Wapinzani tumejiandaa vipi kuiondoa CCM na hatimaye kushika dola?

Lizarazu

JF-Expert Member
Aug 23, 2015
6,334
7,868
Assalumu alaykum ndugu zangu waislamu na kwa wakristu wenzangu tumsifu yesu kristu.

Ni jambo linalofahamika kwa kila mtanzania kwamba ile miaka mitano mizito chini ya serikali dhalimu ya CCM inayoongozwa na Rais Magufuli atimae sasa inaelekea kufika tamati.

Ni takribani miezi kumi na wiki tatu zimebaki kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu ambapo Watanzania watapata nafasi adhimu ya kuchagua viongozi wa kisiasa watakaowaongoza kwa miaka mingine mitano ambao ni madiwani, wabunge na Rais.

Kama inavyofahamika tu kwenye uchaguzi huo mchuano ni kati ya CCM na vyama vya upinzani hasa vile vyenye nguvu, wakati CCM ikitaka kuendelea kutawala na kurudisha viti vyote ilivyopoteza kwenye chaguzi za huko nyuma na tayari kuna dalili zote, lengo kuu la upinzani pia ni kuing'oa CCM kwenye kila nafasi iliyoshikiri kuanzia ngazi ya urais.

CCM kikiwa kama chama dola kina faida kubwa dhidi ya vyama pinzani kuelekea uchaguzi huo, maana chenyewe ndio kinachounda serikali ambayo ndio ina ratibu zoezi zima la uchaguzi na hivyo kutoa mwanya wa wao kujiandalia mazingira ya ushindi kwa urahisi sana.

Kwa kuangalia duru ya kisiasa iliyopo hapa nchini kwetu hasa kwa awamu hii ya tano ni ngumu kusema kwamba CCM imepoteza imani kwa wananchi na pia vile vile ni ngumu kusema wananchi bado wana imani na CCM.

Ninachomaanisha hapa hasa ni kwamba wanaopenda kuendelea kuongozwa na CCM wapo na pia vile vile waliochoshwa na CCM wapo tena wengi tu.

Mimi ni mmoja wa waliochoshwa na utawala huu wa CCM na sitamani kabisa kuona ukiendelea kwani hata hii miaka mitano tu yenyewe nimeiona ni kama miaka nane.

Nakubali yapo mambo yenye tija kitaifa yaliyofanywa na awamu hii tuliyonayo lakini hayajanishawishi hata kidogo kuona kwamba inastahili kuendelea kuniongoza, kwani mimi hayo ninayachukulia kama ni misplacement of priorities (kukosewa kwa vipaumbele).

Sasa basi, matazamio yangu ni kuona upinzani ukiiondosha serikali ya CCM mnamo mwezi October mwaka huu na kutengeneza serikali yenye sura mpya kabisa tangu kuzaliwa kwa taifa hili.

Lakini katika kuwaza hayo kuna maswali kadhaa ninajiuliza:

- Kwa hii miaka minne na nusu upinzani wetu umejiandaa vipi hili kuhakikisha kwamba hilo linawezekana?

- Je, viongozi wa upinzani wamejipanga vilivyo kukabiliana na zile dosari/figisu figisu zilizokuwa zinatunyima nafasi ya kushika dola kwenye chaguzi za nyuma endapo kama zitatokea tena mwaka huu? Au Kuna chochote tulichojifunza kwenye chaguzi zilizopita?

- Je, wapinzani tuko tayari kuingia kwenye uchaguzi chini ya muongozo wa katiba ile ile ambayo ndio kikwazo kikuu miaka yote?

- Je, wapinzani tuko tayari kuingia kwenye uchaguzi bila tume huru ya uchaguzi halafu tutegemee matokeo tofauti na tuliozoea kuyaona?

- Je, Kuna uwezekano tukaona yale yaliotokea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana yakitokea na kwenye uchaguzi mkuu?

- Je, silaha pekee ya upinzani waliyonayo sasa ni kutegemea foreign interference (ufuatiliaji wa kigeni) kwenye uchaguzi mkuu hili kuhakikisha zoezi linaenda kidemokrasia?

- Je, kuna haja ya kutegemea ushindi kweli hasa kwenye kiti cha urais au ndio tujiandae kisaikolojia?

- Je, kuna mgombea sahihi aliyeandaliwa vilivyo kuchuana na Rsis Magufuli kwenye kiti cha urais?

Karibuni kwa michango wana jamvi.

Asanteni.

Sent using Jamii Forums mobile app

Maoni ya wadau:
Kuna theories 2 hapa za kuangalia

1. Tuchukulie kwamba hakuna Figisu zozote je Upinzani umejipanga na una sifa ya kushinda.

2. Je kwa figisu zilizopo kama zipo Upinzani una nafasi na umejiandaa kushinda?

Bahati mbaya umejikita kwenye Dhana no.2 ukiacha theory no.1.

Mimi naanza na no.1.
Kwamba, assume uwanja sawa wa ushindani viashiria vikoje?

1. Idadi ya wanachama ni muhimu kupima uelekeo kwa sababu 85 ya wanachama hukipigia chama chao pasi kuangalia sababu zingine yaani chama kwanza.

Mpaka leo CCM wanadai wana wanachama 15 milion by Polepole wakati CHADEMA wanadai wana 6 milion by Mbowe.

Sasa hapo jiulize nani ana fursa ya kushinda.

2. Potential Candidates, je vyama vina wagombea bora wenye uwezo wa kushindana na wenye ushawishi na fursa kubwa ya kushinda?

Hebu angalia hili kwanza; ni majimbo/kata ngapi ambazo CCM hupita bila kupingwa kwa sababu hakuna mgombea wa upinzani aliyejitokeza (sio wale waliofanyiwa figisu au kununuliwa) kwa mfano serikali za mitaa kabla ya figisu, 15% ya nafasi gombewa wapinzani hawakusimamisha wagombea (rejea salam za mwaka mpya za Kamanda Lissu).

Hapa pia kuna suala la ubora wa wagombea, katika chaguzi kadhaa tumeshuhudia Wapinzani wakija na wagombea dhaifu wasiokubalika katika jamii na mara nyingi wamekuwa wakisubiri kufaidika na minyukano ndani ya CCM (kusalitiana) pamoja na wale walioachwa na CCM ndio wawateuwe kugombea upinzani mfano mzuri ni Lowasa kwenye Urais na watu kama Cecil Mwambe (Ndanda) au
Kalanga wa Monduli.

Takriban asilimia 40 ya walioshinda Ubunge upinzani wamepatikana kwa mfumo huu.

2. Maeneo yenye Ushawishi (Political Strong Holds). Pemba ni ya CUF (samahani nasikia siku hizi ni ACT), Arusha, Kilimanjaro, Mara, Dar, Kigoma Mjini ni maeneo ambayo kwa 100% upinzani unatazamiwa kushinda majority (haya ni maeneo ambayo hata figisu figisu haziwezi kubadili matokeo).

Upinzani una maeneo mangapi kama haya kujihakikishia ushindi?

Pia tuangalie Rekodi nzuri ya utendaji kwa wapinzani walioko madarakani, this is a starting/running capital.

Hivi tukiacha ushabiki na upenzi wa vyama tunaweza kusema kwa dhati kwamba diwani au mbunge wangu toka upinzani amejipambanua kwa utendaji bora, kujitoa na kujituma ipasavyo?

Au tutakuwa na hoja kwamba tulitengwa au mbunge hakusanyi kodi?

Tunaweza kutembea kifua mbele na kujidai kwamba kata, majimbo na halmashauri zinazoongozwa na wapinzani ni mfano wa kuigwa na ndio BORA kuliko CCM. Au tunakuja na visingizio kibao.

Kubwa zaidi Vyama vyetu vimejipangaje na vimesimamiaje ubora/utendaji wa wagombea iliosimamisha au kuwadhamini?

Je tunaweza kusema kwa dhati kwamba kwa kazi nzuri iliyofanywa na diwani au mbunge huyu wa Upinzani mtu yoyote anaweza kuiona na kumchagua tena bila kujali uchama?

Kwa kuchelea kuchosha msomaji niishie hapa nikiwa nimeangalia dhana moja ya kwanza kabla ya kuangalia figisu zilizopo ambayo ni dhana ya pili.

TUJIPIME
 
Wapinzani wakowapi
Tanzania haina wapinzani
Fanya kazi mvua ndio hizi
Au unadanganywa na Vuvuzela za Jf
Zenye I'D Fake
Pole sana
Ccm Itaondolewa na kizazi kijacho sio hiki cha Vilaza fuata upepo
Hawajui wasimame na lipi
Baya la leo ndio zuri la kesho
Mbaya waleo ndio mzuri wa kesho
 
Lizarazu,

..mwaka huu kuna chaguzi za ngazi 3.

1. Uchaguzi wa Madiwani.

2. Uchaguzi wa Wabunge.

3. Uchaguzi wa Raisi.

..Unapozungumzia uchaguzi mkuu ni lazima uuangalie ktk ngazi hizo 3.

..Wapinzani wanatakiwa wawe na wagombea wazuri wanaovutia wapiga kura.

..Pia wawe na sera na ahadi zinazovutia wapiga kura wengi.

..Mwisho, wahakikishe kuwa mchakato wa uchaguzi unakuwa free [ huru] and fair [usawa].

..Sasa ili uchaguzi wetu uwe free and fair itabidi uhusishe wasimamizi na waangalizi wengi kutoka ndani na nje ya nchi.
 
Wapinzani wakowapi
Tanzania haina wapinzani
Fanya kazi mvua ndio hizi
Au unadanganywa na Vuvuzela za Jf
Zenye I'D Fake
Pole sana
Ccm Itaondooewa na kizazi kijacho sio hiki cha Vilaza fuata upepo
Hawajui wasimame na lipi
Baya la leo ndio zuri la kesho
Mbaya waleo ndio mzuri kesho
Hapana Tanzania tangu iingie kwenye multiparty system haijawahi kukosa upinzani.

Pengine labda kama ulitoa hii comment kwa kumaanisha upinzani uliopo sio ule wa kuitetemesha serikali kwa kiwango ambacho wewe unataka.

Kama ni wapinzani wapo na wana wafuasi kibao tu na wengine ndio hao unaowaita vuvu zela, wengine wako hata huko kwenye chama dola na wengine ndio wale bendera fuata upepo fulani akihama wana hama nae.

Imani yangu inaniambia kwamba hata hiki kizazi cha sasa cha upinzani kina nafasi ya kufanya mazuri pengine kuliko hata ccm endapo kama kitapewa nafasi licha ya hayo mapungufu yao unayoyaona.

Kuhusu kulima, nikujuze tu nimekuwa bize tangu mwezi September nashinda kwenye majaruba tu huku miguuni nikiwa na magambuti. Hivi sasa hivi ninavyoandika hapa ninasubiri kuvuna tu. Naomba ikifika mwezi march unikumbushe nikuletee hata gunia moja la ubwabwa wa Pasaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
JokaKuu, Asante sana mkuu JokaKuu kwa mchango wako.

Hili bandiko lako limerekebisha baadhi ya vitu ambavyo vinaonekana kukosekana kwenye bandiko langu(mpangilio wa ngazi za uchaguzi wenyewe).

Binafsi hata mimi naamini, kigezo cha kwanza cha kushinda uchaguzi ni kusimamisha mgombea mwenye ushawishi wa kisera kwa wanainchi. Na kwa hilo huwa sina shaka sana kwa upinzani.

Hofu na uwalakini mkubwa nilionao mimi ni namna zoezi litakavyoendeshwa kwanzia hatua ya awali mpaka ya kutangazwa kwa matokeo.

Na ndio maana hata maswali yangu kwenye hii mada yamejikita zaidi kwenye mazingira ya uchaguzi yatakavyokuwa na hasa ukizingatia awamu tumeona mauza uza mengi sana kwenye mfumo wetu mzima wa kisiasa.

Lakini bado naamini dosari tunazozitarajia zinaweza zikaondolewa kama kukiwepo na nia ya dhati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapinzani kipindi hiki wana wakati mgumu sana wa kupata mgombea urais. Sababu ni moja. Rais Magufuli ndiye atakayekuwa mgombea pekee kama "utaratibu" wa chama chao ulivyo. Hivyo, hakutakuwa na wagombea wengine na wapinzani watakosa kuchagua mgombea kutoka CCM. Kwahiyo watalazimika kuokotezaokoteza kutokà kwao. Usije kushangaa kumuona Mh. Lijualikali ndio mgombea wa Chadema!
 
Lizarazu,
Kuna theories 2 hapa za kuangalia

1. Tuchukulie kwamba hakuna Figisu zozote je Upinzani umejipanga na una sifa ya kushinda.

2. Je kwa figisu zilizopo kama zipo Upinzani una nafasi na umejiandaa kushinda?

Bahati mbaya umejikita kwenye Dhana no.2 ukiacha theory no.1.

Mimi naanza na no.1.
Kwamba, assume uwanja sawa wa ushindani viashiria vikoje?

1. Idadi ya wanachama ni muhimu kupima uelekeo kwa sababu 85 ya wanachama hukipigia chama chao pasi kuangalia sababu zingine yaani chama kwanza.

Mpaka leo CCM wanadai wana wanachama 15 milion by Polepole wakati CHADEMA wanadai wana 6 milion by Mbowe.

Sasa hapo jiulize nani ana fursa ya kushinda.

2. Potential Candidates, je vyama vina wagombea bora wenye uwezo wa kushindana na wenye ushawishi na fursa kubwa ya kushinda?

Hebu angalia hili kwanza; ni majimbo/kata ngapi ambazo CCM hupita bila kupingwa kwa sababu hakuna mgombea wa upinzani aliyejitokeza (sio wale waliofanyiwa figisu au kununuliwa) kwa mfano serikali za mitaa kabla ya figisu, 15% ya nafasi gombewa wapinzani hawakusimamisha wagombea (rejea salam za mwaka mpya za Kamanda Lissu).

Hapa pia kuna suala la ubora wa wagombea, katika chaguzi kadhaa tumeshuhudia Wapinzani wakija na wagombea dhaifu wasiokubalika katika jamii na mara nyingi wamekuwa wakisubiri kufaidika na minyukano ndani ya CCM (kusalitiana) pamoja na wale walioachwa na CCM ndio wawateuwe kugombea upinzani mfano mzuri ni Lowasa kwenye Urais na watu kama Cecil Mwambe (Ndanda) au
Kalanga wa Monduli.

Takriban asilimia 40 ya walioshinda Ubunge upinzani wamepatikana kwa mfumo huu.

2. Maeneo yenye Ushawishi (Political Strong Holds). Pemba ni ya CUF (samahani nasikia siku hizi ni ACT), Arusha, Kilimanjaro, Mara, Dar, Kigoma Mjini ni maeneo ambayo kwa 100% upinzani unatazamiwa kushinda majority (haya ni maeneo ambayo hata figisu figisu haziwezi kubadili matokeo).

Upinzani una maeneo mangapi kama haya kujihakikishia ushindi?

Pia tuangalie Rekodi nzuri ya utendaji kwa wapinzani walioko madarakani, this is a starting/running capital.

Hivi tukiacha ushabiki na upenzi wa vyama tunaweza kusema kwa dhati kwamba diwani au mbunge wangu toka upinzani amejipambanua kwa utendaji bora, kujitoa na kujituma ipasavyo?

Au tutakuwa na hoja kwamba tulitengwa au mbunge hakusanyi kodi?

Tunaweza kutembea kifua mbele na kujidai kwamba kata, majimbo na halmashauri zinazoongozwa na wapinzani ni mfano wa kuigwa na ndio BORA kuliko CCM. Au tunakuja na visingizio kibao.

Kubwa zaidi Vyama vyetu vimejipangaje na vimesimamiaje ubora/utendaji wa wagombea iliosimamisha au kuwadhamini?

Je tunaweza kusema kwa dhati kwamba kwa kazi nzuri iliyofanywa na diwani au mbunge huyu wa Upinzani mtu yoyote anaweza kuiona na kumchagua tena bila kujali uchama?

Kwa kuchelea kuchosha msomaji niishie hapa nikiwa nimeangalia dhana moja ya kwanza kabla ya kuangalia figisu zilizopo ambayo ni dhana ya pili.

TUJIPIME
 
Wapinzani kipindi hiki wana wakati mgumu sana wa kupata mgombea urais. Sababu ni moja. Rais Magufuli ndiye atakayekuwa mgombea pekee kama "utaratibu" wa chama chao ulivyo. Hivyo, hakutakuwa na wagombea wengine na wapinzani watakosa kuchagua mgombea kutoka CCM. Kwahiyo watalazimika kuokotezaokoteza kutokà kwao. Usije kushangaa kumuona Mh. Lijualikali ndio mgombea wa Chadema!
Binafsi sitaki kuamini kabisa kwamba wapinzani hawana mtu sahihi kabisa wa kusimama na Magufuli kwenye kinyang'anyiro, naamini yupo japo ukiniuliza ni nani siwezi kuwa na jibu.

Ngoja tusubiri japo kazi aliyonayo sio nyepesi hata kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Assalumu alaykum ndugu zangu waislamu na kwa wakristu wenzangu tumsifu yesu kristu.

Ni jambo linalofahamika kwa kila mtanzania kwamba ile miaka mitano mizito chini ya serikali dhalimu ya CCM inayoongozwa na Rais Magufuli atimae sasa inaelekea kufika tamati.

Ni takribani miezi kumi na wiki tatu zimebaki kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu ambapo Watanzania watapata nafasi adhimu ya kuchagua viongozi wa kisiasa watakaowaongoza kwa miaka mingine mitano ambao ni madiwani, wabunge na Rais.

Kama inavyofahamika tu kwenye uchaguzi huo mchuano ni kati ya CCM na vyama vya upinzani hasa vile vyenye nguvu, wakati CCM ikitaka kuendelea kutawala na kurudisha viti vyote ilivyopoteza kwenye chaguzi za huko nyuma na tayari kuna dalili zote, lengo kuu la upinzani pia ni kuing'oa CCM kwenye kila nafasi iliyoshikiri kuanzia ngazi ya urais.

CCM kikiwa kama chama dola kina faida kubwa dhidi ya vyama pinzani kuelekea uchaguzi huo, maana chenyewe ndio kinachounda serikali ambayo ndio ina ratibu zoezi zima la uchaguzi na hivyo kutoa mwanya wa wao kujiandalia mazingira ya ushindi kwa urahisi sana.

Kwa kuangalia duru ya kisiasa iliyopo hapa nchini kwetu hasa kwa awamu hii ya tano ni ngumu kusema kwamba CCM imepoteza imani kwa wananchi na pia vile vile ni ngumu kusema wananchi bado wana imani na CCM.

Ninachomaanisha hapa hasa ni kwamba wanaopenda kuendelea kuongozwa na CCM wapo na pia vile vile waliochoshwa na CCM wapo tena wengi tu.

Mimi ni mmoja wa waliochoshwa na utawala huu wa CCM na sitamani kabisa kuona ukiendelea kwani hata hii miaka mitano tu yenyewe nimeiona ni kama miaka nane.

Nakubali yapo mambo yenye tija kitaifa yaliyofanywa na awamu hii tuliyonayo lakini hayajanishawishi hata kidogo kuona kwamba inastahili kuendelea kuniongoza, kwani mimi hayo ninayachukulia kama ni misplacement of priorities (kukosewa kwa vipaumbele).

Sasa basi, matazamio yangu ni kuona upinzani ukiiondosha serikali ya CCM mnamo mwezi October mwaka huu na kutengeneza serikali yenye sura mpya kabisa tangu kuzaliwa kwa taifa hili.

Lakini katika kuwaza hayo kuna maswali kadhaa ninajiuliza:

- Kwa hii miaka minne na nusu upinzani wetu umejiandaa vipi hili kuhakikisha kwamba hilo linawezekana?

- Je, viongozi wa upinzani wamejipanga vilivyo kukabiliana na zile dosari/figisu figisu zilizokuwa zinatunyima nafasi ya kushika dola kwenye chaguzi za nyuma endapo kama zitatokea tena mwaka huu? Au Kuna chochote tulichojifunza kwenye chaguzi zilizopita?

- Je, wapinzani tuko tayari kuingia kwenye uchaguzi chini ya muongozo wa katiba ile ile ambayo ndio kikwazo kikuu miaka yote?

- Je, wapinzani tuko tayari kuingia kwenye uchaguzi bila tume huru ya uchaguzi halafu tutegemee matokeo tofauti na tuliozoea kuyaona?

- Je, Kuna uwezekano tukaona yale yaliotokea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana yakitokea na kwenye uchaguzi mkuu?

- Je, silaha pekee ya upinzani waliyonayo sasa ni kutegemea foreign interference (ufuatiliaji wa kigeni) kwenye uchaguzi mkuu hili kuhakikisha zoezi linaenda kidemokrasia?

- Je, kuna haja ya kutegemea ushindi kweli hasa kwenye kiti cha urais au ndio tujiandae kisaikolojia?

- Je, kuna mgombea sahihi aliyeandaliwa vilivyo kuchuana na Rsis Magufuli kwenye kiti cha urais?

Karibuni kwa michango wana jamvi.

Asanteni.

Sent using Jamii Forums mobile app

Maoni ya wadau:

Kama upinzani ulishindwa kuchukua dola 2015 wakati CCM ilikuwa mahututi ICU, utawezaje kuchukua nchi wakati Rais Dr Magufuli kishafufua CCM? Wapinzani walikuwa na ubinafsi 2015 (egoistic) na hasa Act Wazalendo na Prof maarufu wa uchumi ndo maana upinzani ulishindwa kuchukua dola! Dalili zinaonyesha kuwa chama tawala 2020 itashinda kwa 95% Hii ni garantii na 2025 kitashinda kwa 97%. Someni alama za nyakati - Ndege zisharudishwa, Reli, Mawasiliano na kadhalika.
 
Lizarazu,
Kuna theories 2 hapa za kuangalia

1. Tuchukulie kwamba hakuna Figisu zozote je Upinzani umejipanga na una sifa ya kushinda.

2. Je kwa figisu zilizopo kama zipo Upinzani una nafasi na umejiandaa kushinda?

Bahati mbaya umejikita kwenye Dhana no.2 ukiacha theory no.1.

Mimi naanza na no.1.
Kwamba, assume uwanja sawa wa ushindani viashiria vikoje?

1. Idadi ya wanachama ni muhimu kupima uelekeo kwa sababu 85 ya wanachama hukipigia chama chao pasi kuangalia sababu zingine yaani chama kwanza.

Mpaka leo CCM wanadai wana wanachama 15 milion by Polepole wakati CHADEMA wanadai wana 6 milion by Mbowe.

Sasa hapo jiulize nani ana fursa ya kushinda.

2. Potential Candidates, je vyama vina wagombea bora wenye uwezo wa kushindana na wenye ushawishi na fursa kubwa ya kushinda?

Hebu angalia hili kwanza; ni majimbo/kata ngapi ambazo CCM hupita bila kupingwa kwa sababu hakuna mgombea wa upinzani aliyejitokeza (sio wale waliofanyiwa figisu au kununuliwa) kwa mfano serikali za mitaa kabla ya figisu, 15% ya nafasi gombewa wapinzani hawakusimamisha wagombea (rejea salam za mwaka mpya za Kamanda Lissu).

Hapa pia kuna suala la ubora wa wagombea, katika chaguzi kadhaa tumeshuhudia Wapinzani wakija na wagombea dhaifu wasiokubalika katika jamii na mara nyingi wamekuwa wakisubiri kufaidika na minyukano ndani ya CCM (kusalitiana) pamoja na wale walioachwa na CCM ndio wawateuwe kugombea upinzani mfano mzuri ni Lowasa kwenye Urais na watu kama Cecil Mwambe (Ndanda) au
Kalanga wa Monduli.

Takriban asilimia 40 ya walioshinda Ubunge upinzani wamepatikana kwa mfumo huu.

2. Maeneo yenye Ushawishi (Political Strong Holds). Pemba ni ya CUF (samahani nasikia siku hizi ni ACT), Arusha, Kilimanjaro, Mara, Dar, Kigoma Mjini ni maeneo ambayo kwa 100% upinzani unatazamiwa kushinda majority (haya ni maeneo ambayo hata figisu figisu haziwezi kubadili matokeo).

Upinzani una maeneo mangapi kama haya kujihakikishia ushindi?

Pia tuangalie Rekodi nzuri ya utendaji kwa wapinzani walioko madarakani, this is a starting/running capital.

Hivi tukiacha ushabiki na upenzi wa vyama tunaweza kusema kwa dhati kwamba diwani au mbunge wangu toka upinzani amejipambanua kwa utendaji bora, kujitoa na kujituma ipasavyo?

Au tutakuwa na hoja kwamba tulitengwa au mbunge hakusanyi kodi?

Tunaweza kutembea kifua mbele na kujidai kwamba kata, majimbo na halmashauri zinazoongozwa na wapinzani ni mfano wa kuigwa na ndio BORA kuliko CCM. Au tunakuja na visingizio kibao.

Kubwa zaidi Vyama vyetu vimejipangaje na vimesimamiaje ubora/utendaji wa wagombea iliosimamisha au kuwadhamini?

Je tunaweza kusema kwa dhati kwamba kwa kazi nzuri iliyofanywa na diwani au mbunge huyu wa Upinzani mtu yoyote anaweza kuiona na kumchagua tena bila kujali uchama?

Kwa kuchelea kuchosha msomaji niishie hapa nikiwa nimeangalia dhana moja ya kwanza kabla ya kuangalia figisu zilizopo ambayo ni dhana ya pili.

TUJIPIME
Mchango fikirishi sana huu na haya ndio mawazo niliyotegemea kuyapokea kwenye mada hii chonokozi, asante kwa hilo.

Na mimi naomba niendelee na hii hii dhana no.1 ambapo kwa namna moja ama nyingine ina muingiliano mkubwa sana na ile ya 2.

Hapo kwenye utofauti wa idadi ya wanachama nayo pia ni advantage kubwa kwa CCM maana kwa kuangalia tu hizo figures(ikiwa kama ni za kweli) basi mpaka sasa hivi CCM inaongoza kwa kura milioni 9 kwenye ngazi ya uraisi kabla hata hatujaingia kwenye uchaguzi. Sasa swali ambalo najiuliza mimi ni kwanini pamoja na huu mtaji wa kura milioni 9 walionao lakini bado ccm hawataki uchaguzi uwe wa huru na haki? Yaani ni kwamba hawana imani hata hao wanachama wao kama wako loyal na chama chao ama?

Pia hapo kwenye uhaba wa potential candidates kwa upande wa upinzani kiasi cha wao kushindwa kusimamisha wagombea kwenye baadhi ya maeneo nadhani hilo ni suala linalohusu zaidi ufinyu wa rasilimali zilizopo chamani. Unajua kuna vijiji ukivitembelea hapa nchini hata ofisi tu ya kata ya chama chochote cha upinzani hakuna kabisa, achilia mbali wanachama, tena ni vingi sana na ukijaribu kudadisi utakuta hakuna uwekezaji wowote wa kisiasa kutokana na ufinyu wa rasilimali walizonazo wapinzani. Wakati huo tunafahamu CCM wao wamewekeza kila mtaa kwenye nchi hii. Hapa hakuna wa kumlaumu baada ni financial muscles ndio inaleta huu utofauti.

Kuhusu wapinzani kusimamisha wagombea ambao hapo awali walikuwa upande wa CCM sioni kama sababu ni kutokuwepo kwa wagombea bora ndani ya upinzani, hili mimi naliona kama maamuzi yanayofanyika kulingana na upepo wa kisiasa ulivyo kwa wakati huo, Lowasa hakuwa bora kuliko Dr.Slaa au Mbowe mwaka 2015, lakini mazingira ya kisiasa ndio yalipelekea yeye kupewa nafasi ya kugombea uraisi na kuwaacha wale waliokiangaikia chama.

Wapinzani kipindi hiki wana wakati mgumu sana kwenye kuwashawishi wanainchi, maana ni ukweli uliowazi hii suppression waliofanyiwa kwa hii miaka mitano imewazorotesha sana kiutendaji, na kwa bahati mbaya sana wengi hawaoneshi kulitambua hili. Na siku zote kitu pekee kinachomshawishi hili mwanainchi hili akupe kura yake ni mazuri uliyoyafanya, na kamwe hawezi kukupa kura za huruma kutokana na maswahibu uliyopitia yakiyokufanya mpaka ukashindwa kuwajibika ipasavyo.

Halafu na kitendo cha Raisi kupiga marufuku shughuli za kisiasa kwa muda wa miaka minne na kujipa mwanya wa kutawala ulingo peke yake kama tulivyokuwa tunaona, tayari kimeurudisha nyuma sana upinzani, maana kimepunguza popularity yao na hiyo itawaathiri sana maana kwa sasa wanaonekana hawako relevant kama walivyokuwa miaka ya nyuma.

Kwa hayo maswali yalipo huko mwishoni na mimi ndio bado nayatafutia majibu, je upinzani umejiandaa vipi kwenye mchakato mzima kuhakikisha kwamba unapata matokeo yaliyo bora kuliko ilivyokuwa huko nyuma?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama upinzani ulishindwa kuchukua dola 2015 wakati CCM ilikuwa mahututi ICU, utawezaje kuchukua nchi wakati Rais Dr Magufuli kishafufua CCM? Wapinzani walikuwa na ubinafsi 2015 (egoistic) na hasa Act Wazalendo na Prof maarufu wa uchumi ndo maana upinzani ulishindwa kuchukua dola! Dalili zinaonyesha kuwa chama tawala 2020 itashinda kwa 95% Hii ni garantii na 2025 kitashinda kwa 97%. Someni alama za nyakati - Ndege zisharudishwa, Reli, Mawasiliano na kadhalika.
Nakubaliana na wewe kabisa kwamba upinzani ulikuwa na nafasi kubwa ya kushika dola kwenye uchaguzi mkuu uliopita kutokana na political chaos iliyokuwepo kwa kipindi hicho hasa kwa upande wa CCM, nikiangalia sasa hivi sioni ile faida waliokuwa nayo wapinzani nyakati zile kama wataipata tena mwaka huu, na badala yake wao ndio wameingia kwenye sintofahamu ambayo hata kwenye kampeni itawapa wakati mgumu refer sula la Lowasa kurudi CCM.

Halafu sielewi hapo unaposema kwamba wapinzani walikuwa wabinafsi, kivipi hasa?

Na pia kama ccm wanajiaminisha kuwa huu mwaka watashinda kwa kishindo ni kwanini bado taratibu za uchaguzi ni zile zile tu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa zikiwapa kashifa ya udanganyifu wa matokeo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi sitaki kuamini kabisa kwamba wapinzani hawana mtu sahihi kabisa wa kusimama na Magufuli kwenye kinyang'anyiro, naamini yupo japo ukiniuliza ni nani siwezi kuwa na jibu.

Ngoja tusubiri japo kazi aliyonayo sio nyepesi hata kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app

Tatizo sio wapinzani kuwa na mgombea bora, bali ni kuwa na tume huru itakayoheshimu kura zetu. Tulio wengi hatuko tayari tena kwenda kusimama kwenye mstari wa kura kushiriki zoezi lenye figisu na uhayawani wa wazi. Wakati nyie mnazungumzia uchaguzi utakavyokuwa, sisi wengine tunazidi kuwaambia wananchi wasishiriki kwenye uchaguzi wa kishenzi.

Tulilianza hili wakati wa uchaguzi SM za mitaa na tulipata matokeo stahiki. Na kwenye uchaguzi ujao tuna uhakika tutafanikiwa kwa kishindo. Hiyo itatufanya kuwa na serikali iliyopo kisheria, lakini isiyo na uhalali wa umma. Hapo tutaweza kutumia plan B kupata viongozi wanaokubalika na umma. Kitendo cha kutokushiriki uchaguzi kwa watu wengi ni nguvu ya umma ya amani isiyo na mauaji, kuacha watu na vilema, lakini ni njia nzuri ya kuwaambia chama kinachonajisi uchaguzi hatukikubali.
 
Tatizo sio wapinzani kuwa na mgombea bora, bali ni kuwa na tume huru itakayoheshimu kura zetu. Tulio wengi hatuko tayari tena kwenda kusimama kwenye mstari wa kura kushiriki zoezi lenye figisu na uhayawani wa wazi. Wakati nyie mnazungumzia uchaguzi utakavyokuwa, sisi wengine tunazidi kuwaambia wananchi wasishiriki kwenye uchaguzi wa kishenzi.

Tulilianza hili wakati wa uchaguzi SM za mitaa na tulipata matokeo stahiki. Na kwenye uchaguzi ujao tuna uhakika tutafanikiwa kwa kishindo. Hiyo itatufanya kuwa na serikali iliyopo kisheria, lakini isiyo na uhalali wa umma. Hapo tutaweza kutumia plan B kupata viongozi wanaokubalika na umma. Kitendo cha kutokushiriki uchaguzi kwa watu wengi ni nguvu ya umma ya amani isiyo na mauaji, kuacha watu na vilema, lakini ni njia nzuri ya kuwaambia chama kinachonajisi uchaguzi hatukikubali.
Sawa kabisa mkuu, hichi unachokisema nami pia nimekuwa nakiwaza ndio maana hata hapo kwenye original post miongoni mwa maswali yaliyopo ni "je, tutegemee kuona yale yalitokea kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa yakitokea na kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu"? Kwa maana ya upinzani na wafuasi wao kwa ujumla kususia uchaguzi.

Kikubwa hapo kinachohitajika hili maamuzi hayo yasichukuliwe ni uwepo wa tume huru ya uchaguzi.

Sasa basi, wakati tunapaza sauti kuhusu tume huru, je tuliitumiaje hiyo miaka minne kuhakikisha kwamba mpaka tunafika mwka huu wa uchaguzi tuwe na tume huru? Yaani kuna jitihada gani tuliziweka?

Kwangu mimi ukiniuliza kama wapinzani walikuwa wanapigania hilo suala la tume huru nitakwambia hapana maana jitihada zao zilikuwa ni ndogo sana kwenye hilo.

Obvious tume huru ni zao la katiba mpya, na hili tuwe nayo ni lazima tufanye kwanza mabadiliko ya kikatiba, kwa mantiki hii basi ilipaswa wapinzani tuweke nguvu zaidi kwenye kudai katiba mpya, lakini kwa bahati mbaya sana hilo halijafanyika kwa hii miaka minne na kama limefanyika basi ni kwa kiwango duni sana.

Binafsi hata mimi naona kuna tija ya kutoshiriki uchaguzi wa mwaka huu kwa upande wa upinzani maana tayari mazingira tu yenyewe yanajionesha matokeo yatakayotangazwa ni yapi kabla hata zoezi lenyewe halijafanyika.

Lakini sasa, tukishasusia uchaguzi nini kinafuata baada ya hapo? Ndio serikali itaweka tume huru?

Mfano tu kwenye serikali za mitaa, tulisusia uchaguzi, lakini ukafanyika na matokeo yakatangazwa ccm wameshinda kwa almost 100%, na mpaka hivi sasa mitaa yetu inaongozwa na viongozi wa CCM tu na maisha yanaendelea wanainchi walishasahau kabisa kilichotokea mwaka jana November.

Sasa, kwenye uchaguzi mkuu napo tujiandae kuona hali hiii hii? Yaani kwanzia raisi awe wa CCM, 98% ya wabunge wote wawe ni CCM na madiwani nao wawe hivyo hivyo?

Au labda kuna kitu mimi sikijui kuhusu hili la kususia uchaguzi? Yawezekana labda liko so strategical kana kwamba serikali lazima isalimu amri na kuunda tume huru ya uchaguzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom