Kati ya mambo ambayo wanawake wengi wanakosea au hawajui ni tabia za wanaume. Kimsingi binti au mwanamke anaposhawishiwa na mwanaume na kuwa na uhusiano wa kimapenzi, mara nyingi hupanga malengo ya mbali zaidi bila kujaribu au kutaka kujua kuwa uhusiano ulioanzishwa malengo yake ni yapi. wanawake wengi ni waoga au wanasita kuwauliza lengo la uhusianao wanaotakiwa na hatima yake itakuwa nini.
Wanawake wengi huamini kuwa uhusiano unapopamba moto, hicho ni kigezo tosha kuwa huo uhusiano mwelekeo wake ni mpaka ndoa au kuishi pamoja kama mme na mke. Wanawake wengi wamejeruhiwa wameumizwa kwa kuamini hivyo, hili ni kosa kubwa ambalo wanawake wengi hujikuta wamelifanya na huweza kuwaumiza maishani mwao mwote.
Kitu ambacho wanawake wanatakiwa wakijue fika ni kuwa wanaume waliowengi kinachowasukuma kutongoza si upendo wa dhati walionao bali ni matamanio ya mwili ndiyo humsukuma aanzishe uhusiano, ndiyo maana wanaume waliowengi wapo tayari kufanya mapenzi dakika hiyohiyo kama atakubaliwa ilimradi tu amalize matamanio yalioinuka wakati huo na baada ya hapo anaishia zake.
Kwa wanawake ambao wameshapelekwa sehemu ya faragha watakubaliana na mimi kuwa mwanaume anapomaliza shida yake kinachofuata ni kuondoka na hakuna mjadala wowote utakaotakiwa kuendelea hapo, hii ni kutokana na ukweli kuwa tamaa ya kufanya tendo la ndoa imeisha na hakuna kilichopo moyoni. kwa mwanamke ambaye sio kahaba hii ni tofauti sana kwani baada ya zoezi zima la tendo la ndoa angependa kusikia au kuonyeshwa upendo zaidi, ni wakati huo mwanamke angependa kusikia mustakabari wa uhusiano huo lakini hilo kwa wanaume wengi ni jambo wanaloliepuka na wengi hawapendi kujadili mustakabari wa uhusiano kwani kilichomsukuma sio upendo bali ni tamaa.
kutokana na wanawake kuwaamini na kujitoa kiujumla kwa wapenzi kwa kuamini kuwa huenda ndio mwanzo wa maisha ya mme na mke wengi wamejikuta wakiingia katika matatizo na hasara kubwa ya kimaisha. wanawake wengi wamepoteza mwelekeo na kujikuta wakitaabika kutokana na kipengere hiki cha kuamini mambo ambayo wapenzi wao hawayaamini wala kuyachukulia tahadhari.
Mimba nyingi zisizotarajiwa zimepatikana kwa kosa hili la wanawake wengi kutojua tabia za wanaume hivyo kujikuta wamekwama. Ugonjwa wa UKIMWI ambao ni tishio umekuwa ukienea kwa kasi kubwa ambapo moja ya sababu zinazosababisha ni hili la wanawake kuwaamini kupita kiasi wanaume hata kukubali kufanya mapenzi bila kutumia kondom wakihadaika kuwa uhusiano uliopo ni wa kudumu hivyo hakuna sababu za kutoaminiana.
Pamoja na hali halisi ya maisha, ni lazima wanawake wasiwe wavivu kutaka kujua tabia za wanaume na kuchukua tahadhari, vinginevyo mahangaiko, kujeruhiwa, kukosa mwelekeo wa maisha, kuambukizwa magojwa ya hatari kama UKIMWI hayo yote yatakuwa mwiba kwao.
Wanawake wengi huamini kuwa uhusiano unapopamba moto, hicho ni kigezo tosha kuwa huo uhusiano mwelekeo wake ni mpaka ndoa au kuishi pamoja kama mme na mke. Wanawake wengi wamejeruhiwa wameumizwa kwa kuamini hivyo, hili ni kosa kubwa ambalo wanawake wengi hujikuta wamelifanya na huweza kuwaumiza maishani mwao mwote.
Kitu ambacho wanawake wanatakiwa wakijue fika ni kuwa wanaume waliowengi kinachowasukuma kutongoza si upendo wa dhati walionao bali ni matamanio ya mwili ndiyo humsukuma aanzishe uhusiano, ndiyo maana wanaume waliowengi wapo tayari kufanya mapenzi dakika hiyohiyo kama atakubaliwa ilimradi tu amalize matamanio yalioinuka wakati huo na baada ya hapo anaishia zake.
Kwa wanawake ambao wameshapelekwa sehemu ya faragha watakubaliana na mimi kuwa mwanaume anapomaliza shida yake kinachofuata ni kuondoka na hakuna mjadala wowote utakaotakiwa kuendelea hapo, hii ni kutokana na ukweli kuwa tamaa ya kufanya tendo la ndoa imeisha na hakuna kilichopo moyoni. kwa mwanamke ambaye sio kahaba hii ni tofauti sana kwani baada ya zoezi zima la tendo la ndoa angependa kusikia au kuonyeshwa upendo zaidi, ni wakati huo mwanamke angependa kusikia mustakabari wa uhusiano huo lakini hilo kwa wanaume wengi ni jambo wanaloliepuka na wengi hawapendi kujadili mustakabari wa uhusiano kwani kilichomsukuma sio upendo bali ni tamaa.
kutokana na wanawake kuwaamini na kujitoa kiujumla kwa wapenzi kwa kuamini kuwa huenda ndio mwanzo wa maisha ya mme na mke wengi wamejikuta wakiingia katika matatizo na hasara kubwa ya kimaisha. wanawake wengi wamepoteza mwelekeo na kujikuta wakitaabika kutokana na kipengere hiki cha kuamini mambo ambayo wapenzi wao hawayaamini wala kuyachukulia tahadhari.
Mimba nyingi zisizotarajiwa zimepatikana kwa kosa hili la wanawake wengi kutojua tabia za wanaume hivyo kujikuta wamekwama. Ugonjwa wa UKIMWI ambao ni tishio umekuwa ukienea kwa kasi kubwa ambapo moja ya sababu zinazosababisha ni hili la wanawake kuwaamini kupita kiasi wanaume hata kukubali kufanya mapenzi bila kutumia kondom wakihadaika kuwa uhusiano uliopo ni wa kudumu hivyo hakuna sababu za kutoaminiana.
Pamoja na hali halisi ya maisha, ni lazima wanawake wasiwe wavivu kutaka kujua tabia za wanaume na kuchukua tahadhari, vinginevyo mahangaiko, kujeruhiwa, kukosa mwelekeo wa maisha, kuambukizwa magojwa ya hatari kama UKIMWI hayo yote yatakuwa mwiba kwao.