Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,991
Magufuli hataki kabisa kukosolewa. Amehakikisha anakwibavkura ili wabunge woooote wanaomkosoaga wasirudi bungeni. Magazeticmengi yamefutwa kabisa, na yaliyopo yanapigwacfaini kubwavna maonyo makali kila uchao. Mbowe kaongea sana tu, ona walivyoripoti kwa woga. Tundu Lissu ndio usiseme. Usijali hata hivyo, nondo zitakuja tu. Ulionavjinsi Mbowe alivyotupia za usoni? Yajayo yanafurahisha. Vuta subiraKuna mwaka niliwahi kukutana na mzee mmoja alikuwa akisoma gazeti la Mwanahalisi, kipindi lipo hot kuibua ufisadi na madudu ya awamu ya nne.
Mimi kama mtu mdadisi nilimuuliza swali moja, mzee samahani, sikujui lakini samahani hawa jamaa wa Mwanahalisi wanapata wapi hizi tips na kulipua haya madudu. Madudu ambayo ni ukweli mtupu! Yule mzee alinijibu jibu moja tu kuwa hawa Mwanahalisi wanatoa picha ya jinsi nchi ilivyo.
Wapinzani mbona mpo kimya au bado mnatafakari jinsi Uchaguzi ulivyowatupa kombo?
Tupeni picha ya nchi,kuna ufisadi? Je kuna ubadhirifu?
Jamani kukosa wabunge isiwe sababu ya kukaa kimya. Kama kuna uozo mtuambie.