Kumekuwa na hisia kwamba Zanzibar kwa kuungana na tanganyika aka Tanzania bara, kuna wanyima fursa za kufanya nchi yao kuwa na maendeleo, kama kuifanya Zanzibar iwe Duty Free Port kama ilivyo Dubai , au nafasi ya kujiongoza wao wenyewe vizuri zaidi bila ya kubanwa na Tanganyika(Tanzania Bara), lakini wakati huo huo wanatakiwa waangalie mazuri au mabaya ya kuwa nje ya muungano, kwa kuiangalia Comoro ambayo ina hali kama yao au twawenza kusema ni binamu zao.
Je, kwanini Comoro wameshindwa kufanya visiwa vyao kuwa ni duty free port kama ilivyo dubai?
Sana sana utawaona wa comoro hao hao wakienda dubai kununua mahitaji yao ya biashara au kuja tanzania bara, pili demokrasia yao pia imekuwa ya mashaka mashaka kutokana na kila kisiwa kuona kingine kina ibana, kiasi cha kusababisha umoja wa afrika kwenda kumuondoa kiongozi moja aliye taka kungangania madaraka bila kujali katiba na haki za visiwa vingine.
Sasa Zanzibar hiyo inayo taka kujitenga inaweza vipi kulinda maslahi ya Pemba au Unguja, maana dalili hizo tuliziona wakati wa komandoo alivyo taka kuendelea kuwa madarakani hata pale muda wake ulivyoisha na katiba kuto mruhusu kugombea tena.
Na kuhusu mafuta wataalamu wana sema yapo kati ya Tanga na pemba sasa Unguja watafaidika vipi ikiwa nao Wapemba watasema sisi ni weupe saana kuliko Waunguja hivyo tunataka kujitenga?
Ndipo hapa tunapo ikumbuka kauli ya Mwl Nyerere kwamba nje ya muungano , kuna sisi wanzanibari na wao ni wanzanzibara na akitoka hapo sisi wapemba wao wa unguja,
Je, kwanini Comoro wameshindwa kufanya visiwa vyao kuwa ni duty free port kama ilivyo dubai?
Sana sana utawaona wa comoro hao hao wakienda dubai kununua mahitaji yao ya biashara au kuja tanzania bara, pili demokrasia yao pia imekuwa ya mashaka mashaka kutokana na kila kisiwa kuona kingine kina ibana, kiasi cha kusababisha umoja wa afrika kwenda kumuondoa kiongozi moja aliye taka kungangania madaraka bila kujali katiba na haki za visiwa vingine.
Sasa Zanzibar hiyo inayo taka kujitenga inaweza vipi kulinda maslahi ya Pemba au Unguja, maana dalili hizo tuliziona wakati wa komandoo alivyo taka kuendelea kuwa madarakani hata pale muda wake ulivyoisha na katiba kuto mruhusu kugombea tena.
Na kuhusu mafuta wataalamu wana sema yapo kati ya Tanga na pemba sasa Unguja watafaidika vipi ikiwa nao Wapemba watasema sisi ni weupe saana kuliko Waunguja hivyo tunataka kujitenga?
Ndipo hapa tunapo ikumbuka kauli ya Mwl Nyerere kwamba nje ya muungano , kuna sisi wanzanibari na wao ni wanzanzibara na akitoka hapo sisi wapemba wao wa unguja,