Waraka usio wa siri wa CHADEMA dhidi ya wasaliti

Status
Not open for further replies.

Nduka

JF-Expert Member
Dec 3, 2008
8,552
2,360
Onyo:
  • Sintotoa ushahidi wa haya ninayoyaandika hapa hata kwa vitisho vya kufutwa thread au kufungiwa JF
  • Ushahidi wa jambo hili ni hatari kwa maisha ya yeyote anayeumiliki, hivyo hata kama unao ni marufuku kuunganisha kwenye huu uzi

Mara baada ya CC ya CHADEMA kuwavua nyadhifa zao Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba na Zitto Kabwe, kundi linalojiita la ushindi, kwa kutumuia nafasi zao ndani ya chama liliwatuma watu kwenda huko kwa wanachama kuelezea maamuzi haya. Kundi hili linaundwa na watu wanaoaminika na familia ya mzee Mtei lilikabidhiwa waraka maalum unaolenga kumchafua kwa kila kashfa ikiwemo matusi ya nguoni Zitto Kabwe.

Uchunguzi wa kawaida umebaini kuwepo kwa version mbili za waraka huo, moja ikiwa ni ya kawaida yenye kashfa zile zile za kila siku sema wakati huu zikiunganishwa na matusi ya nguoni dhidi ya Zitto na ule ninaouita usio wa siri ambao hata wagawaji wake ni wale tu wanaotokea mkoa wa Kilimanjaro na wanaamika zaidi na mzee.

Kwenye huu waraka zinajengwa chuki dhidi wasiowatakia mema wachaga na wenye lengo la kuhamisha nguvu ya chama na fursa pekee ya wachaga kuongoza nchi. Waraka huu unamtaja kuanzia muasisi wa nchi katika jitihada za kuzuia nguvu ya wachaga hadi wa huyu aliyepo na mwisho unawataka wachaga wote, ndani na nje ya CHADEMA kuwaunga mkono wale wanaotetea haki yao iliyopokwa.

Huu ndio waraka usio wa siri wa CHADEMA, nawaomba viongozi wa CHADEMA kwa staili ile ile ya kusimamia maamuzi magumu muutoe huu waraka ninyi wenyewe hadharani.
 
We walaka wenyewe ni huu au kuna mwingine tuusubiri?

Mkuu kapime afya ya kichwa?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom