Nyanswe Nsame
Senior Member
- Jul 9, 2019
- 158
- 175
Wanawake watakiwa kupigia kura wanawake wenzao
Baadhi ya Wanawake nchini wamekuwa ni watu wasiokuwa na usubutu katika kupambana na wanaume katika nyanja mbalimbali hususani ni katika nafasi za kugombea nafasi za uongozi ikiwemo kugombea ubunge.
Tatizo hili limesababisha, wanawake wengi kushindwa kujiamini na badala yake wamewapa nafasi kubwa wanaume kuzidi kushika nafasi hizo.
Mkurugenzi mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali la kutetea haki za Wanawake na Watoto (Kivulini) Yassin Ally anasema umefika wakati sasa kwa wanawake kuamka na kugombea nafasi za udiwani na ubunge.
Anasema ni vizuri wanawake wakajitokeza kwa wingi kugombea katika ngazi mbalimbali ili kuleta usawa.
Yassin anasema, endapo wakajitokeza kugombea na kuchaguliwa kwenye nafasi hizo itasaidia kuleta usawa kwenye maamuzi yanayofanyika kwenye ngazi za serikali za vijiji, halmashauri, bunge na nyadhifa mbalimbali za uteuzi.
"Tukichukua kwenye takwimu asilimia 60 ya wapiga kura ni wanawake na wao ndio wanaongoza hata kwa kujiandikisha na kujitokeza kwa wingi kuliko wanaume.
"Tumeona wanawake wengi wanaoamini wanaoshika majimbo, kata na hata walioteuliwa kwenye nyadhifa mbambali wanafanya vizuri," alisema Yassin.
Pia Yassin anasema, kutokana na wanawake ndio wanaongoza kwa kupiga kura inapaswa kuona sasa mwamko wa wanawake wakiwapigia kura wanawake wenzao pindi wanapogombea nafasi hizo.
Yassin akagusia suala la viti maalumu kwa wanawake nchini, akasema sambamba kwa kuendelea kwa viti maalumu lakini wanawake wapanaswa kuamka na kugombea nafasi hizo.
Anasema kwamba uwezo kielimu, uwezo wa kimaamuzi na kiuchumi, unahitaji wanawake watawale uchumi na watawale maamuzi ndipo kizazi cha usawa na maendeleo ya sasa na ya baadae kiweze kupatikana.
Akisoma risala la wanawake wa Misungwi kwa mgeni Rasmi ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Misungwi,zote Juma Sweda, Telesia Mlaku anasema imefika wakati wanawake kuwezeshwa kiutamaduni na kisiasa ili wawe na uwezo wa kujitegemea na kuhudumia jamii.
Kaimu Mkurugenzi wa Misungwi, anasema halmashauri hiyo imezidi kutekeleza sera mbalimbali ikiwemo sera ya maendeleo duniani pia utekelezaji sheria ya fedha za serikali za mitaa na utekelezaji wa mikataba ya kimataifa inayotoa msukumo wa kutambua nafasi ya mwanamke katika kumjengea uwezo katika kutekeleza usawa.
Anasema mila na desturi za kitanzania ziliwachelewesha wanawake, na kwamba sasa imefika mwisho na kilichopo ni kuungana kwa wanawake na wanaume ili kwenda kwenye 50/50 ili kufikia malengo husika.
Jana iliadhimishwa siku ya wanawake duniani ikiwa ni maadhimisho ya miaka 25 ya wanawake, kiwilaya ya Misungwi yalifanyika viwanja vya shule ya sekondari Sanjo na kitaifa yalifanyika mkoani Simiyu
....
Baadhi ya Wanawake nchini wamekuwa ni watu wasiokuwa na usubutu katika kupambana na wanaume katika nyanja mbalimbali hususani ni katika nafasi za kugombea nafasi za uongozi ikiwemo kugombea ubunge.
Tatizo hili limesababisha, wanawake wengi kushindwa kujiamini na badala yake wamewapa nafasi kubwa wanaume kuzidi kushika nafasi hizo.
Mkurugenzi mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali la kutetea haki za Wanawake na Watoto (Kivulini) Yassin Ally anasema umefika wakati sasa kwa wanawake kuamka na kugombea nafasi za udiwani na ubunge.
Anasema ni vizuri wanawake wakajitokeza kwa wingi kugombea katika ngazi mbalimbali ili kuleta usawa.
Yassin anasema, endapo wakajitokeza kugombea na kuchaguliwa kwenye nafasi hizo itasaidia kuleta usawa kwenye maamuzi yanayofanyika kwenye ngazi za serikali za vijiji, halmashauri, bunge na nyadhifa mbalimbali za uteuzi.
"Tukichukua kwenye takwimu asilimia 60 ya wapiga kura ni wanawake na wao ndio wanaongoza hata kwa kujiandikisha na kujitokeza kwa wingi kuliko wanaume.
"Tumeona wanawake wengi wanaoamini wanaoshika majimbo, kata na hata walioteuliwa kwenye nyadhifa mbambali wanafanya vizuri," alisema Yassin.
Pia Yassin anasema, kutokana na wanawake ndio wanaongoza kwa kupiga kura inapaswa kuona sasa mwamko wa wanawake wakiwapigia kura wanawake wenzao pindi wanapogombea nafasi hizo.
Yassin akagusia suala la viti maalumu kwa wanawake nchini, akasema sambamba kwa kuendelea kwa viti maalumu lakini wanawake wapanaswa kuamka na kugombea nafasi hizo.
Anasema kwamba uwezo kielimu, uwezo wa kimaamuzi na kiuchumi, unahitaji wanawake watawale uchumi na watawale maamuzi ndipo kizazi cha usawa na maendeleo ya sasa na ya baadae kiweze kupatikana.
Akisoma risala la wanawake wa Misungwi kwa mgeni Rasmi ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Misungwi,zote Juma Sweda, Telesia Mlaku anasema imefika wakati wanawake kuwezeshwa kiutamaduni na kisiasa ili wawe na uwezo wa kujitegemea na kuhudumia jamii.
Kaimu Mkurugenzi wa Misungwi, anasema halmashauri hiyo imezidi kutekeleza sera mbalimbali ikiwemo sera ya maendeleo duniani pia utekelezaji sheria ya fedha za serikali za mitaa na utekelezaji wa mikataba ya kimataifa inayotoa msukumo wa kutambua nafasi ya mwanamke katika kumjengea uwezo katika kutekeleza usawa.
Anasema mila na desturi za kitanzania ziliwachelewesha wanawake, na kwamba sasa imefika mwisho na kilichopo ni kuungana kwa wanawake na wanaume ili kwenda kwenye 50/50 ili kufikia malengo husika.
Jana iliadhimishwa siku ya wanawake duniani ikiwa ni maadhimisho ya miaka 25 ya wanawake, kiwilaya ya Misungwi yalifanyika viwanja vya shule ya sekondari Sanjo na kitaifa yalifanyika mkoani Simiyu
....