Wapi nipate mbegu modified za mipaina? (pines)

AfroMonster

Member
Jun 7, 2018
67
75
Heshima kwenu wakuu, nalenga kuotesha miche ya mipaina(pines) ili kupunguza gharama za kununua miche iliyooteshwa. Lakini sina uelewa wa kutosha wapi nipate mbegu bora ikiwezekana za kisasa. Nishasikia kuhusu kwenda ofisi za wakala wa misitu lakini bado sijapata ushauri wa kuniwezesha kuchukua maamuzi sahihi.

Naomba ushauri wenu
images.jpeg
 
kama upo morogoro ni sehemu sahihi ya kwenda, unaweza kupata mbeguna utaalamu wa namna ya kuziotesha maana uoteshaji wa baadhi ya mbegu una changamoto kwenye kuziandaa
 
Heshima kwenu wakuu, nalenga kuotesha miche ya mipaina(pines) ili kupunguza gharama za kununua miche iliyooteshwa. Lakini sina uelewa wa kutosha wapi nipate mbegu bora ikiwezekana za kisasa. Nishasikia kuhusu kwenda ofisi za wakala wa misitu lakini bado sijapata ushauri wa kuniwezesha kuchukua maamuzi sahihi.

Naomba ushauri wenuView attachment 1118733
Uko wapi
 
Heshima kwenu wakuu, nalenga kuotesha miche ya mipaina(pines) ili kupunguza gharama za kununua miche iliyooteshwa. Lakini sina uelewa wa kutosha wapi nipate mbegu bora ikiwezekana za kisasa. Nishasikia kuhusu kwenda ofisi za wakala wa misitu lakini bado sijapata ushauri wa kuniwezesha kuchukua maamuzi sahihi.

Naomba ushauri wenuView attachment 1118733
Kuna NGO moja pale Iringa ni marafiki zangu wana mbegu hizo. Kama uko serious sema nikupe simu zao, utawambia Malila kanipa simu yenu, watakupa maana ndo biashara yao.
 
Kuna NGO moja pale Iringa ni marafiki zangu wana mbegu hizo. Kama uko serious sema nikupe simu zao, utawambia Malila kanipa simu yenu, watakupa maana ndo biashara yao.
Malila kumbe bado upo? Kilimo kinaendeleaje?
 
Kuna NGO moja pale Iringa ni marafiki zangu wana mbegu hizo. Kama uko serious sema nikupe simu zao, utawambia Malila kanipa simu yenu, watakupa maana ndo biashara yao.
Niko serious mkuu, pia kama una tetesi kuhusu bei unaweza kunipatia taarifa za awali kabla sijawacheki,,,

lakin swali... sina hakika kama pine inayostawi Iringa inafaa Kagera, nasikia kuna tofauti ya aina(species)

Shukrani

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Niko serious mkuu, pia kama una tetesi kuhusu bei unaweza kunipatia taarifa za awali kabla sijawacheki,,,

lakin swali... sina hakika kama pine inayostawi Iringa inafaa Kagera, nasikia kuna tofauti ya aina(species)

Shukrani

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
Bei ya kilo moja ilikuwa 1,200,000/ huko nyuma ya pinus patula, pines hutofautiana kulingana na altitude. Hapa inabidi uwaulize TTSA wakupe jamii sahihi.
 
Bei ya kilo moja ilikuwa 1,200,000/ huko nyuma ya pinus patula, pines hutofautiana kulingana na altitude. Hapa inabidi uwaulize TTSA wakupe jamii sahihi.
Sawa,
1. Mbona nahisi kama 1kg itakuwa nyingi sana kwa mahitaji yangu ya kupanda ekari 2 kwa sasa, maana nashindwa kukadiria naweza pata kati ya miche kiasi gani kutoka kwenye hiyo kg 1.

2. TTSA kuna namna ya kuwapata tofauti na kufika ofisini kwao Morogoro?
 
Sawa,
1. Mbona nahisi kama 1kg itakuwa nyingi sana kwa mahitaji yangu ya kupanda ekari 2 kwa sasa, maana nashindwa kukadiria naweza pata kati ya miche kiasi gani kutoka kwenye hiyo kg 1.

2. TTSA kuna namna ya kuwapata tofauti na kufika ofisini kwao Morogoro?
Nakupa simu ya hao jamaa wa mbegu, pia simu ya mtu wa TTSA, nipe simu yako nikupe mawasiliano fasta.
 
Bei ya kilo moja ilikuwa 1,200,000/ huko nyuma ya pinus patula, pines hutofautiana kulingana na altitude. Hapa inabidi uwaulize TTSA wakupe jamii sahihi.
Hapo Malila unamaanisha mbegu.zilizomo kwenye kilo au bei?
 
Sawa,
1. Mbona nahisi kama 1kg itakuwa nyingi sana kwa mahitaji yangu ya kupanda ekari 2 kwa sasa, maana nashindwa kukadiria naweza pata kati ya miche kiasi gani kutoka kwenye hiyo kg 1.

2. TTSA kuna namna ya kuwapata tofauti na kufika ofisini kwao Morogoro?
Ekari 2 unahitaji miche 800 tu, hivyo Nashauri ununue miche tu

Ulizia kwa meneja wa shamba la miti rubare huko bukoba

Asante
 
Kama upo kanda ya ziwa tuwasiliane kuna mbegu nzuri kutoka Buhindi forest, ndugu ndo muuzaji na wateja wake ni kutoka Bukoba na Muleba
 
Back
Top Bottom