Wanawake wengi huomba kufanyiwa upasuaji badala ya kujifungua kawaida

Si kweli kwamba mimba ya kwanza ukipigwa kisu basi mimba zinazofuata lazima upigwe kisu tena, inategemeana na sababu iliyopelekea ukafanyiwa operation. Kama sababu iliyopelekea ukafanyiwa CS mara ya kwanza haipo kwenye mimba ya pili unaweza kujifungua kawaida ila muhimu kuwepo hospital inayoweza kufanya operation ili ikishindakana basi ufanyiwe upasuaji haraka

Ila kama mimba ya kwanza na ya pili zote ulifanyiwa operation basi ya tatu haiitaji kusubiri ni moja kwa moja operation
once ukijifungua kwa njia ya upasuaji...mimba zote zitakazofata lazima ufanyiwe upasuaji tena, cases za kusema complications za mimba ya kwanza hazipo kwenye mimba ya pili huwa haitiliwii maanani sana,

kwa usalama wa mama na mtoto ni lazima upasuaji ufanyike tena.
 
Sio kweli,50/50 maana yake nusu ya wanawake wote wajifunguao natural wamekufa,,, is this possible?
Operation ndio njia yenye uhakika wa uzazi salama kwa dunia ya leo

Mijini humu unasikia vifo vya wazazi tena?..

Kupush yataka mtu ambae nyonga yake si lelemama..kuzaa natural na kifo ni suala la 50/50
 
Hivi nasikia ukizaa kwa opereation inaacha alama hapa kwenye tumbo?

Heri nije kuzaa kwa uchungu wa kupush kuliko kubakiza alama tumboni
Kwa upasuaju wa kisasa si kovu persay ila vi alama kama nukta pale ambapo stitch za uzi zilipita na ukipona vizuri kuna lotion ya kitaalamu inafuta vikovu...hayo mambo ya makovu miaka hii labda kule kwenye hospitali zetu ambazo lengo ni kuokoa maisha ya mama na mtoto..ila kwa hizi za kileo wanaokoa maisha na pia wanazingatia urembo baada ya zoezi kuisha.
 
Ooh! Kwani ukizaa kwa upasuaji ndio unakuwa na tumbo kubwa au me ndio sijaelewa hapo?
Au umemaanishaje Dr
Nahisi wanashindwa kulifunga ili lirudi katika ukubwa wa kawaida kutokana na mshono.
 
Wengine wamechelewa kuzaa, kupush wanaogopa kukosa Mtoto, Upasuaji wanakuwa na uhakika wa kupata Mtoto. Umri watu wanawake wengine wanachelewa kupata watoto, wengine mimba kila ukiingia zinatoka, wengine Mtoto anakuwa amejifunga
Hizi ni dharura zinazojulikana , wengine ni uamuzi tu.
 
Nahisi wanashindwa kulifunga ili lirudi katika ukubwa wa kawaida kutokana na mshono.
Yeah...kabla kidonda hakijapona vizuri huruhusiwi kuvaa mikanda au kufunga otherwise unaweza kusababisha balaa kubwa...sasa muda huo ndio utaona tumbo kubwa ila baadae litarudi tu plus kujiongeza.
 
Operation ndio njia yenye uhakika wa uzazi salama kwa dunia ya leo

Mijini humu unasikia vifo vya wazazi tena?..

Kupush yataka mtu ambae nyonga yake si lelemama..kuzaa natural na kifo ni suala la 50/50
Nani kakulisha haya matango pori wewe?
 
Izo nyoga za sikuizi ni za kichina ndio maana zinagoma ovyo ovyo au acheni kupotosha watu bhana tumezaliwa ivyo ivyo sisi sote leo kizazi chetu kuzaa ndio nyonga zinagoma kweli !!!!!!!!!.
Huyo amemezeshwa upuuzi tu na mashosti zake waliopasuliwa ambao nao wamemezeshwa upuuzi huo na madaktari waroho wa hela wanao watisha tisha huko na wenyewe wanajaa kisha wanapasuliwa.

Hizo nyonga zimekuwa ndogo kwa wanawake wa siku hizi tu? Mbona kwa wanawake wa zamani hizi mambo za nyonga kuwa ndogo tulikuwa hatuziskii na wanawake walikuwa wanajifungua kawaida tu tena watoto wa kutosha!?

Mimi nina mama yangu mkubwa ana watoto 13 na hakuna hata mmoja aliyojifungua kwa njia upasuaji, wote aliwasukuma.

Sasa leo hii eti hawa wanawake ambao ndio tunawaita wasomi wanaona kupasuliwa ni bora hata kama hakuna sababu za msingi, yaani wanachukulia kama fashion.. Pumbafuu sana.
 
Dada utazaa salama asikutishe uyo mpka leo watu wanazaa kawaida pasipo kisu tena adi watoto 12 hao wa visu wanajua wanayo yafanya ndio maana awataki kuzaa kawaida.
Hao wanaozalishwa kwa mavisu hata kufikisha watoto wanne tu ni inshu.
 
Sio kila mtu anachagua CS kwa sababu mlizotaja nyie. Km mtu nyonga ni ndogo akaue mwanae sababu anataka kusifiwa kwamba alipush?? Binafsi wakat najifungua mwanangu nilitamani nipush Ila nikajikuta jumatatu asubuhi mpaka J4 asubuhi mtoto amesogea cm 4 wakati zinatakiwa angalau 10 ndipo upush. Drip 2 za uchungu bado hasogei yani ilibidi nikimbilie kisu. Na ndani ya Dk 30 nilikuwa nimeshamuona mwanangu baada ya kuchoka mateso ambayo pia yangehatarisha uhai wa mwanangu na mm mwenyewe.
Kwa kuwa nshajua nyonga zangu ndogo Safari ijayo nitachagua tu kisu mapemaaa. Mungu anilinde maana huko nako kuna complication zake.
Vipi ndonda hilo lilipo ndani ya tumbo lako madaktari wanakwambiaje?

Na kwanini ulijisahau mpaka nyonga zikawa hivyo zilizovyokuwa!? Au nyie ndio mnaoshindaga ndani mmelala tu huku mkifikia machipsi miezi tisa yote?
 
Kwa hiyo HAWALA yako anakupa sili za wagonjwa? huyo atakuwa wa vyeti feki na hana kiapo cha utabibu,tutamfatilia na hatua sitahiki achukuliwe.
Bila shaka wewe utakuwa ni mmoja wapo wa hao madaktari walafi ambao mmeigeuza hii kama biashara, mnadanganya watu kuwa wana complications hili muwapasue mtengeneze hela, sasa unajifanya ku-mind baada ya kuona kuna watu mnaoshirikiana nao hawapendi mnachokifanya na wameamua kuwa disclose.

Acha tamaa za kipuuzi.
 
Back
Top Bottom