Wapinzani wa Bongo wajifunze nini toka siasa ya Kenya?

Kwa hiyo kimsingi mkuu unakubaliana na mimi kuwasio lazima mawaziri wa rais wachaguliwe na rais, inawezekana na rais akachaguliwa na mawaziri wake wakapigwa chini bila yakuiba kura, hiyo ndio iliyokuwa hoja yangu ya msingi, je tunakuabaliana kwenye hilo?

Sidhani kama hiyo ndiyo ilikuwa hoja yako ya msingi katika mfano wa clinton maana hiyo ilitokea katika chaguzi mbili tofauti,

uchaguzi wa kenya umeonyesha kuwa serikali ya kibaki imekataliwa kila sehemu isipokuwa centra ambako pia kuna uvumi kuna utata. the guy aligundua kuwa hawezi kuiba kura zote za urais na za ubunge kama wanavyofanya ccm kwa sababu kura za wabunge ni personal kwa wabunge kuliko za urais.

kuna uwezekano huo kuwa rais akachaguliwa ila wabunge wakapigwa chini lakini hilo halikuwa katika kesi hii kulingana na taarifa za television nyingi za kenya ukiacha kbc.
 
Quote:-

"ccm yaleo ni kama ya idi amini."

Whaaat? na wananchi wanaoichagua CCM ni kama kina nani mkuu?

Umesahau kuwa hata idi amini alikuwa na wafuasi wake kibao kama vile mugabe alivyo na wafuasi huko zimbabwe?

Nakuhakikishia kuwa Tanzania kungekuwa na independent television kama KTN ya kenya ambayo ilipiga picha hadi kambi ya jeshi na polisi kuonyesha polisi na wanajeshi wakipakiwa kwenye mabasi wakiwa na nguvu za raia (plain cloth) ili wakaibe uchaguzi basi story ingekuwa tofauti hapa.
 
Mwafrika,
maneno yako kweli lakini hivi kweli kulikuwepo zero possibility ya rais kushinda kura wakati mawaziri wake wote wameshindwa?...
Binafsi ninaamini possibiity ipo na hata nikitazama leo TZ kuna uwezekana tukawaweka nje mawaziri wengi wa JK kama sio wote na JK akapita tena. Kwa sababu kama Kibaki ameonyesha kuwa na matatizo makubwa ktk kupigana na mafisadi wa Kenya na kutopata ushirikiano mkubwa toka ktk viongozi wenzake, nadhani wapo watu Kenya wanao amini kuwa Kibaki ni safi na akipata mawaziri wengine nje ya hao Mafisadi anaweza kuwa mtawala mzuri... yaani kundi kubwa bado wana imani naye. JK pia akichukua baadhi ya hatua za maneno tu kuonyesha anapiga vita mafisadi isipokuwa wamemzidi nguvu tunaweza kumchagua tena...
Kisha tukumbuke pia zile kanda zote kumi zilizokuwa zimebaki ni kanda ambazo Wakenya wote wanajua kuwa Kibaki ni Popular zaidi ya Raila.
Kumbukeni pia, uchaguzi wa Florida ndio ulotoa ushindi Marekani uchaguzi wa 2000 pamoja na kwamba wenzetu hawakumpa Urais Al Gore ambaye alimshinda Bush ktk Popular vote!...
nadhani kitu cha kujifunza ni mfumo huu wa Popular vote unavyotumika na athari zake, yawezekana ni mzuri zaidi lakini inapofikia swala kama hili la Kenya inatisha zaidi usalama wa nchi kuliko mfumo mwingine.
 
Mkuu hoja yangu ya msingi nilikuwa ninamjbu Mtanzania, kwamba inawezekana, mawaziri wakapigwa chini na rais wao akachaguliwa, ndipo wewe ukaingilia kati na kujaribu kuibadili, lakini haibadiliki,

Clinton, aliposhinda mara ya kwanza 1992 hakukuwa na uchaguzi rasmi wa wabunge, isipokuwa uchaguzi huo ulikuja 1994 chini ya Gingrich na ile Contract yake with Americans, Clinton in two years kwenye power alikuwa tayari ameshaji-establish kama a good president, lakini wananchi wakaamua kuwa anahitaji wabunge wa upinzani, na hta term ya pili pia walimkatalia na haikuibiwa kura yoyote kwenye kuchaguliwa kwake hiyo ndiyo point yangu ya msingi katika kumjibu Mtanzania,

kwamba kuna wabunge wengi wa CCM ambao Kikwete aliambiwa kuwa hawafai na hata kuzomewa, lakini wakampa Kikwete ambaye ni CCM kura zao anyways, kuhusu uchaguzi wa Kenya ni too early kuanza ku-speculate, ingawa kwa haraka haraka hesabu zao za sensa zinaonyesha kuwa wa-Kikuyu, wengi kuliko makabila mengine yote na kwamba wana tabia ya kwenda kupiga kura kwa wingi sana kuliko makabila yote, kwa hiyo binafsi nitasubiri kupata more facts kabla ya kutoa hukumu, maana kwenye uchaguzi kuna mengi sana!

Isipokuwa lingine la msingi kwangu ni kwamba kwenye huu uchaguzi wa Kenya, unaondeshwa kikabila zaidi kuliko demokrasia, kwa maoni yangu Tanzania hatuna cha kujifunza.
 
"Umesahau kuwa hata idi amini alikuwa na wafuasi wake kibao kama vile mugabe alivyo na wafuasi huko zimbabwe?"

Okay, then what is a problem mkuu, maana CCM ni sawa na Idd Amini, meaning kwamba na wananchi wa Tanzania wanaoichagua ni sawa na Idd Amin, maana haiwezekani CCM ikawa kama Idd Amin lakini wananchi wanaoichagua wakawa tofauti na Idd Amin? Does that make a sense to you mkuu kuwa sisi wananchi wa Tanzania akili zetu ni kama Idd Amin?
 
Mwafrika,
maneno yako kweli lakini hivi kweli kulikuwepo zero possibility ya rais kushinda kura wakati mawaziri wake wote wameshindwa?...

Mkandara,

ni kweli kabisa kuna uwezekano huo na mimi sijakataa hilo ila katika kesi hii ya kenya na report zote za tv na magazeti (kwa siku tatu mfululizo nilikuwa nafuatilia feed zote za tv za kenya kuanzia kbc, ktn, national, nk) na ilionyesha kabisa jinsi kibaki alivyokuwa anashindwa lakini nairobi wakawa wanatangaza kura tofauti. wasimamizi wa vituo wanasaini namba fulani lakini nairobi wanatangaza namba tofauti.

inawezekana kabisa lakini kwa kenya this time halikutokea hilo.


Binafsi ninaamini possibiity ipo na hata nikitazama leo TZ kuna uwezekana tukawaweka nje mawaziri wengi wa JK kama sio wote na JK akapita tena.

Mkandara, hata mimi naomba hili litokee lakini baada ya hili la kenya na nikiona mizengwe ya serikali ya tanzania basi sitegemei kabisa kama litakuja tokea. Wewe mwenyewe umesoma hapa baadhi ya watu wakimsifia Malecela kwa kitendo chake cha kupunguza wabunge wa upinzani bungeni. Yaani kuna watu wanaona kuwa kupunguza upinzani bungeni ni kitendo cha kishujaa sasa unategemea kuna lolote Tanzania la kupiga chini mawaziri lakini raisi akapita?

Kwa sababu kama Kibaki ameonyesha kuwa na matatizo makubwa ktk kupigana na mafisadi wa Kenya na kutopata ushirikiano mkubwa toka ktk viongozi wenzake, nadhani wapo watu Kenya wanao amini kuwa Kibaki ni safi na akipata mawaziri wengine nje ya hao Mafisadi anaweza kuwa mtawala mzuri... yaani kundi kubwa bado wana imani naye.

Just wait uone, kuna watu kina moi walijua kuwa raila akiingia basi watalazimishwa kurudisha pesa walizoiba ndio maana moi na kibaki wametumia vyombo vya usalama kuiba kura (kumbuka kuwa wana usalama wengi kenya ni kutoka kabila la kalenjin ambao ni marafiki wakubwa wa moi). kikabi ameshindishwa na mafisadi hivyo usitegemee hili kutokea mkuu.

JK pia akichukua baadhi ya hatua za maneno tu kuonyesha anapiga vita mafisadi isipokuwa wamemzidi nguvu tunaweza kumchagua tena...

Kuna wakati hata mimi nilitegemea sana Kikwete angefanya haya ila kila siku nikisoma connection za kikwete na mafisadi hatari duniani sioni kabisa hili likifanyika.

Kisha tukumbuke pia zile kanda zote kumi zilizokuwa zimebaki ni kanda ambazo Wakenya wote wanajua kuwa Kibaki ni Popular zaidi ya Raila.

No, kuna maeneo kama kajiado north ambayo ni ya wakalenjin na mengine ambayo kibaki sio popular kabisa lakini matokeo yaliyokuwa yakisomwa (kajiado north) kabla wapinzani kuyasimamisha pale kicc yalionesha kuwa kibaki pia ameshinda

Kumbukeni pia, uchaguzi wa Florida ndio ulotoa ushindi Marekani uchaguzi wa 2000 pamoja na kwamba wenzetu hawakumpa Urais Al Gore ambaye alimshinda Bush ktk Popular vote!...
nadhani kitu cha kujifunza ni mfumo huu wa Popular vote unavyotumika na athari zake, yawezekana ni mzuri zaidi lakini inapofikia swala kama hili la Kenya inatisha zaidi usalama wa nchi kuliko mfumo mwingine.

Hii ni ajenda nyingine kabisa na nitaiongelea siku nyingine mkuu
 
Mnajua tatizo ni kuwa kutokana na Kanu mwanzoni kushindwa, CCM walijifunza mengi, sasa tena huyu Kibaki kushindwa na kufanya mazingaombwe yake wamejifunza tena. Kwa kifupi wapinzani na wana ccm wenye uchungu na Tz yetu (kama akina ES) tuna shida zaidi kwani hawa mafisadi wetu kila siku wanajifunza kitu kipya. Wiki hizi mbili tu wamejifunza mengi kutoka ANC, Pakistani na sasa Kenya.
Still, naombea siku moja wafanye makosa wawape akina Kabwe, JJ Mnyika, Field Mrshall ES nk. na ndiyo watajua wanamapiduzi wa kweli wakoje!
 
Mkuu hoja yangu ya msingi nilikuwa ninamjbu Mtanzania, kwamba inawezekana, mawaziri wakapigwa chini na rais wao akachaguliwa, ndipo wewe ukaingilia kati na kujaribu kuibadili, lakini haibadiliki,

Sioni nilichobadili chochote zaidi ya kuchambua kile unachosema kama yafuatayo hapa chini.

Clinton, aliposhinda mara ya kwanza 1992 hakukuwa na uchaguzi rasmi wa wabunge, isipokuwa uchaguzi huo ulikuja 1994 chini ya Gingrich na ile Contract yake with Americans, Clinton in two years kwenye power alikuwa tayari ameshaji-establish kama a good president, lakini wananchi wakaamua kuwa anahitaji wabunge wa upinzani, na hta term ya pili pia walimkatalia na haikuibiwa kura yoyote kwenye kuchaguliwa kwake hiyo ndiyo point yangu ya msingi katika kumjibu Mtanzania,

Mkuu inabidi ucheki facts zako. Maneno yako niliyoweka kwenye bold sio kweli. Marekani kila baada ya miaka miwili kuna uchaguzi rasmi wa wabunge. Kulikuwa na uchaguzi 1992 na 1994.

kwamba kuna wabunge wengi wa CCM ambao Kikwete aliambiwa kuwa hawafai na hata kuzomewa, lakini wakampa Kikwete ambaye ni CCM kura zao anyways, kuhusu uchaguzi wa Kenya ni too early kuanza ku-speculate, ingawa kwa haraka haraka hesabu zao za sensa zinaonyesha kuwa wa-Kikuyu, wengi kuliko makabila mengine yote na kwamba wana tabia ya kwenda kupiga kura kwa wingi sana kuliko makabila yote, kwa hiyo binafsi nitasubiri kupata more facts kabla ya kutoa hukumu, maana kwenye uchaguzi kuna mengi sana!

Wabunge wa ccm hawakuzomewa kabla ya 2005 au kuna habari ulizonazo ambazo sijui. Baada ya zomeazomea ya mwaka 2007 bado hakuna uchaguzi wa wabunge na rais umefanyika kupima athari zake kwa rais.

Issue ya wakenya mkuu kasome pia fact uone kuwa kabila kubwa kenya ni kalenjin ambayo imevote overwhelmingly ODM. Mengine labda nikuache kwanza ufanye research yako.

Isipokuwa lingine la msingi kwangu ni kwamba kwenye huu uchaguzi wa Kenya, unaondeshwa kikabila zaidi kuliko demokrasia, kwa maoni yangu Tanzania hatuna cha kujifunza.

inawezekana hili ni kweli lakini Raila amepata asilimia 75 ya kura zake toka kwa wakenya ambao sio wajaluo.
 
Okay, then what is a problem mkuu, maana CCM ni sawa na Idd Amini, meaning kwamba na wananchi wa Tanzania wanaoichagua ni sawa na Idd Amin, maana haiwezekani CCM ikawa kama Idd Amin lakini wananchi wanaoichagua wakawa tofauti na Idd Amin? Does that make a sense to you mkuu kuwa sisi wananchi wa Tanzania akili zetu ni kama Idd Amin?

Hayo umeyasema wewe na hivyo yatetee uliyoyasema? ukipata sehemu yoyote nimesema kuwa wananchi wa Tanzania na akili zetu ni kama Idd Amin, basi yaweke hapa kisha nitajibu.

kwa sasa sisiemu inauza nchi na kukumbatia ufisadi kama vile idd amini na mafisadi wote wa kiafrika that is what i said na I stand by my statement. mtu kuwa na wafuasi au watu wanaokupigia kura haikufanyi wewe kuwa safi maana hata mugabe naye anapigiwa kura huko zimbabwe na anashinda kwa kishindo!
 
Mkuu Choveki,

Heshima mbele, ukweli ni kwamba hizi siasa za Afrika, zinatisha sana, tena ni mazingaombwe makubwa sana, nasikia sasa kesi ya Zuma, itaanza tena kuunguruma,

kuhusu Kenya, ukweli unaonyesha kuwa bado Moi ana the upperhand na siasa zao, the man is tooo rich na politically very influential, majuzi nilikuwa ninaangalia news za huko, Moi alikuwa ameenda kijiji kimoja na helikopta yake binafsi, na kuwapa mabasi mawili mapya kabisa hicho kijiji, yaani the whole atmosphere ilikuwa kama vile mkuu bado ni rais, kwa kweli ilinisikitisha sana,

Sasa again here we go, amesha-pull another stint, kuna wakati tulimsahngilia sana Kibaki kuwa ni mpinzani na mfano wa kuigwa, ndio maana nilisema huko nyuma kuwa Moi alimpa Kibaki kwa makusudi tu katika his political games, na sasa ndio inaonekana wazi zaidi kuwa alikuwa na nia gani, yaani Moi, alijua kuwa Kibaki ataishia kuwa weak, na again atasimama tena, nasikia mke wa Kibaki huwapiga sana makofi mawaziri na wasaidizi wa Kibaki, siku moja akajribu kuwatishia kuwakanyaga vibao wasaidizi wa Muungwana, kidogo wamuwashe an yeye vibao, ndipo aakambiwa na Membe kuwa bongo we do not play that!

Siasa za Afrika, ni aibu tupu!
 
.....


kuhusu Kenya, ukweli unaonyesha kuwa bado Moi ana the upperhand na siasa zao, the man is tooo rich na politically very influential, majuzi nilikuwa ninaangalia news za huko, Moi alikuwa ameenda kijiji kimoja na helikopta yake binafsi, na kuwapa mabasi mawili mapya kabisa hicho kijiji, yaani the whole atmosphere ilikuwa kama vile mkuu bado ni rais, kwa kweli ilinisikitisha sana,

Mkuu,

Ila ukumbuke kuwa watoto watatu wa moi ambao aliwapigia debe sana wamepigwa chini kwenye uchaguzi. Security system ya kenya ambao wengi wao waliwekwa na moi ndio wamesaidia wizi huu wa kura na TV za kenya zimeonyesha hili maana Raila alikuwa ameahidi kudai pesa zilizoibiwa zirudishwe.

Sasa again here we go, amesha-pull another stint, kuna wakati tulimsahngilia sana Kibaki kuwa ni mpinzani na mfano wa kuigwa, ndio maana nilisema huko nyuma kuwa Moi alimpa Kibaki kwa makusudi tu katika his political games, na sasa ndio inaonekana wazi zaidi kuwa alikuwa na nia gani, yaani Moi, alijua kuwa Kibaki ataishia kuwa weak, na again atasimama tena, nasikia mke wa Kibaki huwapiga sana makofi mawaziri na wasaidizi wa Kibaki, siku moja akajribu kuwatishia kuwakanyaga vibao wasaidizi wa Muungwana, kidogo wamuwashe an yeye vibao, ndipo aakambiwa na Membe kuwa bongo we do not play that!

Siasa za Afrika, ni aibu tupu!

Afrika inalaana toka kwa mungu na shetani na hapa nakubaliana nawe kabisaaaaa!
 
Mwafrika,
Nakusikia mkuu nakusikia isipokuwa gonjwa hili la Kutawaliwa halina dawa kabisa hata kama tulifikiria demokrasia na huu upuuzi wa vyama vingi unaweza saidia. yametokea kwetu miaka ya nyuma lakini ni wangapi kati yetu wanaamini CCM waliiba kura?.... sidhani na hata kama waliiba bado tutatafuta sababu nyingine kama Hivi isipokuwa CCM kuna viongozi huko je ya CCM?...
Kifupi hata kwa kura naamini kabisa kuwa ni Watanzania wachache wanaoamini CCM ilikwiba kura za wananchi. WHY?... hali hatuna ushaidi wa kutoiba ila tunadai ushahidi wa kuiba na bado ushahidi huo tunauwekea mashaka kwa sababu alosema sio Mtawala.
 
Mwafrika,
Nakusikia mkuu nakusikia isipokuwa gonjwa hili la Kutawaliwa halina dawa kabisa hata kama tulifikiria demokrasia na huu upuuzi wa vyama vingi unaweza saidia. yametokea kwetu miaka ya nyuma lakini ni wangapi kati yetu wanaamini CCM waliiba kura?.... sidhani na hata kama waliiba bado tutatafuta sababu nyingine kama Hivi isipokuwa CCM kuna viongozi huko je ya CCM?...
Kifupi hata kwa kura naamini kabisa kuwa ni Watanzania wachache wanaoamini CCM ilikwiba kura za wananchi. WHY?... hali hatuna ushaidi wa kutoiba ila tunadai ushahidi wa kuiba na bado ushahidi huo tunauwekea mashaka kwa sababu alosema sio Mtawala.

Nakubaliana nawe Mkandara ndio maana nasema kuwa kilichotokea kenya leo kinakatisha tamaa kabisa. Umeona report ya EU ikisema kuwa msimamizi wake alikuwepo kwenye kituo cha uchaguzi na kura zikatangazwa elfu 50 lakini walivyofika nairobi wakakuta hizo kura zimetangazwa elfu 70.

yaani jamaa wanaiba bila kujali kuwa wananchi mna kumbukumbu na mnaona kinachoendelea ila kwa vile wao wana jeshi na polisi na mahakama basi nyie ndio imetoka hviyo.
 
Nafikiri, anayetakiwa kujifunza hapa sio viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani peke yao, bali ni Watanzania wote kwa jumla yao.

Inapotokea neema nchini ni ya wote na linapotokea janga ni letu sote.

Wengi wetu, kwa makosa, tunadhani kazi ya kuikomboa nchi kutokana na wenye makucha marefu na makali, ni ya kundi la watu fulani, hilo si kweli.

Naamini, wananchi kwa jumla yetu tunawajibika katika kuleta mageuzi nchini mwetu. Viongozi wa vyama pamoja na wanachama wake, wana kazi ya kuwaimarishia wananchi uwanja (platform) wa kufanyia mageuzi katika nchi yao.

Mageuzi Tanzania, yataletwa na wananchi na sio na CCM, CHADEMA, CUF, UDP, TLP, DP au TADEA. Wananchi, tutakapoamka, tutatumia chombo kimoja au zaidi katika hivi na kujiletea mageuzi yenye manufaa kwetu.

Viongozi wetu watakapojua kuwa tunaweza kuwaajiri na kuwafukuza kazi, ndipo watakapotuheshimu na kututhamini. Kosa ni letu wananchi, sio kosa la vyama vya wapinzani/ushindani. Jukumu la kuisahihisha hii hali ni letu sote kwa jumla yetu.
 
Cha kujifunza ni tuachane na huu ujinga wa shirikisho la afrika mashariki haraka sana ! Kwa nini viongozi wetu hawaweki maslahi ya taifa mbele...mimi nilikuwa najua Kenya wana matatizo ya ukabila but not to this magnitude . Inapofika sehemu kwamba kigezo cha mtu kuchaguliwa ni rais ni kabila ...tuupinge huu muungano kwa nguvu zote kusudi kila nchi ipate muda wa kusolve her problems
 
Mkuu Rufiji,

Mimi binafsi nimeshitushwa na hiii theory, ambayo niliambiwa na kiongozi mmoja mzito sana kwamba katika siasa za Kenya, the bottom line ni M-Kikuyu, hawezi kubali kutawaliwa na Mjaluo,

Meaning kwamba hii kupiga kura na the rst of the story ilikuwa geresha tu, wao huko Kenya wanajua ukweli toka enzi za baba yake Odinga, sasa kama huuu ndio ukweli wenyewe sisi bongo tunafanya nao nini hawa wakabila?
 
Nafikiri, anayetakiwa kujifunza hapa sio viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani peke yao, bali ni Watanzania wote kwa jumla yao.

Inapotokea neema nchini ni ya wote na linapotokea janga ni letu sote.

Wengi wetu, kwa makosa, tunadhani kazi ya kuikomboa nchi kutokana na wenye makucha marefu na makali, ni ya kundi la watu fulani, hilo si kweli.

Naamini, wananchi kwa jumla yetu tunawajibika katika kuleta mageuzi nchini mwetu. Viongozi wa vyama pamoja na wanachama wake, wana kazi ya kuwaimarishia wananchi uwanja (platform) wa kufanyia mageuzi katika nchi yao.

Mageuzi Tanzania, yataletwa na wananchi na sio na CCM, CHADEMA, CUF, UDP, TLP, DP au TADEA. Wananchi, tutakapoamka, tutatumia chombo kimoja au zaidi katika hivi na kujiletea mageuzi yenye manufaa kwetu.

Viongozi wetu watakapojua kuwa tunaweza kuwaajiri na kuwafukuza kazi, ndipo watakapotuheshimu na kututhamini. Kosa ni letu wananchi, sio kosa la vyama vya wapinzani/ushindani. Jukumu la kuisahihisha hii hali ni letu sote kwa jumla yetu.
Very strong point mkuu, wala sitaki kuongeza neno zaidi ya kusema ahsante sana!
 
Mkuu Rufiji,

Meaning kwamba hii kupiga kura na the rst of the story ilikuwa geresha tu, wao huko Kenya wanajua ukweli toka enzi za baba yake Odinga, sasa kama huuu ndio ukweli wenyewe sisi bongo tunafanya nao nini hawa wakabila?


Kwa hiyo yaleyale ya Zanzibar na upemba na unguja wao au ya Salim na uhizbu, kwamba madamu watoka pemba weye hakuna urais au madamu uliwahi kuwa karibu na hizbu basi urais usahau!

Basi waafrika tuna kazi na inawezekana kweli tunalaana kama unavyosema na sijui hii laana tutaitoaje! Huwa nawashawishi sana jamaa zangu waliopo huku majuu wenye moyo wa siasa warudi nyumbani, nafikiri itabdi nipunguze ushawishi wangu maana kwa wale waliokaa huko miaka mingi wakirudi home wakiingia kwenye siasa wanaweza kupasuka nyongo kwa hasira!
 
mie mwenzenu mbona nilichojifunza hapo kenya as nikijibu swali lililoulizwa kwenye thread hii ni kuwa there is no way in africa u can prevent a president from winning for the second time...

so nashauri kila baada ya miaka mi5 tuwe na uchaguzi wa wabunge,madiwani etc ila wa rahisi iwe ni baada ya miaka kumi tuu tusipoteze mijihela mingi sana
 
mie mwenzenu mbona nilichojifunza hapo kenya as nikijibu swali lililoulizwa kwenye thread hii ni kuwa there is no way in africa u can prevent a president from winning for the second time...

so nashauri kila baada ya miaka mi5 tuwe na uchaguzi wa wabunge,madiwani etc ila wa rahisi iwe ni baada ya miaka kumi tuu tusipoteze mijihela mingi sana

Kweli inachekesha na kuchukiza!! Haya haya mambo yalitokea Zambia last year. Sema kule ni wachovu tu kama Bongo. Wakiona police wanaogopa. Si unajua siasa za Kaunda zilikuwa similar na za JKN, kuwatia watu woga. Sasa pamoja na mabadiliko bado hofu ya Kaunda ipo palepale.
 
Back
Top Bottom