Wapiga kelele Lissu alichokisema ndo Rais anakifanya navyo ni kufata sheria, sio kutumbua majukwaani

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Habari wadau!

Kuna mjadala na cha ajabu sana wakeleketwa wa ccm wanamshambulia Lissu kuwa anawatetea Makaburu wakati huo wamesahau wao ndio waliowaleta tena kwa kuwatimua wazawa kwa mtutu wa bunduki na kuwakabidhi kwa ulinzi mkali wa polisi.

Lissu alichokisema haya mambo yanaenda kulingana na sheria either za ndani au nje ya nchi.

Ila akashauri kabla ya kufanya chochote tuangalie tumejifunga wapi ili ikiwezekana tujitoe kwenye hiyo mikataba kisheria then huku ndani nako tutoe sheria zote zinazowalinda hao makaburu. Then tuwatimue vizuri wakose pa kukimbilia.

Kwa tu amjua bwana mkubwa asingechela kusema kutaifisha mitambo na mali iliyopo nchini. Ila akawa mpole hakisema migodi ifungwe na washikirie mali za kampuni. Hii liko wazi ofisi ngapi zimefungwa kwa kutolipa kodi kwa makufuri ya tra? Sasa mbona hawa makaburu wako wazi kama hafuati sheria?

Kwa akili ndogo watu wa ccm wanapongeza kitu walichoshauriw ila wanabaki na kauli ya kukariri kuwa Lissu ni kibaraka? Kibataka gani anayekwambia mmezuia mvhanga na vitofari vinasafiri kama kawaida?

Kama ndo ivyo ataifishe mali za mwizi basi tujue ukweli.
 
Back
Top Bottom