Waraka no. 1 wa mwaka 2012 wa Mbunge kwa Wananchi- “Ukweli ni Uhuru”- Mnyika

John, copernicus alisimamia ukweli dunia nzima ilipotoka! Simamia haki daima, usitishwe mwisho wa siku utakuwa mshindi!
 
safi mnyika huo ndio msimamo wangu pia kuwa sisi watanzania tumekuwa waoga na hivyo wanafiki na ndo maana tumefika hapa kwa kisingizio cha mfumo wetu ni mbaya na dhaifu wakati sisi wenye mfumo hatukubali kuwa ndio wabaya na wadhaifu nambari wani. mimi binafsi najilaumu na kwa kutofanya jambo la kubadilisha hali hii maana itakuwa aibu kwa watoto na wajukuu zetu.mimi nachukia unafiki sana.wakati nikisoma sekondari(O- level) mama yetu alifariki na baba akaoa mwanamke mwingine baada ya muda wa chini ya mwaka 1,nilimwambia wazi bila kumumunya maneno kuwa amefanya haraka sana na zaidi mwanamke aliyemuoa haikuwa chaguo sahihi nikagombezwa sana na ikafikia hatua ya kuitwa kwenye kikao cha wanafamilia nakutakiwa kuomba radhi kwa kuingilia mambo ya mzazi wangu,lakini nikasimamia ukweli kwa gharama ya kunyimwa ada,baadaya miaka mitatu my father admitted that i was dame right!UNAFIKI NA UOGA NDIO CHANZO CHA MATATIZO YETU WATANZANIA! mnyika hongera na kandamizia hapo hapo no matter what !

Woga ni tabia ya watu waliokata tamaa na wachoyo. Tujenge tabia ya kusema hapana kwenye kitu ambacho tunaamini ni cha kweli. Mnyika umefanya jambo la maana kusimamia ukweli.
 
duh nimepitia waraka wote hakuna hata kero za jimbo la ubungo hakuna kwenye waraka mrefu wa ngojera ya ukweli uhuru! ngonjera ngonjera ngonjera! wana ubungo mme-vulugwa mchana kweupe!
 
Ukweli ni uhuru safi sana kamanda na huo ndo ukweli wenyewe tofauti na hivyo ni uongo na ndo magamba wanachopenda kusikia.
 
Mnyika nilikwambia humuwezi Kikwete, shauri lako, wewe endelea tu.
Mkuu ningependa sana kufahamu nini haswa unalowaza, nini unalotaka tulifahamu hapa? Je unavyotoa ni vitisho kwamba wewe ndiye mtekelezaji wa majibu au visasi, ni mtetezi au unajaribu kututhibitshia kuwa Raisi si dhaifu na kwamba anaonewa ? Hebu jaribu kutupatia mwelkeo wa mawazo yako kwa undani zaidi. Wakati mwingine inakaa kama unamfahamu sana Kikwete uwezo wake wa kutenda. Ingekuwa uzalendo mwema kuyajadili mambo kwa uwazi zaidi kama kweli unalipenda Taifa lako.
Ila nikuhakikishie tu kuwa wengi humu tunamuelewa Mh. Mnyika kama "a True Patriot of this Nation".
Please come out clean!
 
Endeleeni kupindisha maneno lakini ukwel uko pale pale, mbunge wenu anajitetea na mnakaa kumsifia.
 
Waraka kama huu huwezi kukurupuka tu na kuanza kujibu hovyo hovyo kama vile umesimama kwenye kamba iliyoning'inizwa hewani. Utaangukia kichogo!
 
Nidhamu ya unafiki na uoga tu. Unaogopa kumwambia mtawala ukweli kwa kuwa tu mnasali pamoja!

Kuna ukweli upi mnaujuwa nyinyi? ukweli "0", kwi kwi kwi teh teh teh, si makosa yenu, mnadanganyana toka Sunday school.
 
ubungo imekula kwenu! ngonjera hizi hadi lini!

Wewe unaona ngonjera kwa sababu ukweli huo unakuumiza. Mlengo wa kati unapaswa kutambua kuwa licha ya kuwajibiga kwa wapiga kura wake, mbunge huwajibika pia kwa taifa lake. Mnyika ni miongoni mwa wabunge wachache wanaojua majukumu yao ipasavyo. Bahati mbaya yupo chini ya uongozi dhaifu wa muhimili mwingine wa dola aka sirikali. Ukweli ni uhuru
 
Kuna ukweli upi mnaujuwa nyinyi? ukweli "0", kwi kwi kwi teh teh teh, si makosa yenu, mnadanganyana toka Sunday school.
Utacheka sana, mwisho utagundua kuwa kinachokuchesha ni kukosa ujasiri wa kukubali kuwa unaye mtetea ni raisi dhaifu kupita kiasi.
 
Kutetea haki ni gharama hasa pale ukweri unaposemwa kuhusu udhaifu wa wakubwa,
pambana kijana tupo nyuma yako
 
Back
Top Bottom