Wanayanga wenzangu ‘ tunaibiwa ‘ mbona hawa ‘ Wadhamini ‘ wetu hawaonekani katika Jezi zetu?

Natambua kuwa kila mwana Yanga SC hapa Jamvini anatambua kuwa Mimi An Eagle ni Mwanachama mwenye Uchungu kabisa na Klabu yetu hii ( nikiwa na Kadi Namba 031....91287...6 ) hivyo mambo ambayo huwa nayasema hapa huwa nakuwa nawapigania Yanga na Maslahi yao pia.

Ndugu zangu wana Yanga huenda wengi wenu mkawa hamjui au hamjatambua lolote lile ila Mimi kama mwana Yanga lia lia najua kuwa Timu yetu inadhaminiwa na Azam tv pamoja na SpotiPesa pekee lakini nimeshangaa hivi karibuni baada ya tu Uongozi huu mpya Kuingia Madarakani naona Wadhamini wapya ambao hata katika Jezi zetu hawapo kabisa.

Wana Yanga wenzangu naona ‘ tunaibiwa ‘ na Uongozi wetu hivyo tusikubali, tuandamane upesi kwenda pale Klabuni kuwatoa na ikiwezekana hata Mechi yetu na Zesco United Jumamosi tusiende kabisa ili tuwakomesha kwani Uongozi huu mpya unatufanya wana Yanga SC wote tuna Akili za ‘ Kipa Katoka ‘ namaanisha za ‘ Kipumbavu ‘ wakati kumbe si kweli bali na Sisi tuna Akili kuliko hata Wao.

Hawa Wadhamini wafuatao hapa chini wanaifaidisha vipi Yanga SC yetu? Na mbona ujio wao Sisi Wanachama akina An Eagle hatukufahamishwa katika Mikutano ya Klabu?

1. Taifa Gas
2. GSM Foam
3. Afya Water

Kama Uongozi wa Yanga SC hautanijibu Mimi An Eagle basi muda si mrefu nahamia rasmi kwa Watani zetu Simba SC ambao naona kwa sasa angalau Wao wanaendesha Timu yao Kisasa, Kisomi na Kiuweledi kabisa. Na nashauri pia kwa Wanachama wenzangu wote wa Yanga SC kuwa nanyi pia hamieni Simba SC ili ' tuukomoe ' huu Uongozi wetu kwani ' unatuibia ' Sisi wana Yanga.

Nikiwa kama mwana Yanga SC lia lia kabisa nimekasirika sana juu ya hili na nauomba Uongozi wa Yanga SC ' Ujiuzulu ' upesi.
Yaani we chizi ulitakiwa uwepo siku ileee pale msamvu
 
Hahahaaaaaaaaaa
Screenshot_20190912-172318.jpeg
 
Mbona uandishi wako unafanana na yule ‘popoma’ flani hivi mnazi wa simba asiye choka kuinanga nanga timu pendwa ya wananchi au ndiyo wewe umekuja kivingine?
 
Maswala ya wadhani we yanakuhusu nini? Kazi yako ni kwenda uwanjani na kushabikia timu tu, Mengine waachie viongozi.
 
Ulifahamishwa peke yako labda ukiwa Chumbani na Mwenyekiti na Makamu wake au? Sisi kama wana Yanga SC hatuna taarifa yoyote ile na acha Kutupandisha Hasira kisha tususe hata Kuja Uwanjani Jumamosi Kuishangilia Timu yetu ikicheza na Zesco United au ukasababisha tukaenda kwa Mganga wetu Mwanza ambaye juzi aliwaogesha Wachezaji wetu wote wa Yanga SC Maji ya Maiti ya Hospitali moja Kubwa pale Mwanza ili abadilishe ' Uchawi ' wake na hatimaye tufungwe na tuumbuke? Unajua ni kwanini Beki wetu Juma Abdul ambaye alikuja Kumzika Mama yake Kesho yaka akalazimishwa apande Bung'o ( Ndege ) haraka ili aende Mwanza Kuungana na Wenzake na wamerejea wote Dar es Salaam jana Usiku? Hebu tuachie tunaoijua Yanga SC yetu tulalamike hapa na Wewe Simba SC tupishe tafadhali sawa?
WENZENU TANASAJILI WACHEZAJI WAZURI NYIE MNASAJILI WAGANGA NA WACHAWI HIYO NDIO YANGA YA KISASA.
 
WENZENU TANASAJILI WACHEZAJI WAZURI NYIE MNASAJILI WAGANGA NA WACHAWI HIYO NDIO YANGA YA KISASA.

Sijakuelewa huu Ujumbe wako hapa unaniambia Mimi mwana Yanga SC Mwenzako au wale wa Simba SC Ndugu?
 
Tunaibiwa kwahiyo wana Yanga SC tunyamaze Ndugu? au Wewe ni Simba SC lia lia kabisa kama Frank Wanjiru?
Wewe mikia unalala unaiota Yanga. Ingekuwa kwenye maswala ya upelelezi ningekuambia hongera kwa ku-win,kutwa kutafuta yanayohusu Yanga. Lakini kwa sbb ni soka,wewe ni fara #1,ksbb hii nguvu yote unayoitumia kuichunguza Yanga ungeitumia vizuri kuichunguza Ud Songo kabla ya ile mechi mngekuwa mmevuka kibabe. Shida ndio hiyo mikia mnaelekeza nguvu kuichunguza Yanga tu
 
Mbona uandishi wako unafanana na yule ‘popoma’ flani hivi mnazi wa simba asiye choka kuinanga nanga timu pendwa ya wananchi au ndiyo wewe umekuja kivingine?
Yani GENTA hayupo smart kabisa ameshindwa kujitofautisha kiuandishi na kimtazamo. Watu tuna ID kumi kumi hunu ila si rahisi kushtukiwa labda mods waamue kukuumbua
 
Yani GENTA hayupo smart kabisa ameshindwa kujitofautisha kiuandishi na kimtazamo. Watu tuna ID kumi kumi hunu ila si rahisi kushtukiwa labda mods waamue kukuumbua

Kwanini unateseka Ndugu? Kama unao uhakika wote thibitisha hapa kwa Ushahidi wako kamili na unaobaki uwasilishe kwa hao Mods kama ulivyosema hapa ila ninachojua Mimi ni An Eagle na siyo huyo Bwana Wenu ambaye Kutwa mnamuimba na Kumtajataja hapa utadhani mmembebea Mimba zake. Wapuuzi wakubwa nyie!
 
Back
Top Bottom