Wanawake walio wengi hawana upendo na ndugu wa waume zao

Wild sniper

JF-Expert Member
Apr 3, 2015
4,346
8,448
Wanawake walio wengi hawana upendo na ndugu wa waume zao.

Ilikua siku moja hivi nimekaa na mzee mmoja mjeshi mstaafu akawa ananiambia tabia za wanawake kutowapenda ndugu wa mume. Akaanza kwa kuniambia ukitaka kujua hilo fanya hivi;
1. Nunua doti za vitenge hata 10 mpelekee mkeo mwambie hivi mpelekee mama mkwe wako, uone ataanza kusema "oooh dear vyote hivi halafu atakubali kupeleka lakini hatafikisha vyote lazima apunguze". Sababu anajua huwezi kumuuliza mama yako kama kavipata vingapi.

Sasa lete vingine hata 20 mwambie ampelekee mama yake hapo atatoa nguo zote kabatini kwa madai hazivai atamfungashia mzigo kama anapeleka lumbesa Kariakoo.

Swali ni: Je kwa wale mliooa haya mambo yana ukweli?
 
Ndio haswa, kuliko mke wako awapende ndugu zako hasa wa kiume,maumivu tu.
 
Tatizo ndugu zetu nao wanaendekeza NJAA.
Kua na mahusiano na ndugu si kitu kibaya lakini ndugu wa sisi wanaume huvuka mipaka.
Mawifi, mashemeji ni watu wa ovyo ovyo sana. Mbaya zaidi ukiwa na vijisenti watatumia njia yeyote ile kumfanya WI-FI aonekane hafai.
 
Tatizo ndugu zetu nao wanaendekeza NJAA.
Kua na mahusiano na ndugu si kitu kibaya lakini ndugu wa sisi wanaume huvuka mipaka.
Mawifi, mashemeji ni watu wa ovyo ovyo sana. Mbaya zaidi ukiwa na vijisenti watatumia njia yeyote ile kumfanya WI-FI aonekane hafai.
Bora umeona na upande wa pili
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom