Waraka: Kanisa Katoliki laandaa waumini uchaguzi 2010

Status
Not open for further replies.
Huyu anayejiita Mzee wa Upako simfahamu vizuri hivyo siwezi kuchangia lolote kuhusu upeo wake, ingawa 'Mchukia Fisadi' amedokeza kwamba tatizo lake kubwa ni kwamba hana elimu. Tutamsamehe kwa hilo. Lakini Makwaia wa Kuhenga namfahamu fika! Huyu ni mwandishi wa habari wa siku nyingi. Ila ana chuki sana na Kanisa Katoliki. Sijui ni kwa nini! Ila namuonya iwapo ataendeleza chuki hiyo nitashusha tuhuma zake nzito kuhusu mwenendo wake unaotia shaka.
 
......Aliendelea kusisitiza kuwa; "Kinachonitisha ni kuona baadhi ya viongozi wanag'ang'ania watu waishi kwenye giza, najiuliza hawa ni viongozi wa aina gani? Hii siyo alama ya demokrasia, bali ndani yake kuna chembechembe za udikteta."

Padre Mapunda alisema wakati umefika sasa wa viongozi, kuongozwa na elimu na siyo uzoefu. "Watu wanafanyakazi kwa mazoea ndiyo maana hatuendelei!" alilalamika Padre Mapunda....

Naona hii ndio inawatisha hasa wana ccm, namnukuu mkubwa mmoja huko busanda "..kwanza wananchi wenyewe hawana umeme, hizo TV watazionea wapi, ... hawana hata hela,... hayo magazeti watatunua na nini?......, hata hivyo wengi hawajui kusoma" at the end tutaendelea kupata ushindi, .....kwani pia tuna mizizi na kukubalika zaidi vijijini...

Kuumbe ndio maana waraka unapingwa na serikali kwa kuwa utafika hadi vijijini kuwaelimisha hao waliokuwa marginalised haki zao!
 
Mama Joe tatizo hapa ni huyo mzee wa Upako umesikia hapo juu yaani ana chuki zake na Wakatoriki nae aandae wa kwake.
Basi ndugu wanaomfahamu naona wanasema hana elimu, pia sijui kwanini vyombo vya habari vinamtumia sana, mhh chuki haijengi!
 
Mimi naungana na wewe tatizo lake Mzee wa Upako ni elimu ndogo na kwa sababu hiyo upeo wake wa kuchambua mambo ni mdogo pia,asamehewe bure kwa kua hajui asemalo.

Wenye 'upeo mdogo' ndio wanaomfaa Makwaia wa Kuhenga kwa sababu anaweza kuwa-manipulate atakavyo. Keshampata victim wake, Mzee wa Upako, ambaye nimekuwa nikimuona mara nyingi kwenye vipindi vyake. A better match for Makwaia is Dr. Ndodi!!
 
Basi ndugu wanaomfahamu naona wanasema hana elimu, pia sijui kwanini vyombo vya habari vinamtumia sana, mhh chuki haijengi!

Ni mikakati yake ya kujaza kanisa si unajua anavuna kondoo kwa kutoa mipako maswala ya kanisa bana ndo maana mm nipo kando kabisa yanaumiza vichwa huyu anasema hiki yule kile mwisho wa yote viongozi wanapandikiza chuki kwa waumini na kujiona wao ni bora kuliko wengine.
 
Makwaia wa Kuhenga, ..... kama angeunga mkono huo waraka isingekuwa mada. Suala ukipinga Waraka ndio inakuwa mada. Spika na Lipumba wameunga mkono, hapo wote furaha, Kingunge na walioutolea tahadhari wanaonekana wabaya.

Lakini kama moderator unatakiwa kuwa nyutro. Ndivyo hata sheria zote zilivyo, iwe kwa mahakimu, marefarii na wengine wote wanaogonganisha makundi mawili tofauti..., au wewe ungekuwa moderata ungesimama upande upi?
 
Kipindi cha Makwaia jana usiku nilikiona. Kilikuwa ni marudio. Mamabo machache niyaseme bila kurudia yaliyokwishasemwa:
-Shehe Mattaka na mwenzake walifanya vizuri na wako informed na somo husika.
-Shehe Mattaka anahitaji muda wa kutosha kueleza dhana yake yake ya U-sekula, lakini
Makwaia hakumpa nafasi ya kutosha.
-Ajiitaye Mzee wa Upako ni disaster. Unashindwa kuelewa alikwenda pale kufanya nini.
Tetesi ni kuwa alienda pale ili kutimiza masharti ya mwenye TV ili apate free airtime
kurusha mahubiri yake kila jumatano usiku. Hii ilijitokeza pia wakati wa sakata la
misamaha, pale alipoweka kipindi maalum na huyu Lusekelo akawatukana maaskofu.

Hii yaweza pia kuwa issue kwa Makwaia, kuwa analazimika kusimamia anachosimamia ili kupata discount ya kipindi chake cha je Tutafika? Msimamo wake uliomo katika kitabu cha CCM na Hatima ya Tanzania ni tofauti na vipindi vyake anavyoendesha hivi sasa huko Zanzibar na kila J5 usiku.

Ukiishi sana utaona mengi. Tuliomjua Makwaia tangu ujana, tunashangaa.
 
Lakini kama moderator unatakiwa kuwa nyutro. Ndivyo hata sheria zote zilivyo, iwe kwa mahakimu, marefarii na wengine wote wanaogonganisha makundi mawili tofauti..., au wewe ungekuwa moderata ungesimama upande upi?

Moderator angeegemea upande wa kushoto (kwa waraka) isingekuwa tatizo, tatizo kaegemea kwa mujibu wa muanzisha mada na wengineo upande wa kulia. Angekuwa Neutral, ingeangaliwa pia wachangiaji wameegemea wapi?. Kama ni kuunga mkono Waraka hapo kila mtu hapa ngemuona Makwaia ni mtu safi sana, ila ukipinga Waraka basi hufai.
 
Naona hii ndio inawatisha hasa wana ccm, namnukuu mkubwa mmoja huko busanda "..kwanza wananchi wenyewe hawana umeme, hizo TV watazionea wapi, ... hawana hata hela,... hayo magazeti watatunua na nini?......, hata hivyo wengi hawajui kusoma" at the end tutaendelea kupata ushindi, .....kwani pia tuna mizizi na kukubalika zaidi vijijini...

Kuumbe ndio maana waraka unapingwa na serikali kwa kuwa utafika hadi vijijini kuwaelimisha hao waliokuwa marginalised haki zao!

..umenifuraisha sana...kwa hiyo..ujinga wetu na umaskini wetu ndio uhakika wa ccm kuendelea kushinda.....elimu ya uraia ni mwanga utakaofukuza ..giza [watawala wabaya[sio ccm wote wabaya]]
 
Kwa maoni yangu binafsi, napenda waraka huu, naufagilia sana, mimi sio mkatoliki, lakini kwa hili nawaheshimu sana, na ninawasapoti. wengi hapa pamoja na kikwete mwenyewe tumesoma shule zilizojengwa na wakatoliki, hospitali tumezaliwa etc. hawa jamaa wana mchango mkubwa sana. ninawapongeza kwanza kwasababu hakika wana network moja kali sana, kuanzia kwa pengo mwenyewe hadi kwenye familia kwenye vigango vyao, kuna vigango vingi tu hapa bongo vingine vimenunua hadi mabasi, yaani wanakusanyika nyumba kwa nyumba ktk wiki asubuhi kabla ya kwenda kazini, na ikitokea msiba au arusi, hakika huwezi kujua hela wametoa wapi, wanachangiana kiasi kwamba mhusika hagarimii kabisa. kitu hiki kimefanya wao kuwa na network kubwa sana sana. na waraka huu karibia kila mtu kwa sasa huku mijini, hadi kwenye vigango wanaufahamu na wanaujadili na wamefundishwa. jinsi unavyozidi kujadiliwa, they feel as if they are attacked, au kwamba watu wana attack dhehebu lao hivyo kuutafuta na kusoma kuona what is happening. kitu hiki ni kizuri kwasababu kinawafanya wausomi wakatoliki karibia wote.

mimi sio mkatoliki,ila nawaheshimu. kwa ufupi, wakristo wachache tu, nao ni wale ambao hawana uelewa mzuri, wameukataa na kuuponda huu waraka. kwanza sijaona hata mmoja isipokuwa mchungaji mmoja tu, naye hawakilishi waumini wake wote b'se nijuavyo kanisani huwa tunaenda kusali tu, si kila anachosema mchungaji tunafuata hata kama ameteleza, yeye nibinadamu pia.

Nimependa Waluthelani kupitia malasusa kuufagilia waraka. nimependa wapentecost kuufagilia, nimependa cct kuufagilia, nimependa angrican kuufagilia, madhehebu yoote ya kikristo yameufagilia, tofauti na kipindi cha nyuma. hapo nyuma tulizoea kutokuwa na umoja, wakatoliki wamekuwa wakiwa attacked sana hata pale wanapofanya mambo mema, lakini lilipotokea jambo linalohusu maslahi ya taifa, wakristo woote tumeungana bila kujali mlokole wala mwanauamusho au mwanakigango n.k. hii ni kitu kizuri. yoote hii imetokea kwasababu ya fikra za mahakama ya kadhi na oic. Mungu ibariki Tanzania. may God send mahakama ya kadhi na oic to hell. amin.
 
Jamaniee, ninatafuta uhakika wa Breaking nuz hapa, ndio nitatoa taarifa yoote kama ilivyo. ila kwa kifupi, inasemekana sio muda wakatoliki sio muda wanaweza wakadai warudishiwe mashule yao yoote yaliyochukuliwa na selikali ili wayafanye seminari kama kawaida, pia na mahospitali yao yote. Kuna mtu ameongea tu hapa, ila nitatoa full story nikikomfemu soon. sijui kama patatosha.
 
Last edited by a moderator:
Mara kadhaa nimewahi kumsikia Mzee wa Upako katika mahubiri yake akikandia makanisa mengine. Kumbe ni elimu inagomba. Kafika darasa la ngapi?
 
Jamaniee, ninatafuta uhakika wa Breaking nuz hapa, ndio nitatoa taarifa yoote kama ilivyo. ila kwa kifupi, inasemekana sio muda wakatoliki sio muda wanaweza wakadai warudishiwe mashule yao yoote yaliyochukuliwa na selikali ili wayafanye seminari kama kawaida, pia na mahospitali yao yote. Kuna mtu ameongea tu hapa, ila nitatoa full story nikikomfemu soon. sijui kama patatosha.


Sasa kwa nini usipate uhakika kwanza ndo uilete hapa, tena unaifanya kuwa breaking news while it is not yet news?

Mods pelekeni kule kwen tetesi please
 
Una uhakika mzee, mbona ingekuwa hivyo mimi ningefurahi, kwasababu pindi shule zile zilipokuwa chini ya kanisa zilikuwa zinafaulisha sana, lakini selikali imezipumbaza tu. wakatolika wako very serious katika kila kitu wanachofanya, iwe kwenye shule, hospitali nk. Pia, kama waislam wanataka mahakama ya kadhi, basi wakatoliki pia wachukue shule zao zote waweke seminari, walutherani pia chukueni mashule yenu yote na vyuo wekeni seminari, mahospitali yoote ya kidini kama lile la mwanza wekeni misalaba hadi wodini na vyooni, kila sehemu misalaba. ili kieleweke.

ila naogopa, kwasababu ikiwa hivyo, wahindi nao watadai magorofa yao yoote yaliyochukuliwa kule kariakoo.hahaha.

Jamani mnaona haya mambo ya dini dini yanavyoanza kuligawa taifa? can't you people see it? kuwa tayari wakristo na waislam waliokuwa wanaishi kwa amani safi sasa wameanza kunyosheana vidole, huko mashuleni na vyuoni sasa kutakuwa na dini mbili zisizokaa pamoja, mahospitalini na makazini kutakuwa na ubaguzi nk. HIVI KWANINI JAMANI? KWANINI MAMBO YA DINI YASIPELEKWETU KANISANI NA MISIKITINI halafu watuachie selikali ifanye kazi yake kwa uhuru wake vizuri tu? haya mambo yanatupeleka wap watz? hivi tutafika kweli? E MUNGU TUEPUSHE NA MGAWANYIKO HUU.

BY THE WAY, CCM UWE MACHO, MWAKANI UNANG'OKA. Mungu akubariki mtoa taarifa. safi sana. tuletee ukweli ukishaupata mzee.
 
Sikupata fursa ya kupitia humu na kuona kuna hii mada ambayo nami kwa wakati wangu nikaanzisha mada kama hiyo huko jukwaa la hoja. Wakati fulani mawazo hugongana. Mods mnaeza kuhamisha mada yangu kuiingiza humu
 
Una uhakika mzee, mbona ingekuwa hivyo mimi ningefurahi, kwasababu pindi shule zile zilipokuwa chini ya kanisa zilikuwa zinafaulisha sana, lakini selikali imezipumbaza tu. wakatolika wako very serious katika kila kitu wanachofanya, iwe kwenye shule, hospitali nk. Pia, kama waislam wanataka mahakama ya kadhi, basi wakatoliki pia wachukue shule zao zote waweke seminari, walutherani pia chukueni mashule yenu yote na vyuo wekeni seminari, mahospitali yoote ya kidini kama lile la mwanza wekeni misalaba hadi wodini na vyooni, kila sehemu misalaba. ili kieleweke.

ila naogopa, kwasababu ikiwa hivyo, wahindi nao watadai magorofa yao yoote yaliyochukuliwa kule kariakoo.hahaha.

Jamani mnaona haya mambo ya dini dini yanavyoanza kuligawa taifa? can't you people see it? kuwa tayari wakristo na waislam waliokuwa wanaishi kwa amani safi sasa wameanza kunyosheana vidole, huko mashuleni na vyuoni sasa kutakuwa na dini mbili zisizokaa pamoja, mahospitalini na makazini kutakuwa na ubaguzi nk. HIVI KWANINI JAMANI? KWANINI MAMBO YA DINI YASIPELEKWETU KANISANI NA MISIKITINI halafu watuachie selikali ifanye kazi yake kwa uhuru wake vizuri tu? haya mambo yanatupeleka wap watz? hivi tutafika kweli? E MUNGU TUEPUSHE NA MGAWANYIKO HUU.

BY THE WAY, CCM UWE MACHO, MWAKANI UNANG'OKA. Mungu akubariki mtoa taarifa. safi sana. tuletee ukweli ukishaupata mzee.

teh teh teh hizi ni nyepesi nyepesi tu
 
asee kusema ukweli, napenda ije, kusudi waislam wajue kuwa, hapa tz hatutakiwi kugawanyika wala kuingiza mambo ya dini kwenye selikali. selikali yetu ni secular, haina dini. SITAKI KODI YANGU MIMI NA WATOTO WANGU IJE ITUMIKE KULIPIA KITU KINACHOITWA KADHI, yaani sitaki hela yangu iguse huko kabisa, kwasababu mimi siiamini hiyo dini. hatutaki, kwanza hatutaki aisee.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom