Wapi Nitapata Mkopo wa TZS 10M Haraka?

Big Lady

JF-Expert Member
Nov 23, 2009
546
75
Salaam sana.

Nahitaji mkopo wa haraka wa TZS 10 M nitakaorudisha katika kipindi cha miezi mitatu with or without interest.

Nina securities kama gari na hati ya kiwanja/nyumba. Niko DSM.

Je ni wapi naweza kupata mkopo wa TZS 10 M immediately?

Je vigezo na masharti ni yapi including re-payment terms?

Nitashukuru kwa information za tija nitakazopata.
 
njo na hati yako nikupe, you will just sign deeds of transfer if no payment after three months we will poses the land without majadiliano ya ziada
Watu, no problem. Milion 10 siyo pesa nyingi sana ila nina shida ya haraka na siko vizuri.

Je vigezo na masharti mengine ni yapi including re-payment terms na interest?
 
Last edited by a moderator:
KAMA UNA SECURITY YA HATI YA KIWANJA NA KADI YA GARI ambavyo havina mashaka KWANINI USIENDE BANK?
waubani benki nenda rudi zitakuwa nyingi. Unaweza kupiga kwata hata mwezi moja.

Lakini kama una benki unaifahamu wanaweza kunipa kwa haraka niko tayari.
 
Last edited by a moderator:
njo na hati yako nikupe, you will just sign deeds of transfer if no payment after three months we will poses the land without majadiliano ya ziada
Mkuu nyumba yenye thamani ya Tshs million 100 kwa mkopo milioni 10,naona hapa hakuna uwiano hata kidogo!!
 
Nafahamu kuna baadhi ya Moslems hawatozi riba including bank ya Amana inayofanya Moslem Banking!
Hakuna kitu ni usanii mtupu,wanasema watakuwa wana 'share' na wewe 'profit and loss','in real life context,this is hidden interest'
 
Mkuu nyumba yenye thamani ya Tshs million 100 kwa mkopo milioni 10,naona hapa hakuna uwiano hata kidogo!!

Umeona eeh! Chezeya wenye pesa weye?

Nyumba ina thamani ya around TZS 300 Milion.

Ni vile tu katika maisha kuna kupanda na kushuka. Nikijua terms zake kwa uwazi naweza kuchukua hata January au February nikamrudishia.
 
Big Lady unauzoefu na Micro Finance? Nenda pale Sinza Mapambano jengo la mwanamboka kuna EFL watakupa mara moja,Uwe na mdhani na salary slip na hizo securities zako.Ni PM kwa maelezo zaidi

Duh! Bingo!

Ngoja niende leo. Interest zao zikoje? Terms?
 
Umeona eeh! Chezeya wenye pesa weye?

Nyumba ina thamani ya around TZS 300 Milion.

Ni vile tu katika maisha kuna kupanda na kushuka. Nikijua terms zake kwa uwazi naweza kuchukua hata January au February nikamrudishia.
Kweli kabisa Dada yangu wenye pesa wanatunyanyasa sana sisi masikini!!
 
Jamani hakuna mwingine mwenye some information?

I need the $$$ like yesterday!
 
Salaam sana.

Nahitaji mkopo wa haraka wa TZS 10 M nitakaorudisha katika kipindi cha miezi mitatu with or without interest.

Nina securities kama gari na hati ya kiwanja/nyumba. Niko DSM.

Je ni wapi naweza kupata mkopo wa TZS 10 M immediately?

Je vigezo na masharti ni yapi including re-payment terms?

Nitashukuru kwa information za tija nitakazopata.

nenda bank yoyote
 
Kwa uelewa wangu hakuna bank au Microfinance yeyote ambayo inakusumbua endapo umetimiza documents zote za muhimu na ndo kazi yao kukopesha...Kuna jamaa yangu yeye ana uwezo wa kukopesha mpaka millioni kumi(ila riba yake ni 30% kwa mwezi) na mnaandikishiana na kama gari sharti iwe na thamani ya zaidi ya iyo millioni kumi na gari pamoja na kadi anakaa nazo mkopeshaji mpaka utakapomaliza deni kama utaweza niambie nikutumie mawasiliano...
 
Big Lady, uwe makini sana na shida yako ya haraka, usije ukawa umekutana na matapeli wakakujazia hela kwenye briefcase na kukudanya kuwa ni milioni zaidi ya mia moja halafu wakakuambia leta milioni kumi uzichukue. Kama ni hivyo watakufirisi sana. Hakikisha ni dili halali la sivyo itakula kwako. Yangu ni hayo tu.
 
be careful but better uende kwenye bank institution usije ukalizwa.Kama issue ni kupata mkopo faster jaribu
1.BANC ABC
2.PIA EQUITY BANK
3.AFRICAN MICROFINANCE hawa wako survey
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom