaliyofanywa na Awamu zilizopita, Serikali na Viongozi hao walijitahidi kuheshimu Katiba, Uhuru, Sheria na Haki za binadamu. Huo ndiyo msingi wa Uongozi Bora Duniani".

Kama haya kweli ni maneno ya Membe, basi amemaliza! Need we say more?
 
Kwanza nimsifu Askofu kwa kusimama kwenye ukweli kwa ujasiri. Watu wa Mungu hawastahili kuwa waoga maana aliyetuumba hakutuumba hivyo. Alitupatia roho ya ujasiri ipendayo kweli. Ibilisi ametutia uoga na unafiki sisi na viongozi wetu wa dini, serikali na makundi mbalimbali.

Namshukuru Mungu pia kwa kumjalia Bernard roho ya ujasiri. Ujasiri wa kuunena ukweli. Kwa hali ya sasa ambapo wengi wamepigwa ganzi na sindano ya uoga, inahitaji msaada wa Mungu kuunena ukweli. Wengi tumebakia kuwa majasiri wa mtandaoni. Hata huku pia tumeyaficha majina yetu kwa uoga. Naomba siku moja Roho wa Mungu atujilie, sote tuamue kuyaweka majina yetu dhahiri, ikiwezekana na namba zetu na mahali tuishipo. Ili kama kuna shetani aliyewahi kuushinda ukweli atukamate wote tunaounena ukweli (ukiacha wanaotusi).

Kwa upande mwingine hekima iwaingie watawala ili watambue hawabebi chochote katika miili yao zaidi ya kile Mungu aliwaumba nacho:

1) hawatuzidi wengine katika ubinadamu

2) hawakupewa akili kutuzidi sisi sote

3) hawakupewa roho nyingi zaidi ya wengine

4) wamepewa madaraka yanayoweza kuwafanya wabarikiwe au walaanike kutokana na kiburi cha mamlaka au unyenyekevu utokanao na hekima ya Mungu

Wakipata hekima, watayafanya haya:

1) watakuwa watumishi wa vitendo badala ya kuwa watawala wanafiki wanaonena tofauti na wanayotenda

2) watakubali hekima za wazee wetu kuwa ukubwa ni jalala, watayapokea mema na mabaya dhidi yao lakini wao watatenda mema hata dhidi ya wale wawaneneao mabaya kwa husda

3) watatmbua kuwa hawakuletwa duniani wala hawakupewa mamlaka kwaajili ya kutesa, kuteka, kupoteza watu au kuua bali walistahili kusimama katika hekima ya utawala yaani kuwa kama jabali lenye kutoa kivuli kwenye jangwa (kukiwa na joto kali la jua, watu wajikinge nalo), na pia wawe kama kijito kitiririshacho maji katika ardhi kame (watu wakifuate hicho kijito ili kupata tulizo la kiu)

4) hawatahangaika na kisasi wala kuwakomoa watu kwa kuwatengenezea kesi za utakatishaji fedha au uhujumu uchumi pasipo haki wala hawatapora mali za watu kwa sababu tu wana mamlaka

5) hawatawakomoa wapinzani wao kwa kuwafilisi bali watakuwa wanyenyekevu na wenye hamu kuwasikiliza wapinzani wao ili wayasikie mapungufu yao

6) hawatafanya teuzi za upendeleo wala utumbuaji wa kisasi bali kila jambo kwa kweli ya Mungu

7) Hawatajificha katika jina la Mungu katika kuuficha uovu wao bali wataenda mbele za Mungu kumwomba awajalie roho ya kutenda haki, kuondoa chuki na upendeleo, kuyaishi wanayoyatamka na kuongoza kwa kweli yake na wala siyo kwa hadaa.

8) hawatatenda kwaajili ya kutafuta sifa, wala hawatataka kuwatweza watawala na watendaji waliotangulia bali kwa unyenyekevu watasawazisha ambapo hapakuwa sawasawa maana na wao ya kwao yatasawazishwa na wengine

9) watatamani kusikia mapungufu yao kuliko kusifiwa kwa unafiki

10) watatambua kuwa ukiwa mtawala, wengi wanafiki watakuimbia sifa usiku na mchana, lakini ukiwa na hekima utawasikiliza zaidi wenye mawazo tofauti kuliko wanaokusifia tu.
 
Upuuzi na uomgo , eti kampeni na ufisadi.
Hivi huyu siyo yule wa mabilion ya Gaddafi, siyo yule wa clip za kupindua serikali?
Shetani hana tone la aibu.
Hayo mabilioni ya Libya, una kielelezo chochote? Naamini siyo kweli.

Kama ingekuwa ni kweli, yaani kwa utawala huu na jinsi unavyomchukia Membe, angekuwa wa kwanza kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha.

Kwa sababu hakuna lolote mpaka sasa dhidi yake, itakuwa ni kweli kuwa anasingiziwa.
 
baba askofu Emmaus Mwamakula! .....usiingie kunako mtego ..... Mtu akishasema nimetokewa na Yesu, usimuamini haraka haraka utakuwa umenasa kwenye mtego wa ibilisi, maana jicho litamuangalia yeye kwa kila kitu hata akibolonga bolonga mambo, tayari mawazo ni ametokewa na Yesu kwa hiyo kila kitu kiko sawa...........
 
KAMWE SITAABUDU MTU WALA MIUNGU WENGINE.

***akimaanisha kamwe hataenda jumba jeupe kupiga magoti kuomba msamaha**
Hiyo ni kauli thabiti. Ni sawa na ile ya shahidi wa uganda aliyeifia dini ya Kikristo. Alipewa vitisho, aliona wenzake wakiuawa, na yeye akielekea kwenye njia ya kifo lakini bado kwa ujasiri mkubwa alinena:

INANIPASA KUMHESHIMU MUNGU ZAIDI KULIKO MWANADAMU

Kama raia wema kwa Taifa letu na watu tunaomtii Mungu, pale viongozi wetu wanapokengeuka na kutoheshimu katiba yetu, SISI TUNASTAHILI KUSIMAMA KATIKA UKWELI WA KUHESHIMU NA KULINDA KATIBA. Yatupasa kunena kwa ujasiri:

TUNASTAHILI KUILINDA, KUHESHIMU NA KUIFUATA KATIBA kuliko kauli ya mtawala iendayo kinyume na katiba yetu. Na kauli yetu iwe thabiti hasa, na mtawala mwenye kutenda kinyume na katiba aweze kufahamu kuwa hana nafasi ya kuongoza Taifa letu.
 
80 Reactions
Reply
Back
Top Bottom