Mtini
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 1,487
- 2,344
Nakumbuka wakati nakua tulikuwa tunatengeneza magari ya waya za tairi na waya zile zenye rangi rangi za TTCl. Kipindi hicho tulikuwa tunazunguka mitaa ya wazito maarufu kama uzunguni ambako ndio kulikuwa na watumiaji wengi wa simu za mezani kipindi hicho, basi tunatafuta zile njia zilizopita ardhini. Tukifanikiwa kuzipata tunafukua tunakata pande la maana tunasepa.
Kuna kipindi TTCL walipiga mkwara kuwa wakimkamata mtoto anaendesha gari lenye waya zao atakula mbarati. Basi tukaona isiwe tabu tukawa tunazichuna maganda kupoteza ushahidi. Kipindi hicho TTCL walipata tabu sana na hasara za kutosha.
Leo naangalia wanangu wanavyopenda kushinda ndani kwenye udigitali hawaelewi kabisa mambo kama yale.
Kuna kipindi TTCL walipiga mkwara kuwa wakimkamata mtoto anaendesha gari lenye waya zao atakula mbarati. Basi tukaona isiwe tabu tukawa tunazichuna maganda kupoteza ushahidi. Kipindi hicho TTCL walipata tabu sana na hasara za kutosha.
Leo naangalia wanangu wanavyopenda kushinda ndani kwenye udigitali hawaelewi kabisa mambo kama yale.