Wapinzani, ni wakati wa kuanzaa vikao vya kuweka mikakati ya pamoja kuelekea 2020

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Nawashauri viongozi wa vyama vya upinzani kukutana haraka iwezekanavyo na kuandaa ratiba nzima ya vikao vya pamoja vya kimkakatiti kuelekea uchaguzi mkuu wa baadae mwaka huu.

Kamati ndogo iundwe (wajumbe watoke kutoka vyama vyote vilivyo tayari), ikae na ipange agenda na mambo mengine na baadae vifuate vikao vya viongozi wa juu wa vyama vya siasa na yatakayoamuliwa yapelekwe kwenye vikao vya kamati kuu vya kila chama cha siasa kupata baraka kabla ya kuanza utekelezaji.

Kumbukeni mnahitaji pia kushirikisha wadau wengine wa maswala ya uchaguzi wa ndani na wa nje ya nchi na pia mnahiutaji kupata muda wa kutosha wa kushirikisha umma juu ya mtakayoyaamua(kuwapa elimu/ufafanuzi wa mtakayoyaamua).

Muda hautoshi hivyo msiendelee kupoteza muda.
 
Speaking of Uchaguzi Mkuu. Bila tume huru hata upinzani wanisimamishe nini hawashindi.
 
Wajue fika hoja kuu mbali ya nani agombee nafasi gani kwenye huo uchaguzi ni tume huru ya uchaguzi. Hakuna tume huru ya uchaguzi, wasitegemee kutuona sisi wapiga kura wa upinzani tunaojitambua kushiriki huo uhuni.
 
Wajue fika hoja kuu mbali ya nani agombee nafasi gani kwenye huo uchaguzi ni tume huru ya uchaguzi. Hakuna tume huru ya uchaguzi, wasitegemee kutuona sisi wapiga kura wa upinzani tunaojitambua kushiriki huo uhuni.
Tutawatambuaje hao wapiga kura wa upinzani? Au mmepànga kuvaa gwanda zenu siku ya kupiga kura?

Ripoti ya idadi ya wanachama wa CCM inaonesha kuwa CCM kina wanachama zaidi ya mil 18 nchi zima ukiachilia mbali wanachama wa idara zake kama UVCCM ,UWT na WAZAZI kwa mantiki hiyo kama wakijiandikisha watu milion 20 ,CCM Ina uhakika wa kura mil 18 sawa na 90%
 
Tutawatambuaje hao wapiga kura wa upinzani? Au mmepànga kuvaa gwanda zenu siku ya kupiga kura?

Ripoti ya idadi ya wanachama wa CCM inaonesha kuwa CCM kina wanachama zaidi ya mil 18 nchi zima ukiachilia mbali wanachama wa idara zake kama UVCCM ,UWT na WAZAZI kwa mantiki hiyo kama wakijiandikisha watu milion 20 ,CCM Ina uhakika wa kura mil 18 sawa na 90%

Hapana ww umekosea figure, ccm ina wanachama 48m, wasiliana na kitengo cha kupika data, kisha uje uweke hiyo figure yako sawa.
 
Kamanda tulia dawa iwaingie, uchaguzi wa mwaka huu utaacha kilio kikubwa ufipa na kuanzia 2021 ofisi za ufipa zitakuwa mazalia ya ñdege na viumbe vingine hatarishi

Hakuna uchaguzi 2020 bali kuna kipimo halisi cha ujinga wa mtu mweusi inapokuja suala la kusaka madaraka. Sio kufunga tu hizo ofisi za ufipa, ikibidi hata viongozi wake wote muwafanyie kile mlichomfanyia Lissu.
 
Ukweli anaouma nikua vijana wa Chadema wamekua mstari wambele katika kaharibu mafahamiano mazuri baina ya CHADEMA na ACT.

Wakae wakifahamu tu bila ya ACT pembeni yao wao hawana safari. ACT ya sasa sio chama cha kigoma tena, nawala si Zanzibar tu. ACT ya sasa pia Kime replace ngome zote zilizokua za CUF kuanzia Lindi, Mtwara, Tanga, Dar na kwengineko.

Waache upuuzi wao wakae mezani na wenzao.

Mabeberu wanasema PRIDE KILLS.
 
Tutawatambuaje hao wapiga kura wa upinzani? Au mmepànga kuvaa gwanda zenu siku ya kupiga kura?

Ripoti ya idadi ya wanachama wa CCM inaonesha kuwa CCM kina wanachama zaidi ya mil 18 nchi zima ukiachilia mbali wanachama wa idara zake kama UVCCM ,UWT na WAZAZI kwa mantiki hiyo kama wakijiandikisha watu milion 20 ,CCM Ina uhakika wa kura mil 18 sawa na 90%
Unatumia masaburi kwenye bandiko zako zote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unatumia masaburi kwenye bandiko zako zote

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkiambiwa ukweli nguvu yenu bado ni changa ya kuweza kukabiliana na CCM mnakuja na ngonjera oooh! CCM ilipunguza upana wa goli ,mara oooh! Ccm ilihonga refa, Mara ooooh! CCM iliweka mpira kwapani na kukimbia.

Tulieni tuingize dawa kwenye matundu ya miili yenu
 
Inaonekana hiyo ndiyo kazi yako ya kudaka na kumeza mitaa ya makaburini kino
Mkiambiwa ukweli nguvu yenu bado ni changa ya kuweza kukabiliana na CCM mnakuja na ngonjera oooh! CCM ilipunguza upana wa goli ,mara oooh! Ccm ilihonga refa, Mara ooooh! CCM iliweka mpira kwapani na kukimbia.

Tulieni tuingize dawa kwenye matundu ya miili yenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom