Wapinzani waendelee kuhakikisha inapatikana Tume Mpya ya Uchaguzi kabla ya 2022 au 2023

Shocker

JF-Expert Member
Sep 15, 2012
1,930
3,803
Waacheni CCM waseme usiku watalala huku upinzani hakuna kulala; tunafahamu Samia hagombei, hili halina utata anawaachia Watanganyika zigo lao.

Timu zilizopo CCM ni nyingi na kila moja ina mtu wake agombee urais, mjue ndani ya CCM kuna mito kama iliyopo ndani ya bahari na mingine ni mikondo ya volcano kama iliyopo chini ya ardhi.

Wapinzani waendelee kujipanga na wakati ni huu kuhakikisha inapatikana tume mpya ya Uchaguzi hili ni lazima kablaya 2022 au 2023, ni muhimu kuliko jambo lingine lolote lile na pia muendeleze kujikita ndani ya vyombo vya usalama kimikakati na ndani ya vyombo vya serikali kama CCM wanavyojipenyeza ndani ya Vyama vya Upinzani.

CCM wamekwisha, wote waliobakia ni half knowledge.
 
Back
Top Bottom