Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Mbele yetu tunawaona akina mdee na wenzake kama wasaliti wa nafsi zetu lakini tunasau sisi ni wasaliti wa Kwanza kutokea.
Toka uchaguzi umalizike tumekaa kimya tukiandika mitandaoni na kushangilia wanachofanya wanasiasa wa upinzani bila kutilia maanani kwamba wapo watu wapo gerezani kwa sababu tu yakututetea sisi.
Tukio la jana la Nasrat na wenzake kutoka gerezani na kufutiwa kesi kisha leo kuonekana viunga vya Bungo linatoa tafsiri kubwa sana kwa watu wanaotafuta haki ndani ya ardhi yetu.
Tusiwalaumu akina Mdee kwa sababu nao ni wanadamu, wanatupigania lakini wanapaswa kuwa na mbinu zaidi ya moja. Tunaweza jiuliza wasingekwenda bungeni Nini kingetokea chenye mabdailiko chanya kwetu? Ukweli ni kwamba hakuna ambacho kingetokea kwa sababu baadhi ya waliopewa dhamana hawana roho wa Mungu ndani yao bali kwao maslahi binafsi ni muhimu.
Leo hii tunaweza kuwalaumu CHADEMA lakini ukweli ni kwamba wamefanya mengi na wataendelea kufanya mengi ikiwemo kuiondoa CCM miyoyoni mwa watu.
Leo hii ukiitafuta CCM haionekani inaonekana dola, si kwa sababu nyingine bali ni kwa sababu ccm ilishashindwa kusimamia maslahi ya watu, ilishapoteza wanachama na wafuasi ilishapoteza misingi.
Niwaombe tuwaonee huruma Wafungwa waliopo gerezani ambao kutoka kwao si kwa nguvu ya sheria bali ni kwa maamuzi ya mtu mmoja. Tukiona Jambo hili katika angle ya kukosekana haki tutaelewa aina ya Vita wanayopigana wanawake wa viti maalumu wa nchi hii.
Naamini waliopo magereza wataachiwa na kurejea kwenye familia zao, naamini waliopo Zanzibar pia wanasubiri maalim seif aungane na watawala ili binadamu wachache na wasio na hati waweze kuwa huru ndani ya Taifa lao na kuzisimamia familia zao Kama ambavyo Mimi na wewe tunazisimamia familia zetu.
Hakuna Jambo la muhimu kuliko imani, ukiabudu Mali, madaraka,heshima ya Dunia ipo siku utaondoka na waliobaki wataacha kukuheshimu.
Huu tuseme ni ushindi wa wafungwa na mahabusu wa kisiasa ambao Uhuru wao unatokana na viumbe wachache wanaoamini pumzi wanatoa wao na bila wao hatuwezi kupumua. Tuendelee kupumua tukisubiri kipindi chao kipite maana tayari walishajitwalia imaya hii.
Haya yanayotokea hayaui upinzani yanaiua ccm kimya kimya.....ogopa kuwa na taifa la wenye njaa.
Toka uchaguzi umalizike tumekaa kimya tukiandika mitandaoni na kushangilia wanachofanya wanasiasa wa upinzani bila kutilia maanani kwamba wapo watu wapo gerezani kwa sababu tu yakututetea sisi.
Tukio la jana la Nasrat na wenzake kutoka gerezani na kufutiwa kesi kisha leo kuonekana viunga vya Bungo linatoa tafsiri kubwa sana kwa watu wanaotafuta haki ndani ya ardhi yetu.
Tusiwalaumu akina Mdee kwa sababu nao ni wanadamu, wanatupigania lakini wanapaswa kuwa na mbinu zaidi ya moja. Tunaweza jiuliza wasingekwenda bungeni Nini kingetokea chenye mabdailiko chanya kwetu? Ukweli ni kwamba hakuna ambacho kingetokea kwa sababu baadhi ya waliopewa dhamana hawana roho wa Mungu ndani yao bali kwao maslahi binafsi ni muhimu.
Leo hii tunaweza kuwalaumu CHADEMA lakini ukweli ni kwamba wamefanya mengi na wataendelea kufanya mengi ikiwemo kuiondoa CCM miyoyoni mwa watu.
Leo hii ukiitafuta CCM haionekani inaonekana dola, si kwa sababu nyingine bali ni kwa sababu ccm ilishashindwa kusimamia maslahi ya watu, ilishapoteza wanachama na wafuasi ilishapoteza misingi.
Niwaombe tuwaonee huruma Wafungwa waliopo gerezani ambao kutoka kwao si kwa nguvu ya sheria bali ni kwa maamuzi ya mtu mmoja. Tukiona Jambo hili katika angle ya kukosekana haki tutaelewa aina ya Vita wanayopigana wanawake wa viti maalumu wa nchi hii.
Naamini waliopo magereza wataachiwa na kurejea kwenye familia zao, naamini waliopo Zanzibar pia wanasubiri maalim seif aungane na watawala ili binadamu wachache na wasio na hati waweze kuwa huru ndani ya Taifa lao na kuzisimamia familia zao Kama ambavyo Mimi na wewe tunazisimamia familia zetu.
Hakuna Jambo la muhimu kuliko imani, ukiabudu Mali, madaraka,heshima ya Dunia ipo siku utaondoka na waliobaki wataacha kukuheshimu.
Huu tuseme ni ushindi wa wafungwa na mahabusu wa kisiasa ambao Uhuru wao unatokana na viumbe wachache wanaoamini pumzi wanatoa wao na bila wao hatuwezi kupumua. Tuendelee kupumua tukisubiri kipindi chao kipite maana tayari walishajitwalia imaya hii.
Haya yanayotokea hayaui upinzani yanaiua ccm kimya kimya.....ogopa kuwa na taifa la wenye njaa.