Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Inazidi kuthibitika sasa kwamba,wanawake huwa wanatoa harufu fulani chini ya kwapa zao ambayo huwafanya wanaume kuvutika kimapenzi kwao.Harufu hiyo ambayo inafahamika kama pheromone haisikiki katika hali ya kawaida.Utafiti wa hivi karibuni kama ulivyoripotiwa na jarida la Physiology and Behavior umeonesha wanawake ambao walipakwa kemikali ambayo inaipa harufu hiyo walitokea kufuatwa sana na wanaume kuliko wakati walipokuwa hawajapaka kemikali hiyo.Kufuatwa kwao na wanaume kuliongezeka karibu mara saba zaidi kuliko ilivyokuwa kabla.Wanawake hao waliripoti kwamba,walibusiwa zaidi,walitongozwa zaidi na waliombwa urafiki zaidi na walijikuta wakikutana kimwili na wapenzi wao mara nying zaidi.Mmoja kati ya 36 waliofanyiwa utafiti aliripoti kwamba alipopaka kemikali hiyo,rafiki yake wa kiume alifanya nae mapenzi mara 4 kwa wiki ukilinganisha na mara moja ya awali.Harufu hii ambayo si mwanaume au mwanamke anaeweza kuihisi moja kwa moja bali kwa kupitia viungo maalumu vilivyo juu ndani ya pua,ina nguvu sana ya kumvuta mtu kimapenzi.Kama wataalam wameweza kutengeneza kemikali ya kuiga harufu hii,ni wazi wanawake watakuwa tayari kuinunua na kuitumia endapo itaingia sokoni!!