Wapinzani waanze kampeni za 2015 sasa

Kiranga

Platinum Member
Jan 29, 2009
71,261
105,421
Nimetoka kusoma thread ya Regia Mtema anasema "amerudi" kutoka Kilombero, apparently Kilombero si base yake ni sehemu ya kwenda wakati wa uchaguzi, na uchaguzi ukiisha ni muda wa "kurudi mjini" kutoka Kilombero.

Najua nimekuwa critical kwa wapinzani huko nyuma, particularly Regia. Lakini nafikiri ni muhimu watu wawe critical ili wapinzani wajue wanakosea wapi na wajirekebishe vipi.

Moja ya vitu vilivyotajwa katika uchaguzi huu uliopita ni kwamba wapinzani wamekuwa na "vyama vya uchaguzi" vinavyopata muamko wakati wa karibu na uchaguzi, na uchaguzi ukiisha vinafifia uhai.

Ningependa kuona wapinzani, hususan CHADEMA na CUF vyama vilivyoonyesha muamko wa kisiasa na kiasi kikubwa cha uhamasishaji wa wananchi, vianze kufanya kampeni za chinichini za 2015 kuanzia sasa. Mwisho wa uchaguzi mmoja ndiyo mwanzo wa uchaguzi mwingine.

Vyama vianze kuwajua watu wenye potential ya kusimamishwa kushindania ubunge mapema, vianze kuwaweka katika nafasi za majimboni huko watakapoweza kushirikiana na wananchi moja kwa moja na kujulikana, pamoja na kuimarisha vyama hivi. Ni muhimu kuanza hizi shughuli mapema na kutongojea mpaka mwaka wa uchaguzi ambapo mambo mengi yanakuwa yanatokea pamoja.

Nisingependa kuona uchaguzi wa 2015 unafika halafu wanaupinzani hawajajifunza makosa ya 2010, wanaanza kuokoteza wagombea wa ajabu ajabu dakika za mwisho, na hawana mkakati madhubuti wa kuchukua majimbo haya.

Nawakilisha hili na ningependa kusikia strategist wa upinzani wanasema nini.
 
Hilo si wazo baya lakini miaka mitano kwenye siasa is more than a lifetime! Mimi ningependa kuona hawa young guns wa chadema na wengineo walio kambi ya upinzani wana spearhead mabadiliko ya katiba na sheria ya (za) uchaguzi mkuu. It was painful to watch the electoral commission chairman announce the results by reading on a piece of paper knowing damn well he is beholden to the man who appointed him. We need clear separation of powers. Its not a good look when one person has the mandate to appoint just about every high ranking official without even parliamentary vetting and approval.
 
Hilo si wazo baya lakini miaka mitano kwenye siasa is more than a lifetime! Mimi ningependa kuona hawa young guns wa chadema na wengineo walio kambi ya upinzani wana spearhead mabadiliko ya katiba na sheria ya (za) uchaguzi mkuu. It was painful to watch the electoral commission chairman announce the results by reading on a piece of paper knowing damn well he is beholden to the man who appointed him. We need clear separation of powers. Its not a good look when one person has the mandate to appoint just about every high ranking official without even parliamentary vetting and approval.

Hear you, hear you son. Kuna watu fulani fulani tu wanaoweza ku think ahead that far in TZ.

Part ya mkakati huo wa 2015 ni mabadiliko ya katiba, huu ndio mzizi wa fitina kama wanavyosema waswahili.

Kwa hiyo ninavyosema kampeni za 2015 zianze sasa maana yake mpaka kampeni za hayo mabadiliko ya katiba zianze sasa.
 
Kiranga na NN nakubaliana na nyinyi kwa asilimia 101. Mimi binafsi nafikiria sana jinsi ninavyoweza kubadilisha hali ya uchaguzi ujao kuanzia sasa. Bila shaka baada ya muda mfupi ujao Chadema itatakiwa kuwa na mikakati mikubwa na itakayoleta ushindi mkubwa zaidi 2015.
Bila shaka na kudai katiba na tume huru kama moja ya mikakati. Na kwa haya hatutayaomba bali tutayadai kwa hoja ya nguvu.
 
Jitihada za kuanzisha, kuendeleza na kupanuwa matawi, mashina na ofisi za wilaya inabidi zinshike hatamu sasa. Na pia itapendeza kuona jitihada za dhati za kukusanya fedha zinaendelea. Chama ni lazima kijijenge na hii ndio siku zote imekuwa ni dira ya Chadema. Consolidation ya support katika mikoa ambayo Chama kilikubalika mwaka huu ni lazima ifanyike na pia mikakati ya kujipenyeza kwenye mikoa kama vile ya Morogoro, Rukwa na Njoluma ni muhimu pia.
 
Back
Top Bottom