Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,830
- 976
Wanajamvi,
Kumbukumbu zangu zimenichukua mpaka kwenye miaka 5 ya mwisho ya utawala wa Mzee Kikwete, yaani 2010 - 2015. Nimejaribu kupitia vyanzo mbalimbali pamoja na kumbukumbu zangu binafsi kuhusu zipi hasa zilikuwa ajenda za wapinzani.
Wapinzani walipigia kelele sana suala la rushwa (ufisadi), Kukuza uchumi kwa kuhakikisha wanaimarisha shirika la ndege, reli, bandari n.k
Waliongea pia kuhusu madini na jinsi watakavyofumua mikataba ya madini
Hawakuishia hapo, waliahidi elimu bure mpaka chuo kikuu.
Uchaguzi ukafika 2015 na watanzania wakaamua Dr. John Magufuli ndio awe nahodha. Tangu hapo, Rais. Magufuli ametekeleza kwa ufasaha ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2015 - 2020 na akaenda mbali kutekeleza Yale yote wapinzani waliyoahidi. Ukiacha elimu bure mpaka chuo kikuu, ni kipi hajafanya? Hata Hilo la elimu bure mpaka chuo kikuu limefanyika kwa mtindo mwingine. Unapomkopesha mtoto wa masikini ili asome, maana yake umemuwezeshea kufikia ndoto zake na hapohapo kulisaidia taifa kwa kuhakikisha linapata wataalamu wa kutosha.
Rais Dr. Magufuli aliweka bayana, mpaka 2020 Upinzani utakuwa umekufa Tanzania, wasioelewa walitafsiri watakavyo ila kifo hicho kilitabiriwa kutokana na ukweli kuwa alijipanga, na amefanikiwa kutekeleza kile watanzania walio CCM na Upinzani walichotaka. Je, hapo kutakuwa na Upinzani tena?
Hebu niambieni, wapinzani wanna ajenda gani ya maana mwaka huu? Mnawasikia Tena wqkiongelea ajenda ya ufisadi?
Nataka niwakumbushe wapinzani kuwa watanzania tunakumbuka kuwa waliiacha ajenda ya ufisadi tangu balozi Dkt. Slaa alipowachomoka pyuuu. Sasa hawana nyimbo.
Mgombea wao alikubali kula matapishi yake kwa kumpokea mtu aliyewaaminisha watanzania kuwa ni fisadi. Alikaa kimyaaaaa, mbona hakuonesha hayo makeke. Duru zinaarifu kuwa ukiacha balozi Dkt. Slaa ambaye alipinga hadharani, Mnyika inaaminika kuwa alikwazwa sana.
Hatujasahau kuwa ni yeye mgombea wao aliyeshadadia Mwami afukuzwe chamani kwa kutamani kiti. Demokrasia anayoihubiri iko wapi? Kama alishindwa kutuonesha hivyo tangu awali, tutamuaminije sasa?
2020 kura yangu ni kwa John.
Kumbukumbu zangu zimenichukua mpaka kwenye miaka 5 ya mwisho ya utawala wa Mzee Kikwete, yaani 2010 - 2015. Nimejaribu kupitia vyanzo mbalimbali pamoja na kumbukumbu zangu binafsi kuhusu zipi hasa zilikuwa ajenda za wapinzani.
Wapinzani walipigia kelele sana suala la rushwa (ufisadi), Kukuza uchumi kwa kuhakikisha wanaimarisha shirika la ndege, reli, bandari n.k
Waliongea pia kuhusu madini na jinsi watakavyofumua mikataba ya madini
Hawakuishia hapo, waliahidi elimu bure mpaka chuo kikuu.
Uchaguzi ukafika 2015 na watanzania wakaamua Dr. John Magufuli ndio awe nahodha. Tangu hapo, Rais. Magufuli ametekeleza kwa ufasaha ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2015 - 2020 na akaenda mbali kutekeleza Yale yote wapinzani waliyoahidi. Ukiacha elimu bure mpaka chuo kikuu, ni kipi hajafanya? Hata Hilo la elimu bure mpaka chuo kikuu limefanyika kwa mtindo mwingine. Unapomkopesha mtoto wa masikini ili asome, maana yake umemuwezeshea kufikia ndoto zake na hapohapo kulisaidia taifa kwa kuhakikisha linapata wataalamu wa kutosha.
Rais Dr. Magufuli aliweka bayana, mpaka 2020 Upinzani utakuwa umekufa Tanzania, wasioelewa walitafsiri watakavyo ila kifo hicho kilitabiriwa kutokana na ukweli kuwa alijipanga, na amefanikiwa kutekeleza kile watanzania walio CCM na Upinzani walichotaka. Je, hapo kutakuwa na Upinzani tena?
Hebu niambieni, wapinzani wanna ajenda gani ya maana mwaka huu? Mnawasikia Tena wqkiongelea ajenda ya ufisadi?
Nataka niwakumbushe wapinzani kuwa watanzania tunakumbuka kuwa waliiacha ajenda ya ufisadi tangu balozi Dkt. Slaa alipowachomoka pyuuu. Sasa hawana nyimbo.
Mgombea wao alikubali kula matapishi yake kwa kumpokea mtu aliyewaaminisha watanzania kuwa ni fisadi. Alikaa kimyaaaaa, mbona hakuonesha hayo makeke. Duru zinaarifu kuwa ukiacha balozi Dkt. Slaa ambaye alipinga hadharani, Mnyika inaaminika kuwa alikwazwa sana.
Hatujasahau kuwa ni yeye mgombea wao aliyeshadadia Mwami afukuzwe chamani kwa kutamani kiti. Demokrasia anayoihubiri iko wapi? Kama alishindwa kutuonesha hivyo tangu awali, tutamuaminije sasa?
2020 kura yangu ni kwa John.