We pimbi badala ya kuja na mkakati wa kupata katiba mpya Ili domorasia ipanuke zaidi Ili vyama viwe huru kufanya siasa vitanue viwe vya kitaifaNasema hivo kwa sabau zifatazo:.
•CCM imekuwa madarakani tokea kaundwa kwake mwaka 1977 na kwa sababu hiyo kutokana na hurka za wanadamu kimeonesha kupoteza ushawishi kadri siku zinavoenda.
•CCM kukosa sera au kupungukiwa mawazo mbadala kutokana na mfumo wake ila kwa sasbubu CCM inamuundo wenye sura ya kitaifa imekuwa ikikubarika katika maeneo mengi kutoka na wananchi kujisikia huru kukichagua hata kama hawakitaki au wamekichoka kwa kujihisi kuwa huru zaidi ukilinganisha na vyama vingine vyenye kukosa sura ya kitaifa!
•CHADEMA chama hiki kimekuwa na ukuaji mzuri ila kinachangamoto ya kuonekana na baadhi ya watanzania kuwa ni chama chenye chembechembe za ukabila na ukanda na kwa sababu hiyo kupoteza mvuto kwa baadhi ya watu katika jamii.
•CHADEMA imeonekana hususani katika siku za hivi karibuni kugeuka kuwa chama cha wanaharakati zaidi na kukosa sera madhubuti kwa ajili ya wananchi, hali hii imeadhiri sana ukuaji wa chama hiki kwa siku hizi!
•ACT WAZALENDO! ni chama kichanga lakini kinachangamoto ya kukosa sura ya kitaifa kwa kuegemea zaidi katika upande ya dini ya kiislam na kukifanya kupoteza mvuto katika maeneo mengi yasiyokuwa na waumimi wengi wa dini hiyo! Hili unaweza kuliona kwenye safu yake ya uongozi!
•ACT WAZALENDO ikumbukee kuwa ukuaji wake pia umechagizwa zaidi na mgogoro ndani ya chama cha CUF kwa hiyo bado ni chama kichanga sana hususani kwa tanzania bara!
•CUF ni chama kikongwe lakini kilichokosa ubunifu na kuibuka kwa migogoro ndani yake na kusababisa kusambaratika kwa wafuasi wake kwa kiasi kikubwa upande wa zanzibar!
•CUF ni chama kilichojiwekeza zaidi maeneo ya pwani na kukosa ushawishi wa kitaifa kwa miaka mingi kwa hiyo si chama chenye matumaini tena kwa watanzania kwa sasa!
PENDEKEZO
Nawaomba wazalendo na wapinzani wa kweli ndani ya nchi yetu wajitokeze ili kuunda chama kipya chenye sura ya kitaifa, na hili likifanyika mapema ili kuweza kukitamburisha kwa wananchi na ninauhakika kitatoa upinzani mkubwa sana kwa CCM 2025. Na kwa hilo tutapata serkali bora yenye kaundwa na watu wenye mawazo mseto kwa mustakabari mwema wa taifa letu!
HITIMISHO
Watanzania waliowengi wanasubiri sana chama kitakachowapa matumaini mapya katika kizazi hiki! Kuna na vyama vya upinzani vyenye sura ya kitaifa ni muhimu sana ili kufikia ndoto ya kuwa na demokrasia makini na chaguzi zenye ushindani. Naomba Mungu awabariki sana!
We unaleta blah blah tu