WaPemba wafanya kweli

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Ni mwanzo wa mapambano na wahafidhina wa CCM,hivi ndivyo inavyotakiwa ifanywe kwa wale ambao wapo mstari wa mbele katika kuona haki haifuati mkondo wake ,ikiwa Sheha amepewa mamlaka ya kutoa barua na anawanyima wakazi barua hizo au anazitoa kwa ubaguzi kutokana na shinikizo la CCM basi sasa dawa yao ndio hio imeanza kuchemka ,itabidi wazifahamu na sauti badala ya sura ,kuwa sauti hii ni ya mwanachama wa CCM hivyo tumpe barua ya kupata kadi ya Uraia na hii ni sauti ya mtu asieitakia mema CCM. Ila kitu kimoja kikumbukwe kuwa baadhi ya mikakati hii hufanywa na CCM wenyewe (Badboys) ili kuipaka matope CUF ,kuna yale yaliotokea siku za miaka ya nyuma,ulipuaji wa mabomu Unguja ,wachunguzi walitoka makao makuu ya upelelezi Dar mpaka leo hawakutoa jawabu la waliohusika,alielipukiwa na bomu kisiwani Pemba katika matayarisho ni CCM ,hakuulizwa kitu alipelekwa Dar kutibiwa ,waliokuwa wakitia vinyesi katika visima Pemba walijulikana kuwa ni CCM na wakikusanya vinyesi kwenye magereza hawakufanywa kitu ,wala hakuna hatua yeyote waliochukuliwa ,hivyo hata na hili linawezekana kabisa ni la CCM ,ili kuvipa nguvu vyombo vya dola kufanya maovu na kuonyesha kuwa Pemba kuna matatizo,ni katika mbinu za kuwafanya iwe rahisi kukwiba kura na kuwatisha watu kwa kutumia vyombo hivyo,kwa ilikwisha chunguzwa kuwa hakuna haja ya kupeleka majeshi na mapolisi kwa wingi ,ili kurudisha upotofu imewabidi wafanye lolote lile litakalowawezesha kuendelea kuweka vyombo vya dola ili kurahisisha wizi wao. Ila itakavyopigwa ndivyo hivyo itakavyochezwa ,Wenyewe wanasema Pemba peremba.

SHEHA wa Shehia ya Ole Muhogoni Mkoa wa Kaskazini Pemba Mussa Ali Kombo amemwagiwa tindikali usoni na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana.

Kamanda wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Yahya Rashid Bugi amethibitisha kutokea tukio hilo majira ya saa mbili usiku na kuahidi kuwatafuta wote waliohusika na kuwachukulia hatua kali za kisheria.

Alisema jeshi la polisi bado linafanya uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo ili kuweza kujua zaidi chanzo cha tukio hilo pamoja na kuwatia mikononi watu waliofanya kitendo hicho cha kikatili.

Chanzo cha tukio hilo inasadikiwa ni kufuatia zoezi la daftari la uendelezaji kastika daftari la kudumu la wapiga kura katika kisiwa cha Pemba,ambalo linaratibu wapiga kura wapya na wale wa zamani kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu mwakani.

Chama cha mapinduzi Mkoa wa Mjini Magharibi kimetoa taarifa kwa vyombo vya habari leo hii mjini Unguja huku kikilaani kutokea kwa tukio hilo linalotishia amani

Aidha CCM Katibu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ramadhan Abdallah Ali imeelezea kusikitishwa kwake na tukio hilo kupitia taarifa hiyo kwa vyombo vya habari

Akizungumza na gazeti hili Sheha wa Shehia ya Ole Muhogoni, Mussa Ali Kombo amesema majira ya saa mbili uziku amekutwa na mkasa huo wakati akirudi dukani kununua sirgireti baada ya kurejea msikitiki kusali sala ya ishaa ndipo alipowaona vijana mbele yake na kumwagia kitu alichokuwa hajakifahamu lakini alihisi maumivu makali kama ya kuchinjwa na kisu mwilini.

Zoezi la uandikishaji kwa wapiga kura wapiya lilianza Kisiwani Pemba katika wilaya ya Micheweni ambapo zoezi hilo mwezi uliopita.

Katika salamu za masikitiko Katibu wa huyo wa CCM alisema CCM imesikitishwa na kitendo hicho ambacho wamekiita ni cha kikatili chenye lengo la kujenga chuki na kuvuruga zoezi la daftari la kudumu la wapiga kura.

Ali alitoa amekitupia lawama chama cha wananchi CUF akidai tangu kuanza kwa daftari la kudumu la wapiga kura kimekuwa kikilalamika kwamba wafuasi wake hawaandikishwi.

'Tumepokea taarifa za kutiwa tindikali sheha wa Ole kwa masikitiko makubwa...tunaitaka serikali kuchukuwa hatua kali za kisheria pamoja na kuwapatia ulinzi masheha wote 'ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Hivi karibuni akizungumza na waandishi wa habari,katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF Seif Shariff Hamad alielezea kutoridhishwa na zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura linaloendelea katika kisiwa cha Pemba ambapo wafuasi wengi wa CU inadaiwa wamekataliwa ikiwemo pamoja na kupewa kitambulisho cha ukaazi.

Hamad alisema hadi sasa katika majimbo matano ya wilaya ya Kaskazini A Unguja watu 12,363 wameripoti katika idara ya vitambulisho kudai vitambulisho vyao, watu 2584 wamenyimwa kupewa vitambulisho ambapo katika jimbo la Konde watu 1559 wamekataliwa kuandikishwa wakati katika jimbo la Mgogoni ni watu 1237 wamewekwa kando katika zoezi hilo.

Wajumbe wa Baraza la wawakilisji wa CUF kwa nyakati tofauti waliitahadharisha serikali wakati wakichangia bajeti mbalimbali za SMZ na kuitaka kuwa makini kutokana na idadi kubwa ya wananchi kunyimwa nafasi za kujiandikisha.

Chama cha CUF kimetoa wito na kuutaka Umoja wa Mataifa kusimamia uchaguzi mkuu ujao mwaka 2010 na pia wakilitaka shirika la umoja huo la UNDP kuijiaondoa katika ufadhili wa zoezi hilo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya SMZ Suleiman Othman Nyanga alisema hakuna mtu atakayenyimwa haki ya kuandikishwa na kila mtu anatakiwa kufuata sheria.

Vituko vya uvunjaji wa amani katika kisiwa cha Pwemba aghalab hutokea wakati huu kuelekea katika uchaguzi mkuu wa nchi ambapo mwaka 1995 Afisa mmoja wa CCM Ali Mwinyi Msuko pia alimwagiwa tindikali.

MWISHO
 
Ni mwanzo wa mapambano na wahafidhina wa CCM,hivi ndivyo inavyotakiwa ifanywe kwa wale ambao wapo mstari wa mbele katika kuona haki haifuati mkondo wake ,ikiwa Sheha amepewa mamlaka ya kutoa barua na anawanyima wakazi barua hizo au anazitoa kwa ubaguzi kutokana na shinikizo la CCM basi sasa dawa yao ndio hio imeanza kuchemka ,itabidi wazifahamu na sauti badala ya sura ,kuwa sauti hii ni ya mwanachama wa CCM hivyo tumpe barua ya kupata kadi ya Uraia na hii ni sauti ya mtu asieitakia mema CCM. Ila kitu kimoja kikumbukwe kuwa baadhi ya mikakati hii hufanywa na CCM wenyewe (Badboys) ili kuipaka matope CUF ,kuna yale yaliotokea siku za miaka ya nyuma,ulipuaji wa mabomu Unguja ,wachunguzi walitoka makao makuu ya upelelezi Dar mpaka leo hawakutoa jawabu la waliohusika,alielipukiwa na bomu kisiwani Pemba katika matayarisho ni CCM ,hakuulizwa kitu alipelekwa Dar kutibiwa ,waliokuwa wakitia vinyesi katika visima Pemba walijulikana kuwa ni CCM na wakikusanya vinyesi kwenye magereza hawakufanywa kitu ,wala hakuna hatua yeyote waliochukuliwa ,hivyo hata na hili linawezekana kabisa ni la CCM ,ili kuvipa nguvu vyombo vya dola kufanya maovu na kuonyesha kuwa Pemba kuna matatizo,ni katika mbinu za kuwafanya iwe rahisi kukwiba kura na kuwatisha watu kwa kutumia vyombo hivyo,kwa ilikwisha chunguzwa kuwa hakuna haja ya kupeleka majeshi na mapolisi kwa wingi ,ili kurudisha upotofu imewabidi wafanye lolote lile litakalowawezesha kuendelea kuweka vyombo vya dola ili kurahisisha wizi wao. Ila itakavyopigwa ndivyo hivyo itakavyochezwa ,Wenyewe wanasema Pemba peremba.
Kwanza jifunze kuweka paragraph kwenye maandishi yako, Pili wacha uongo!
 
dsc01016.jpg



Sasa kuna kila dalili kuwa zoezi la uandishaji wa wapiga kura katika daftari la kudumu la wapiga Kura (DKWK) ndio litakaloiingiza nchi katika machafuko makubwa kutokana na kuzuiwa kwa watu wengi kuingizwa kwenye Daftari hilo.Hayo yamebainishwa jana(wiki iliyopita)na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, alipokuwa akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kiwanja cha Herous Mkwajuni Kibeni,Mkoa wa Kaskazini Unguja.Katika mkutano huo uliokusudiwa kuhitimisha ziara za Katibu Mkuu huyo katika wilaya ya Kaskazini ‘A', Maalim Seif aliwaambia wananchi kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ikishirikiana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na Idara ya Vitambulisho imeandaa mpango maalumu unaokusudiwa kuwaengua katika zoezi la uandikishaji kiasi ya Wazanzibari 80,000 kufikia mwakani ambapo zoezi hilo litakuwa limekamilika."Hawa jamaa wana mpango maalum wa kuwanyima Wazanzibari haki yao ya kupiga kura. Wanajuwa kwamba bila ya kufanya hivyo, hawana uwezo wa kushinda Zanzibar. Lakini tunasema kwamba, mara hii hatukubali, hatukubali, hatukubali. Wanavyotaka tunataka. Wakitaka iwe noma, itakuwa noma kwenye nchi hii mara hii," Alisema Maalim Seif kwa hasira huku akishangiliwa na wafuasi wake.

ZANZIBAR YETU BLOG WEB.

msisitizo ni wangu.
 
wazanzibari wanaboa sana

kwa nini hawatakikujiunga na JF?


But who knows inawezekana ni fitna za waTanganyika ndizo zinazowatisha
 
Huyu Seif kwa kutaka public sympathy hajambo. Pia ni mtaalamu sana wa kutafuta support ya kimataifa. Huko UN ahesabu maumivu kwa kuwa CCM walishawapa shule kuwa CUF chama cha magaidi! Sasa hivi hata wapige kelele vipi hawatapenya UN na nchi za Ulaya kuwaunga mkono. Tz bara kwenyewe nyumbani hawana kitu, ni chama cha wapemba tu, ije iwe UN? Kufulia kubaya jamani!
 
Ikifikia mahali kila kiongozi awe analindwa na askari kuanzia mjumbe wa nyumba kumi mpaka juu, basi hapo ndipo tutajifunza kuwa haki ni bodyguard mkubwa sana wa viongozi, na dhulma kila siku huleta maafa na majuto. Hapa ndiyo kampeni za uchaguzi hazijaanza je zikianza kutakuwa na utulivu kweli.

Kwani wakiwaandikisha halafu wawaibie kura kama kawaida na kuitisha muafaka kutakuwa na ubaya gani?. CUF nao haya yote wameyataka ule ungangari wao umekufa kabisa ndiyo maana wanatiwa vidole tu, wanatiwa vidole vya machoni wao wanacheka tu. Ngangari irudi ndiyo haki itapatikana, mkianza vitisho vya "kucheza itakavyopigwa, mtajikuta mnachezo Bluzz wakati inayopigwa ni sindimba.
 
Naamini serikali ya muungano inacheza na moto kwani taarifa nilizonazo kuna vikundi vya wazawa vina record haya matukio na wako kwenye mfuko wa umoja wa Ulaya kwa hiyo CCM isifikiri inajificha gongo nje .
 
Kwa taarifa yenu huo ni mwanzo tu kubwa lijalo,hata usalama wa Taifa kumbe wamechoka na utumwa huu wa CCM ,wamechoka kutumika ,inasemekana japo hawajitokezi kama mimi,lakini kuna hatari kubwa ya wanaotuma na kutumiliwa kuanikwa kwa ushahidi wa kideo na vinasa sauti ambavyo huchukua hata sauti ya kufusa ,kideo na sauti hizo zimekuwa na bei kwa vyama vya upinzani,maana ni mali sana kwa wakati huu tunaoelekea nao,dau la chini kabisa ni 50,000 na kideo inaweza kufika kwenye laki tano,WaChadema nawapa mbinu hizo za kununua mikakati ya CCM inayoshirikisha vyombo vya dola ,kama vile walivyoekewa wabunge fulani chini ya vitanda pale DODOMA ,kubwa ambalo ni hatari ni kuchomwa moto kwa wale wanaotumiwa kununuwa vipande au shahada ya mpiga kura ,hawa kwa taarifa iliyopo watanadiwa kama wezi na hapo ndipo watakapoonja joto ya tairi. MaCCM mnayo kazi kubwa mwakani ,sio nawatisha ila hata Badboys wa CCM wako mbioni kupanga mikakati ni vipi watalihusisha jeshi na polisi katika kuwalinda. Na hii ifahamike safari hii jua limekuchwa si Pemba peke yake bali Tz nzima ,walokole wa CCM watakiona cha moto ,kilichomfanya Jogoo kuwika alfajiri.
 
Mungu iokoe nchi yetu na matatizo ya kisiasa,kwa kweli hali inatisha na kwa jinsi ccm wanavofanya,naona safari hii wananchi wamechoka,jamani hayo ya kukataliwa watu kupiga kura tena ni waznz halisi ambao hawana sababu ya kukataliwa,yameanza pemba,jamani bado unguja,tujue tu ikiwa hali hii haijarekebisha basi tujue tuna kazi nzito huko mbele,kweli mznz ananyimwa haki yake ya kupiga kura? kwa sababu gani? hana kitambulisho? hana pasport? hana driving lincence? kwa maana hiyo huyo si mznz? kwa maana hiyo akaandikishe wapi? akapige kura wapi? basi mfukuzeni kwenye hiyo nchi yenu! mwambieni aende kwenye nchi yake! duh! hii ndo ccm.. kwa kweli hali inatisha,jamanwasaidieni waznz la sivyo mwaka huu watauliwa wengi kuliko miaka iliyopita.. majuto ni mjukuu
 
wazanzibari wanaboa sana

kwa nini hawatakikujiunga na JF?


But who knows inawezekana ni fitna za waTanganyika ndizo zinazowatisha

GT
taadab tafadhali.juzi timu ya u-17 ya MJINI MAGHARIBI imeifunga TABORA 2-1 katika fainali za copa coca cola mbele ya alhaj JK.
 
Jamanwasaidieni waznz la sivyo mwaka huu watauliwa wengi kuliko miaka iliyopita.. majuto ni mjukuu

Tutauwana ,maana depo zote tutazipiga kiberiti kuanzia Pemba Unguja hadi Tanganyika,ila ukumbuke watakaochoma moto ni hao hao CCM wakisaidiwa na vyombo vya dola kama walivyolipua mabomu na transformer halafu uchunguzi haukujulikana umeishia wapi ,ila wawasingizie WaPemba na kuwapandisha chati.
 
Tutauwana ,maana depo zote tutazipiga kiberiti kuanzia Pemba Unguja hadi Tanganyika,ila ukumbuke watakaochoma moto ni hao hao CCM wakisaidiwa na vyombo vya dola kama walivyolipua mabomu na transformer halafu uchunguzi haukujulikana umeishia wapi ,ila wawasingizie WaPemba na kuwapandisha chati.
ccm wanatafuta njia hivi sasa ya kuhakikisha uchaguzi znz haufanyiki,sasa cuf na wananchi wa znz wawe makini sana kwa hilo,miongoni mwa mambo hayo ni kujaribu kuchochea vurugu ili wapate mwanya wa kuchafua uchaguzi..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom