Waraka maalum wa kujivua Uanachama ndani ya CCM

WARAKA MAALUM WA KUJIVUA UANACHAMA NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI- CCM.

Leo 29 January 2017, Mimi Deogratius Kisandu niliyejiunga CCM tarehe 27 September 2014 na kupokelewa na Mh. kinana Katibu Mkuu wa CCM na Mh. Nape mwenezi wa CCM wilayani Lushoto,Tanga katika kata ya Mlola. Leo ninatangazia umma wa Tanzania kuwa nimeipa talaka CCM. Kuanzia Leo Mimi sio Mwana chama wa CCM tena.

KWANINI NIMEIPA TALAKA CCM.

Kuna mambo mengi sana maovu na ya kinyama yaliyofanywa juu yangu na CCM na viongozi wake kwa miaka mingi sasa. Kwakuwa wao kama chama wameshapanga tangu zamani kuwa nikitaka kuondoka CCM watajifanya kama walikuwa hawajui maovu na unyama uliokuwa unaendelea. Hivyo Mimi sio mtoto mdogo najitambua na ninajua nafanya nini.

CCM kila mtu anatumia nafasi yake kudhalilisha walio chini. Huwezi amini Balozi anauwezo wa kumdhalilisha Mtanzania mwenzie kisa anategemea nguvu ya DC au RC au agizo la Waziri Fulani.

Kesi nyingi za Watanzania ni za kubambikwa ambao ndio mchezo mchafu unaochezwa na CCM, hata hivyo wameahidi kuniteka kama nitaondoka CCM, Mimi nasema Niko tayari. Japo viongozi WA juu wa CCM wao wamepanga nifunguliwe kesi yoyote ili kunizima kisiasa tena wakitaka kuniondolea sifa ya kugombea Urais 2020.

Nachelea kusema vijana wengi kutoka upinzani watabambikwa sana kesi ili wapoteze sifa ya kugombea 2020, na kuna ma DC na Ma RC wanataka majimbo 2020 hivyo wanatumia fursa hiyo ya udhalilishaji wa kubambika kesi ili wenzao wapoteze sifa 2020 na wao wapate kugombea majimbo hayo.

Katiba ya CCM inasema DC na RC ni wajumbe katika vikao vya CCM wilaya na MKOA. Hivyo sishangai mateso niliyopata kuagizwa na wajumbe hao. Wapo Mawaziri walio wahi kuagiza nibambikwe kesi lakini watu wema wakakataa.

CCM wanatumia maandiko yangu ya mitandaoni kuongoza Nchi, CCM wanatumia Vitabu vyangu kuongoza nchi(Utani wa serikali na Wananchi, kijarida cha Ukombozi wa Pili wa Taifa Letu) halafu wanakana kwamba sio Mimi, tena mwezi Jana kunamtu kawavujishia kitabu changu kipya cha Mwanamalundi, na wameiba mawazo yangu na kuanza kuyatumia, huku wakijipanga kunipinga.

Kadi yangu ya CCM niliyopewa Lushoto ni No. AF 5864962. Na kwa utaratibu wa CCM nilienda kwenye tawi la Shunu, Kahama ,Shinyanga ili kunitambulisha na kupewa kadi No. AI 8229534 na kwenye daftari ni mwanachama wa 905.

CCM ni chama kisichokuwa na mawasiliano kila kiongozi anaweza Fanya jambo bila kutoa taarifa kwa mwenzake. Kwa mtindo huo ni rahisi sana hata kufanya mauaji maana hakuna kutarifiana. CCM watu wenye nguvu kama Deo Kisandu wanawekwa Vizuizini na kuwekewa vikwazo vya kimaisha ili Wafe au wadhalilike na wao kunona.

CCM inahitaji wana chama ambao ni Wababaishaji na waongo waongo ndio ambao wanafaa kwa mamlaka yao.

Mimi Leo nimekuwa kama CHOKORAA na ni baba wa watoto, basi wao CCM ndio furaha kwao. Upuuzi huu waliufanya mpaka kwa marehemu Mzee wangu. Sasa imefika tamati.

CCM wanaagiza watu waniwekee makamera na vinasa sauti darasani nikiwa na fundisha halafu baada ya siku mbili unasikia DC au RC au Waziri kaibuka na ajenda zangu. Wamekuwa pia wakinitegeshea makamera sehemu Nazo panga vyumba vya kuishi ili wapate mawazo yangu watumie kuongoza nchi.

CCM wanapanga kunidhulumu hata mashamba, CCM wanatembelea NYOTA YANGU ili wang'ae. Mungu hadhihakiwi, tutashuhudia mengi ya kuboronga ndani ya CCM. Kuniua hamuwezi, labda mkakati ule wakunihamisha kituo kwenda kijijini.

CCM nawatakia safari njema ya utawala wenu, jitazameni sana,,,,siasa za kufanyiana unyama zimefika mwisho.

Hata hivyo bakini na CCM yenu, na sisi tutasajili chama kipya cha Arena for Correcting Africa-Tanzania (ACA) na usajili lazima mtupatie maana ni haki yetu Kikatiba. Nchi yetu ni ya mfumo wa vyama vingi.

Wana CCM muda mrefu wamekuwa wakisema Deo Kisandu tusimfukuze Bali tusubiri aondoke mwenyewe halafu tugawane vyeo. Haya sasa nimeondoka gawaneni vyeo, tumeni na Polisi waje wanikamate kwa utovu wa nidhamu.

Kwaherini Majembe ya CCM. Ninyi ni majembe sana nawakubali sana. Lakini mimi sio jembe, Mimi ni Mpini wa jembe.

Wakolosai 4:5-6 itawasaidieni. Najua mmepanga kuniwekea Vikwazo zaidi baada ya kunidhalilisha. Nasema nitakuwa tayari kuvunja sheria kama mtanikandamiza kwasababu zenu za kimaslahi yenu.Na Kadi yenu hiyo chukueni. Hata mkivujisha video ya kujiunga CCM mliyokuwa mmeificha haitasaidia. Endeleeni kunizushia ujambazi na ugaidi mazara yake mtayaona kwenye familia zenu soon. MUNGU ANAONA.

Ndimi:
Deogratius Nalimi Kisandu
Niliyekuwa Mwana Chama wa CCM wa Mpito.
29 Januari 2017.

MWANZA, Tanzania.
I have been following up this guy posts for quite some time now.
The guy is seriously mentally disturbed.... He shows features consistent with a mental illness remarkably and persistently.
-delusions
-flight of ideas
-thought broadcasting
-delusions of grandiosity
Kama kuna ndugu zake/watu wake wa karibu/rafiki zake humu ndaniz fanyeni hima muongee na huyu mtu na hata kumkutanisha na mwanasaikolojia au mtaalamu wa afya ya akili before its too late.
This is serious.
 
Umefanya uamuzi wa sahihi japokuwa umechelewa Hongera kwa kutoka utumwani.
Kuna mambo mengi sana maovu na ya kinyama yaliyofanywa juu yangu na CCM na viongozi wake kwa miaka mingi sasa. Kwakuwa wao kama chama wameshapanga tangu zamani kuwa nikitaka kuondoka CCM watajifanya kama walikuwa hawajui maovu na unyama uliokuwa unaendelea. Hivyo Mimi sio mtoto mdogo najitambua na ninajua nafanya nini.

CCM kila mtu anatumia nafasi yake kudhalilisha walio chini. Huwezi amini Balozi anauwezo wa kumdhalilisha Mtanzania mwenzie kisa anategemea nguvu ya DC au RC au agizo la Waziri Fulani.
 
Na anasema anafundisha, mtu mwenye mawazo ya hivi hatuwezi kumuacha karibu na jumuiya ya wanafunzi kuna siku atakuja na dumu la petroli na kuwatia kibiriti.

Mnaohusika acheni uzembe kamateni huyu mtu akapokee matibabu kwa lazima.
This guy us mentally disturbed for sure. Kama unamfahamu jamaa/rafiki yake waambie wafanye hima huyu mtu apate tiba. Majuto ni mjukuu. Castr
 
Huu upuuzi wameshaanza kufanya Arusha.
Nachelea kusema vijana wengi kutoka upinzani watabambikwa sana kesi ili wapoteze sifa ya kugombea 2020, na kuna ma DC na Ma RC wanataka majimbo 2020 hivyo wanatumia fursa hiyo ya udhalilishaji wa kubambika kesi ili wenzao wapoteze sifa 2020 na wao wapate kugombea majimbo hayo.
 
Hii ni post genuine kutoka kwa really person au ni utani tuu? Maana naona comments za ziaka kwenye post yake (if any) kama ni joke tuambiwe na kama ni genuine ajibiwe in line with hoja alizotoa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom