Wapenzi wa Fm academia, twanga, akudo nyimbo za miaka ya 2002- 2012 tukumbushane hapa

toplemon

JF-Expert Member
Mar 26, 2017
4,581
4,626
Wale wapenzi wa twanga pepeta,akudo impact na fm academia nyimbo zao kuanzia 2002 mpaka 2012 tukumbushane enzi

Mimi nakumbuka

Mtu na pesa zake-twanga pepeta

Password- password ya maisha yangu naijua mimi na yako waijua wewe.....tukutane saa saba tukapata lunch kwa mama sabina yule
Hii nyimbo ya
twanga pepeta hii naipenda sana hadi leo

Fm academia
Heshima ya mwanamke-sio kila mwanamke anayekwenda bar ni malaya

Akudo impact
Mama vanessa

Walimwengu si binadamu=hawataki kuona wawili wakipendana

Miaka ya juzi juzi hizi bendi zilikua moto kisawa sawa miaka hii sijui wanakwama wapi
Haya nambie unaikumbuka ipi kali?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwana Daresalam...Twanga

Tutokapo out watu wanakujua, tukiingia popote salamu haziishi, najua mwenzangu umezaliwa hapa mjini, na hata kusoma.........

Ooh mama usiniteseee..
Ninasikitisha sana unapopigiwa simu usiku wa manane.....msg gani usiku wa manane, salamu gani saa tisa za usiku
Kujulikana kwako isiwe sababu ya kuniweka roho juu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vionjo ninavyo vikubali
"Pilipili ya shamba yawawashia nini pilipili ya shamba yawawashia nini.....eeeh mmesutwa mnamanga...."-Ali Choki

"Yeyeyeee kitimutimu kitimukitimu tumekiona leo kweli ..."-Banza stone.

"Ale twanga twanga twanga twanga twanga ..........."-Banza Stone

Hichi kionjo ilikuwa nusu tupigwe na rafiki yangu na mzee mmoja alikuwa anajenga,alitupiga mikwala na sisi tulikuwa tunamfanyia maksudi basi anatukata jicho.

"Kutesa kwa zamu ehe kutesa kwa zamu....minyaaaaato...ale nyata nyata nyata nyata eeehh...."
Banza stone

"Ale igwe igwe leleleee....igwe lele lelelele aaahhh...." Pappi Kocha.

Alafu kuna kionjo cha kihaya kakisimamia Ndada Kosovo hatari nacho hicho.



Ila yote kwa yote Banza Stone alikuwa hana mpinzani upande wa utunzi wa nyimbo zenye ujumbe.
 
Mkuu, unaweza kunipa majina ya nyimbo ulizotoa hivo vionjo hapo juu ?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Wakuu naombeni mwenye wimbo ule wa Extra Bongo una maneno haya "extra bongo wana bongo sisi site tuko fiti tunajinafasi" cha mutu ukikiona kiogopee" au anayejua jina la wimbo huo nimeutafuta sana....
 
Back
Top Bottom