Wapinzani mnapaswa kujitafakari sana kama siasa mnazofanya zinafaa kwenye zama za Hapa Kazi Tu

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Nimetafakari sana juu ya hii hali ambayo wanasiasa wa vyama vya upinzani wanakumbana nayo. Hata kabla mwaka haujaisha, yapo matukio kadhaa ya viongozi wa upinzani kujikuta wakivuka mipaka ya siasa zao kutokana ama na kutamka maneno yanayovuka mipaka yao ama wanafanya matendo ambayo yumkini hayaendani na kasi ya Serikali ya Hapa Kazi Tu.

Hadi sasa tumeshuhudia wabunge 8 wa upinzani wakiadhibiwa Bungeni. Viongozi wa CHADEMA na Zitto Kabwe wamehojiwa mara kadhaa na jeshi la polisi na huenda wakafunguliwa mashtaka ikiwa upelelezi wa jeshi la polisi utawakuta na makosa.

Nilichogundua ni kwamba viongozi wa upinzani ama uwezo wao wa kufanya siasa safi ni mdogo na hivyo kujikuta wakiendelea na siasa zao za maji taka ama wanafanya makusudi kwa kuendelea kumchezea Rais ili aache mambo yake ya msingi ya kuwaletea maendeleo wananchi na badala yake akimbizane nao. Ama wanafanya hivyo kwa lengo la kutaka kualikwa Ikulu kunywa juice na kupiga Selfie.

Niwatahadhalishe wapinzani. Hizi ni zama za kuwaletea maendeleo wananchi na si vinginevyo. Rais ameshatamka kuwa hatapenda kuona mtu akikwamisha utekelezaji wa Ilani ya CCM, chama kilichopewa ridhaa na wananchi ya kuongoza nchi hii. Maana yake ni kwamba, wale watakaojaribu kukwamisha utekelezaji wa Ilani hiyo, lazima watakiona cha Mtema kuni. Na hii ni dhahiri kabisa na uzuri wa Rais wetu ni kwamba hafichi kitu.

Kwa hali hiyo, kama wapinzani mnaona kuwa hamna uwezo wa kudhibiti midomo yenu na maneno machafu, you better plaster your mouths as you did in the House of Parliament. Vinginevyo hakika ni dhahiri kwamba mtaumia. Siasa za Magufuli ni za Hapa Kazi Tu
 
Unakosea unapotishia wapinzani "wataumia". Wewe huoni sasa hapo husaidii kitu? Hapa unasababisha utengano na unapaswa uelewe nchi ya vyama vingi inafaa kuendeshwa kwa maridhiano. Tanzania hii inajengwa na watanzania wote, wapinzani na walioshika dola. Majigambo, kutisha watu sidhani itafaa kitu.
 
Unakosea unapotishia wapinzani "wataumia". Wewe huoni sasa hapo husaidii kitu? Hapa unasababisha utengano na unapaswa uelewe nchi ya vyama vingi inafaa kuendeshwa kwa maridhiano. Tanzania hii inajengwa na watanzania wote, wapinzani na walioshika dola. Majigambo, kutisha watu sidhani itafaa kitu.
Mkuu, siwatishi ila ukweli ndio huo. Nchi hii imechezewa sana na miongoni mwa waliokuwa wanachezea ni hawa wanasiasa uchwara. Tanzania tumeendesha siasa za uvumilivu kwa muda mrefu na ndio maana mpaka sasa hakuna kingozi wa upinzani hata mmoja amefungwa tofauti na nchi za wenzetu
 
Tatizo lako Lizabon hujui kitu chochote kuhusu demokrasia ya vyama vingi na wala hujui vipi kisheria! pia hupo rational. unashangaza sana unaposhangilia wanayofanyiwa wapinzani kwa msukumo wa ikulu kama ulivotujuza. mbunge mmoja aliwaadhalilisha wabunge viti maalumu ukawa hakuuulizwa kitu! je wabunge kudai muongozo kuhusu zaidi ya wanafunzi 7000 Kufukuzwa udom lilikuwa kosa la kufukuzwa bungeni? ondoa utando wa ujinga kichwani kwako na panua uwezo wa kufikiria nje ya box ulimojifungia!
 
Mkuu, siwatishi ila ukweli ndio huo. Nchi hii imechezewa sana na miongoni mwa waliokuwa wanachezea ni hawa wanasiasa uchwara. Tanzania tumeendesha siasa za uvumilivu kwa muda mrefu na ndio maana mpaka sasa hakuna kingozi wa upinzani hata mmoja amefungwa tofauti na nchi za wenzetu

Nchi imechezewa sana......maana yake serikali ya CCM ilisababisha yote hayo sivyo? Kwahiyo ili kujikwamua inaona kutumia "udikteta uchwara" itaweza kutatua matatizo ya watanzania? Mimi nasema maridhiano ndiyo way forward. Viongozi wakuu wanapaswa waongoze nchi kwa upendo mkuu, unyenyekevu, akili kubwa, tena wasiwe wepesi kukasirishwa na wapinzani wao.
 
Mkuu, siwatishi ila ukweli ndio huo. Nchi hii imechezewa sana na miongoni mwa waliokuwa wanachezea ni hawa wanasiasa uchwara. Tanzania tumeendesha siasa za uvumilivu kwa muda mrefu na ndio maana mpaka sasa hakuna kingozi wa upinzani hata mmoja amefungwa tofauti na nchi za wenzetu
Huna lolote unalolijua,

Mana hujui hata kama RC ni mtumishi wa umma....yote unayoongea humu huwa ni matakataka tu
 
Nchi imechezewa sana......maana yake serikali ya CCM ilisababisha yote hayo sivyo? Kwahiyo ili kujikwamua inaona kutumia "udikteta uchwara" itaweza kutatua matatizo ya watanzania? Mimi nasema maridhiano ndiyo way forward. Viongozi wakuu wanapaswa waongoze nchi kwa upendo mkuu, unyenyekevu, akili kubwa, tena wasiwe wepesi kukasirishwa na wapinzani wao.
Tuliwalea lea sana wapinzani. Sasa ni zamu ya kuisoma namba
 
Tuliwalea lea sana wapinzani. Sasa ni zamu ya kuisoma namba

Haitasaidia kitu.....katiba imetamka uwepo wa vyama vingi. See? Utamzuia huyu atatokea yule. ....mwisho watakushinda na watatwaa madaraka. Trust me.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Nimetafakari sana juu ya hii hali ambayo wanasiasa wa vyama vya upinzani wanakumbana nayo. Hata kabla mwaka haujaisha, yapo matukio kadhaa ya viongozi wa upinzani kujikuta wakivuka mipaka ya siasa zao kutokana ama na kutamka maneno yanayovuka mipaka yao ama wanafanya matendo ambayo yumkini hayaendani na kasi ya Serikali ya Hapa Kazi Tu.

Hadi sasa tumeshuhudia wabunge 8 wa upinzani wakiadhibiwa Bungeni. Viongozi wa CHADEMA na Zitto Kabwe wamehojiwa mara kadhaa na jeshi la polisi na huenda wakafunguliwa mashtaka ikiwa upelelezi wa jeshi la polisi utawakuta na makosa.

Nilichogundua ni kwamba viongozi wa upinzani ama uwezo wao wa kufanya siasa safi ni mdogo na hivyo kujikuta wakiendelea na siasa zao za maji taka ama wanafanya makusudi kwa kuendelea kumchezea Rais ili aache mambo yake ya msingi ya kuwaletea maendeleo wananchi na badala yake akimbizane nao. Ama wanafanya hivyo kwa lengo la kutaka kualikwa Ikulu kunywa juice na kupiga Selfie.

Niwatahadhalishe wapinzani. Hizi ni zama za kuwaletea maendeleo wananchi na si vinginevyo. Rais ameshatamka kuwa hatapenda kuona mtu akikwamisha utekelezaji wa Ilani ya CCM, chama kilichopewa ridhaa na wananchi ya kuongoza nchi hii. Maana yake ni kwamba, wale watakaojaribu kukwamisha utekelezaji wa Ilani hiyo, lazima watakiona cha Mtema kuni. Na hii ni dhahiri kabisa na uzuri wa Rais wetu ni kwamba hafichi kitu.

Kwa hali hiyo, kama wapinzani mnaona kuwa hamna uwezo wa kudhibiti midomo yenu na maneno machafu, you better plaster your mouths as you did in the House of Parliament. Vinginevyo hakika ni dhahiri kwamba mtaumia. Siasa za Magufuli ni za Hapa Kazi Tu

Tuliza munkari mdada. Huna uwezo wa kuwapangia watu kitu cha kufanya. ccm inaendelea kuyeyuka mioyoni mwa wengi; huku upinzani ukizidi kuungwa mkono. Uwe unafikiri kwanza binti.
 
Back
Top Bottom