Wanazuoni wengi Tanzania ni waoga

KABIDI BODO

Senior Member
Jan 19, 2017
184
252
Nimekuwa nikitafakari juu ya uamuzi wa serikali kufuta fao la kujitoa na kuongeza makato bodi ya mikopo kwa wanufaika kinyume na mikataba ya wanufaika bila majibu stahiki.. Mwisho nimegundua kuwa wanazuoni wengi wa nchi hii ni waoga wakuichagiza serikali pindi inapofanya maamuzi yakuumiza.

Hata wanasheria wamekubali kirahisi tu kuwa wahanga wa mambo haya, unabaki unatafakari kuwa kama ukoloni ungerudi leo hii sidhani kama tungeweza kujikomboa, maana vijana wa leo wamekuwa sio jasiri kama walivokuwa mashujaa wetu walotutoa katika ukoloni..

Mpaka muda huu bado sina imani na sitaweza kuwa na imani hata siku moja na chama cha wafanyakazi ndani ya nchi hii, naona kipo kisiasa zaidi na kimeshindwa kujipambambanua kama mtetezi wa kweli wa wafanyakazi..

Hili limeonekana hata kwenye swala la vyeti feki, kuna waliokuwa fake kweli na kuna walioonewa, lkn sijaona chama cha wafanyakazi kikisimama kuwatetea walioonewa..

Ni kweli na niwajibu wa kila mnufaika wa mkopo kutoka bodi ya mikopo ya elimu ya juu ni sharti alipe maana dawa ya deni ni kulipa, lkn ktk kipindi hiki kwa nini umtoe mtu aliyekua kishaanza kulipa kutoka 8% hadi 15% nje ya mkataba aliosaini mnufaika wakati anajaza fomu za kuomba mkopo na hata alipokubaliwa.. Cha kusikitisha zaidi TUCTA walituhadaa wanaenda mahakamani kupinga lakini sioni hili likitendeka maana wanakula kwa urefu wa kamba yao..

Wanasheria nao ni wahanga wa haya mambo lakini wapo kimya na wamekubali tu haki ipindishwe kotekote..

Katika kipindi hiki ambapo makampuni mengi yanapunguza wafanyakazi, watu wanaenda mtaani na hawawezi kuchukua mafao yao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii ili japo waweze kufanya miradi mingine katika kujikwamua kimaisha, lakini hakuna ambae anathubutu kulihoji wala kulichokoza popote pale..

kama chama cha wafanyakazi kingekuwa mtetezi wa kweli wa wafanyakazi, haya yasingefanyika na kumuacha mfanyakazi katika hali ngum.

Kiukweli wanazuoni wengi wa Tanzania ni waoga na laiti mkoloni angetawala zama hizi ingekua ngumu sana kumng'oa...
 
Blah blah hebu uthibitishie umma kwa'evidence' kwamba kuna watu waatakuwa wameonewa kwenye suala la vyeti feki ' otherwise ' ni porojo tu.
 
awamu ya kikwete madaktari walikuwa wanagomaa sana...mara walimu nao mikwara mingi.. mara watumishi wa wapi wanagomaa tu kirahisi rahis..

mara waislam wanaandamana mara wanavyuo wanagomaa kila siku..

ila toka mwanaume kaingia ikulu migomoo yote imeingia mitini..

huyu mzee hataki mchezo unaanzia wapi kupingaa au kugoma huku bodi unadaiwa kweli na umekopa mwenyewe bila kulazimishwa
 
Nimekuwa nikitafakari juu ya uamuzi wa serikali kufuta fao la kujitoa na kuongeza makato bodi ya mikopo kwa wanufaika kinyume na mikataba ya wanufaika bila majibu stahiki.. Mwisho nimegundua kuwa wanazuoni wengi wa nchi hii ni waoga wakuichagiza serikali pindi inapofanya maamuzi yakuumiza.
Hata wanasheria wamekubali kirahisi tu kuwa wahanga wa mambo haya, unabaki unatafakari kuwa kama ukoloni ungerudi leo hii sidhani kama tungeweza kujikomboa, maana vijana wa leo wamekuwa sio jasiri kama walivokuwa mashujaa wetu walotutoa katika ukoloni..
Mpaka muda huu bado sina imani na sitaweza kuwa na imani hata siku moja na chama cha wafanyakazi ndani ya nchi hii, naona kipo kisiasa zaidi na kimeshindwa kujipambambanua kama mtetezi wa kweli wa wafanyakazi..
Hili limeonekana hata kwenye swala la vyeti feki, kuna waliokuwa fake kweli na kuna walioonewa, lkn sijaona chama cha wafanyakazi kikisimama kuwatetea walioonewa..
Ni kweli na niwajibu wa kila mnufaika wa mkopo kutoka bodi ya mikopo ya elimu ya juu ni sharti alipe maana dawa ya deni ni kulipa, lkn ktk kipindi hiki kwa nini umtoe mtu aliyekua kishaanza kulipa kutoka 8% hadi 15% nje ya mkataba aliosaini mnufaika wakati anajaza fomu za kuomba mkopo na hata alipokubaliwa.. Cha kusikitisha zaidi TUCTA walituhadaa wanaenda mahakamani kupinga lakini sioni hili likitendeka maana wanakula kwa urefu wa kamba yao..
Wanasheria nao ni wahanga wa haya mambo lakini wapo kimya na wamekubali tu haki ipindishwe kotekote..
Katika kipindi hiki ambapo makampuni mengi yanapunguza wafanyakazi, watu wanaenda mtaani na hawawezi kuchukua mafao yao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii ili japo waweze kufanya miradi mingine katika kujikwamua kimaisha, lakini hakuna ambae anathubutu kulihoji wala kulichokoza popote pale..
kama chama cha wafanyakazi kingekuwa mtetezi wa kweli wa wafanyakazi, haya yasingefanyika na kumuacha mfanyakazi katika hali ngum.
Kiukweli wanazuoni wengi wa Tanzania ni waoga na laiti mkoloni angetawala zama hizi ingekua ngumu sana kumng'oa...
Sio waoga....wanakariri tu bila kuwa practical kwanini wasiogope?
 
Blah blah hebu uthibitishie umma kwa'evidence' kwamba kuna watu waatakuwa wameonewa kwenye suala la vyeti feki ' otherwise ' ni porojo tu.

hahahaaaaaa... ninazo evidence katika hili, kwa sababu kuna mtu wangu wakaribu kabisa nimesoama nae amekumbwa na hili, na ndio maana hata serikali imetoa nafasi ya rufaa, ana evidence zote..

Kwa kifupi ameachiwa anaekushtaki ndio akuhukum, hata hizi rufaa wakiamua kuzipiga chini hakuna pakwenda
 
awamu ya kikwete madaktari walikuwa wanagomaa sana...mara walimu nao mikwara mingi.. mara watumishi wa wapi wanagomaa tu kirahisi rahis..

mara waislam wanaandamana mara wanavyuo wanagomaa kila siku..

ila toka mwanaume kaingia ikulu migomoo yote imeingia mitini..

huyu mzee hataki mchezo unaanzia wapi kupingaa au kugoma huku bodi unadaiwa kweli na umekopa mwenyewe bila kulazimishwa
Ndio maana nikasema kama wakoloni wangetawala zama hizi, tungetawaliwa milele..
 
hahahaaaaaa... ninazo evidence katika hili, kwa sababu kuna mtu wangu wakaribu kabisa nimesoama nae amekumbwa na hili, na ndio maana hata serikali imetoa nafasi ya rufaa, ana evidence zote..

Kwa kifupi ameachiwa anaekushtaki ndio akuhukum, hata hizi rufaa wakiamua kuzipiga chini hakuna pakwenda
Unadhani rufaa zipo kwa ajili ya nini?
Na shaka na uelewa wako , ukumbuke binadamu sio wakamilifu kwa asilimia mia moja unaouita uonevu ndio uo uo pia umewapatia watu kazi na pia ndio uo uo umewaondosha kazini?

Kama binadamu huwa wanalaumu hadi kazi za Muumba je zinazofanywa na wanadamu ndio zisilaumike? Acha mawazo yanayotuzama upande mmoja.
 
Unadhani rufaa zipo kwa ajili ya nini?
Na shaka na uelewa wako , ukumbuke binadamu sio wakamilifu kwa asilimia mia moja unaouita uonevu ndio uo uo pia umewapatia watu kazi na pia ndio uo uo umewaondosha kazini?

Kama binadamu huwa wanalaumu hadi kazi za Muumba je zinazofanywa na wanadamu ndio zisilaumike? Acha mawazo yanayotuzama upande mmoja.
Sawa mkuu uelewa wangu inawezekana ni mdogo, nieleweshe.. lakini pia unadhani chama cha wafanyakazi kipo kwa ajili ya nini?
 
Back
Top Bottom