Wapinzani kumwomba radhi JK

Zee la shamba

Member
Oct 17, 2007
55
3
Vyama vinne vya upinzani vilivyoanzisha ushirikiano, vinafanya utaratibu wa kumuomba radhi Rais Jakaya Mrisho Kikwete kutokana na kitendo chao cha kumuweka katika orodha ya mafisadi iliyotolewa katika viwanja vya Mwembe Yanga mapema mwezi uliopita.

Habari ambazo Rai imezipata kutoka kwa baadhi ya viongozi wa upinzani, zinaeleza kwamba kimsingi vyama hivyo vimegundua kwamba yalikuwa ni makosa ya kimkakati kumtaja Rais katika tuhuma hizo kwa sababu tuhuma walizotoa juu yake ni nyepesi.

Rai imeelezwa kwamba iwapo mambo yatakwenda vizuri, wataifanya kazi hiyo siku ya Jumamosi kwa kumuomba radhi rasmi Kikwete ikiwa ni pamoja na watu wengine wawili. Rai haikufanikiwa kupata jina la mtu wa tatu lakini mtu wa pili ameelezwa kuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Patrick Rutabanzibwa.

Katika tuhuma zilizosomwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Wilbroad Slaa, wapinzani walisema kuwa pamoja na mambo mengine, Agosti mwaka 1994, Kikwete aliingia katika mkataba na kampuni ya madini ya Kahama Mining Corporation Ltd.

Tuhuma hizo zilieleza kwamba ingawa mkataba ulionyesha kuwa ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation walivamia eneo la Bulyanhulu, na kuwaondosha kwa nguvu watu waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baadaye Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada.

Mmoja kati ya viongozi wa kambi ya upinzani, ameiambia Rai kwamba baada ya kuangalia athari za tuhuma dhidi ya rais, wamegundua kwamba hilo lilikuwa kosa la kimkakati.

“Strategically hilo lilikuwa kosa kumtaja Rais. Pia tuhuma dhidi yake zilikuwa nyepesi sana. Tunamtoa rais na wengine wawili, lakini tunaongeza wapya. Oktoba 27 tutamtoa na kumuomba radhi,” alisema kiongozi huyo ambaye hata hivyo hakutaka jina lake litajwe.

Soorce Rai
 
Mmoja kati ya viongozi wa kambi ya upinzani, ameiambia Rai kwamba baada ya kuangalia athari za tuhuma dhidi ya rais, wamegundua kwamba hilo lilikuwa kosa la kimkakati.

Huu ni udaku, jukwaa la siasa sio mahali pake. Kwani kiongozi wa upinzani aliyeonea na rai hana jina?
 
Vyama vinne vya upinzani vilivyoanzisha ushirikiano, vinafanya utaratibu wa kumuomba radhi Rais Jakaya Mrisho Kikwete kutokana na kitendo chao cha kumuweka katika orodha ya mafisadi iliyotolewa katika viwanja vya Mwembe Yanga mapema mwezi uliopita.

Habari ambazo Rai imezipata kutoka kwa baadhi ya viongozi wa upinzani, zinaeleza kwamba kimsingi vyama hivyo vimegundua kwamba yalikuwa ni makosa ya kimkakati kumtaja Rais katika tuhuma hizo kwa sababu tuhuma walizotoa juu yake ni nyepesi.

Rai imeelezwa kwamba iwapo mambo yatakwenda vizuri, wataifanya kazi hiyo siku ya Jumamosi kwa kumuomba radhi rasmi Kikwete ikiwa ni pamoja na watu wengine wawili. Rai haikufanikiwa kupata jina la mtu wa tatu lakini mtu wa pili ameelezwa kuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Patrick Rutabanzibwa.

Katika tuhuma zilizosomwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Wilbroad Slaa, wapinzani walisema kuwa pamoja na mambo mengine, Agosti mwaka 1994, Kikwete aliingia katika mkataba na kampuni ya madini ya Kahama Mining Corporation Ltd.

Tuhuma hizo zilieleza kwamba ingawa mkataba ulionyesha kuwa ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation walivamia eneo la Bulyanhulu, na kuwaondosha kwa nguvu watu waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baadaye Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada.

Mmoja kati ya viongozi wa kambi ya upinzani, ameiambia Rai kwamba baada ya kuangalia athari za tuhuma dhidi ya rais, wamegundua kwamba hilo lilikuwa kosa la kimkakati.

“Strategically hilo lilikuwa kosa kumtaja Rais. Pia tuhuma dhidi yake zilikuwa nyepesi sana. Tunamtoa rais na wengine wawili, lakini tunaongeza wapya. Oktoba 27 tutamtoa na kumuomba radhi,” alisema kiongozi huyo ambaye hata hivyo hakutaka jina lake litajwe.

Soorce Rai

List inapungua taratibu, kinachohitajika sasa hivi ni kuwa karibu na viongozi wetu wa serikali kuanzia ngazi za chini hadi za juu wakiwemo viongozi wa vyama vya upinzani na wa vyama tawala kukaa meza moja na kuanza kuchapa kazi ili kuleta maendeleo katika taifa letu na sio kupiga kelele za vyama vya siasa maana hizo kelele zishapigwa sana tokea mfumo wa vyama vya siasa ulipoanzishwa hadi sasa, hivyo ukaribu wa vyama vyooote vya siasa kuanzia upinzani hadi wa vyama tawala wakae pamoja na kuandaa mikakati ili kuleta maendeleo na kelele za vyama vya siasa zianze pale wakati wa kampeni !
 
Hivi RA ana share ngapi vile ndami ya Rai ? This is a true spinning

Nakuunga mkono.Hata mie naweza kukurupuka usingizini kisha nikaja na headline "JK AAMURU WALA RUSHWA WOTE WARIPOTI SEGEREA KWA HIARI YAO WENYEWE,IKULU IMESHAANDAA USAFIRI..." na si ajabu wazembe wa uchambuzi na mantiki wakaamini porojo hiyo.

Lakini mie nakwenda mbali zaidi ya hapo.Sidhani kwamba m-babaishaji aliyetoa stori hiyo kwenye Rai (licha ya gazeti hilo kumilikiwa na RA) alifanya hivyo kwa utashi wake tu.Jana tumesoma stori za "KUNG'ARA KWA KIKWETE DUNIANI".Sintoshangaa kuskia kuwa kuna ka-kitengo kalikoandaliwa fungu zuri tu ambako kana jukumu la propaganda beyond zile za kina Makamba,Mwanri,etc.

Kazi kwao walio wavivu wa ku-read between lines.
 
lakini habari ile ile ya mafisadi ingetolewa kwenye hili gazeti sidhani kama kuna yeyote angetokea kuhoji haya !
 
lakini habari ile ile ya mafisadi ingetolewa kwenye hili gazeti sidhani kama kuna yeyote angetokea kuhoji haya !

Lakini usisahau kwamba ni ukweli usiofichika RAI haliwezi kutoa habari kama ile labda kama likiwa linamilikiwa na mtu mwingine tofauti na RA.
 
and the point is .... maana sasa hapa naona anayeongelewa ni mwenye gazeti (angalau sina uhakika) na sio gazeti lenyewe !
 
List inapungua taratibu, kinachohitajika sasa hivi ni kuwa karibu na viongozi wetu wa serikali kuanzia ngazi za chini hadi za juu wakiwemo viongozi wa vyama vya upinzani na wa vyama tawala kukaa meza moja na kuanza kuchapa kazi ili kuleta maendeleo katika taifa letu na sio kupiga kelele za vyama vya siasa maana hizo kelele zishapigwa sana tokea mfumo wa vyama vya siasa ulipoanzishwa hadi sasa, hivyo ukaribu wa vyama vyooote vya siasa kuanzia upinzani hadi wa vyama tawala wakae pamoja na kuandaa mikakati ili kuleta maendeleo na kelele za vyama vya siasa zianze pale wakati wa kampeni !

Tutakuwa tunadanganyana kama kelele za rushwa zikipuuzwa, No dout rushwa na ufisadi ni matatizo yanayokwamisha maendeleo yetu Tanzania, hiyo inayosemwa kuwa ni kosa la kimkakati naweza kuiita ni kosa lenye manufaa, a blessing in disguise. Na ikizingatiwa kuwa imetoka kwenye gazeti la RAI uchwara, siipi uzito wowote. Sikubaliani na hii na siamini kama kweli tuhuma kama hizi zinakwamisha maendeleo, tukiwa na opposition ambayo ni faithful kwa taifa no doubt kutakuwa na maendeleo.
 
and the point is .... maana sasa hapa naona anayeongelewa ni mwenye gazeti (angalau sina uhakika) na sio gazeti lenyewe !

Mwenye gazeti anatoa maamuzi ni kitu gani kiandikwe kwenye magazeti yake. Ndiyo maana kwenye RAI huwezi kuona habari za ufisadi, wala rushwa, mikataba mibovu na viongozi wanaojilimbikizia mali ambalo ni gumzo katika kila kona ya nchi yetu. Angewapa uhuru waandishi wa gazeti hilo basi hayo pia tungeyaona kwenye RAI.
 
ni kheri nisome magazeti ya udaku kuliko kusoma RAI,hilo gazeti lilishakufa zamani sana,sidhani kama lina wasomaji tena.
 
List inapungua taratibu, kinachohitajika sasa hivi ni kuwa karibu na viongozi wetu wa serikali kuanzia ngazi za chini hadi za juu wakiwemo viongozi wa vyama vya upinzani na wa vyama tawala kukaa meza moja na kuanza kuchapa kazi ili kuleta maendeleo katika taifa letu na sio kupiga kelele za vyama vya siasa maana hizo kelele zishapigwa sana tokea mfumo wa vyama vya siasa ulipoanzishwa hadi sasa, hivyo ukaribu wa vyama vyooote vya siasa kuanzia upinzani hadi wa vyama tawala wakae pamoja na kuandaa mikakati ili kuleta maendeleo na kelele za vyama vya siasa zianze pale wakati wa kampeni !

Kadakadakada!

Usijimalize kwa udaku

Halafu CCM ya MAFISADI wako Tayari kuleta maendeleo Tanzania? Je ulisoma Mkataba wa BUZWAGI, ukiambiwa uliandikiwa pale darajani MAnzese utakataaa? Tuachane na propaganda za Rai na RA.Hakuna wa kumwomba radhi JK ni ndoto tu, mwambie afanye aliyoyaahidi.
 
Kumbukeni habari ya kwamba Mzee Mtei alipingana na hoja ya Kabwe kwa sababu hata yeye alisaini Mjini Perking, Mzee Mtei alikuja kukanusha. Wakaandika tena kwamba Jaji Mark Bomani amwmwonya Dr. Slaa kuhusu madai yake ya ufisadi, akakanusha.

Hata hii naamini ndani ya moyo wangu kwamba ni miongoni mwa jitihada zile zile za kuisafisha serikali. Lakini viongozi wa upinzani watoe tamko kuliweka jambo hili sawa.
 
Hawahitaji kutoa tamko lolote, watu wasubiri hayo yatakayosemwa. Nimbehatika kuyaona kwa mbali, kama ni movie basi orodha ya mafisadi ilikuwa Preview...
 
Kumbukeni habari ya kwamba Mzee Mtei alipingana na hoja ya Kabwe kwa sababu hata yeye alisaini Mjini Perking, Mzee Mtei alikuja kukanusha. Wakaandika tena kwamba Jaji Mark Bomani amwmwonya Dr. Slaa kuhusu madai yake ya ufisadi, akakanusha.

Hata hii naamini ndani ya moyo wangu kwamba ni miongoni mwa jitihada zile zile za kuisafisha serikali. Lakini viongozi wa upinzani watoe tamko kuliweka jambo hili sawa.

Mwigamba,

ukisoma hii habari ambayo kama kawaida imepikwa na spin master mwenyewe - mkoloni, mwizi, na mkwepa kodi Rostam Aziz - utaona kuwa hakuna jina la kiongozi yeyote limetajwa kuwa ametoa hilo tamko.

Nani atakanusha kitu ambacho hakusema au hausiki nacho?
 
Kadakadakada!

Usijimalize kwa udaku

Halafu CCM ya MAFISADI wako Tayari kuleta maendeleo Tanzania? Je ulisoma Mkataba wa BUZWAGI, ukiambiwa uliandikiwa pale darajani MAnzese utakataaa? Tuachane na propaganda za Rai na RA.Hakuna wa kumwomba radhi JK ni ndoto tu, mwambie afanye aliyoyaahidi.

umeelewa nilichosema ?? tatizo ni kwamba RA amewakaa mbele, hivi ushawahi kunisikia nikimtaja huyo RA kwenye post yoyote kumrefer ? unless mmemtaja then hapo ndipo nami nitamtaja lakini siangalii ccm wala wapinzani na hicho ndicho ninachosema hapa kila siku !
 
Nadhani ndio kwanza wakuu mtakuwa mnamjenga huyo RA baada ya kumbomoa regardless na hizo accusations ! (simtetei mtu) bali thats how i see it !
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom