Wanene kuongezewa marupurupu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Wabunge Tanzania waongezewa marupurupu
*Ni mapendekezo ya bajeti ya 2007/2008
*Waongezewa posho, mafuta katika magari
*Mikopo ya elimu ya juu pia yaongezwa

Na Mwandishi Wetu


WAKATI sekta ya maendeleo ikitengewa fedha kidogo kwenye bajeti ya mwaka 2007/08, neema imewashukia wabunge baada ya serikali kusikiliza kilio chao cha muda mrefu.

Kilio cha wabunge kimekuwa ni kuongezewa maslahi na katika bajeti inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni wiki ijayo na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji na sasa kimezaa matunda kwa kuwa mapendekezo ya bajeti yanaonyesha kuwa wameongezwa Sh9.3 bilioni kwenye posho.

Wabunge wamekuwa wakilalamikia posho wanazolipwa kuwa hazikidhi mahitaji kulingana na hali ya uchumi ilivyo sasa.

Baada ya kuchaguliwa kushika nafasi ya Spika, Samwel Sitta aliahidi kuhakikisha maslahi ya wabunge yanaboreshwa kwa kuzingatia hali halisi ya uchumi.

Hivi sasa wabunge wanalipwa lita 500 za mafuta, Sh1.2 milioni kama mshahara na Sh1.2 milioni za kuhudumia jimbo kwa mwezi na katika nyongeza mpya, sasa wataongezewa mafuta kutoka lita 500 hadi 1,000 kwa mwezi.

Katika kila kikao, mbunge hulipwa Sh140,000 kwa siku, ikiwamo Sh55,000 posho ya kujikimu na Sh85,000 kwa ajili ya posho ya kuhudhuria kikao.

Katika bajeti ya mwaka jana, Bunge lilitengewa Sh34.5, lakini mwaka huu fedha hizo zimeongezwa na iwapo mapendekezo yatapitishwa, Bunge litatengewa Sh42.5 bilioni, ikimaanisha kuwa taasisi hiyo imepangiwa kuongezwa Sh8 bilioni.

Katika maboresho ya masilahi ya wafanyakazi kwa mwaka wa fedha 2007/08, pia serikali imetenga Sh91.5 bilioni kwa ajili ya nyongeza za mishahara na inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya kuboresha maslahi ya watumishi wa umma kulingana na mapendekezo ya Tume ya Rais.

Akiwasilisha taarifa ya makadirio ya bajeti kwa mwaka 2007/08 kwenye Kamati ya Fedha na Uchumi jana, Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, alisema kiasi hicho ni hatua ya kwanza ya mapendekezo ya tume hiyo.

Katika Wizara ya Elimu ya Juu, serikali imetenga nyongeza ya Sh54 bilioni kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi. Mwaka jana, mahitaji ya mikopo kwa wanafunzi yalikuwa Sh140 bilioni, lakini serikali ikatoa Sh63.5 bilioni. Baada ya kuonekana fedha zilizotolewa zilikuwa ndogo sana, serikali ikakopa Sh47 bilioni kutoka benki za ndani na hivyo jumla ya fedha za mikopo kwa wanafunzi kuwa Sh111.3 bilioni.

Meghji alisema, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeongezewa Sh7 bilioni kwa ajili ya posho ya chakula kwa askari. Wakati bajeti nzima ya Ngome mwaka jana ilikuwa ni Sh189.5 bilioni, mwaka huu fedha hizo zimeongezwa hadi kufikia Sh199.8 bilioni.

Kulingana na taarifa ya Wizara ya Fedha, Sh5 bilioni zimetengwa kwa ajili ya wafanyakazi watakaopunguzwa Mamlaka ya Majitaka na Majisafi Dar es Salaam (Dawasco) na Sh4 bilioni zimetengwa kushughulikia kesi zinazohusu mamlaka hiyo.

Bonde la Ihefu limetengewa Sh1.5 bilioni kuhifadhi mazingira, huku bajeti ya mishahara ya Wizara ya Maji ikipungua kutokana na kuhamisha wahandisi 83 wa maji kwenda halmashauri.

Kuhusu ruzuku iliyotolewa kwa Tanesco kutokana na ukame na mafuta kupanda, inaonyesha Sh20 bilioni zilitumika kulipia nishati hiyo kutoka Songas na IPTL na Sh101.4 bilioni zilinunua mitambo ya kuzalisha na kusambaza umeme.

Taarifa hiyo inaonyesha Sh103.6 bilioni zilitumika kukodi mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura na Sh125 bilioni ni dhamana ya mikopo kwa ajili ya kulipa umeme kutoka Songas na IPTL.

Hata hivyo, wabunge walihoji hatua ya kuendelea kutoa ruzuku kwa Tanesco, wakati hakuna ukame na uzalishaji wa umeme unaendelea kama kawaida.
 
Hawa viongozi wetu wabianasi sana, badala ya kuwaongezea walala hoi kwanza wanajianzia wenyewe. Hivi wanaposema posho haiendani na hali ya sasa ya uchumi wana maana gani? Wanataka kutuambia hali ya uchumi ni nzuri? Mafuta kutoka lita 500 to 1000 inamaana kazi za safari zimekuwa mara mbili zaidi? Kweli, aliyeshiba hamkumbuki mwenye njaaa!!!!!!!!! HAya JK last time alijifanya kuwapiga break!!! this time mbona kimyaa!!!!!!!!!!!!!
 
Mzee Es,
Maneno yako kweli kabisa nimewahi kusikia kuwa pato la Wabunge lilisha panda kitambo!... sasa hapa kweli tuna vyama vya Upinzani? ikiwa wao wamo ktk ongezeko la pato hilo bila musada kupita na wamekaa kimyaaaa!.. kweli huko Bungeni kuna mwakilishi wa raia?...
Zitto njoo tafadhali tunakuhitaji utupe kweli ya jambo hili! Na ukiingia mitini mjomba bora ubakie hukohuko maanake tunataka maelezo kamili ya swala hili!... yaani sintakuwa na imani kabisaaaaa!
Vipi muswada upelekwe bungeni hali wabunge tayari wameisha pokea ongezeko la matupurupu?
 
Sio mara ya kwanza utekelezaji kuanza kabla ya sheria! Nyerere aliwahi kupandisha kodi, akawambia wananchi waanze kulipa ingawa waziri muhusika alikuwa anategemea kupeleka mswaada wa hiyo kodi bungeni.....Its like that..Banana Republic ndivyo zilivyo.
 
Mikuki,
Nitashukuru kama utanipa mwaka!... hata hivyo navyoelewa mimi kupanda ama kupungua kwa baadhi ya kodi ni sera ya chama si lazima ipitie bunge la taifa!
 
Jana niliandika hapa kuhusu jambo hili. Ukiangalia, ni kuwa ongezeko kubwa liko kwenye posho, ambapo kabla ya kuongezewa, walikuwa wakilipwa TShs145,000 kwa siku wakati wakiwa Dodoma bungeni. Kati ya hizo, TSh.85,000 zilikuwa ni posho ya wao kuhudhuria kikao cha bunge! Ni kama vile kuhudhuria kwao bunge wanatufanyia favor wakati ndiyo kazi waliyoomba! It does not make sense!!!!!
 
Mkandara..... Uliona wapi...mtu analipa kodi ambayo haijawa sanctioned na sheria? Please, please..revisit your simple civics. Sitaki kwenda mbali, nadhani umenielewa...Anyway nitaangalia record proper lakini itakuwa nadhani ni kati ya 1980, 81 au 82..Iam not sure..maana nakumbuka niliiandikia paper hiyo issue those days.......
 
Hivi mimi naomba kuuliza..Lita 1000 kwa mafuta kwa mwezi hawa wabunge wanashinda wakiendesha hayo magari au wanagawana na vimada?

Kweli inalipa kuwa mbunge...sasa hizi posho pia vinawahusu wale Wabunge wa kuteuliwa na Rais na Viti Maalumu ambao hawana majimbo...no wonder kila mbabaishaji anakimbilia kwenye siasa.
 
Mkandara..... Uliona wapi...mtu analipa kodi ambayo haijawa sanctioned na sheria? Please, please..revisit your simple civics. Sitaki kwenda mbali, nadhani umenielewa...Anyway nitaangalia record proper lakini itakuwa nadhani ni kati ya 1980, 81 au 82..Iam not sure..maana nakumbuka niliiandikia paper hiyo issue those days.......

Nafaikiri unachoongea ni ile kodi iliyopachikwa jina "kodi ya maendeleo." Kama ni hiyo, ilikuwa introduced kama local tax ambayo ingekuwa inasimamiwa na halmashauri za wilaya, kwa hiyo haikuwa ya kitaifa na hivyo haikuhitaji baraka za bunge. Hata hivyo jambo la kushangaza ni kuwa kodi ile ilifanyika nchi nzima pamoja na kuitwa local tax, na kuna watu walifungwa miezi mitatu kwa kushindwa kuilipa.
 
Hivi mimi naomba kuuliza..Lita 1000 kwa mafuta kwa mwezi hawa wabunge wanashinda wakiendesha hayo magari au wanagawana na vimada?

Kweli inalipa kuwa mbunge...sasa hizi posho pia vinawahusu wale Wabunge wa kuteuliwa na Rais na Viti Maalumu ambao hawana majimbo...no wonder kila mbabaishaji anakimbilia kwenye siasa.

That is a million Dollar quest......
 
Lita ya mafuta = 1500/Lt
Lita 1000 x 1500 = 1,500,000
Idadi ya wabunge = 320
Gharama kwa wabunge wote kwa mwezi: 1500000 x 320 =480,000,000
Gharama ya wabunge wote kwa mwaka 480,000,000 x 12 = 5,760,000,000 (bilioni tano na nusu)

Wanafunzi wa Ukraine

Idadi 26
Kiasi cha ada: 3000000 kwa mwaka
Gharama yao kwa mwaka 3000000 x 26 = 78,000,000
Gharama kwa miaka mitano ya elimu ya madaktari, wahandisi na wanasheria hawa = 390,000,000!

Kuwalipia wanafunzi 93 kusoma China kwa mwaka mmoja 2006/2007 = 818,000,000
Kuwalipia wanafunzi hao kwa miaka 5 (ceteris paribus) = 4 090 000 000
 
Mikuki,

Nia yangu ni kujifunza sio kama unavyofikiria. Labda ile kuweka kuwa baadhi ya kodi huwa ni sera za chama imekushtua. Nasema hivyo kwa experience yangu ya huku majuu sina maana hayo ulosema hayawezi fanyika TZ chini ya mwl. after all wakati ule kulikuwa na chama kimoja tu.
Kwa hiyo mjomba nipe tu elimu kesho niweze kuitumia ndio maana nimeomba mwaka,kesho nisije kwama nikitumia maneno haya haya.
 
Mwanakijiji,

Niliwahi kuuliza humu, where are our priorities? Je vyama vya upinzani kwanini
wasianze wao kukataa Mashangingi? Kidogo Chadema waniue hapa ndani.

Priorities zetu Tanzania zimepinda kushoto. Leo nilikuwa naongea na mtu TZ kuhusu harusi. Akaniambia walichanga 5M, huko ni wilayani, nikamwuliza mlitumia ngapi kuwanunulia mahitaji muhimu wanandoa wapya. Akaniambia laki nne, where are our priorities in Tanzania? Ina maana 4.6 zilikuwa ulaji na kunywa kunywa.

Tusiwashangae hawa Wabunge, jamii nzima imeoza. Wewe uliona wapi wanafunzi hawana madawati, wilaya haina barabara, mbunge wao ana shangingi, kweli sisi tuna akili? Ninabaki kushangaa!

Watoto wao wanasomeshwa kwa mamilioni, kwanini wajali hawa watoto wa maskini huko Ukraine?
 
Poa mkuu..nitaifanyia kazi. Cha ajabu kilichostua wengi hapa..mpaka tukaamua kufanya research ni kwamba mwalimu alikuwa categoriacal kwamba waziri muhusika atapeleka sheria bungeni baadaye, meanwhile kodi ianze kulipwa mara moja! The moral of the story ni kwamba mwalimu alijua kabisa kwamba hakuna kodi inayolipwa bila baraka za bunge kwa hiyo alichokuwa anakifanya ilikuwa kinyume cha sheria. ..lakini aliamua kuignore. ....

Kichuguu hata kama ni local tax lazima iwe sanctioned/iwe na baraka za sheria mama. Kwa mfano hizi kodi za halmashauri na nyinginezo ni kanuni (au sheria ndogo ndogo zinazobarikiwa na mheshimiwa Mizengo Pinda) sio sheria as ACT....... Tukiwa objective swala linabakia kwamba katika hizi nchi zetu ni rahisi kwa viongozi kuignore sheria zilizopo na kutuswaga tuu....as we have seen and continue seeing........
 
Mauritania's new President Sidi Ould Sheikh Abdallahi and his cabinet have decided to take a 25% pay cut.

Local journalist Hamdi Ould Nohamed el-Hacen told the BBC it has come into effect immediately.

It was prompted by "reduced petroleum revenues", AFP news agency quotes a cabinet statement as saying.

Mr Abdallahi won run-off elections in March to become Mauritania's first democratically elected leader since independence from France in 1960.

The country was under the autocratic rule of Maaouiya Ould Taya for 25 years until a military coup in 2005

One of the world's poorest countries, Mauritania has pinned hopes for future prosperity on the exploitation of its offshore reserves of oil and gas.

Correspondents says oil production in Mauritania is currently around 18,000 barrels a day, compared to the originally anticipated 75,000 bpd.

According to AFP news agency, until Thursday ministers earned a monthly salary of about $3,500, compared to an average civil servants' pay packet of $260.

The president's salary was not reported.

The austerity measure follows last week's government announcement of a $112m budget deficit, the agency reports
.

Story from BBC NEWS:
http://news.bbc.co.uk/go/pr/fr/-/2/hi/africa/6734463.stm

Published: 2007/06/08 13:23:55 GMT

© BBC MMVII

Hii habari imenifanya nijiulize maswali mengi sana kuhusiana na Serikali yetu kama kweli wanaweza kufanya kitu kama hiki...
 
Habari za masiku tele ndugu zangu.

Nimeona ni muhimu niingie katika mjadala huu ili niweze kuweka wazi baadhi ya facts zisaidie mjadala wetu.

Mshahara wa Mbunge kwa mwezi Tshs. 1,200,000. Kodi inakatwa asilimia 30 ambayo ni sawa na Tshs. 360,000. Kwa wale ambao wamechukua mkopo wa magari kila mwezi analipa Tshs. 500,000. hivyo pato la mbuge baada ya makato ni Tshs 340,000.

Posho ya ubunge

Hii tunapewa shs 1,000,000 kila mwezi. pesa hii ni kwa ajili ya huduma za ubunge kama mawasiliano, kulipa wasaidizi, kuganya utafiti kwa ajili ya miswada na pia mafuta. Mafuta tunalipwa kwa sasa lita 500 kwa mwezi kwa wastani wa shs 1000 kwa lita.

Posho ya kujikimu na vikao
katika hili tunalipwa shs 55,000 tunapokuwa dodoma kwa ajili ya malazi na chakula. kuna habari kuwa tunapewa nyumba dodoma, sio kweli bali kila mbunge anatafuta makazi yake.
mbunge akihudhuria kikao cha bunge analipwa shs 70,000 kwa kikao. hivyo kwa wale wanaohudhuria kwa siku ni 125,000.

maombi ya wabunge:
wabunge walitaka kulipwa zaidi pesa ya mafuta ili iendane na bei ya mafuta na pia kulingana na ukweli kuwa baadhi ya wabunge majimbo ni makubwa sana na hivyo lita 500 kwa mwezi ni kidogo. mfano, mimi kutoka dodoma mpaka kigoma kwenda na kurudi ni km 1100 hivi.

pili, wabunge walitaka kuongezewa uwezo wa kuajiri wasaidizi wenye elimu kubwa zaidi. mfano mimi msadizi wangu ambae ana shahada ya sheria ninamlipa shs 500,000 kwa mwezi. kwa malipo ya sasa ninatakiwa kulipa shs 70,000 kwa mwezi.

mimi sijajua kwa malipo ya sasa yaliongozeka ni kiasi gani kitakwenda kwa mishahara na maeneo mengine. hivyo siwezi kucomment na kusema nini.

ukweli ni kwamba mjadala wa malipo kwa wabunge vs matunda ya kazi zao ni mjadala muhimu sana. lengo liwe ni kuzuia malipo makubwa bila tija na pia kuepuka kuwa na wabunge wasioweza kufanya kazi sawasawa ya kuisimamia serikali
 
Juzi alhamis kamati ya fedha ya bunge,ambayo mimi ni mjumbe, ilimwagiza waziri wa fedha kuondoa asilimia 15 kutoka katika bajeti ya matumizi mengineyo na kupeleka pesa yote kujenga barabara.
Hii ilifuatia taarifa tuliyopata kutoka kamati ya miundombinu kuwa hakuna barabara mpya zitakazojengwa maana pesa zilizotengwa ni kidogo. Uamuzi huu wa kamati ya bunge utaongeza bajeti ya miuondombinu kwa zaidi shs 393 bilions.

uamuzi huu wa kamati ya bunge unaonesha kuwa hata Tanzania tunaouwezo wa kupunguza gharama na kupeleka pesa katika vipaumbele muhimu. Mfanowa Mauritania ni mzuri sana. Lakini Tanzania Waziri analipwa dola 1100 tu, theluthi tu ya malipo ya waziri wa mauritania, nchi masikini kuliko tanzania
 
Back
Top Bottom