Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,337
113,178
Wanabodi,

Tangu baada ya Uingereza kupiga kura kujitoa kwenye EU, wanabodi wetu humu ambao ni Wanzanzibari, wanashadadia sana uamuzi huo, na kushinikiza wananchi wa Zanzibar nao, wapewe fursa ya kupiga kura ya maoni kwa kuulizwa kama bado wanataka kuendelea kusalia kuwa ndani ya muungano wetu, au wanataka kujitoa!. Wanaotaka kujitoa wakishinda, utaratibu wa jinsi ya kuuvunja muungano huu adhimu ziandaliwe, tuuvunje rasmi huu muungano wetu, na tuachane kwa amani, kuliko kuendelea huku baadhi ya wenzetu ni kila siku malalamiko, manung'uniko, na ghubu lisiloisha la kutwa kucha!.

Swali kwa wenzetu wa Zanzibari, sheria ya kura ya maoni si mnayo?!, sasa nini kinachowazuia kuitumia sheria hiyo kupiga hiyo kura ya maoni kuhusu muungano?!.

Kwa msio jua kuwa wenzetu Zanzibar, waliishaipitisha sheria hiyo ya kura ya maoni toka mwaka 2010, na ndio iliyotumika kuunda SUK!.

Kura ya Maoni Zanzibar ni Sheria Nambari 6 ya 2010 kuhusu uendeshaji wa kura ya maoni ilipitishwa na Baraza la Wawakilishi mnamo mwezi wa Machi 2010 na kutiwa saini na Mheshimiwa Rais Karume mnamo mwezi wa Aprili 2010.

Tayari sheria hiyo iliishatumiwa na wananchi wa Zanzibar walipopiga kura ya maoni siku ya
Jumamosi tarehe 31 Julai 2010. Kura hiyo ilikuwa na lengo la kutafuta ridhaa ya wananchi wa visiwa hivyo vya Unguja na Pemba, kuamua iwapo wanalikubali wazo la kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010.

Auamuzi wa kupigwa kwa kura hiyo ya maoni ulianzia katika kikao cha BLW ambacho kilipitisha Azimio la Baraza kufanywa kura ya maoni (referendum) iliyowashirikisha wananchi wa Zanzibar moja kwa moja katika kupata ridhaa ya wananchi kuanzisha mfumo na muundo wa Serikali ya
Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

Kura hiyo iliendeshwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na kwa mujibu wa Kifungu cha 11(1) cha
Sheria ya Kura ya Maoni Nambari 6 ya 2010, ushindi wa Kura ya Maoni utaamuliwa kwa
wingi wa kura. Hivyo, kwa mujibu wa matokeo hayo, Wazanzibari waliopiga kura
ya NDIO kuunga mkono kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SUK ikaendwa!.

Hayo yote yalifanyika Zanzibar bila kuishirikisha JMT, hadi ninavyozungumza hapa, japo SUK inatambuliwa rasmi na serikali ya JMT, lakini hadi leo, Katiba ya JMT ya 1977, bado haitambui SUK, hakuna kipengele chochote kinachoitambua SUK, wala katiba yetu haiwatambui wale makamo wawili wa rais wa Zanzibar, bali bado inamtambua Waziri Kiongozi ambaye doesn't exist anymore!.

Mabadiliko hayo ya Katiba ya Zanzibar ya 2010, yalikiuka katiba ya JMT na kuuvunja rasmi muungano kikatiba kwa katiba hiyo kuitangaza Zanzibar kuwa ni nchi, wakati katiba ya JMT inatamka nchi ni moja tuu JMT, na kuitambua Zanzibar kama sehemu ya JMT!.

Katiba hiyo ya Zanzibar ilivunja mamlaka yote ya Bunge la JMT, na mamlaka yote ya rais wa JMT, kwa kumtangaza rais wa Zanzibar ndio mkuu wa nchi ya Zanzibar na Amiri Jeshi Mkuu wa Vokosi vya SMZ!, na kuamua sheria yoyote itakayotungwa na Bunge la JMT, haitatumika Zanzibar mpaka BLW liridhie!, hii ni dharau kiasi gani kwa rais wa JMT na Bunge la JMT?!.

Kama yote haya yaliweza kufanyika bila kuishirikisha JMT, sasa ni nini kinachowashinda Wazanzibari kujiitishia kura yake ya maoni, kuamua kama isalie katika muungano au ijitoe?!.

Sasa tumechoshwa na hizi kelele, hivyo natoa wito kwa wenzetu Wazanzibari, waamue moja, ama waache kelele watulie, ama wafikie maamuzi waamue!.

Nawatakia Jumapili Njema.

Paskali
NB. Paskali ni muumini wa falsafa ya Nyerere kuhusu muungano, Nchi Moja, Serikali Moja chini ya Rais Mmoja wa JMT!, ila pia ni mtu mwenye maslahi fulani binafsi na Zanzibar!.

Rejea.
Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, Then "Twende kwenye Serikali Moja!.

Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?
Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?! .
Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano?
Je, wajua kuwa kuna uwezekano Tanzania sio nchi halali Kisheria ...
Zanzibar: Japo SMZ ya SUK sio de jure tena bali ni de facto ...
CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima .
Je, kunahitajika affirmative action ili Mzanzibari aweze tena
Muundo wa Serikali Tatu ni Illegal, Unjustifiable, na Ni Kuvunja ...
Kumbe Sultan Jamshid Alifurahia Kuuawa kwa Karume!. Alitaraji ..
Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein ...
Zanzibar Issue: Kwanini watu wanapiga kelele tu bila kuchukua ...
Balozi Karume: 'CCM pekee iwe inasimamisha mgombea urais Zanzibar
Kuna haja ya kuhofia kurudiwa Uchaguzi Zanzibar? |
Mbowe Alipua Bomu la Siri ya Ushindi Wa CCM Zanzibar
Imethibitishwa pasi na shaka kuwa CUF Ilishinda, Zanzibar ...
Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano ...
Inawezekana Vipi Zanzibar Hakuna Div I, Div II, wala Div III , Wao ..
Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na .
 
Mkuu Pasco

Hoja yako inaweza kuangaliwa juu juu na kuonekana imekosa utashi wa kisheria
Kwa hakika ulichokieleza ni sahihi kabisa

Hoja inayoangaliwa ni kuwa kujitoa katika muungano ni si suala la nchi likihusisha JMT
Na kikatiba ndivyo inavyopaswa kuwa kwa mujibu wa katiba ya sasa

Hata hivyo, tayari katiba ya sasa 'ilinyimwa' uhalali na Zanzibar kwa sharia ya kura ya maoni ya 2010. Zanzibar wakawa na mamlaka ya kuamua mambo bila kushirikisha JMT

Hivyo hakuna tatizo endapo wanataka kura ya maoni.
Sheria ile ile waliyoitumia kuanzisha SUK kinyume na taratibu na ambayo SUK haitambuliwi na JMT waitumie kuamua hatma yao

Hakuna sababu za Wazazibar kusubiri majadiliano na JMT, hawakusubiri kuunda SUK iweje leo wasubiri?

Mwaka 2010 hapa jamvini tukiwa na wenzetu wengine waloamua kuweka utaifa pembeni kwa muda, tulionya,Kikwete ame set bad precedent kwa siku za usoni, na hii ni moja

Wazanzibar badala ya kulalamika wanaonewa, wanataka mabalozi Zaidi wanataka kila kitu, watumie BLW lililopo iwe halali au la, kuamua hatma yao.

Mkuu una point kubwa sana kwa bandiko hili
 
Naam. Wazanzibar wajiamulie wenyewe wanayoytaka. Hata sisi watu wa Tanganyika tupige kura tuwaachie nchi yao nasi tubaki na yetu. Tumechoka kuyasikia manung'uniko yao wakidai wanaonewa kila kukicha. Mh Mbunge Ally Nkasi amekuwa akiyaongelea haya Mara nyingi Sana na siku zote imekuwa mwiba Kwa Wazanzibar.
 
Kuamua kuichagua CCM kwa zaid ya 90% kwny uchaguzi wa March 20,2016 ni ushahid tosha wanahitaji kuendelea na Serikal mbili kwny Muungano wetu.
 
Ni mara chache sana kura ya maoni inatoa suluhu kwa matatizo ya muungano.
Mara nyingi kura ya maoni ni hukumu ya umaarufu wa mtu au chama wakati wa kampeni yake.
Iko wazi CUF ni maarufu Zanzibar na Maalim ni maarufu zaidi.
Hivyo ni kama kusema, matokeo ya kura ya maoni anayo Maalim Seif.
Binafsi nataka kuuona Muungano ukiendelea, ila muungano wenye muundo bora, unaotoa suluhu kwa kero zilizopo.
Ule muungano wa kichawi wa kuchanganya udongo ndio shida.
Kile kitendawili ndio kimepelekea a racist union that we have na kuigeuza Zanzibar kuwa koloni la Tanganyika!
 
Mkuu Pasco

Hoja yako inaweza kuangaliwa juu juu na kuonekana imekosa utashi wa kisheria
Kwa hakika ulichokieleza ni sahihi kabisa

Hoja inayoangaliwa ni kuwa kujitoa katika muungano ni si suala la nchi likihusisha JMT
Na kikatiba ndivyo inavyopaswa kuwa kwa mujibu wa katiba ya sasa

Hata hivyo, tayari katiba ya sasa 'ilinyimwa' uhalali na Zanzibar kwa sharia ya kura ya maoni ya 2010. Zanzibar wakawa na mamlaka ya kuamua mambo bila kushirikisha JMT

Hivyo hakuna tatizo endapo wanataka kura ya maoni.
Sheria ile ile waliyoitumia kuanzisha SUK kinyume na taratibu na ambayo SUK haitambuliwi na JMT waitumie kuamua hatma yao

Hakuna sababu za Wazazibar kusubiri majadiliano na JMT, hawakusubiri kuunda SUK iweje leo wasubiri?

Mwaka 2010 hapa jamvini tukiwa na wenzetu wengine waloamua kuweka utaifa pembeni kwa muda, tulionya,Kikwete ame set bad precedent kwa siku za usoni, na hii ni moja

Wazanzibar badala ya kulalamika wanaonewa, wanataka mabalozi Zaidi wanataka kila kitu, watumie BLW lililopo iwe halali au la, kuamua hatma yao.

Mkuu una point kubwa sana kwa bandiko hili
MkuuMkuu Nguruvi heshima kwako.
Kwa wa Zanzibar na hii set up ya mfumo wa utawala itakuwa ni vigumu sana kuitisha kura ya maoni kuhusu kujitoa katika muungano huu, sababu kuu wanufaika wakubwa wa huu muungano ni CCM Zanzibar ambao kwa mfumo huu unawapa nafasi ya kuendelea kubakia madarakani wakitumia JMT.

Huu muungano unalindwa na kudumishwa Dodoma, nina imani kama si nguvu za dola zilizokuwa nyuma ya Jecha visiwa hivi vingekuwa chini ya Maalim Seif ambaye CCM hawaamini hatma yao chini yake. Rejea kauli ya Mkapa kuwa muungano utalindwa kwa gharama yeyote na akaonyesha kwa vitendo kwa kumwaga damu mwaka 2001, hata uchaguzi uliopita ilikuwa hivyo.

Tatizo kubwa ni unafiki mkubwa waliokuwa nao wa Zanzibari, ndani ya wabunge na wawakilishi wa CCM wanalalama na kulaumu, lakini deep within wanajua kuwa bila uwepo wao CCM wao hawatasalia madarakani kwa hiyo hata ile dhamira ya wazanzibari walio wengi ya kutaka kuwa huru nje ya muungano kwa kiu ya madaraka hawatokubaliana nayo.

Na wakiitisha kura ya maoni fairly muungano unaodumishwa na kufanywa imara kwa vifaru vya kivita hautodumu, sababu hakuna uchaguzi wowote ambao CCM hata ASP waliowahi kushinda kihalali. BWZ liko chini ya CCM, bunge licha ya kuwa na wabunge wengi wa CCM bado kwa maelekezo ya ofisi kubwa wabunge wote wa upinzani outspoken wanabanwa na kuwekewa mizengwe wasisikike.

Unadhani kwa kaliba ya wabunge kama Lusinde na bosi wao Tulia au kwenye BLW kuna anayeweza kuanzisha na kuruhusu motion ya kura ya maoni ya Zanzibar kujitoa kwenye muungano? Kwa maamiri jeshi tulio nao(Magufuli na Dk Shein) Sioni wapi itakapochipulia
 
Ni mara chache sana kura ya maoni inatoa suluhu kwa matatizo ya muungano.
Mara nyingi kura ya maoni ni hukumu ya umaarufu wa mtu au chama wakati wa kampeni yake.
Iko wazi CUF ni maarufu Zanzibar na Maalim ni maarufu zaidi.
Hivyo ni kama kusema, matokeo ya kura ya maoni anayo Maalim Seif.
Binafsi nataka kuuona Muungano ukiendelea, ila muungano wenye muundo bora, unaotoa suluhu kwa kero zilizopo.
Ule muungano wa kichawi wa kuchanganya udongo ndio shida.
Kile kitendawili ndio kimepelekea a racist union that we have na kuigeuza Zanzibar kuwa koloni la Tanganyika!
Muungano huu kwa jinsi ulivyo ni ngumu kuwa ndani ya mioyo ya watanzania walio wengi, na sijui wapi uliwahi kufanikiwa na sisi siyo kisiwa, na adui mkubwa wa muungano wa kweli mark my words ni CCM! Hawataki marekebisho yeyote kwenye muundo huu wa muungano wanaogopa ku relinquish their hold in power, wanajua hawawezi kushinda Zanzibar kihalali na trend ya kushindwa ikianza inawezekana ikaingia Tanganyika. Kama tunapenda muungano basi tutengeneze muungano imara na bora wa Afrika mashariki siyo huu muungano wa kishirikina na kichawi usioulizwa wala kukosolewa
 
Pasco!! Unachozungumza ni sawa!! Lakini kwa bahati mbaya hilo haliwezi kutokea leo labda miaka 100 ijayo. Hatujafkia demokrasia ya Uingereza na uzuri wewe mwenyewe umeona mgongano wa katiba ya JMT na katiba ya Zanzibar.
 
Kwanza hiyo sheria ya kura ya maoni ilikuwa mahususi kuhusu kuunda SUK na wala si jambo lingine lolote,pili hata kama ingekuwa inahusu kuhoji muungano lakini kuna wenye mamlaka ya kuitisha hiyo kura si jambo la mtu yeyote tu anaweza kuamua,sasa inashangaza mtu mwenye akili timamu kuja na mawazo ya kipuuzi kiasi hiki ilihali anajua kabisa wengi wa hao wanaolalamikia muungano hawana mamlaka yoyote lakini pia muanzisha uzi anashangaza sana kuwashambulia Wazanzibar utadhani ni wao tu wanaolalamikia huu muungano wakati anajua kabisa hata upande wa Tanganyika wapo wasioutaka,Naamini ni chuki tu hasa za udini ndio zimemsukuma kuanzisha mada hii si kingine.
 
Kwanza hiyo referenduma kura ya maoni ilikuwa mahususi kuhusu kuunda SUK na wala si jambo lingine lolote,pili hata kama ingekuwa inahusu kuhoji muungano lakini kuna wenye mamlaka ya kuitisha hiyo kura si jambo la mtu yeyote tu anaweza kuamua,sasa inashangaza mtu mwenye akili timamu kuja na mawazo ya kipuuzi kiasi hiki ilihali anajua kabisa wengi wa hao wanaolalamikia muungano hawana mamlaka yoyote lakini pia muanzisha uzi anashangaza sana kuwashambulia Wazanzibar utadhani ni wao tu wanaolalamikia huu muungano wakati anajua kabisa hata upande wa Tanganyika wapo wasioutaka,Naamini ni chuki tu hasa za udini ndio zimemsukuma kuanzisha mada hii si kingine.
Umeeleza vyema kuhusu nani mwenye mamlaka ya kuitisha hiyo referendum, lakini bahati mbaya umekuwa harsh isivyotakiwa. Mara mawazo ya kipuuzi, mara udini, aaaaaa sheikh wangu vumilia bado siku kidogo tutaanza kula mchana na nadhani hata hizo hasira zitaisha.
 
Wana bodi
Si vizuri wala si uungwana kumwita mwenzako kizabizabina, lakini kauli za ndugu yangu huyu wa kulazimishwa nashurutika kumsanifu hivyo.
PASCO anasema

  • Tangu baada ya Uingereza kupiga kura kujitoa kwenye EU, wanabodi wetu humu ambao ni Wanzanzibari, wanashadadia sana uamuzi huo, na kushinikiza wananchi wa Zanzibar nao, wapewe fursa ya kupiga kura ya maoni kwa kuulizwa kama bado wanataka kuendelea kusalia kuwa ndani ya muungano wetu, au wanataka kujitoa!.
JIBU: Si wazanzibari tu waliofurahia Uamuzi huo na si kwa ajili ya kujiondoa UK kujiondoa kutoka EU, lakini vipi Serikali ya Uingereza jinsi ilivyojali na kuisimamia demokrasia kwa vitendo na kuheshimu uamuzi wa raia wake.
  • Swali kwa wenzetu wa Zanzibari, sheria ya kura ya maoni si mnayo?!, sasa nini kinachowazuia kuitumia sheria hiyo kupiga hiyo kura ya maoni kuhusu muungano?
JIBU: Tunaogopa kukusanywa na kupelekwa bara na kufunguliwa mashtaka ya ugaidi, kama waasisi wa mawazo kama hayo yalivyowakuta
  • japo SUK inatambuliwa rasmi na serikali ya JMT, lakini hadi leo, Katiba ya JMT ya 1977, bado haitambui SUK Mabadiliko hayo ya Katiba ya Zanzibar ya 2010, yalikiuka katiba ya JMT
JIBU:1.Kipengele gani cha Katiba ya JMT kinachoelezea hiyo " supremecy" dhidi ya Katiba ya SMZ.
2.Mabadiliko yaliofanywa 2010 tena katika Katiba ya Zanzibar na kuzaliwa kwa SUK vipi yatakuwemo kwenye Katiba iliotengenezwa 1977 na kuitambua SUK ambayo wakati huo haijazaliwa!

  • falsafa ya Nyerere kuhusu muungano, Nchi Moja, Serikali Moja chini ya Rais Mmoja wa JMT!, ila pia ni mtu mwenye maslahi fulani binafsi na Zanzibar!.
JIBU: Unamzulia marehemu Nyerere, hajawahi kusema hivyo mbele ya Karume mwasisi wa Muungano wala pahali popote pale na amekuwa muumini wa serikali mbili ya "tatu iliojificha" na alitetea hilo na kulitamka bayana hata pele alipochukua uamuzi wa kibabe kumfukuza Alhaj Jumbe, Rais wa Zanzibar aliechaguliwa kwa asilimia 84% na kusema kwa kejeli kuwa 1+1+=3
  • Katiba hiyo ya Zanzibar ilivunja mamlaka yote ya Bunge la JMT, na mamlaka yote ya rais wa JMT, kwa kumtangaza rais wa Zanzibar ndio mkuu wa nchi ya Zanzibar na Amiri Jeshi Mkuu wa Vokosi vya SMZ!, na kuamua
JIBU:Hili ni dhihirisho kuwa hakuna Katiba iliokuwa juu ya mwenziwe
  • sheria yoyote itakayotungwa na Bunge la JMT, haitatumika Zanzibar mpaka BLW liridhie!, hii ni dharau kiasi gani kwa rais wa JMT na Bunge la JMT?!
JIBU: Hili limo kwenye Katiba zote mbili ya SUK na JMT na hukueleza yote ya kuwa kwanza lazima ipatikane 2/3 ya wabunge wote kutoka Zanzibar1
  • Kama yote haya yaliweza kufanyika bila kuishirikisha JMT, sasa ni nini kinachowashinda Wazanzibari kujiitishia kura yake ya maoni, kuamua kama isalie katika muungano au ijitoe?!.
JIBU: Kinachotushinda kuitisha kura ya maamuzi ni vifaru vyenu, ma-bazooka, Rocket Launhers na magari ya washawasha na yale mambo wanayoyadai masheikh waliopelekwa bara kufanyiwa.

Kura zote za maoni ziliitishwa kwa baraka za JMT wazanzibari waliamua k.m. walisema; kwa zaidi 60% wanataka serikali ya Mkataba badala ya mfumo huu wa muungano Je, matokeo yake uliyaona? Jaji Warioba ameyatupilia mbali!
 
Hakuna sababu za Wazazibar kusubiri majadiliano na JMT, hawakusubiri kuunda SUK iweje leo wasubiri?
Inachekesha sana, nimemsikia kwa masikio yangu mawili jinsi ya Dr.Kikwete alivyojinasibu vipi ameweza kusimamia mpaka maridhiano ya kisiasa Zanzibar kupatikana; halafu leo eti unasema JMT haikushirikwishwa. Lipi CCM Zanzibar walifanye bila ya ridhaa ya Dodoma? hawawezi hata kuweka mgombea wa Urais wamtakae. Acha kusinzia, Zinduka.
 
Kuamua kuichagua CCM kwa zaid ya 90% kwny uchaguzi wa March 20,2016 ni ushahid tosha wanahitaji kuendelea na Serikal mbili kwny Muungano wetu.
Kuamua kwa zaidi ya asilimia 60% bila ya kususiwa na vyama, kwenye Tume ya Warioba kwa mfumo wa Muungano wazanzibari ni ushahidi tosha kuwa watu wanahitaji Serikali ya yenye Mamlaka kamili, ili watu wapumuwe!
 
Sasa kibaraka atakubali vipi wananchi wapige kura ya maoni wakati hapo kawekwa na wanakitengo labda wanakitengo waridhie vinginevyo hata wakipiga kura Leo nyeusi itakua njano I meant truth will not publicized.
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom