Dotto Bulendu anaandika fb page
Moja ya madhaifu makubwa tuliyonayo Tanzania hasa kwenye sekta ya utalii ni namna ya kufanya "Branding Compaign" ya nchi yetu ama vivutio vyetu vya utalii.
Kwa mfano "The most amazing place in the world" ipo Tanzania pale Ngorongoro,sehemu pekee duniani ambapo mnyama mkali simba anapisha barabarani na binadamu ni Ngorongoro Tanzania,"Longest freshwater lake in the world"linapatikana Tanzania na hili ni ziwa Tanganyika, sehemu pekee ambapo wanyama hupata ujauzito sehemu moja ya nchi na kwenye kujifungulia sehemu nyingine ya nchi na kisha kuja kuwalea watoto sehemu nyingine ni Tanzania,Nyumbu wanapata mimba Tanzania,wanakwenda kuzaa Masai Mara kisha wanakuja kuwalea watoto mkoani Mara.
Kwenye sekta ya utalii Tanzania ina kila kitu,lakini hatui namna ya kujibrand kama taifa ili watalii wote wanapokuwa likizo waje nchini. Yaani VICENT WANYAMA anakuja nchini vyombo vya habari vya Uingereza vinaandika ujui wake hasa mtaa mmoja kupewa jina lake, sisi kama nchi tunavuana nguo hadharani kwa kusimika na kung'oa bango lake huku tukijipiga picha?yani unang'oa bango la mtaa wenye jina la WANYAMA halafu unajipiga picha na kuweka mtandaoni,unadhani ni sawa.
Hivi ndivyo gazeti la The SUN la Uingereza walivyoandika kuhusu Mwanyama
"I'M AVENUE Tottenham midfielder Victor Wanyama turns up in Tanzania to officially open street named in his honour.Kenya captain meets Dar es Salaam mayor and delighted fans at official ceremony for brand new V. Wanyama Street". Nafahamu utoaji wa majina ya mtaa nisuala la kisheria chini ya sheria namba 8 ya mwaka 1982 sura namba 288 na sheria namba 6 ya mwaka 1999 hizi zinatoa mamlaka kwa serikali za mitaa kutunga ama kutoa majina ya mitaa ama barabara za ndani ya halmashauri!
Binafsi sitazungumzia tofauti hizi kwa jicho la kisheria,wabobezi wameshachambua huko, mimi nitazungumzia katika jicho la kimawasiliano zaidi hasa! Kaja Wanyama nchini, tunamuacha anazunguka DSM, anakwenda kushuhudia Ndondo CUP, anakwenda kwenye vyombo vya habari, anakwenda kwenye migahawa maarufu DSM kula, lakini sisi kama taifa hatumuoni WANYAMA kama mtu ambaye tunaweza mtumia kuitangaza Tanzania, yaani mtu anacheza timu inayoshiriki ligi ya mabingwa Ulaya, anacheza ligi yenye mashabiki wengi Ulaya, sisi hatumuoni kwa jicho la kibiashara?
Unapotaka kufanya branding compaign tunatumia mbinu nyingi sana(kama 13) za namba ya kufanya branding compaign, leo nitaizungumzia hii moja tu ili nikuache upumzike na sikukuu.
1.Tafuta watu wenye mashabiki wengi sana, watu ambao wanafuatiliwa sana kila walifanyalo, watumie hao kujitangaza, kwa hili la wanyama, tulitakiwa tufanye uchunguzi Wanyama ana mashabiki wangapi kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii? Watu wangapi wanamfuatilia?
Wanyama alivyopost tu kwenye ukurasa wake akiwa kwenye bango lililoandikwa WANYAMA STREET, alipata views 36.5K, hebu tazama waliotazama, na aliandika kwa kiswahili. Hivi tungemchukua WANYAMA, tukampa ofa ya kwenda pale Crator ya Ngorongoro bure, tukamuomba tu apige picha akiwa kwenye crator na aandike ujumbe mfupi tu mfano "Welcome at Ngorongoro crator in Tanzania, the most amazing place in the world"watalii wangapi wangekuja nchini?
Hatujua kuibrand nchi yetu kwa kutumia watu maarufu, ndiyo maana hata Mbwana Samata anakuja nchini yaani hata kumwambia Samata aende pale Ngorongoro Crator apige picha akiwa pale na kuiweka kwenye social media hatuoni, yaani hatujui namna ya kuwatumia watu maarufu kujitangaza.
Hakukuwa na haja kwa wakubwa wetu kuvuana nguo na kuoneshana nani mbabe kwenye hili la WANYAMA,naamini watu wetu wa sekta ya utalii hii dhana ya BRANDING, wanaijua vizuri sana, sijui shida ni nini?
Ilitakiwa tu serikali inpump pesa wizara wizara ya maliasili na utalii,ije ya "Brandig compagn strategies"mfano inasema mwaka huu tutahakikisha tunaingia makubaliano na nyota ishirini maarufu wanaokioiga kwenye ligi ya mabingwa barani Ulaya, wizara ina andaa mkakati kabambe inahakikisha nyota hawa wanakuja free, unamleta Ronaldo Ngorongo.
Pale Ngorongoro unampandisha kwenye crator, unazungumza na CNN, unawalipa wafanye live coverage ya dakika 5 wakati Ronaldo akiwa kwenye crator, kutoka CNN unakubaliana nao wamlete mtangazji maarufu kama Christin Amanpour, RONALDO na AMANPOUR wote wakiandika kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii kuwa wapo Ngorongoro Crator, CNN ikaenda live kwa dakika tano, idadi ya watalii itakayokuja nchini itavunja rekodi.
Sasa sisi anakuja WANYAMA nchini, ofa ya kwenda kwenye vivutio vya utalii na kumwambia apost kuwa yupo "at the most amazing place in th e world where you can see live lions having sex, this happening only in Tanzania"tunabaki kung'oa mabango ya mtaa uliobatizwa jina lake.
Anyway, nisiwachoshe sana, ipi siku nitakuja na mada ya "BRANDING COMPAIGN"hususani "how to brand our nation"kama tulivyojifunza HOW TO ESTABLISH BRAND"
Moja ya madhaifu makubwa tuliyonayo Tanzania hasa kwenye sekta ya utalii ni namna ya kufanya "Branding Compaign" ya nchi yetu ama vivutio vyetu vya utalii.
Kwa mfano "The most amazing place in the world" ipo Tanzania pale Ngorongoro,sehemu pekee duniani ambapo mnyama mkali simba anapisha barabarani na binadamu ni Ngorongoro Tanzania,"Longest freshwater lake in the world"linapatikana Tanzania na hili ni ziwa Tanganyika, sehemu pekee ambapo wanyama hupata ujauzito sehemu moja ya nchi na kwenye kujifungulia sehemu nyingine ya nchi na kisha kuja kuwalea watoto sehemu nyingine ni Tanzania,Nyumbu wanapata mimba Tanzania,wanakwenda kuzaa Masai Mara kisha wanakuja kuwalea watoto mkoani Mara.
Kwenye sekta ya utalii Tanzania ina kila kitu,lakini hatui namna ya kujibrand kama taifa ili watalii wote wanapokuwa likizo waje nchini. Yaani VICENT WANYAMA anakuja nchini vyombo vya habari vya Uingereza vinaandika ujui wake hasa mtaa mmoja kupewa jina lake, sisi kama nchi tunavuana nguo hadharani kwa kusimika na kung'oa bango lake huku tukijipiga picha?yani unang'oa bango la mtaa wenye jina la WANYAMA halafu unajipiga picha na kuweka mtandaoni,unadhani ni sawa.
Hivi ndivyo gazeti la The SUN la Uingereza walivyoandika kuhusu Mwanyama
"I'M AVENUE Tottenham midfielder Victor Wanyama turns up in Tanzania to officially open street named in his honour.Kenya captain meets Dar es Salaam mayor and delighted fans at official ceremony for brand new V. Wanyama Street". Nafahamu utoaji wa majina ya mtaa nisuala la kisheria chini ya sheria namba 8 ya mwaka 1982 sura namba 288 na sheria namba 6 ya mwaka 1999 hizi zinatoa mamlaka kwa serikali za mitaa kutunga ama kutoa majina ya mitaa ama barabara za ndani ya halmashauri!
Binafsi sitazungumzia tofauti hizi kwa jicho la kisheria,wabobezi wameshachambua huko, mimi nitazungumzia katika jicho la kimawasiliano zaidi hasa! Kaja Wanyama nchini, tunamuacha anazunguka DSM, anakwenda kushuhudia Ndondo CUP, anakwenda kwenye vyombo vya habari, anakwenda kwenye migahawa maarufu DSM kula, lakini sisi kama taifa hatumuoni WANYAMA kama mtu ambaye tunaweza mtumia kuitangaza Tanzania, yaani mtu anacheza timu inayoshiriki ligi ya mabingwa Ulaya, anacheza ligi yenye mashabiki wengi Ulaya, sisi hatumuoni kwa jicho la kibiashara?
Unapotaka kufanya branding compaign tunatumia mbinu nyingi sana(kama 13) za namba ya kufanya branding compaign, leo nitaizungumzia hii moja tu ili nikuache upumzike na sikukuu.
1.Tafuta watu wenye mashabiki wengi sana, watu ambao wanafuatiliwa sana kila walifanyalo, watumie hao kujitangaza, kwa hili la wanyama, tulitakiwa tufanye uchunguzi Wanyama ana mashabiki wangapi kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii? Watu wangapi wanamfuatilia?
Wanyama alivyopost tu kwenye ukurasa wake akiwa kwenye bango lililoandikwa WANYAMA STREET, alipata views 36.5K, hebu tazama waliotazama, na aliandika kwa kiswahili. Hivi tungemchukua WANYAMA, tukampa ofa ya kwenda pale Crator ya Ngorongoro bure, tukamuomba tu apige picha akiwa kwenye crator na aandike ujumbe mfupi tu mfano "Welcome at Ngorongoro crator in Tanzania, the most amazing place in the world"watalii wangapi wangekuja nchini?
Hatujua kuibrand nchi yetu kwa kutumia watu maarufu, ndiyo maana hata Mbwana Samata anakuja nchini yaani hata kumwambia Samata aende pale Ngorongoro Crator apige picha akiwa pale na kuiweka kwenye social media hatuoni, yaani hatujui namna ya kuwatumia watu maarufu kujitangaza.
Hakukuwa na haja kwa wakubwa wetu kuvuana nguo na kuoneshana nani mbabe kwenye hili la WANYAMA,naamini watu wetu wa sekta ya utalii hii dhana ya BRANDING, wanaijua vizuri sana, sijui shida ni nini?
Ilitakiwa tu serikali inpump pesa wizara wizara ya maliasili na utalii,ije ya "Brandig compagn strategies"mfano inasema mwaka huu tutahakikisha tunaingia makubaliano na nyota ishirini maarufu wanaokioiga kwenye ligi ya mabingwa barani Ulaya, wizara ina andaa mkakati kabambe inahakikisha nyota hawa wanakuja free, unamleta Ronaldo Ngorongo.
Pale Ngorongoro unampandisha kwenye crator, unazungumza na CNN, unawalipa wafanye live coverage ya dakika 5 wakati Ronaldo akiwa kwenye crator, kutoka CNN unakubaliana nao wamlete mtangazji maarufu kama Christin Amanpour, RONALDO na AMANPOUR wote wakiandika kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii kuwa wapo Ngorongoro Crator, CNN ikaenda live kwa dakika tano, idadi ya watalii itakayokuja nchini itavunja rekodi.
Sasa sisi anakuja WANYAMA nchini, ofa ya kwenda kwenye vivutio vya utalii na kumwambia apost kuwa yupo "at the most amazing place in th e world where you can see live lions having sex, this happening only in Tanzania"tunabaki kung'oa mabango ya mtaa uliobatizwa jina lake.
Anyway, nisiwachoshe sana, ipi siku nitakuja na mada ya "BRANDING COMPAIGN"hususani "how to brand our nation"kama tulivyojifunza HOW TO ESTABLISH BRAND"