Wapi nianike Chupi yangu?

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,627
154,983
Mwanzoni nilikuwa nikianika bafuni, kuna siku tumbo la kuaibisha likanishika. Nikatoka nduki hadi bafuni kwetu ambako choo na bafu viko ndani ya chumba kimoja, huko kilichonitokea sitakaa nisahau. Nilikuta mke wa mpangaji mwenzangu akiitumia chupi yangu niliyokuwa nimeifua asubuhi kujisugulia mwilini mwake. Tumbo langu la kuhara likaishia hapo na yule bibie sikumuuliza kisa cha yeye kuifanya chupi yangu dodoki lake la mwilini. Tangu siku hiyo nikawa naanika chumbani.

Jana nimetembelewa na mke wangu mtarajiwa. Yeye anajiendeleza katika chuo cha mahakama kilichopo Lushoto.
Alipoona chupi nimeanika chumbani akaanza nigombeza kuwa ni mwiko na aibu kuanika chupi chumbani. Nimejaribu kumuuliza kuwa nianike wapi? Badala ya kunielewesha kaanza kunilaumu kuwa simjali wala simsikilizi. Mimi ni mtu jeuri nisiyemthamini na kumuenzi.
Tangu jana hadi muda huu kanuna.
Jamani wana MMU nyie chupi zenu mnaanika wapi nami nije kuanika yangu?
 
mimi huwa nakadust bin kangu ka chupi
wiki nzima nikivua nazitupa huko
wkend naloweka kama lisaa nazifua mdogomdogo nasugua nasuuza fresh naanika kwenye kamba mchana live
haya mambo ya kufua chupi na maji uliyoogea yenye mapovu ya sabuni ndo maana mafangasi hayawaishi huko down
kuna watu uchi umezeeka maana..sabuni na uvundo vimezila

kama huwezi kutunza chupi asi usivae
 
kwa afya anika juani....mbona hakuna shida ktk hilo,chupi zenyewe si mali kitu siku hizi....wamachinga wanatembeza mikononi,zinamwaga barabarani.....kujipa fangazi wa bure kwa kuanika ndani wamuogopa nani hasa???
 
"Boxer" ni neno la kigeni lenye kumaanisha nguo ya ndan ya kiume kwa muktadha huu,yangu mm huanika nje ili ikauke kwa jua,
 
kwanini ukonde kaka mkubwa? nguo zote tunazofua tunaanika nje juani, hizo nazo ni nguo za kawaida yafaa kuanikwa nje juani! sasa pole yako ikiwa imetoboka kama hii

374940_293257847375887_868562802_n.jpg


au
302218_185733054832117_8109993_n.jpg
au uanike kama hivi hapa

428255_10151343110867829_1360268432_n.jpg
 
Mwanzoni nilikuwa nikianika bafuni, kuna siku tumbo la kuaibisha likanishika. Nikatoka nduki hadi bafuni kwetu ambako choo na bafu viko ndani ya chumba kimoja, huko kilichonitokea sitakaa nisahau. Nilikuta mke wa mpangaji mwenzangu akiitumia chupi yangu niliyokuwa nimeifua asubuhi kujisugulia mwilini mwake. Tumbo langu la kuhara likaishia hapo na yule bibie sikumuuliza kisa cha yeye kuifanya chupi yangu dodoki lake la mwilini. Tangu siku hiyo nikawa naanika chumbani.

Jana nimetembelewa na mke wangu mtarajiwa. Yeye anajiendeleza katika chuo cha mahakama kilichopo Lushoto.
Alipoona chupi nimeanika chumbani akaanza nigombeza kuwa ni mwiko na aibu kuanika chupi chumbani. Nimejaribu kumuuliza kuwa nianike wapi? Badala ya kunielewesha kaanza kunilaumu kuwa simjali wala simsikilizi. Mimi ni mtu jeuri nisiyemthamini na kumuenzi.
Tangu jana hadi muda huu kanuna.
Jamani wana MMU nyie chupi zenu mnaanika wapi nami nije kuanika yangu?

huyo mchumba wako anamapepo.
 
Du! Kiongozi bado wavaa kyupi! Bora boxer mwonekano wake unaanika hadharani kama uko kwenye upangaj wachumba! Lakini kama uko kwako sidhani kama inasumbua kuanika hata kama ni kyupi!
 
Back
Top Bottom