Elections 2010 Wapi wameshinda cuf

Alwaz

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
6,822
10,349
Mbona sijaona mahala CUF imeshinda ubunge bara kama wenzao akina CHADEMA hata nccr mageuzi.Au nimepitiwa tu.
Nilisikia Mbeya,Mtwara halafu Tanga na bUKOBA,lakini sijaona !.
 
Mbona sijaona mahala CUF imeshinda ubunge bara kama wenzao akina CHADEMA hata nccr mageuzi.Au nimepitiwa tu.
Nilisikia Mbeya,Mtwara halafu Tanga na bUKOBA,lakini sijaona !.

Lindi Mjini, japo sina hakika kama wameishatangaza rasmi.
 
Cuf wameshinda lindi mjini nec wametangaza rasmi,na zenj wamepata majimbo 22 jumla mpk sasa wana wabunge 23 safi, wakubaliane na chadema waungane bungeni waipeleke puta ccm na mafisadi wake,aluta continua.
 
CUF hawawezi kushinda bara kwa kuwa ni chama cha uchaguzi na si chama cha siasa.CUF wao baada ya uchaguzi huwa wanajisahau hawazunguki mikoani kujenga chama,huku bara si kama Pemba ,huku chama kilicho karibu na wananchi ndicho kinachoweza kushinda viti vya ubunge na udiwani.


Hii inaonesha kuwa kwa miaka karibuni 15 Prof.Lipumba aliyokaa madarakani kama mwenyekiti ameshindwa kukiuza chama cha CUF kwa wananchi.

Mimi nawashukuru sana CHADEMA chini ya uongozi wa MBOWE,SLAA,ZITTO NA MNYIKA wamefanikiwa kukiuza chama kwa wananchi kupitia Operasheni Sangara na wameweza kuonesha kuwa CHADEMA si chama cha maeneo fulani kama kilivyo CUF(Pemba) BALI cha KITAIFA
 
Dafirs hapo umenena cuf wamejisahau wamekaa zenj tu bara wanasubir uchaguzi ndio wanaamka,sasa wamevuna walichopanda,ila cuf wenyewe wanadai wamelishinda lindimjini,lindivijijini,kigamböni,temeke,tangamjini,lushoto,uyui,na data wanazo zavituoni,ila wanadai ccm imechakachua matokeo,
 
Kama CUF ni chama cha Pemba sawa, nambie sasa kama CHADEMA sio chama cha Bara. Maana Pemba hawana ofisi wala hawakuja kukampeni, kwani Pemba sio Tanzania? Acheni maneno ya vijiweni nyie.
 
Dafirs hapo umenena cuf wamejisahau wamekaa zenj tu bara wanasubir uchaguzi ndio wanaamka,sasa wamevuna walichopanda,ila cuf wenyewe wanadai wamelishinda lindimjini,lindivijijini,kigamböni,temeke,tangamjini,lushoto,uyui,na data wanazo zavituoni,ila wanadai ccm imechakachua matokeo,
Hizo data zina dalili ya ukweli.Kuhusu kujitangaza hakuna kama CUF.Tatizo lililopo chaguzi Tanzania na Afrika ni kuppotezeana muda tu.uwamuzi huchukuliwa mezani.
Watu wa CHADEMA mukiwa na msimamo kwamba CUF hawajitangazi basi mukubali kuwa uchaguzi uliomalizika na matokeo yanayotangazwa ndio ukweli,hivyo kaeni kimya.
 
JAMAN TUWE MAKIINI ILI JF IWE JUU, TUSIKURUPUKE KUTOA TAARifA kAmA hujvERIFY.
MWEnzetU KAULIZA CUF WAMESHINDA WAPI BARA?
JIBU SahiHI:
CUF wako Lindi Mjini na KILWA KUSINI TU. HIVYO WANAMAJIMBO MAWILI HUKU BARA
 
Hawa kila wakipata nafasi ya kuikandamiza CUF madongo basi hawachelewi kufanya hivyo. Huu ni uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani. CUF imenyakua viti vingi tu vya udiwani huku Bara na hivyo kufanya hayo madai ya kuwa CUF ni chama cha wakati wa uchaguzi ni za uongo, uzushi na fitna za kike. Mwaka jana (miezi 12 tu iliyopita) ulifanyika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji Tanzania Bara tu na CUF ilishika nafasi ya pili baada ya CCM ikifuatiwa kwa mbali na Chadema. Hiyo nayo inathibitisha kuwa anayedai kuwa CUF ni chama cha wakati wa uchaguzi tu kuonekana ni mbumbumbu na asiyejua mambo ya upinzani. Sana sana ni mtu wa juzi alitoka CCM.

Kilichofanyika uchaguzi huu ni yale maneno ya Prof. Lipumba kuwa "mapapa, nyangumi, na masangara yanashirikiana kuihujumu CUF".
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom