Wapinzani watatu kuwa pamoja ni kosa ndani ya Mkoa wa Morogoro

SONGOKA

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
1,843
1,841
Wakati CCM ikisisitiza kuandaa mkutano wao wa kisiasa tarehe 23 July huko Dodoma, Mkuu wa mkoa wa Morogoro ambaye ni kada wa CCM amesema ni marufuku kufanyika kikao chochote cha kisiasa ndani ya mkoa wake na wapinzani hata wakiwa watatu ndani ya nyumba, atatumia polisi kuwatoa huko ndani na kuwashughulikia.

Kwa kauli hii, wale makada wa CHADEMA wenzangu ambao ndani ya nyumba mke, mme na watoto ni wanachama wa CHADEMA jiandaeni kuvamiwa, kwani mmezidi watatu na mko katika jengo moja, hivyo ni kikao cha kisiasa.

Huu ni udikteta wa kiwango cha rami? Au demokrasia ya kiwango cha aina gani?

Chanzo: Redio one - Nipashe
 
SHERIA INARUHUSU WATU WATATU AU ZAIDI WAKIKUSANYIKA NA POLISI WAKAHISI WANATAKA KUVUNJA AMANI BASI WATAAMULIWA KUTAWANYIKA.

RC anaongea sheria iliyopo tu ...sio udikteta
 
M
SHERIA INARUHUSU WATU WATATU AU ZAIDI WAKIKUSANYIKA NA POLISI WAKAHISI WANATAKA KUVUNJA AMANI BASI WATAAMULIWA KUTAWANYIKA.

RC anaongea sheria iliyopo tu ...sio udikteta
Mbona haujataja vifungu vya vilivyo ndani ya katiba mkuu
 
SHERIA INARUHUSU WATU WATATU AU ZAIDI WAKIKUSANYIKA NA POLISI WAKAHISI WANATAKA KUVUNJA AMANI BASI WATAAMULIWA KUTAWANYIKA.

RC anaongea sheria iliyopo tu ...sio udikteta

Tupe vifungu vya sheria mkuu.
 
Back
Top Bottom