Idugunde
JF-Expert Member
- May 21, 2020
- 6,273
- 6,637
Kuna mambo mengi yanaweza kufanya wapinzani hapa nchini mpaka kujenga upya imani kwa wananchi. Hili la kushadidia mkuu wa dola anaumwa au haonekani halina mantiki
Nimeangalia kwa ukaribu matamko ya ACT Wazalendo na Chadema yote kimsingi ni porojo ambazo hazina mashiko. Maana kuanza kuhubiri kuwa nani anatakiwa ashike mikoba ya Rais wakati hamna uhakika kama anaumwa au haumwi ni kukosa fikra pevu za kisiasa. Maana kama kutoonekana ni tatizo tayari mmeshapata majibu toka kwa wasaidizi wake.
Ninyi kama mna busara za kisiasa mnatakiwa muipeleke mchakamchaka hii serikali ya CCM iweze kujibadili, ajira ziwepo, sekta binafsi zipate uhai na hujuma kwa wajasiriamali wadogo zisiwepo. Tena muwe na hoja mujarabu ambazo zitasababisha mujenge imani tena kwa wananchi.
Kudandia matukio kama haya ambayo yameshapoa ni kupoteza muda wa kisiasa.
Nimeangalia kwa ukaribu matamko ya ACT Wazalendo na Chadema yote kimsingi ni porojo ambazo hazina mashiko. Maana kuanza kuhubiri kuwa nani anatakiwa ashike mikoba ya Rais wakati hamna uhakika kama anaumwa au haumwi ni kukosa fikra pevu za kisiasa. Maana kama kutoonekana ni tatizo tayari mmeshapata majibu toka kwa wasaidizi wake.
Ninyi kama mna busara za kisiasa mnatakiwa muipeleke mchakamchaka hii serikali ya CCM iweze kujibadili, ajira ziwepo, sekta binafsi zipate uhai na hujuma kwa wajasiriamali wadogo zisiwepo. Tena muwe na hoja mujarabu ambazo zitasababisha mujenge imani tena kwa wananchi.
Kudandia matukio kama haya ambayo yameshapoa ni kupoteza muda wa kisiasa.