Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja

Tunaongea sana ila katika duania hakuna taifa linalojitambua linaruhusu kataifa kadogo kujiuendesha karibu na mipaka yake. Ndo yaliyopo Macao, Taiwan, Hong Kong, Gilblatar, hata visiwa vingi vidogo vinavyo zunguka Marekani, UK, Uholanzi, Ufaransa, Uturuki, Urusi, n.k.

Kwa maana moja hata nyingine, huwa watawala hawako radhi kuachia maeneo kama haya. Sisi tunalalamika ila itabaki hivyo.
 
Wazanzibar wengi hawajui wanataka nini. trust me. wapo hivyo.... hata wakipitisha hiyo kura ya maoni wenyewe kwa wenyewe watasalitiana. Mfano mzuri tu kwenye maoni ya katiba mpya na pia hata kwenye Bunge la Katiba utaona ni wanafiki sana. Wazanzibar wanapenda kuwa na jambo la kuzungumzia kwa muda mrefu na libaki kuwa hilo hilo. nimekaa nao nawafaham yaani hawatak jambo lishe. isipokuwa kama hilo jambo laleta madhara kwao ndo watasema bore lishe. TANGANYIKA TUTAWAUNGA TU watake wastake. Tutawaunga.
 
Wazanzibar wengi hawajui wanataka nini. trust me. wapo hivyo.... hata wakipitisha hiyo kura ya maoni wenyewe kwa wenyewe watasalitiana. Mfano mzuri tu kwenye maoni ya katiba mpya na pia hata kwenye Bunge la Katiba utaona ni wanafiki sana. Wazanzibar wanapenda kuwa na jambo la kuzungumzia kwa muda mrefu na libaki kuwa hilo hilo. nimekaa nao nawafaham yaani hawatak jambo lishe. isipokuwa kama hilo jambo laleta madhara kwao ndo watasema bore lishe. TANGANYIKA TUTAWAUNGA TU watake wastake. Tutawaunga.
Na ni watu wa kubadilika badilika.

Leo wanasema wanaogopa majeshi vinginevyo wangekuwa na kura ya maoni! Walipokaa mwaka 2010 hawakuogopa mabomu! Nani aliwasumbua?

Halafu wanasema eti wanataka muungano wa mkataba

Hivi nani amewapa mamlaka ya kuamua aina ya muungano!
Kwa nguvu gani na umuhimu gani wanaweza kusema wanataka abcd

Tunajua kwa huu muungano wao ni mzigo tu.
Hawana hoja nyingine zaidi ya kutaka mablaozi na mafao tu

Utashangaa wanasema hawataki muungano, lakini wanataka mkataba

Tunasema hivi mkataba na ZNZ utakuwa kupitia EAC. Period

Wakitaka waondoke wazima wazima, na hawana sababu za kusubiri.
Wabunge wao wasije Dodoma, wamwite makamu wa Rais, na wale zaidi ya laki 6 warudi kwao tu. Muungano wasioutaka utafikia mwisho

Tumechoka na kelele za kila siku, majukumu yakiweka wanakimbia!

Ni wakati wznz sasa wazungumzie majukumu n.k. si kila siku kulalamaaa tuu , tunataka, tupewe n.k. Wakiambiwa jukumu hata dogo wanakimbia, hawawezi

Wanataka mabalozi, hawawezi kulipia wabunge wao wanaokuja Dodoma!
Wakitaka mabalozi wapewe na wizara nzima ya mambo ya nje kuhudumia.
 
Uroda upi, taja mmoja!

Taja kitu kimoja ambacho Tanganyika ina benefit toka Zanzibar!

Ireland haipo UK
1. kutumia bure miundombinu ya bahari kwa dahari -Zanzibar Channel
2.Kukitumia bure kwa shughuli za kitalii na katika uchotaji wa mafuta na gesi kisiwa cha Latham(Fungu Kizimkazi)
3. kushindwa kulipa madeni ya Zanzibar katika mgawanyo wa EAC iliokufa - orodha ni refu
 
Wanabodi,

Tangu baada ya Uingereza kupiga kura kujitoa kwenye EU, wanabodi wetu humu ambao ni Wanzanzibari, wanashadadia sana uamuzi huo, na kushinikiza wananchi wa Zanzibar nao, wapewe fursa ya kupiga kura ya maoni kwa kuulizwa kama bado wanataka kuendelea kusalia kuwa ndani ya muungano wetu, au wanataka kujitoa!. Wanaotaka kujitoa wakishinda, utaratibu wa jinsi ya kuuvunja muungano huu adhimu ziandaliwe, tuuvunje rasmi huu muungano wetu, na tuachane kwa amani, kuliko kuendelea huku baadhi ya wenzetu ni kila siku malalamiko, manung'uniko, na ghubu lisiloisha la kutwa kucha!.

Swali kwa wenzetu wa Zanzibari, sheria ya kura ya maoni si mnayo?!, sasa nini kinachowazuia kuitumia sheria hiyo kupiga hiyo kura ya maoni kuhusu muungano?!.

Kwa msio jua kuwa wenzetu Zanzibar, waliishaipitisha sheria hiyo ya kura ya maoni toka mwaka 2010, na ndio iliyotumika kuunda SUK!.

Kura ya Maoni Zanzibar ni Sheria Nambari 6 ya 2010 kuhusu uendeshaji wa kura ya maoni ilipitishwa na Baraza la Wawakilishi mnamo mwezi wa Machi 2010 na kutiwa saini na Mheshimiwa Rais Karume mnamo mwezi wa Aprili 2010.

Tayari sheria hiyo iliishatumiwa na wananchi wa Zanzibar walipopiga kura ya maoni siku ya
Jumamosi tarehe 31 Julai 2010. Kura hiyo ilikuwa na lengo la kutafuta ridhaa ya wananchi wa visiwa hivyo vya Unguja na Pemba, kuamua iwapo wanalikubali wazo la kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010.

Auamuzi wa kupigwa kwa kura hiyo ya maoni ulianzia katika kikao cha BLW ambacho kilipitisha Azimio la Baraza kufanywa kura ya maoni (referendum) iliyowashirikisha wananchi wa Zanzibar moja kwa moja katika kupata ridhaa ya wananchi kuanzisha mfumo na muundo wa Serikali ya
Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

Kura hiyo iliendeshwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na kwa mujibu wa Kifungu cha 11(1) cha
Sheria ya Kura ya Maoni Nambari 6 ya 2010, ushindi wa Kura ya Maoni utaamuliwa kwa
wingi wa kura. Hivyo, kwa mujibu wa matokeo hayo, Wazanzibari waliopiga kura
ya NDIO kuunga mkono kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SUK ikaendwa!.

Hayo yote yalifanyika Zanzibar bila kuishirikisha JMT, hadi ninavyozungumza hapa, japo SUK inatambuliwa rasmi na serikali ya JMT, lakini hadi leo, Katiba ya JMT ya 1977, bado haitambui SUK, hakuna kipengele chochote kinachoitambua SUK, wala katiba yetu haiwatambui wale makamo wawili wa rais wa Zanzibar, bali bado inamtambua Waziri Kiongozi ambaye doesn't exist anymore!.

Mabadiliko hayo ya Katiba ya Zanzibar ya 2010, yalikiuka katiba ya JMT na kuuvunja rasmi muungano kikatiba kwa katiba hiyo kuitangaza Zanzibar kuwa ni nchi, wakati katiba ya JMT inatamka nchi ni moja tuu JMT, na kuitambua Zanzibar kama sehemu ya JMT!.

Katiba hiyo ya Zanzibar ilivunja mamlaka yote ya Bunge la JMT, na mamlaka yote ya rais wa JMT, kwa kumtangaza rais wa Zanzibar ndio mkuu wa nchi ya Zanzibar na Amiri Jeshi Mkuu wa Vokosi vya SMZ!, na kuamua sheria yoyote itakayotungwa na Bunge la JMT, haitatumika Zanzibar mpaka BLW liridhie!, hii ni dharau kiasi gani kwa rais wa JMT na Bunge la JMT?!.

Kama yote haya yaliweza kufanyika bila kuishirikisha JMT, sasa ni nini kinachowashinda Wazanzibari kujiitishia kura yake ya maoni, kuamua kama isalie katika muungano au ijitoe?!.

Sasa tumechoshwa na hizi kelele, hivyo natoa wito kwa wenzetu Wazanzibari, waamue moja, ama waache kelele watulie, ama wafikie maamuzi waamue!.

Nawatakia Jumapili Njema.

Pasco
NB. Pasco wa JF ni muumini wa falsafa ya Nyerere kuhusu muungano, Nchi Moja, Serikali Moja chini ya Rais Mmoja wa JMT!, ila pia ni mtu mwenye maslahi fulani binafsi na Zanzibar!.

Rejea.
Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, Then "Twende kwenye Serikali Moja!.

Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?
Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?! .
Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano?
Je, wajua kuwa kuna uwezekano Tanzania sio nchi halali Kisheria ...
Zanzibar: Japo SMZ ya SUK sio de jure tena bali ni de facto ...
CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima .
Je, kunahitajika affirmative action ili Mzanzibari aweze tena
Muundo wa Serikali Tatu ni Illegal, Unjustifiable, na Ni Kuvunja ...
Kumbe Sultan Jamshid Alifurahia Kuuawa kwa Karume!. Alitaraji ..
Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein ...
Zanzibar Issue: Kwanini watu wanapiga kelele tu bila kuchukua ...
Balozi Karume: 'CCM pekee iwe inasimamisha mgombea urais Zanzibar
Kuna haja ya kuhofia kurudiwa Uchaguzi Zanzibar? |
Mbowe Alipua Bomu la Siri ya Ushindi Wa CCM Zanzibar
Imethibitishwa pasi na shaka kuwa CUF Ilishinda, Zanzibar ...
Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano ...
Inawezekana Vipi Zanzibar Hakuna Div I, Div II, wala Div III , Wao ..
Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na .

Pasco umejitahidi kueleza vema kwenye hili bandiko lako lkn umeharibu padogo ya kuwaeleza wapige kura ya kuamua, hivi ktk hii serkali ya ccm inayo lazimisha huu muungano unategemea hata kura zikipigwa watawala wapo tayari kukubali?
 
Naam. Wazanzibar wajiamulie wenyewe wanayoytaka. Hata sisi watu wa Tanganyika tupige kura tuwaachie nchi yao nasi tubaki na yetu. Tumechoka kuyasikia manung'uniko yao wakidai wanaonewa kila kukicha. Mh Mbunge Ally Nkasi amekuwa akiyaongelea haya Mara nyingi Sana na siku zote imekuwa mwiba Kwa Wazanzibar.
Kwahiyo huo mwiba wa kesy ni wa kujenga au kubomoa? Yeye anqchofanya ni kucheza na akili za wapiga kura wake tu ili aonekane anachangia kitu bungeni
 
Kuamua kuichagua CCM kwa zaid ya 90% kwny uchaguzi wa March 20,2016 ni ushahid tosha wanahitaji kuendelea na Serikal mbili kwny Muungano wetu.
Mtu kuwa kichaa siyo lazima uvae chupi kichwani bali ni pamoja na kuwa na mawazo dhaifu kama haya yako
 
hamuko tayari Tanganyika, Warioba alikwisha yaweka sawa haya mukayapindua mukaweka yenu. Kama nyinyi munanyonywa na mtoto keshapea unatakiwa umuachishe uangalie jengine sio umlazimishe wakati kashapea muache aanze maisha yako, msitafune huku munapuliza
 
Znz wanajitambua toka kitambo,na walisha amua,titizo lipo kwa huyu MKOLONI mweusi TANGANYIKA aliyejivika koti la TANZANIA tena mchana wa jua kali bila kuona hata JOTO
 
One day yes
Mkuu Kakke, japo heading haiendani na maudhui, lakini kelele za vitimbakwiri wa Zanzibar wanaotaka huu muungano wetu adhimu uvunjike, tumeisha wazoea.

Mabadiliko ya 10 ya katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 yameitangaza Zanzibar kuwa ni nchi, na ikaitaja mipaka yake, bendera yake na wimbo wake wa taifa, nayo ikaelezwa kuwa ni dola, ina vyombo vyake vya dola, rais wa Zanzibar ni Amiri Jeshi wa Vikosi vya ile migambo ya KMKM na JKU. Zanzibar ilichokosa ni sarafu yake tuu, mabalozi wake na hati ya kusafiria.

Kwa vile Zanzibar tayari mnayo sheria ya kura ya maoni, then kwa nini msipige kura ya maoni na kuamua to walk out kwa amani?!.

Niliwahi kuashauri hapa

Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja!.

Paskali
 
Mkuu Kakke, japo heading haiendani na maudhui, lakini kelele za vitimbakwiri wa Zanzibar wanaotaka huu muungano wetu adhimu uvunjike, tumeisha wazoea.

Mabadiliko ya 10 ya katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 yameitangaza Zanzibar kuwa ni nchi, na ikaitaja mipaka yake, bendera yake na wimbo wake wa taifa, nayo ikaelezwa kuwa ni dola, ina vyombo vyake vya dola, rais wa Zanzibar ni Amiri Jeshi wa Vikosi vya ile migambo ya KMKM na JKU. Zanzibar ilichokosa ni sarafu yake tuu, mabalozi wake na hati ya kusafiria.

Kwa vile Zanzibar tayari mnayo sheria ya kura ya maoni, then kwa nini msipige kura ya maoni na kuamua to walk out kwa amani?!.

Niliwahi kuashauri hapa

Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja!.

Paskali
Hakuna namna yoyote ile tutaweza kuicha Zanzibar ijitenge na kuwa taifa. Ni eneo muhimu sana kimkakati hasa ulinzi na usalama wetu

Sent from my Lenovo A2010-a using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom