Wapinzani mna la kusema Uchaguzi wa Udiwani?

Mnyika,,,

Kama unavyofahamu mimi sio pendera fuata upepo,,,sikubali mambo kirahisi rahisi. Hebu naomba definition ya tume huru!!!

NB:
Remember Zanzibar walitafsiri tume huru kwa namna yao,,, Bunge la Jamhuri likatafsiri kwa namna nyingine,,,


Kilitime:

Tume Huru ni dhana pana. Ni zaidi ya kuwa na wapinzani katika Tume ya Uchaguzi. Nimeshawahi kuandika kuhusu suala hili- ukitaka kujua mtazamo wangu bonyeza hapa: http://www.chadema.net/habari/misc/misc_10.html

JJ

Maoni yangu ni pamoja na-

Tume ya uchaguzi si huru: Kwa nini?

Kwa mara ya tatu chini ya mfumo wa vyama vingi; Tume ya Uchaguzi ilisimamia na kuratibu uchaguzi mwaka 2005 kwa kutumia uzoefu ilioupata katika chaguzi za mwaka 1995 na mwaka 2000. Kwa ujumla Tume ya Uchaguzi iliendesha vizuri zaidi uchaguzi uliopita ukilinganisha na chaguzi zilizotangulia lakini bado mchakato wa uchaguzi haukukidhi vigezo vyote vya uchaguzi huru na haki.
i. Mifumo ya kisheria na kiuchaguzi kwa ajili ya uchaguzi na Muundo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Pamoja na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sheria mbalimbali zimekuwa zikisimamia uchaguzi hususani: Sheria ya Uchaguzi na. 1 ya mwaka 1985; Sheria ya Vyama vya siasa na. 5 ya mwaka 1992 na Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambazo zimetoa mamlaka kwa tume kusimamia na kuratibu uchaguzi ikiwemo kutoa maelekezo na taratibu mbalimbali.
Muundo wa Tume ulichukua mfumo ule ule ambao ulitumika katika uchaguzi mkuu 2005 unatokana na Katiba Kifungu 74(1) kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria na. 4 ya 1992 na Sheria na. 7 ya mwaka 1993; Tume inateuliwa na Rais(Katiba na Sheria husika zimeeleza sifa za wanaoweza kuteuliwa). Mkurugenzi wa Uchaguzi naye anateuliwa na Rais kwa mapendekezo ya Tume. Katiba kifungu 74 imebainisha majukumu ya Tume ya Uchaguzi. Vyama vya siasa viliendelea kudai tume huru ya uchaguzi wakati wa marekebisho ya 14 ya katiba yaliyofanyika karibu na uchaguzi mkuu. Hata hivyo suala la muundo wa tume huru ya uchaguzi halikujadiliwa wala kuingizwa kama sehemu ya marekebisho hayo. Matokeo yake maandalizi ya uchaguzi yalifanywa na tume ile ile ambayo ilisemwa kipindi chote kwamba haiko huru. Kamati mbalimbali ziliundwa na kufanya kazi kipindi cha uchaguzi pekee.


Nini kifanyike ili pawe na Tume huru:

Pawepo na Sheria ya Tume ya Uchaguzi ili kuipa uhuru na mamlaka zaidi tume ya uchaguzi kama ilivyo katika nchi kadhaa za Kusini mwa Afrika.(Pendekezo hili limetolewa pia na Tume ya Uchaguzi na Vyombo mbalimbali vya Ufuatiliaji/Uangalizi wa uchaguzi)
Kamati za Tume ziwe ni za kudumu; ziendelee na kazi hata baada ya uchaguzi. Vitengo vya TEKNOHAMA (ICT) na Elimu ya Uraia view sehemu ya vitengo vya kudumu vya Tume.
Katiba na Sheria vifanyiwe mabadiliko/marekebisho ili kutoa uhuru na mamlaka ya Tume ya Uchaguzi wa Kuzingatia vigezo vya Kanuni/Matamko na Misingi mbalimbali ya Uchaguzi ya Kimataifa ambayo taifa letu limeridhia. Baadhi ya masuala mahususi ni pamoja na: Tume iwe nje ya mfumo wa kiutendaji wa kiserikali(Watendaji wa Serikali kama Wakurugenzi na Watendaji wa Kata wasiwe watumishi wa Tume ya uchaguzi hata wakati wa uchaguzi); Wajumbe wa Tume wachaguliwe kwa mashauriano na Wadau wengine vikiwemo vyama vya siasa na baadaye wathibitishwe na Bunge; Utumishi wa Wajumbe waandamizi wa Tume wa ulindwe(durability and security of tenure) kisheria na kikatiba kama walivyo majaji; Uwakilishi wa Tume uzingatie jinsia, uwakilishi wa kijamii na makundi rika; Tume ya Uchaguzi iwajibike kwa Bunge badala ya Kuwajibika kwa Serikali; Tume ya Uchaguzi iwe na Bajeti inayojitegemea itakayopitishwa moja kwa moja na Bunge.
ii. Rasilimali kwa ajili ya usimamizi wa uchaguzi na Usimamizi wa Uchaguzi
Tofauti na chaguzi za 1995 na 2000, katika uchaguzi mkuu 2005 fedha za uchaguzi kwa ajili ya shughuli za uendeshaji wa Tume ya Uchaguzi zilitolewa katika wakati mwafaka na sehumu kubwa zilitolewa na serikali. Kupungua kwa utegemezi kwa wahisani katika kutoa fedha za kusimamia uchaguzi pamoja na kutoa fedha mapema vilisaidia kuboresha uendweshwaji wa uchaguzi.
Uhusiano katika ya vyama vya siasa na Tume ya Uchaguzi katika ngazi ya Taifa ulikuwa mzuri; vyama vilialikwa katika vikao mbalimbali na vilikuwa na wajumbe katika kamati mbalimbali za tume ya Uchaguzi. Hata hivyo, malalamiko yametolewa baadhi ya maeneo hususani yale yaliyokuwa na upinzani mkali kwamba vyama havikushirikishwa ipasavyo na watendaji wa tume ya taifa ya uchaguzi ngazi ya wilaya, majimbo na kata. Wakati wa kampeni watendaji hawa wameonekana kuegemea chama tawala. Hali hii iliendelea katika maeneo mengi hata katika hatua za kuhesabu kura, kujumlisha kura na kutangaza matokeo hususani katika ngazi za majimbo. Katika mfumo wa tume hakuna utenganisho kati ya usimamizi na utekelezaji katika muundo wa tume ngazi za chini ya makao makuu ya tume. Uteuzi wa watendaji wa chini ulifanywa na wasimamizi wa uchaguzi ambao ni watekelezaji(ambao walikuwa ni watumishi wa serikali) badala ya chombo huru cha kusimamia uchaguzi hivyo walitumiwa na dola kupika ama kuchezea matokeo.
Tume ya Uchaguzi iwe na watendaji wa Kudumu katika ngazi mbalimbali; utaratibu wa kuwatumia maofisa wa serikali kama wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi usitishwe.
 
Yes, haitoshi lakini tumepiga hatua sana. Ndiyo nikasema jana kuwa wakati mwingine ukiangalia tu jinsi safari ilivyo bado ndefu bila kuangalia ulipotoka utakosa taswira kamili. Leo hii kama wapinzani wanaweza kupata viti 4 kati ya 11 vilivyokuwa vinagombaniwa, is a big step by any standard. Tukumbuke huko nyuma wapinzani walikuwa wanaweza kupata pengine kiti 1 au 2 kati ya mamia.

That said, bado tunahitaji kufanya bidii zaidi na kutumia vizuri good will ambayo upinzani umeipata kutoka kwa jamii. Na tusikubali tena kuwaachia ccm wapite bila kupingwa, huu ni uzembe ambao lazima tukubali kuwajibike nao na tukitaka kuwa serious kuna watu wanapaswa kuwajibika ikiwemo kuwafukuza uwanachama wale waliotusaliti kwa kurubuniwa na CCM hata wasirudishe fomu au kufanya other technical errors. Tuanze kuwajibishana, yeyote anayetaka kuwa na sisi ajue we are in a serious business.

CCM are now very shaky; they are defeatable even under the present poor democratic state of affair. We can do it, lets play our cards well!
 
hONGERENI WAPINZANI KWA KUANZA KUWAONDOA HAO ccm MIJINI KWANI MATOKEO YANAONYESHA KUWA MMEWASHINDA VITI VYOTE VILIVYOKUWA MIJINI.

hII NI DALILI YA KUNGUKA KWA ccm KWANI KUSHINDWA MIJINI SIO DALILI NJEMA KWA CHAMA TAWALA .

ANGALIENI HISTORIA KILICHOTOKEA KENYA, MALAWI, ZAMBIA, N'K.
 
CCM are now very shaky; they are defeatable even under the present poor democratic state of affair. We can do it, lets play our cards well!

Mawazo Mazuri,

Lakini lazima pia tuangalie upande mwingine, kuna wakati waliopita ni kwa sababu ya uwezo wao zaidi kuliko vyama vyao vya siasa,,,

Nitakupa mfano; Zitto akisimama kule Kigoma hata bila chama anapita!!!

Kwa hiyo liangalieni hili, wananchi wako makini siku hizi,,, sasa mkiamini wako makini tu kuikataa CCM mmeliwa... wekeni wagombea wazuri,,, kazi itakuwa rahisi.
 
Mawazo Mazuri,

Lakini lazima pia tuangalie upande mwingine, kuna wakati waliopita ni kwa sababu ya uwezo wao zaidi kuliko vyama vyao vya siasa,,,

Nitakupa mfano; Zitto akisimama kule Kigoma hata bila chama anapita!!!

Kwa hiyo liangalieni hili, wananchi wako makini siku hizi,,, sasa mkiamini wako makini tu kuikataa CCM mmeliwa... wekeni wagombea wazuri,,, kazi itakuwa rahisi.

Kilitime:

Nakubaliana nawe katika hili.

Ili chama kishinde uchaguzi kinahitaji mambo manne yanayofuatana kwa kadiri ya umuhimu.

Mosi, Mgombea Bora sio bora mgombea.

Pili; ajenda/sera- nini haswa ambacho wanataka kukifanya; kinafaa kiwaguse wananchi.

Tatu; oganizesheni-netweki ya kichama na hata ya kijamii pamoja na mifumo ya mawasiliano.

Nne; Fedha na rasilimali zingine, ni matokeo ya hayo matatu ya kwanza.

JJ
 
Ndugu zangu tusipoteze muda na hawa kina dada mtu wa pwani na kundi lake. Lengo lao kubwa ni kututoa kwenye mada tata na muhimu kwa taifa letu na kutuingiza huku na inaonekana wameanza kufanikiwa kwa sababu kila mmoja anataka kuwajibu pamoja na mtazamo wao finyu sana wa kutoa hoja.

Ombi langu waopendwa tulipendalo taifa hili chonde tusiingie mtego wa hawa jamaa. Mtu wa pwani ukiangalia pattern yake yuko hapa JF 24 hrs ikimaanisha hana cha kufanya lakini watu wengi humu wana muda maarumu wa kuingia.
 
Mtu wa Pwani:

.....chenga twawala!

Kabla ya Mechi(Ushindi wa mezani). Upinzani( TLP, chunya)-1 CCM 5(tulianza kushinda bao la mwanzo mwanzo kabisa, halafu yakatokea ya wapinzani kujitoa kiasi kikubwa wagombea wa CUF). Hapa kuna uzoefu fulani fulani tumeupata kwa chaguzi zijazo).

Mechi ilipoanza mpaka kipindi cha mwisho: Upinzani 3( TLP Sombetini, CHADEMA Songea Mjini na Kabwe) CCM 6( hii ni sawa na asilimia 50%; ni mwanzo mzuri kwamba chama tawala kinaweza kushindwa nusu ya uchaguzi wa moja kwa moja! Tena tukiwashinda mijini!, ni mwanzo mzuri wa ushirikiano).

Uchambuzi huu nimeufanya nikiwa sifahamu matokeo ya kata mbili- moja ni ya Moshi Vijijini(Vunjo) ambao uchaguzi umepangwa novemba. Na moja sifahamu matokeo yamekuwa nini huku kijijini nilipo).

Swala la kupoteza mbili. Ni kweli tunapaswa kuongeza nguvu zaidi katika kulinda goli letu. Lakini tumepoteza mbili, tumeongeza nne. Hivyo ni kama hatujapoteza ila tumeongeza mbili. Kama unatumia kigezo cha kuongeza namba na si kulinda maeneo. Hata hivyo, ni vyema upinzani tukaendelea kulinda kwa nguvu zote maeneo tunayoshinda.

Ila mechi ilikuwa nzuri, ni mwanzo mzuri. CCM ilipeleka mziki mkubwa ikiwemo mawaziri lakini bado wamehema.

Sasa tusubiri uamuzi wa mahakama, uchaguzi ukirudiwa- Mambo yatakuwaje?

Natabaruku, bado niko msamvu

JJ

Kwi kwi kwi kwi!!!! Mnyika bwana!

Hayo mahesabu yako babu kubwa. Kuna jamaa secondary school aliwahi kutumia assumptions nyingi, na kufanya kila kitu negligible mpaka akaja kwenye jibu alilokuwa analitaka yeye, of course alipata zero mark.

Kubalini tu mmeshindwa. Siku ya mwisho mungemwaga viongozi wenu wakuu huko vijijini, huenda mungepata jimbo moja au mawili zaidi. Jifunzeni jamani, kura ziko vijijini, nendeni hata huko vinginevyo, CCM watachukua kura zote za vijijini na mtagawana nao za mjini, matokeo wao 75%, upinzani 25%.
 
Kwi kwi kwi kwi!!!! Mnyika bwana!

Hayo mahesabu yako babu kubwa. Kuna jamaa secondary school aliwahi kutumia assumptions nyingi, na kufanya kila kitu negligible mpaka akaja kwenye jibu alilokuwa analitaka yeye, of course alipata zero mark.

Kubalini tu mmeshindwa. Siku ya mwisho mungemwaga viongozi wenu wakuu huko vijijini, huenda mungepata jimbo moja au mawili zaidi. Jifunzeni jamani, kura ziko vijijini, nendeni hata huko vinginevyo, CCM watachukua kura zote za vijijini na mtagawana nao za mjini, matokeo wao 75%, upinzani 25%.

Teh teh teh teh

Hatma ya mapambano yote ya kuchukua dola ni mijini. Ukiikamata Dar es salaam hivi sasa kisawa sawa; huko kwingine kote kunafuata.

DSM asilimia kumi ya watanzania

DSM ndipo wagombea wengi hususani wa ubunge wanatoka

DSM inawatu ambao ndio wanaoathiri siasa za vijijini walipotoka.

DSM ndio Ikulu ilipo.

DSM ina vyombo vya habari vingi vya Kitaifa

DSM ina makao makuu ya vyama na taasisi za kitaifa na kimataifa kwa wingi zaidi.

DSM ndio mapambano ya kumwondoa mkoloni yaliposhikia kasi.

DSM ndipo makao makuu ya vyombo vingi vya dola.

Nimetumia DSM kuonyesha jinsi miji ilivyo ya muhimu.

Lakini hii haimaanishi hatutambui uhuhimu wa vijijijini- halmashauri zote ambazo CHADEMA ni chama tawala ni za vijijini.

We are struggling to do it both ways my brother.

Pamoja tutashinda

JJ
 
Mawazo Mazuri,

Lakini lazima pia tuangalie upande mwingine, kuna wakati waliopita ni kwa sababu ya uwezo wao zaidi kuliko vyama vyao vya siasa,,,

Nitakupa mfano; Zitto akisimama kule Kigoma hata bila chama anapita!!!

Kwa hiyo liangalieni hili, wananchi wako makini siku hizi,,, sasa mkiamini wako makini tu kuikataa CCM mmeliwa... wekeni wagombea wazuri,,, kazi itakuwa rahisi.

Hasa! Na wagombea wazuri watapatikana kama watu makini kama wewe watajiunga na upinzani!
 
Teh teh teh teh

Hatma ya mapambano yote ya kuchukua dola ni mijini. Ukiikamata Dar es salaam hivi sasa kisawa sawa; huko kwingine kote kunafuata.

DSM asilimia kumi ya watanzania

DSM ndipo wagombea wengi hususani wa ubunge wanatoka

DSM inawatu ambao ndio wanaoathiri siasa za vijijini walipotoka.

DSM ndio Ikulu ilipo.

DSM ina vyombo vya habari vingi vya Kitaifa

DSM ina makao makuu ya vyama na taasisi za kitaifa na kimataifa kwa wingi zaidi.

DSM ndio mapambano ya kumwondoa mkoloni yaliposhikia kasi.

DSM ndipo makao makuu ya vyombo vingi vya dola.

Nimetumia DSM kuonyesha jinsi miji ilivyo ya muhimu.

Lakini hii haimaanishi hatutambui uhuhimu wa vijijijini- halmashauri zote ambazo CHADEMA ni chama tawala ni za vijijini.

We are struggling to do it both ways my brother.

Pamoja tutashinda

JJ

Saana tu. Na kote upinzani ulipopata nguvu na hatimaye kushinda walianza kwanza kushinda mijini. Mifano ipo tele, na sisi hatuwezi kuwa kisiwa. Ni muhimu sana kukamata town.
 
"CCM CHAMA CHA KIMAPINDUZI
IMARA DAIMA KINA CHAPA KAZI"

hivi hayo maneno umeyatoa wewe mtu wa pwani?

mimi napata shida kuelewa huo uimara wa SISIEM, ni rushwa? ufisadi? au? maana kama ni maendeleo hakuna zaidi ya maneno ya mdomoni, viongozi wote wa SISIEM siku hizi kazi zao wanazifanyia mdomoni kwa kuongea na sio vitendo, mmesababisha imekuwa BORA MAISHA kwa kila mmtanzania tofauti na ahadi yenu ya MAISHA BORA kwa kila mtanzania.

ukiniambia kuwa SISISEM ni imara katika rushwa na ufisadi nitakubaliana na wewe
 
Hasa! Na wagombea wazuri watapatikana kama watu makini kama wewe watajiunga na upinzani!


Kitila,

Unajua kwenye gurudumu la maendeleo kila mtu/mwananchi atakuwa anafanya sehemu fulani tu, hatuwezi fanya wote sehemu moja kwa wakati mmoja,,,

Katika hiyo sehemu yangu haitakuwa kwa kuwa mwanachama wa upande wowote, lakini kura nitapiga siku zote;;; na kwangu kwa wagombea wa Udiwani, Ubunge na Rais, nitaanza na uwezo wa mtu, then Chama Chake...

Na sehemu yangu ya pili ni kuwaunga mkono, na kuwapa moyo wenye uwezo kama wewe,,, na kuwa-discourage wasiokuwa na uwezo hata kama wako kwenye chama tawala au Pinzani...

Kwa hiyo sina mambo ya jumla jumla, i'm going to specifics,,, kwa mfano siunge mkono kwamba CCM ni Mafisadi, lakini naamini CCM kuna mafisadi.. Siungi Mkono kwamba CHADEMA inaweza kukamata nchi 2010, na kama naamini hivyo natakiwa kuwaamini pia kwamba serikali ya CHADEMA itakuwa na mafisadi kibao, maana mafisadi ndio wana uwezo wakuangalia nyakati,,, wakiona jahazi la CCM linazama wataondoka wote kwenda CCM,,, fisadi au mafia hana itikadi ndugu yangu...

Ila nakukubali ndugu yangu Kitila, lakini piganeni kwa mkakati,,, msipende ushindi rahisi, mtapoteza pia kirahisi... Msisherehekee ushindi kama wa Taifa stars,,, maana mtaaibika kwenye uwanja wenu wa nyumbani...Msipende sifa zisizokuwa na base maana base ikilegea tu mtashuka kwa kasi ya kishindo...
 
kwa watu kama mtu wa pwani kwao CHAMA ni muhimu kuliko TAIFA..yaani hata akisikia pesa yote hazina imekombwa kusaidia CCM ishinde uchaguzi hata wa madiwani..na nchi imebaki kaputi hatuwezi kununua hata CHANJO yeye anaona sawa tu....

hivi mtu wa pwani unajua kwa mara ya kwanza tangu uhuru taifa limekubwa na uhaba mkubwa wa CHANJO za watoto wadogo?????
 
Saana tu. Na kote upinzani ulipopata nguvu na hatimaye kushinda walianza kwanza kushinda mijini. Mifano ipo tele, na sisi hatuwezi kuwa kisiwa. Ni muhimu sana kukamata town.

Mimi nimefurahia matokeo ya Songea mjini-Majengo. Ndiko ku-nyumba. Hilo ni onyo! Nchimbi angalia ubunge wako mwaka 2010. Natumaini wapinzani wataiondoa sisi M kwenye ubunge.
 
gademu, walikuwa na viti 6 before, na sasa 3 ?????????????

mpo wapi nyie wapinzani tawi la JF ????

mbona siwasikii, !!

yuko wapi, yuko wapi, yule pale KIKWETEEEEE.
Tumsindikizeni Dodoma, kada wetu wa ccm !
apewe kura za NDIOOOOOOOOOOOOOOOOOO !!

<<Huku pembeni wazee kuanzia Malecela, AlHaji Mwinyi, Mkapa, Kingunge, Frederick Suamye,Karume, Dr. Shein na wengineo weeengi walitinga mashati ya kung'aa ya kijani kibichi wakimsindikiza Kada wa CCM Dodoma, makao makuu ya CCM kuchukua fomu>>*CCM ilionyesha umoja wa hali ya juu ukizingatia tofauti zao za kisera*najua ntatibua watu* lakini hawakuwa na ubinafsi )

(ASIKWAMBIE MTU BANA HAPO NDIO PATAMU, )

Napenda kumnukuu member mmoja, aliyesema changes zitonekana kwenye ballots, na sasa kweli zinaonekana !!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom