Elections 2010 Wapenda CCM ndani ya JF, mnazungumziaje mwenendo wa uchaguzi na matokeo yake?

Utotole

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,604
4,259
Uchaguzi umemalizika sasa na matokeo yameshatangazwa. Ma-Rais waliochaguliwa wameshatangazwa, mmoja alishaapishwa, mwingine bado ni mteule naye ataapishwa muda si mrefu (kama bado). Wabunge nao wataapishwa mara baada ya Rais kuapishwa na wote waliopewa dhamana wataingia kazini.

Sitaki kuzungumzia mchakato wa uchaguzi na mema na mabaya yake mwaka huu maana mengi yameshasemwa na yataendelea kusemwa. Yaliyotokea wote tumeyasikia, kuyaona au hata kuyashiriki.

Matokeo ya uchaguzi mwaka huu yameonyesha sura tofauti ya kukua kwa uelewa wa wananchi katika masuala ya demokrasia kuelekea uchaguzi mkuu. Hapa naongelea kwa wale waliojitokeza kupiga kura, japo ni asilimia ndogo ya waliostahili kupiga kura. Imeonyesha kuwa watu wanaelewa kuwa katika demokrasia haitoshi tu kuwepo pale kama kisiki kisichotikisika kutokana na mizizi yako ya muda mrefu. Siku ikifika watu wanaweza kuja na sururu, shoka, hata tingatinga na kukung'oa. Tuliona kwenye kura za maoni na tumeona hayo katika uchaguzi mkuu.

Kwa muda mrefu sasa, katika chaguzi zote CCM imekuwa ikifaidi mtaji mkubwa utokanao na 'ujinga' wa watanzania walio wengi. Kutokana na CCM kuwa 'chaguo-msingi' (default party) hasa kwa sababu kimeendeleza utawala wa enzi za chama kimoja, kilipata faida ya kuwa na misingi tangu kwenye mashina na matawi. Watu wengi waliendelea kuchukulia uongozi wa mitaa, kata n.k kama sehemu ya CCM hata baada ya chama na serikali kutenganishwa. Ikawa sasa ni jukumu la vyama shindani kupeleka sera zake kwa hawa watu kwamba sasa hivi si CCM pekee iliyopo Tanzania, jaribuni na vyama vingine. Ni zoezi gumu lakini baadhi ya vyama maendeleo yake ni mazuri katika hili.

Suala ninalotaka kuzungumzia ni kuwa CCM imetumia uelewa mdogo w raia wengi juu ya siasa za vyama vingi kuendelea kuwa na 'support' mahali pengi hasa vijijini. Matokeo ya mwaka huu yanaonyesha hali inaanza kubadilika. Vuguvugu lililoanzia kwa wasomi na wale wa mijini linaelekea kuendelea hadi vijijini na hii imepelekea CCM kupoteza viti vingi vya ubunge na udiwani ikilinganishwa na chaguzi zilizopita. Hata ushindi wa Rais umekuwa mdogo sana ikilinganishwa na JK 2005. CCm ilipanga ushindi wa kishindo lakini wakati namsilikiliza Kinana akitoa tathmini ya uchaguzi, alisema CCM imepata ushindi 'mzuri' si wa 'kishindo' tena.

CCM inatakiwa ifahamu kuwa ujinga si kilema cha kudumu. Mtu mwenye akili zake ila asiyeelewa jambo fulani, akieleweshwa vizuri ataelewa tu na ujinga utamtoka. Hili ndo tunaloliona. Kama CCM itaendelea kuwahadaa watu na kutowatimizia ahadi ambazo imemwaga wakati wa kampeni; kama CCM itaendelea kukumbatia mafisadi ambao wanelekea kukiendesha chama; Kama mwenyekiti wake ambaye pia ni Rais wa Tanzania ataendelea kuufanya uenyekiti na u-Rais kuwa wa ubia na wa ki-familia; kama JK ataendelea kudanganywa na wafuasi wake, na kuendelea kudanganya wananchi akishadanganywa...(na mengineyo) na vyama-shindani vikaendeleza elimu ya uraia na haki ya mwananchi na mpiga kura wakati wa miaka mitano, na mitano tena ijayo basi inawezekana CCM hawatasema wamepata ushindi 'mzuri' tena maana watakuwa wameshindwa hata kabla ya uchaguzi.

Ujumbe hapa ni kuwa watanzania si wajinga tena na wale ambao uelewa haujawafikia, watabadilika muda si mrefu.

Ni jukumu la wapenda CCM kama kweli wapo kufanya tathmini na kujua nini wafanye ili watanzania wawaamini tena. Wasipange mbinu za kubadilisha matakwa ya wananchi kwa uchakachuaji. Waelewe kuwa enzi za kutembea gizani zimepita na hawatakiwi tena kutembea uchi wakijidanganya kwa kufumba macho wakiamini kuwa kama wao hawawaoni watu njiani (kwani wamefumba macho) basi na wtu hawawaoni...Watu wako macho sasa na wanaona.

Kazi kwenu CCM, mi yangu macho!
 
Yaelekea hakuna wapenda CCM ndani ya JF, ila kuna mashabiki tu wa CCM. Chama chenu cha mapinduzi kinahitaji utayari wenu maana vinginevyo kitapata mtikisiko zaidi ndani ya miaka mitano ijayo. Na kama katiba ikibadilishwa na kuruhusu mid-term evaluation, basi kazi ingekuwa kubwa zaidi!!
 
Uchaguzi ulikuwa ni Huru na wa Haki.....

Bado haujasimama kuitetea CCM kama mwanachama hai... Tuambie mwaelekea wapi baada ya yaliyotokea mwaka huu? Mtaendelea kuwakumbatia mafisadi walioporomosha umaarufu wa chama chenu kiasi hiki au mtaisafisha nyumba yenu upya? Hilo ndilo watani wenu tunataka kujua, siyo suala la uchaguzi kuwa huru na haki maana hilo twajua kwa hakika haukuwa huru wala haki!!
 
Huru na Haki kwenu CCM maana yake ni nini?

Hawajui maana yake kama vile Rais asivyojua kwa nini Tanzania ni maskini na wakati huo huo angombea (na kugombania) aweze kutawala zaidi huku akiahidi kuboresha maisha ya watanzania na kuwaondolea umaskini ambao hajui unasababishwa na nini, in the first place. Unaondoaje tatizo ambalo haujui kama lipo au limetokana na nini? Unatumia nguvu za sheikh Yahya?
 
Uchaguzi ulikuwa huru na haki.mimi kama mwanaCCM nachukua nafasi hii kuweka bayana kuwa CCM haijafanya kaz inayotakiwa ktk miaka 5 iliyopita.ufisadi sio siri ulikithiri kupita kiasi.swala muhimu kwa wana Ccm wenzangu ni kwamba tuwe makini sana na maisha ya watanzania kwani wao ndo wanaopiga kura.Tusijaribu kbsa kuwatetea mafisadi.kumbuka hata kama chadema ingechukua madaraka ktk uchaguz huu cases za ufisadi bado zisingeisha kwani Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.unaweza ukapata chadema ndo wangekuwa wabaya zaidi.muhimu tujirekebishe ktk miaka mitano 2weze kuyarudisha majimbo ye2 tuliyoyapoteza ktk uchaguz huu ulopita.kidumu chama cha mapinduzi
 
Uchaguzi umemalizika sasa na matokeo yameshatangazwa. Ma-Rais waliochaguliwa wameshatangazwa, mmoja alishaapishwa, mwingine bado ni mteule naye ataapishwa muda si mrefu (kama bado). Wabunge nao wataapishwa mara baada ya Rais kuapishwa na wote waliopewa dhamana wataingia kazini.

Sitaki kuzungumzia mchakato wa uchaguzi na mema na mabaya yake mwaka huu maana mengi yameshasemwa na yataendelea kusemwa. Yaliyotokea wote tumeyasikia, kuyaona au hata kuyashiriki.

Matokeo ya uchaguzi mwaka huu yameonyesha sura tofauti ya kukua kwa uelewa wa wananchi katika masuala ya demokrasia kuelekea uchaguzi mkuu. Hapa naongelea kwa wale waliojitokeza kupiga kura, japo ni asilimia ndogo ya waliostahili kupiga kura. Imeonyesha kuwa watu wanaelewa kuwa katika demokrasia haitoshi tu kuwepo pale kama kisiki kisichotikisika kutokana na mizizi yako ya muda mrefu. Siku ikifika watu wanaweza kuja na sururu, shoka, hata tingatinga na kukung'oa. Tuliona kwenye kura za maoni na tumeona hayo katika uchaguzi mkuu.

Kwa muda mrefu sasa, katika chaguzi zote CCM imekuwa ikifaidi mtaji mkubwa utokanao na 'ujinga' wa watanzania walio wengi. Kutokana na CCM kuwa 'chaguo-msingi' (default party) hasa kwa sababu kimeendeleza utawala wa enzi za chama kimoja, kilipata faida ya kuwa na misingi tangu kwenye mashina na matawi. Watu wengi waliendelea kuchukulia uongozi wa mitaa, kata n.k kama sehemu ya CCM hata baada ya chama na serikali kutenganishwa. Ikawa sasa ni jukumu la vyama shindani kupeleka sera zake kwa hawa watu kwamba sasa hivi si CCM pekee iliyopo Tanzania, jaribuni na vyama vingine. Ni zoezi gumu lakini baadhi ya vyama maendeleo yake ni mazuri katika hili.

Suala ninalotaka kuzungumzia ni kuwa CCM imetumia uelewa mdogo w raia wengi juu ya siasa za vyama vingi kuendelea kuwa na 'support' mahali pengi hasa vijijini. Matokeo ya mwaka huu yanaonyesha hali inaanza kubadilika. Vuguvugu lililoanzia kwa wasomi na wale wa mijini linaelekea kuendelea hadi vijijini na hii imepelekea CCM kupoteza viti vingi vya ubunge na udiwani ikilinganishwa na chaguzi zilizopita. Hata ushindi wa Rais umekuwa mdogo sana ikilinganishwa na JK 2005. CCm ilipanga ushindi wa kishindo lakini wakati namsilikiliza Kinana akitoa tathmini ya uchaguzi, alisema CCM imepata ushindi 'mzuri' si wa 'kishindo' tena.

CCM inatakiwa ifahamu kuwa ujinga si kilema cha kudumu. Mtu mwenye akili zake ila asiyeelewa jambo fulani, akieleweshwa vizuri ataelewa tu na ujinga utamtoka. Hili ndo tunaloliona. Kama CCM itaendelea kuwahadaa watu na kutowatimizia ahadi ambazo imemwaga wakati wa kampeni; kama CCM itaendelea kukumbatia mafisadi ambao wanelekea kukiendesha chama; Kama mwenyekiti wake ambaye pia ni Rais wa Tanzania ataendelea kuufanya uenyekiti na u-Rais kuwa wa ubia na wa ki-familia; kama JK ataendelea kudanganywa na wafuasi wake, na kuendelea kudanganya wananchi akishadanganywa...(na mengineyo) na vyama-shindani vikaendeleza elimu ya uraia na haki ya mwananchi na mpiga kura wakati wa miaka mitano, na mitano tena ijayo basi inawezekana CCM hawatasema wamepata ushindi 'mzuri' tena maana watakuwa wameshindwa hata kabla ya uchaguzi.

Ujumbe hapa ni kuwa watanzania si wajinga tena na wale ambao uelewa haujawafikia, watabadilika muda si mrefu.

Ni jukumu la wapenda CCM kama kweli wapo kufanya tathmini na kujua nini wafanye ili watanzania wawaamini tena. Wasipange mbinu za kubadilisha matakwa ya wananchi kwa uchakachuaji. Waelewe kuwa enzi za kutembea gizani zimepita na hawatakiwi tena kutembea uchi wakijidanganya kwa kufumba macho wakiamini kuwa kama wao hawawaoni watu njiani (kwani wamefumba macho) basi na wtu hawawaoni...Watu wako macho sasa na wanaona.

Kazi kwenu CCM, mi yangu macho!


Mimi si mwanachama wa chama chochote ca siasa, bali ni mtanzania nadhani kama ilivyo kwa nchi za wenzetu, wapo watu indipendent nami ni indipendent kama nikuchagua na chagua mtu si chama.
Hivyo basi kwa mtizamo wangu uchaguzi wa mwaka huu umeonyesha changamoto kubwa sana kwamba wananchi sasa wana anza kufunguka macho, wakati wa kuchagua mtu kwa vile amepabwa na nyimbo za TOT "uzuri wa chama mulolile" umekwisha. wana CCM kama wanakitakia mema chama hicho waache kukumbatia uchafu,chama wakisafishe wapo watu walioingia chamani kwa lengo la kuchumia tumbo na si kutumikia wananchama wao na umma kwa ujumla. CCM ya Nyerere haikuwa na
wasomi wengi lakini ilikuwa na wazee wenye busara wengi kina "Mtandika, Ndejebi,Budodi"na wengine wengi.Sasa hivi wazee wa busara ni wakutafuta katika chama hicho hayamkini ndo maaana maadili yanaporomoka kwa kasi sana.

Baadhi ya majibu tuliyoshuhudia yakitolewa na viongozi ktk chama ni maneno ya mtu aliye na busara ambayo hawezi kuyatamkaa, kuna wazee wameitwa "wehu" hawakujibu baada ya kuitwa hivyo nadhani hawakutaka walinganishwe na mheshimiwa aliye waita hivyo japokuwa baadhi yao wali wahii kuwa maboss wa mheshimiwa aliyewaita wehu.Naona walitumia methali inayosema "usibishane na mjinga usije ukaonekana na wewe ni mjinga",(Sikutumia mpumbavu kwa makusudi). Hilo la kutobishana na mtu ambaye umwemwelewa matatizo yake linawezekana likawa limetumiwa na baadhi ya watu ambao wameuona mwelekeo mzima wa uchaguzi kuwa na dosari lakini kwa kuepusha balaa wakaona wanyamanze kimya.Sasa siku zote kimya kingi kina mshindo CCM isibweteke ikadhani ndo mwisho.
Mara zote mwisho wa vita huwa ni mwanzo wa vita nyingine hilo walijue.

Sasa kuhusu vyama vingine vya siasa nitatoa mawazo yangu kwa ujumla, mimi binafsi huwa najiuliza kwa nini mnakuwa na utiriri wa vyama, ile nguvu ya kura ambayo huwa mnagawana gawana hamuoni kuwa inadhoofisha ushindi?, na hilo CCM inalifurahia sana "Vita vyenu huwa furaha ya kungulu".
Je hamwezi kusoma nyakati na majira na kutambua kuwa ktika eneo hili ni chama gani kina nguvu wapinzania wote mkaelekeza nguvu hapo? huo mgawanyioko unawatafuna na wengine wanaweza kutafsiri kama ni dalili za uchu wa madaraka, kama siyo ujanja wa kupandikiziwa vyama ili mgawane kula wakati CCM inazoa zote za wanachama na washabiki wake.

Ni kweli tunahitaji mtu makini kiungia Ikulu,kama Nyerere alivyosema (ni mahali pa takatifu) maana ndugu zangu tunayemwingiza ikulu tunamkabidhi hazina yote ya nchi tukipeleka mtu mroho tutalia kama mbwa wa kienyeji (mbwa wa kienyeji hulia akiwa ameangalia juu).Hivyo basi hakuna jinsi ambavyo chama kingine kile kitamwingiza mtu Ikulu kwa katiba iliyopo,ambayo inaelekea kupendelea chama kilicho madarakani maana kinatoa mianya mingi kwa kiongozi aliye madarakani kuchangua
marefali na washika vibendera(NEC, Vyombo vya dola n.k). Sasa mimi sijui mnalionaje ninyi kama timu moja inaingia na marefaa na washika vibendera kama timu ya pili inategemea ushindi.
kwa hiyo vyama vya siasa ni maoni yangu kwamba nguvu kubwa ielekezwe uibadili katiba, na uwezekano wa kuibadili ni lazima kuwe na nguvu zaidi kwenye bunge,kwa hiyo vyama vielekeze kuingiza wabunge wengi wa upinzani bungeni ili kuwezesha mabadiliko ya katiba itakayoleta demokrasia ya kweli.
 
Mimi si mwanachama wa chama chochote ca siasa, bali ni mtanzania nadhani kama ilivyo kwa nchi za wenzetu, wapo watu indipendent nami ni indipendent kama nikuchagua na chagua mtu si chama.
Hivyo basi kwa mtizamo wangu uchaguzi wa mwaka huu umeonyesha changamoto kubwa sana kwamba wananchi sasa wana anza kufunguka macho, wakati wa kuchagua mtu kwa vile amepabwa na nyimbo za TOT "uzuri wa chama mulolile" umekwisha. wana CCM kama wanakitakia mema chama hicho waache kukumbatia uchafu,chama wakisafishe wapo watu walioingia chamani kwa lengo la kuchumia tumbo na si kutumikia wananchama wao na umma kwa ujumla. CCM ya Nyerere haikuwa na
wasomi wengi lakini ilikuwa na wazee wenye busara wengi kina "Mtandika, Ndejebi,Budodi"na wengine wengi.Sasa hivi wazee wa busara ni wakutafuta katika chama hicho hayamkini ndo maaana maadili yanaporomoka kwa kasi sana.

Baadhi ya majibu tuliyoshuhudia yakitolewa na viongozi ktk chama ni maneno ya mtu aliye na busara ambayo hawezi kuyatamkaa, kuna wazee wameitwa "wehu" hawakujibu baada ya kuitwa hivyo nadhani hawakutaka walinganishwe na mheshimiwa aliye waita hivyo japokuwa baadhi yao wali wahii kuwa maboss wa mheshimiwa aliyewaita wehu.Naona walitumia methali inayosema "usibishane na mjinga usije ukaonekana na wewe ni mjinga",(Sikutumia mpumbavu kwa makusudi). Hilo la kutobishana na mtu ambaye umwemwelewa matatizo yake linawezekana likawa limetumiwa na baadhi ya watu ambao wameuona mwelekeo mzima wa uchaguzi kuwa na dosari lakini kwa kuepusha balaa wakaona wanyamanze kimya.Sasa siku zote kimya kingi kina mshindo CCM isibweteke ikadhani ndo mwisho.
Mara zote mwisho wa vita huwa ni mwanzo wa vita nyingine hilo walijue.

Sasa kuhusu vyama vingine vya siasa nitatoa mawazo yangu kwa ujumla, mimi binafsi huwa najiuliza kwa nini mnakuwa na utiriri wa vyama, ile nguvu ya kura ambayo huwa mnagawana gawana hamuoni kuwa inadhoofisha ushindi?, na hilo CCM inalifurahia sana "Vita vyenu huwa furaha ya kungulu".
Je hamwezi kusoma nyakati na majira na kutambua kuwa ktika eneo hili ni chama gani kina nguvu wapinzania wote mkaelekeza nguvu hapo? huo mgawanyioko unawatafuna na wengine wanaweza kutafsiri kama ni dalili za uchu wa madaraka, kama siyo ujanja wa kupandikiziwa vyama ili mgawane kula wakati CCM inazoa zote za wanachama na washabiki wake.

Ni kweli tunahitaji mtu makini kiungia Ikulu,kama Nyerere alivyosema (ni mahali pa takatifu) maana ndugu zangu tunayemwingiza ikulu tunamkabidhi hazina yote ya nchi tukipeleka mtu mroho tutalia kama mbwa wa kienyeji (mbwa wa kienyeji hulia akiwa ameangalia juu).Hivyo basi hakuna jinsi ambavyo chama kingine kile kitamwingiza mtu Ikulu kwa katiba iliyopo,ambayo inaelekea kupendelea chama kilicho madarakani maana kinatoa mianya mingi kwa kiongozi aliye madarakani kuchangua
marefali na washika vibendera(NEC, Vyombo vya dola n.k). Sasa mimi sijui mnalionaje ninyi kama timu moja inaingia na marefaa na washika vibendera kama timu ya pili inategemea ushindi.
kwa hiyo vyama vya siasa ni maoni yangu kwamba nguvu kubwa ielekezwe uibadili katiba, na uwezekano wa kuibadili ni lazima kuwe na nguvu zaidi kwenye bunge,kwa hiyo vyama vielekeze kuingiza wabunge wengi wa upinzani bungeni ili kuwezesha mabadiliko ya katiba itakayoleta demokrasia ya kweli.

Naamini wamekusikia, wana CCM na wale wa vyama mbadala
 
Ndugu zangu tuamke kwa sasa KATIBA MPYA ni ya lazima.
Kila mtanzania awe tayari kuidai hata kwa kuandamana. Tukipata KATIBA MPYA tutaweza kuendelea kwani itaweka maslahi ya Taifa mbele siyo maslahi ya Viongozi (ambao kwa sasa wengi wao ni MAFISADI). Na kwa chama tawala CCM FISADI anaheshimika kama mungu mtu ..........................
INCHI YETU MNAIPELEKA WAPI CCM ???????????????????????

Tukipata KATIBA MPYA, hiyo KATIBA MPYA itatupatia TUME HURU YA UCHAGUZI, TAKUKURU HURU, BARAZA DOGO LA MAWAZILI, NA VIONGOZI KUTUMIA MAGARI YA KAWAIDA. Kwani kwa sasa mawaziri, wakurugenzi wa Idara za serikali, Mkurugenzi wa halmashauri wanatumia magari ya TShs milioni 180-200 kwa kila mtu wakati mashuleni watoto hawana vitabu, wanakaa chini na mahospitali hayana dawa.

Magari ya kifahari yanatakiwa kubaki Ikulu tu. Wenzetu wa RWANDA na KENYA viongozi wote niliowataja hapo juu magari yao hayazidi cc 2000.
 
Back
Top Bottom