Wapi naweza kupata tiketi kwa ajili ya Usafiri wa treni (TRC)?

Hajto

JF-Expert Member
Sep 30, 2013
5,571
5,345
Habari zenu wana jamiiforum,

Leo jioni ninataraji kutaka kusafiri kwa kutumia usafiri wa tren kwenda Moshi. Je, ni wapi hapa Dar naweza kupata tiketi,Na pia wakati wa kupanda treni nitapandia wapii na zipi kero na raha zilizopo ndani ya Treni,Maoni yenu muhimu ni muhimu sana
 
Usitegemee sana humu inaweza kufika jioni bila kupata maelekezo wapi ilipo station ya treni..

Siyo mwenyeji sana Dar ila jaribu kupanda treni la Pugu uone litakupeleka wapi.
 
Habari zenu wana jamiiforum,Leo jioni ninataraji kutaka kusafiri kwa kutumia usafiri wa tren kwenda Moshi,Je ni wapi hapa Dar naweza kupata tiketi,Na pia wakati wa kupanda treni nitapandia wapi,Na zipi kero na raha zilizopo ndani ya Treni,Maoni yenu muhimu ni muhimu sana
Sipajui jina vizuri ila ni karibu na Central Police Posta.
 
Habari zenu wana jamiiforum,

Leo jioni ninataraji kutaka kusafiri kwa kutumia usafiri wa tren kwenda Moshi. Je, ni wapi hapa Dar naweza kupata tiketi,Na pia wakati wa kupanda treni nitapandia wapii na zipi kero na raha zilizopo ndani ya Treni,Maoni yenu muhimu ni muhimu sana
Inashangaza sana tunakuwa na treni halafu ukataji wa ticket haujawekwa mitandaoni au kwenye vituo kila mahali. Hatujui kufanya biashara na rasilimali zetu ndio maana reli zilikufa.
 
Chukua uber umueleze kuwa unaenda Dar Railway Station. Hapo utapata tiketi na maelezo yote ya safari. Hapo pia ndo mahali salama pa kupandia.
 
Mkuu nyoosha maelezo ueleweke vizuri, unataka kufanya nini ili jukwaa hili liwe msaada kwako. :oops:
Nataka kusafiri na treni kwa iyo nimeingia kwenye website hakuna maelezo yoyote yale mfano vituo vya kukatia tiketi na jinsi ya upandaji wa ndani ya treni
 
Inashangaza sana tunakuwa na treni halafu ukataji wa ticket haujawekwa mitandaoni au kwenye vituo kila mahali. Hatujui kufanya biashara na rasilimali zetu ndio maana reli zilikufa.
Yaani wana mambo ya kiswahili sana hao Trc,mie nilitegemea ukiingia kwenye mtandao ingekuwa unakata tiketi kwa njia ya Online lakini wapi halafu ndio wanategemea kuliendesha shirika kwa ufanisi yaani waswahili sana
 
Kiukweli,shirika letu lina safari ndefu. Makampuni mengi sasa hivi ili liweze kujiendesha kiufanisi teknolojia haikwepeki,ukiikwepa basi ujue hutafanikiwa aidha una ushindani au huna ushindani. We got to change they way we do business.
 
Habari zenu wana jamiiforum,

Leo jioni ninataraji kutaka kusafiri kwa kutumia usafiri wa tren kwenda Moshi. Je, ni wapi hapa Dar naweza kupata tiketi,Na pia wakati wa kupanda treni nitapandia wapii na zipi kero na raha zilizopo ndani ya Treni,Maoni yenu muhimu ni muhimu sana
Acha uongo wewe unataka kusafiri jioni ila hujui utapata vipi wabongo bana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nenda kamata K KOO unakata tiket ata saa tano sa 10 unaondoka
Siku za safari kwenda Moshi ni j3,j5,ijumaa
All the best huduma nzuri kwenye treni tu ila uku nje ni mbovu i.e ofisi za kukatia
Kama una kata daraja la 3 16,500 ukiwa na mzigo usizidi kilo 20 zaidi ya apo ni fine 9000, nkushauri kata daraja la pili23,500 utaenjoy coz utalala vzr watu wachache sana tofauti na daraja la tatu mnakua wengi kama sisimizi , chakula elfu 3000 walinyama, chips nyama ila chps kuku 4000 chakula ni kizuri kinalidhish japo kidogo, bia 2500 kwa 2000
Uwe na safari njema


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu Kituo kikuu cha Railway hapa Dar kinafahamika, maeneo jirani na Posta ya zamani... Chukua taxi au boda boda unafika fasta..
Usitegemee sana humu inaweza kufika jioni bila kupata maelekezo wapi ilipo station ya treni..

Siyo mwenyeji sana Dar ila jaribu kupanda treni la Pugu uone litakupeleka wapi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sahihi kabisa, ikiwa kampuni binafsi ya ma Bus kama Darlux tiketi unakata mwenyewe kwa mtandao kwenye simu yako, sembuse shirika kubwa la umma?? Eti mpaka uende ofisini kwao upange foleni...
Inashangaza sana tunakuwa na treni halafu ukataji wa ticket haujawekwa mitandaoni au kwenye vituo kila mahali. Hatujui kufanya biashara na rasilimali zetu ndio maana reli zilikufa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nataka kusafiri na treni kwa iyo nimeingia kwenye website hakuna maelezo yoyote yale mfano vituo vya kukatia tiketi na jinsi ya upandaji wa ndani ya treni
Hawana lolote kwenye website mkuu, bado wako kizamani kabisa, fanya tuu uende pale Railway upange foleni na mengine utajua huko huko...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom