Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,806
- 15,379
Hiyo hapo juu ni sura ya mwanamke. Ni sura ambayo pengine umeshakutana nayo mahali au ambayo unaijua vizuri. Kama kuna mwanamke mwenye sura ya aina hiyo, ambaye unamjua vizuri au ambaye uko karibu naye, msome tabia zake, halafu uniambie ulichogundua. Ni wazi utagundua kile nitakachoeleza humu kuhusu tabia za wanawake wenye sura za aina hiyo.
Angalia mdomo, pua, macho na paji la uso. Hayo ndiyo maeneo ambayo yanakupa sura. Bila shaka ukiangalia kwa makini, sura hiyo ni nzuri kwa mujibu wa mazoea yetu katika kutazama tulichofundishwa kwamba ni kizuri au kibaya. Wanawake wenye sura hiyo, kwa kawaida ni wenye aibu zinazotokana na kutojiamini. Kwa sababu ya kutojiamini, kuna wakati hujaribu kufanya mambo kwa kupita kiwango chake na kutafsiriwa kwamba wanaringa au wana dharau.
Wanawake wenye sura kama hiyo hudanganyika kirahisi kwa wanaume kwa sababu wenyewe ni waaminifu kwa kiasi cha kutosha. Huamini wanaume kirahisi kwa sababu, wanadhani kila mtu ni mwaminifu na mkweli kama wao. Kukuta mwanamke wa sura hiyo akiwa anaendeshwa na mwanaume ni jambo la kawaida.
Lakini kuna wale wenye sura kama hiyo ambao wamjikagua vibaya kwenye kioo au wameambiwa kitu tofauti utotoni, ambao huwa wahuni, yaani wasioaminika. Hata hivyo, ukiwaangalia hao kwa makini, suala linarudi palepale kwenye kutojiamini. Hata hivyo ni wanawake wenye bahati ya kuaminika, ingawa huharibu bahati hiyo wao wenyewe bila kujua. Wanaaminika kwa sababu ni waadilifu na wanaojua kuishi na watu kwa sehemu kubwa.
Wanawake wa sura hiyo hawana makuu, isipokuwa ni wababe sana. Wana aina fulani ya ubabe ambao ukiuangalia sana ni kutokana na kutojiamini kwao. Kwa hiyo wanawake wenye sura hii wanaharibiwa na kukosa kwao kujiamini tu. Kama wakijenga kujiamini, hutokea kuwa watu wenye kuaminika zaidi na kufika mbali sana.
Wanajua kupenda, lakini wanajiachia sana hadi wanajikuta hawana kauli tena kwa wapenzi wao. Ni wagumu kufanya uamuzi wenye kushika kwenye uhusiano. Na wanaweza kuamua kuondoka na kesho wakarudi kubembeleza wenyewe. Wana huruma na wako tayari kushiriki kidogo walicho nacho na wapenzi wao au watu wengine.
Wanapenda sana mzaha ili kuwafanya wengine wajisikie vizuri. Lakini wao wanapotaniwa, mtaniaji ni lazima awe mwangalifu, vinginevyo hakawii kuwaudhi. Hata hivyo upole hutokea kuwaonea pia. Mwanaume akipata mke wa aina hii anaweza kujidai kwamba, ana mke wa maana kwa sababu ya sifa ya uadilifu na upendo wa dhati lakini kama nilivyosema, inabidi mwanaume huyo amsaidie mwanamke huyu kujiamini.
Uzi huu uwafikie kina, gfsonwin, nivea, nyumba kubwa, BADILI TABIA, farkhina, jouneGwalu, charminglady, Ciello, Madame B, MadameX, lara 1, Paloma, NATA, Neylu, Yummy, SnowBall, Mwita Maranya, platozoom, Eiyer, MwanajamiiOne, Angel Msoffe, fabinyo, King'asti, Arushaone, Mungi, Erotica, Natalia, Zinduna, matumbo, Jiwe Linaloishi Mentor, Kijino, Kaunga, BelindaJacob, HorsePower, Kongosho na wengineo nisiowataja........