MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Kama navyosema siku zote mimi ni kada hai wa CCM na naendelea kukipenda CCM. Lakini nitafurahi sana chama changu kiadabishwe awamu moja au kichachafwe ili kipate adabu kisirudie makosa yale yale na kiache kudharau wanyonge wahali ya chini.
KWANINI NASEMA CHAMA CHANGU KIADABISHWE?
1. Serikali ya chama changu imeweka ubaguzi mkubwa sana kwenye utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, eti mtu anakopeshwa halafu anawekewa vigezo kibao. Unamwekeaje masharti kijana ambaye amesoma shule ya kulipia kama pesa ni ya mkopo na atarudisha?
Kijana wa miaka zaidi ya 33 ana kadiploma chake anataka apate mkopo huenda ada ya chuo ni ndefu imsaidie apandishe elimu yake wewe unamnyima mkopo eti ni umri?
Mbona wakati wa JK wanafunzi wote wenye sifa walipata mikopo bila kujali backgrounds zao wala umri ilimradi ni Watanzania tu?
*#Kama huwezi kutoa mkopo kwa watu wote wenye sifa unawaweka masharti magumu wasipate ujue wewe huna pesa ya kutosha na huwezi kuwapa wote. Wewe hufai kuendesha serikali.
2. Makato ya marejesho ya mikopo kutoka asilimia 8%-15%, hivi kwa mishahara yetu hii hii ya Tanzania kwa ngazi ya shahada hasa ualimu iwe private au sekta za umma, unampandishia mtu makato ili tu makusanyo yaongezeke ukidhi mahitaji yako wewe si uonevu huo? Kwani ukimkata 8% mtu huru katika taifa lake na alikopa pesa ya Umma unaumia nini?
Mtu unakata 15%, mshahara hujsmpandishia miaka 5 sasa, kodi kubwa, sasa unataka aishije?
Narudia tena, Chama changu kiadabiwe angalau awamu moja haya makosa hayatojirudia tena.
Nawatakia weekend njema.
CCM OYEEE!!!
KWANINI NASEMA CHAMA CHANGU KIADABISHWE?
1. Serikali ya chama changu imeweka ubaguzi mkubwa sana kwenye utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, eti mtu anakopeshwa halafu anawekewa vigezo kibao. Unamwekeaje masharti kijana ambaye amesoma shule ya kulipia kama pesa ni ya mkopo na atarudisha?
Kijana wa miaka zaidi ya 33 ana kadiploma chake anataka apate mkopo huenda ada ya chuo ni ndefu imsaidie apandishe elimu yake wewe unamnyima mkopo eti ni umri?
Mbona wakati wa JK wanafunzi wote wenye sifa walipata mikopo bila kujali backgrounds zao wala umri ilimradi ni Watanzania tu?
*#Kama huwezi kutoa mkopo kwa watu wote wenye sifa unawaweka masharti magumu wasipate ujue wewe huna pesa ya kutosha na huwezi kuwapa wote. Wewe hufai kuendesha serikali.
2. Makato ya marejesho ya mikopo kutoka asilimia 8%-15%, hivi kwa mishahara yetu hii hii ya Tanzania kwa ngazi ya shahada hasa ualimu iwe private au sekta za umma, unampandishia mtu makato ili tu makusanyo yaongezeke ukidhi mahitaji yako wewe si uonevu huo? Kwani ukimkata 8% mtu huru katika taifa lake na alikopa pesa ya Umma unaumia nini?
Mtu unakata 15%, mshahara hujsmpandishia miaka 5 sasa, kodi kubwa, sasa unataka aishije?
Narudia tena, Chama changu kiadabiwe angalau awamu moja haya makosa hayatojirudia tena.
Nawatakia weekend njema.
CCM OYEEE!!!