Wapigania uhuru wa Zanzibar waungwe mkono!

Maswali yako hayatajibiwa kwasababu WZN hawana majibu. Jibu moja rahisi tunataka muunga
1.jpg
no wa mkataba.

Kwani Muungano mlionao sasa wa Tanganyika na Zanzibar ni wa aina gani?

 
Mwanakijiji.

kama kupe huyo pamoja na kubebwa kote huko lakin anakuwa mlalamishi KWANINI USIMTOSE?

Lakin kuna suala dogo nitaka kukuuliza.

Je kama kunatokea maasi upande wa Tanganyika kwa kuwafukuza waZnz, je Znz itakuwa na ubavu wa kutoa majeshi kwenda kuzuia maasi hayo.


of course isingeweza; lakini Zanzibar ilipokuwa huru na majeshi yake na kila kitu chake iliomba Tanganyika msaada wa kutuliza mapinduzi! Zanzibar hata ikiwa na kila kitu chake na vifaru vyake si tishio kwa namna yoyote kwa Tanganyika. Ila Tanganyika itaendelea kuweka kivuli Zanzibar (iwe ndani ya Muungano au nje).
 
of course isingeweza; lakini Zanzibar ilipokuwa huru na majeshi yake na kila kitu chake iliomba Tanganyika msaada wa kutuliza mapinduzi! Zanzibar hata ikiwa na kila kitu chake na vifaru vyake si tishio kwa namna yoyote kwa Tanganyika. Ila Tanganyika itaendelea kuweka kivuli Zanzibar (iwe ndani ya Muungano au nje).
Jusa amekiri hili katika kongamano la Jumamosi.Ametamaka kwa kinywa mbele ya kadamnasi kuwa kijiografia, kindugu, kiuchumi na kiusalama ZNZ inaiihitaji Tanganyika.! Big confession of the year
 
Kwani Muungano mlionao sasa wa Tanganyika na Zanzibar ni wa aina gani?

Muungano wa kikatiba.
Another confession from Baru baru kuwa huu ni mkataba. For so long amekuwa katika denial state but now we're on the same page. ZNZ haihitaji mkataba mwingine kabla ya kuvunja uliopo.
 
Muungano wa kikatiba.
Another confession from Baru baru kuwa huu ni mkataba. For so long amekuwa katika denial state but now we're on the same page. ZNZ haihitaji mkataba mwingine kabla ya kuvunja uliopo.

Nguruvi3.

Ndio maana nakwambia huujui hata kidogo muungano wenu ni wa aina gani na ndio maana kila wakti unakuwa mtu wa kupinga.

Ngoja nikudarsishe kidogo hapa kuhusu muungano wenu.

Kwa kukusaidia Ahali yangu Muungano wenu SIO WA KIKATIBA BALI NI MUUNGANO WA MKATABA. Kwani kila nchi ina Katiba yake na sharia zake za ndani isipokuwa kwa mambo yale tu mliokubaliana katika MKATABA wenu ya kushirikiana. Na mambo yenyewe nakuwekea hapa chini kwa faida yako na wale wenzako wasioyajua.

The initial Union Matters included the following eleven areas as Union matters:
·
The constitution and government of the United Republic;
· External affairs;

· Defense;

· Police;

· Emergency powers;

· Citizenship;

· Immigration;

· External trade and borrowing;

· The Public service of the United Republic;

· Income tax, corporation tax, customs and excise duties,and

· Harbours, civil aviation, posts and telegraph.


Between 1964-1977
: through an amendment of the Interim
Constitution which had reproduced the list of union matters and not

an amendment of Acts of Union, new items were added to the list of

Union matters giving the Union parliament and executive more Powers.

ADDITIONAL ARTICLES OF UNION

Other issues added to the list to make the Union matters 22 were
:
·
All matters concern coinage, currency for the
Purposes of legal tender (including notes), banks

(Including savings banks) and all banking business;

Foreign exchange and exchange control

·
Industrial licensing and statistics
·
Higher education
·
Mineral oil resources, including crude oil and natural gas
·
The National Examinations Council of Tanzania and all matters connected with the functions of that Council
·
Civil Aviation
·
Research
·
Meteorology
·
Statistics
·
The Court of Appeal of the United Republic
·
Registration of political parties and other matters
Related to political parties



·Zanzibar retains jurisdiction over issues which
Include:
· Information, Agriculture,Natural Resources,
Environment and Cooperatives, Trade, Industry,

Marketing, Tourism, Education, Culture and Sports,

Health and Social Welfare, Water, Construction,

Energy and Land, Communication and Transport and finally, youth,
employment, women and children development, etc
 
of course isingeweza; lakini Zanzibar ilipokuwa huru na majeshi yake na kila kitu chake iliomba Tanganyika msaada wa kutuliza mapinduzi! Zanzibar hata ikiwa na kila kitu chake na vifaru vyake si tishio kwa namna yoyote kwa Tanganyika. Ila Tanganyika itaendelea kuweka kivuli Zanzibar (iwe ndani ya Muungano au nje).

Na vile vile unatakiwa kujua hata Znz ikiwa huru na kila kitu chake, Tanganyika itakuwa si tishio kwa namna yoyote kwa Znz.


Lakin kuna suala dogo nilikuuliza.

Je kama kunatokea maasi upande wa Tanganyika kwa kuwafukuza waZnz, je Znz itakuwa na ubavu wa kutoa majeshi kwenda kuzuia maasi hayo.

 
Nguruvi3.

Ndio maana nakwambia huujui hata kidogo muungano wenu ni wa aina gani na ndio maana kila wakti unakuwa mtu wa kupinga.

Ngoja nikudarsishe kidogo hapa kuhusu muungano wenu.

Kwa kukusaidia Ahali yangu Muungano wenu SIO WA KIKATIBA BALI NI MUUNGANO WA MKATABA. Kwani kila nchi ina Katiba yake na sharia zake za ndani isipokuwa kwa mambo yale tu mliokubaliana katika MKATABA
ZNZ wanataka mkataba upi kabla ya kuvunja huu uliopo? Ahali wangu, hakuna shaka WZNZ hawajui wanataka nini.
 
Na vile vile unatakiwa kujua hata Znz ikiwa huru na kila kitu chake, Tanganyika itakuwa si tishio kwa namna yoyote kwa Znz.


Lakin kuna suala dogo nilikuuliza.

Je kama kunatokea maasi upande wa Tanganyika kwa kuwafukuza waZnz, je Znz itakuwa na ubavu wa kutoa majeshi kwenda kuzuia maasi hayo.


Hili swali ni la kinafik. WaTanganyika hawawezi kuwafukuza waZanzibari lakini waZanzibari wanaweza. Swali lingekuwa je Tanganyika itaweza kusimama kimya wakati raia zake wanatendewa unyama Zanziba? Je, ingekuwepo Tanganyika, viongozi wake wangenyamaza tu wakati raia wake wanachomewa sehemu zao za biashara? Mimi nadhani wasingekaa kimya lakini wasingevamia nchi ya Zanziba kuwanusuru raia wake. Lakini Zanziba ingeendeleza wimbi hilo bila shaka Tanganyika wangetuma askari wake kuwanusuru raia zake.

WaTanganyika hawawezi kuwafukuza waZanzibari maana hawajawahi kutaka kuweka tofauti kati ya mZanzibari na mTanganyika. MZanzibari anaweza maana siku zote amekuwa akitofautisha mZanzibari ni nani na mTanganyika. Na mara nyingi amefanya hivi ili kumpunguzia usawa mTanganyika. Palikuwa na wakati mTanganyika alihitaji kibali maalum kuoa binti wa kiZanzibari. Kuna wakati mTanganyika alihitaji pasi kutembelea Zanziba. MTanganyika amezuiwa kumilki ardhi Zanziba. Jaribio la kutaka MTanganyika aombe kibali cha kufanya kazi Zanziba lilishindwa kwenye BLW kwa kura chache. Leo hii kuna zoezi la kutoa vitambulisho vitakavyoonyesha nani mZanzibari na nani mgeni. MTanganyika akiwa katika kundi la mgeni. Baada ya kumtofautisha hivyo na kumfanya kiumbe cha chini kuliko mZanzibari ni hatua ndogo kuchukua hatua za kumfukuza. Kama vile mlivyofanya baada ya kufanya mapinduzi na kuainisha waarabu kuwa si waZanzibari. Mliwachinja, kuwafukia kwenye visima, kuwafungia kwenye viwanja vya michezo vilivyogeuzwa kuwa concentration camps n.k. Ni waTanganyika waliowapokea hao mliowakataa kuanzia Sultani wenu. Mlipotaka kufanya orgy ya kuchinja baada ya kuuawa kwa Karume, ni Tanganyika iliyowapa hifadhi wakina Babu. Mlipoanza ubaguzi wa wazi dhidi ya wapemba, ni waTanganyika waliowapa hifadhi Sharif Shamba, Namanga na maeneo mengine Tanganyika bila kuwabagua kwa aina yeyote. Wakati nyinyi mliwaona waPemba waTanganyika waliwakubali kama waTanzania wenzao! Leo hii ni baadhi ya viongozi wenu ambao wanapaza sauti wakiongea lugha ya kebehi na matusi dhidi ya waTanganyika. Utashangaa nini kama hao hao mara baada ya kupata uhuru hawatatangaza Zanziba kwa ajili ya waZanzibari na kuwafukuza wanyamwezi wote! Yote haya unayaona lakini bila aibu unadiriki kudai kuwa ni waTanganyika ndio watakaowafukuza waZanzibari? Kitakachotokea ni kuwa baada ya Muungano kuvunjika, waTanganyika hawataona taabu kuwakubali waZanzibari wote watakaochaguwa kuwa raia wa Tanganyika. Swali ni kuwa, waZanzibari watakubali kuwapa uraia wanyamwezi wote amabao watataka kuwa raia wa huko? Sisi tutaendelea kuwapokea kama tulivyowapokea viongozi wenu waliostaafu na wajane wao. Lakini kama Tanganyika hatutakubali kuangalia wakati mnawatendea dhulma waTanganyika wenzetu. Mkifanya hivyo mtaukumbuka Muungano. Kama wanavyosema waChina, uwe mwangalifu unachomuomba Mwenyezi maana anaweza akakupa!

Amandla.............................
 
ZNZ wanataka mkataba upi kabla ya kuvunja huu uliopo? Ahali wangu, hakuna shaka WZNZ hawajui wanataka nini.

Awali ya yote nimeshukuru sana kuwa umeelewa kuwa Muungano wenu ni MUUNGANO WA MKATABA na SIO WA KIKATIBA.

Na hata ukisome Katiba ya Muungano ya JMTz imelibainisha hilo kama utasona
Utekelezaji wa shughuli za Mamlaka ya Nchi Sheria namba Na.15 ib.6 ya 1984, kifungu cha 4
4.-
(1) Shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri

ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili

vyenye mamlaka ya utendaji, vyombo viwili vyenye mamlaka

ya kutekeleza utoaji haki, na pia vyombo viwili vyenye

mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa

shughuli za umma.


(2) Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni

Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, vyombo vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki

vitakuwa ni Idara ya Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya

Muungano na Idara ya Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar, na vyombo vyenye mamlaka ya kutunga sheria na

kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma vitakuwa ni

Bunge na Baraza la Wawakilishi.


(3) Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za umma

katika Jamhuri ya Muungano, na kwa ajili ya mgawanyo wa

madaraka juu ya shughuli hizo baina ya vyombo vilivyotajwa

katika ibara hii, kutakuwa na Mambo ya Muungano kama

yalivyoorodheshwa katika Nyongeza ya Kwanza iliyoko mwishoni mwa Katiba hii, na pia kutakuwa na Mambo yasiyo

ya Muungano ambayo ni mambo mengine yote yasiyo Mambo

ya Muungano.

(4) Kila chombo kilichotajwa katika ibara hii kitaundwa

na kutekeleza majukumu yake kwa kufuata masharti mengine

yaliyomo katika Katiba hii.



 
Hili swali ni la kinafik. WaTanganyika hawawezi kuwafukuza waZanzibari lakini waZanzibari wanaweza. Swali lingekuwa je Tanganyika itaweza kusimama kimya wakati raia zake wanatendewa unyama Zanziba? Je, ingekuwepo Tanganyika, viongozi wake wangenyamaza tu wakati raia wake wanachomewa sehemu zao za biashara? Mimi nadhani wasingekaa kimya lakini wasingevamia nchi ya Zanziba kuwanusuru raia wake. Lakini Zanziba ingeendeleza wimbi hilo bila shaka Tanganyika wangetuma askari wake kuwanusuru raia zake.

WaTanganyika hawawezi kuwafukuza waZanzibari maana hawajawahi kutaka kuweka tofauti kati ya mZanzibari na mTanganyika. MZanzibari anaweza maana siku zote amekuwa akitofautisha mZanzibari ni nani na mTanganyika. Na mara nyingi amefanya hivi ili kumpunguzia usawa mTanganyika. Palikuwa na wakati mTanganyika alihitaji kibali maalum kuoa binti wa kiZanzibari. Kuna wakati mTanganyika alihitaji pasi kutembelea Zanziba. MTanganyika amezuiwa kumilki ardhi Zanziba. Jaribio la kutaka MTanganyika aombe kibali cha kufanya kazi Zanziba lilishindwa kwenye BLW kwa kura chache. Leo hii kuna zoezi la kutoa vitambulisho vitakavyoonyesha nani mZanzibari na nani mgeni. MTanganyika akiwa katika kundi la mgeni. Baada ya kumtofautisha hivyo na kumfanya kiumbe cha chini kuliko mZanzibari ni hatua ndogo kuchukua hatua za kumfukuza. Kama vile mlivyofanya baada ya kufanya mapinduzi na kuainisha waarabu kuwa si waZanzibari. Mliwachinja, kuwafukia kwenye visima, kuwafungia kwenye viwanja vya michezo vilivyogeuzwa kuwa concentration camps n.k. Ni waTanganyika waliowapokea hao mliowakataa kuanzia Sultani wenu. Mlipotaka kufanya orgy ya kuchinja baada ya kuuawa kwa Karume, ni Tanganyika iliyowapa hifadhi wakina Babu. Mlipoanza ubaguzi wa wazi dhidi ya wapemba, ni waTanganyika waliowapa hifadhi Sharif Shamba, Namanga na maeneo mengine Tanganyika bila kuwabagua kwa aina yeyote. Wakati nyinyi mliwaona waPemba waTanganyika waliwakubali kama waTanzania wenzao! Leo hii ni baadhi ya viongozi wenu ambao wanapaza sauti wakiongea lugha ya kebehi na matusi dhidi ya waTanganyika. Utashangaa nini kama hao hao mara baada ya kupata uhuru hawatatangaza Zanziba kwa ajili ya waZanzibari na kuwafukuza wanyamwezi wote! Yote haya unayaona lakini bila aibu unadiriki kudai kuwa ni waTanganyika ndio watakaowafukuza waZanzibari? Kitakachotokea ni kuwa baada ya Muungano kuvunjika, waTanganyika hawataona taabu kuwakubali waZanzibari wote watakaochaguwa kuwa raia wa Tanganyika. Swali ni kuwa, waZanzibari watakubali kuwapa uraia wanyamwezi wote amabao watataka kuwa raia wa huko? Sisi tutaendelea kuwapokea kama tulivyowapokea viongozi wenu waliostaafu na wajane wao. Lakini kama Tanganyika hatutakubali kuangalia wakati mnawatendea dhulma waTanganyika wenzetu. Mkifanya hivyo mtaukumbuka Muungano. Kama wanavyosema waChina, uwe mwangalifu unachomuomba Mwenyezi maana anaweza akakupa!

Amandla.............................

Fundi Mchundo,

Labda ulikuwa mdogo sana ima ujazaliwa wakti ilipovunjika Jumuiya ya Afrika mashariki (EAC). Itakumbukwa kuwa Watanzania waliwafukuza wakenya na Waganda wote kama nchi hizo navyo zilipowafukuza raia wasio wake.

Sasa kama waliweza kuwafukuza wakenya na waganda ilipovunjika EAC watashindwaje sasa kuwafukuza WaZanzibari?

Au ndio kisebusebu na kiroho papo?
 
ZNZ wanataka mkataba upi kabla ya kuvunja huu uliopo? Ahali wangu, hakuna shaka WZNZ hawajui wanataka nini.

Mimi nafikiri waZanzibari wapo wazi saaaana na kila wakti wanasema msimamo wao hivi ni wakti muafaka kuungalia kwa kina sana muungano wenyewe kabla ya kuangalia kero za muungano kwa vile Muungano umechangi kwa kiwango kikubwa kuathiri sekta ya uchumi visiwani.

Na wapo tayari kwa lolote litakalo amuliwa na mjadala huo.

Labda na wewe utudadavulie maana yake hakuna sehemu yoote WATANGANYIKA walipoweka Msimamo wao kuhusu Muungano. Tupe msimamo wenu?

 
Nina shaka sana yanayotokea Dar-es-salaam,Mombasa na Zanzibar naona kuwa yana ajenda iliyojificha.Yanapotokea Dar yanajitokeza kama tatizo la kidini directly,kule Mombasa kupitia kikundi cha Republic of Mombasa yanapitia kwenye dini indirectly na Zanzibar kupitia kikundi cha uamsho yanapitia kwenye dini indirectly.

The common denominator ni dini iliyo na ajenda ya kisiasa.Najaribu kurudisha mawazo yangu nyuma kuhusu andiko fulani la kisiasa lililojadili the Greater Sultanate of Zanzibar ambayo ilijumuisha Coastal area ya Tanganyika na Kenya.Hapa tuwe macho na nashauri intelligency community itafiti na kupeleleza mienendo ya wanaharakati hawa na mwenendo mzima wa ghasia zinazoendelea sasa hivi kwenye maeneo niliyoyataja kwenye bandiko hili.

Nina shaka sana kuwa hawa watu ni welevu sana kuliko tunavyowafikiria.Mwanzo naona wanataka kutumia soft spot ya Muungano kupenyeza ajenda yao.Mwanzoni walikuwa wanataka serikali tatu,watu haohao leo wanataka muungano wa mkataba hamuoni hapo kuna tatizo la kuanza kulifuatilia?Wamegundua wazi kuwa wakivunja muungano, Zanzibar itageuka kituo kikuu cha kueneza itikadi ya siasa kali za kidini kwenye ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Kivuli cha dini kinawavutia sana watu hawa katika ajenda yao ya kujitanua hapo mbeleni.Kikundi hiki kinajua sana umuhimu wa muungano kuwa ni muhimu kiuchumi na kijamii.Sisi wapenda muungano tuna karata nzuri ya kuwapiku hawa jamaa kwa kutumia manufaa ya kiuchumi na kijamii.Mfano ni Hong kong inavyoinufaisha The Greater Republic of China na kuifanya tishio kwa mataifa makubwa duniani.

Kwa mfano nilioutolea hapo juu Zanzibar ina umuhimu mkubwa wa kuwa part of United Republic of Tanzania ndani ya shirikisho la Afrika Mashariki.Ni bahati mbaya sisi Pan-Africanist tumeshikwa na kigugumizi kuyaleta haya mawazo hadharani na wenye siasa kali za kidini kutamalaki hapa Afrika Mashariki.Tukiruhusu Zanzibar kujitenga wenye siasa kali za kidini watawazidi nguvu hawa wazalendo wa Zanzibar,maana mtandao wao haushirikishi serikali za kiarabu hivi ni vikundi tu vya kiharifu vyenye kutumia mwamvuli wa dini.
 
Fundi Mchundo,

Labda ulikuwa mdogo sana ima ujazaliwa wakti ilipovunjika Jumuiya ya Afrika mashariki (EAC). Itakumbukwa kuwa Watanzania waliwafukuza wakenya na Waganda wote kama nchi hizo navyo zilipowafukuza raia wasio wake.

Sasa kama waliweza kuwafukuza wakenya na waganda ilipovunjika EAC watashindwaje sasa kuwafukuza WaZanzibari?

Au ndio kisebusebu na kiroho papo?
Kama kawaida yako, unatumia mifano isiyofaa.

Kenya na Uganda hazijawahi kuwa sehemu ya Tanzania. Wakenya na waGanda siku zote wamekuwa wageni. Hiki ni kitu ambacho waZanzibari hawajawahi kuwa Tanzania Bara. Lakini machogo wamekuwa wageni siku zote huko Zanziba.

Wakati wa kuvunjika kwa EAC, juhudi za maksudi zilifanywa na waTanzania kuwa-demonise waKenya haswa. Labda ulikuwa ushakimbia wakati ule lakini palikuwa na kipindi kinachoitwa "mazungumzo baada ya habari". katika kipindi hiki waKenya waliitwa manyang'anyua na majina mengine kama hayo. Tanzania Bara haijawahi fanya hivyo kwa waZanzibari. Lakini waZanzibari hawajachoka kutu-demonize kwa kutubandika majina watu wa bara, machogo, wakoloni, wezi, n.k. Tabia hii ndiyo iliyochangia kwa kiasi kikubwa katika fujo zilizofanywa na baadhi ya waZanzibari dhidi ya watu kutoka bara.

Ni kutokana na ukweli huu ndio ninasema kuwa kuna uwezekano mkubwa wa waZanzibari kuwafanyia fujo watu kutoka bara kuliko waTanzania bara kuwafanyia fujo waZanzibari. Swali lako halina mantik wala tija.

Amandla........
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mimi nafikiri waZanzibari wapo wazi saaaana na kila wakti wanasema msimamo wao hivi ni wakti muafaka kuungalia kwa kina sana muungano wenyewe kabla ya kuangalia kero za muungano kwa vile Muungano umechangi kwa kiwango kikubwa kuathiri sekta ya uchumi visiwani.

Na wapo tayari kwa lolote litakalo amuliwa na mjadala huo.

Labda na wewe utudadavulie maana yake hakuna sehemu yoote WATANGANYIKA walipoweka Msimamo wao kuhusu Muungano. Tupe msimamo wenu?

Kwanini tuweke msimamo! Kwa shida gani hebu fafanua! Do we need ZNZ in any way!
 
Mimi nafikiri waZanzibari wapo wazi saaaana na kila wakti wanasema msimamo wao hivi ni wakti muafaka kuungalia kwa kina sana muungano wenyewe kabla ya kuangalia kero za muungano kwa vile Muungano umechangi kwa kiwango kikubwa kuathiri sekta ya uchumi visiwani.

Na wapo tayari kwa lolote litakalo amuliwa na mjadala huo.

Labda na wewe utudadavulie maana yake hakuna sehemu yoote WATANGANYIKA walipoweka Msimamo wao kuhusu Muungano. Tupe msimamo wenu?


Barubaru, madai ya Zanzibar ni kwamba Muungano umegeuza Zanzibar kuwa koloni la Tanganyika. Na kwenye post yako (kwenye red) unasema kuwa Muungano umechangia kwa kiasi kikubwa kuathiri uchumi wa Visima. Assuming hayo madai ni ya kweli.

Now, in your right mind kwanini Zanzibar watake Mkataba na huyu mkoloni aliyeathiri uchumi wake (Visiwani) kwa kiasi kikubwa kama unavyodai? Ni kwanini Zanzibar msijenge uzio wa nguvu Chumbe ili kujikinga na huyu mkoloni?

Pili, hapo ulipo-underline, sio kweli. Zanzibar hawako tayari kwa lolote, na ndio maana mnataka Mkataba. The only way unaweza kusema Zanzibar iko tayari kwa lolote ni kuachana na hizi chorus za kitoto za Mkataba na kuvunja muungano kimoja.

Maalim Seif na wenzake wanawaaminisha watu kuwa 'Zanzibar iko tayari kwa lolote' na kwa bahati mbaya wapo-tena wengi tu wanaoamini hizo hoja bila kuuliza kama kweli wako tayari kwanini wanamng'ang'ania mkoloni? Kwanini asimalize hii issue BLW? Kwanini asiwapige marafuku wabunge wake kuja Dodoma? Mkataba wa kitu gani, wa ATM?

Mwisho, Kama umefuatilia vizuri utagundua kwamba Muungano sio issue kubwa sana kwa Tanganyika, na sababu kubwa ni kuwa Zanzibar can vanish from the map of this planet and it will not affect Tanganyika one bit! Sanasana ajira zitarudi kwa Tangayika.


Kwa Tanganyika, watu wanajua huduma duni za afya hazitokani na Muungano, barabara mbovu hazitokani na Muungano, ukosefu wa madawati shuleni hautokani na Muungano. Na nguvu kubwa ya watanganyika inaelekezwa kwenye hayo matatizo.

Niliwahi kuuliza, lakini naomba niulize tena, ahadi za Seif za kuifanya Zanzibar kuwa Singapore zimefikia wapi?
 
Barubaru, madai ya Zanzibar ni kwamba Muungano umegeuza Zanzibar kuwa koloni la Tanganyika. Na kwenye post yako (kwenye red) unasema kuwa Muungano umechangia kwa kiasi kikubwa kuathiri uchumi wa Visima. Assuming hayo madai ni ya kweli.

Now, in your right mind kwanini Zanzibar watake Mkataba na huyu mkoloni aliyeathiri uchumi wake (Visiwani) kwa kiasi kikubwa kama unavyodai? Ni kwanini Zanzibar msijenge uzio wa nguvu Chumbe ili kujikinga na huyu mkoloni?

Pili, hapo ulipo-underline, sio kweli. Zanzibar hawako tayari kwa lolote, na ndio maana mnataka Mkataba. The only way unaweza kusema Zanzibar iko tayari kwa lolote ni kuachana na hizi chorus za kitoto za Mkataba na kuvunja muungano kimoja.

Maalim Seif na wenzake wanawaaminisha watu kuwa 'Zanzibar iko tayari kwa lolote' na kwa bahati mbaya wapo-tena wengi tu wanaoamini hizo hoja bila kuuliza kama kweli wako tayari kwanini wanamng'ang'ania mkoloni? Kwanini asimalize hii issue BLW? Kwanini asiwapige marafuku wabunge wake kuja Dodoma? Mkataba wa kitu gani, wa ATM?

Mwisho, Kama umefuatilia vizuri utagundua kwamba Muungano sio issue kubwa sana kwa Tanganyika, na sababu kubwa ni kuwa Zanzibar can vanish from the map of this planet and it will not affect Tanganyika one bit! Sanasana ajira zitarudi kwa Tangayika.


Kwa Tanganyika, watu wanajua huduma duni za afya hazitokani na Muungano, barabara mbovu hazitokani na Muungano, ukosefu wa madawati shuleni hautokani na Muungano. Na nguvu kubwa ya watanganyika inaelekezwa kwenye hayo matatizo.

Niliwahi kuuliza, lakini naomba niulize tena, ahadi za Seif za kuifanya Zanzibar kuwa Singapore zimefikia wapi?

FjM,

Ahali yangu naona uelewa wako ulikuwa sawa na alivyokuwa anaelewa mwenzako Nguruvi3.

Napenda nikufahamishe kuwa MUUNGANO WENU NI WA KIMKATABA NA SIO WA KIKATIBA. Nimefafanua zaidi kwenye post no 108 na nikanukuu kutoka kwenye katiba yenu kwenye post no 112 ya mada hii.

naomba nisome humu kwani nimebainisha bila kificho kuwa Muungano wenu ni wa MKATABA na sio KATIBA.

Sasa wewe unazungumzia muungano upi tena wa Mkataba?



 
Kwanini tuweke msimamo! Kwa shida gani hebu fafanua! Do we need ZNZ in any way!

Ndio maana kila wakti nasema hamna msimamo nyie ni bendera kufuata upepo.

Sasa kwa kuwa hamna msimamo kaeni kimya muwaache wenye msimamo wanaposema kweli? na kama mnaona inawakera basi chukueni hatua.

Poleni sana

 
Back
Top Bottom