WANAWAKE roho mbaya namna hii mnaitoa wapi mnapokua MAMA WA KAMBO?

BAGAH

JF-Expert Member
Jan 17, 2012
4,523
1,060
huwa sielewi mwanamke anapopewa jukumu la kulea mtoto ambaye si wake (namaanisha mama wa kambo) anakua na roho ya tofauti (mbaya)....
ni mara chache unasikia mtoto anaelelewa na mama wa kambo akawa na raha katika maisha!...

huwa ni fujo mvutano mafarakano kusingiziana,ili mtadi tu kupanda na kushuka kwa majambo!...
je haiwezekani mtoto na mama wa kambo kuishi pasi majungu na mivutano???

je baba wa mtoto nae ana nafasi gani katika hili sekeseke?

GTs your highness!.
 
Halafu nimegundua mtoto anayekulia kwenye misukosuko kama ya kina mama wa kambo hua anakua imara sana kifikra awapo mtu mzima. Pamoja na hayo mimi napingana sana na unyanyasaji unaofanywa na BAADHI ya mama wa kambo, chondechonde kinamama na kinababa, inapaswa kutambua kua mtoto wa mwenzio ni wako pia.
 
mimi nimelelewa na mama wa kambo karibia maisha yangu yote maana mama yangu alifariki tangu nikiwa darasa la kwanza lakini sijawahi kunyayasika kwa njia yoyote ile huyu mama amekuwa mtu mwenye upendo sana na nimejifunza mengi kutoka kwake na nitaendelea kumshukuru sana maisha yangu yote.

SIO MAMA WA KAMBO WOTE WANA ROHO MBAYA .
 
Ingawa sio wote wenye ukatili ila wapo na ni wengi kuliko wenye wema kwa watoto wa wenzao.
Mimi ni mhanga so najua ubaya wa hawa watu dingi akirudi huwa anajikomba ili tusianike maovu yake dingi akiwa hayupo.
Mbaya zaidi wengine ni waumini wa mstari wa mbele wa madhehu tena ni viongozi
 
mimi nimelelewa na mama wa kambo karibia maisha yangu yote maana mama yangu alifariki tangu nikiwa darasa la kwanza lakini sijawahi kunyayasika kwa njia yoyote ile huyu mama amekuwa mtu mwenye upendo sana na nimejifunza mengi kutoka kwake na nitaendelea kumshukuru sana maisha yangu yote.

SIO MAMA WA KAMBO WOTE WANA ROHO MBAYA .

Zay nimekukubalia vyema!...mshike sana huyo mama wako wachache!..
 
Ingawa sio wote wenye ukatili ila wapo na ni wengi kuliko wenye wema kwa watoto wa wenzao.
Mimi ni mhanga so najua ubaya wa hawa watu dingi akirudi huwa anajikomba ili tusianike maovu yake dingi akiwa hayupo.
Mbaya zaidi wengine ni waumini wa mstari wa mbele wa madhehu tena ni viongozi

tena usiombe ukute dingi nae amekua zoba kwa uyo mama...lolote analoambiwa na mama anaamini na kukufokea ww!!
 
Inategema na wanawake sio wote, kuna mwanamke mimi namjua analea mtoto wa mme wake kwa mapenzi zaidi, kuliko watoto zake wenyewe wa kuzaa na huyo mme wake.

Sio wanawake wote wana roho mbaya, matatizo sisi wanaume tunatazama upande mmoja tu, hatutazami upande wetu pia.


Usisahau kuna parcentage kubwa ya wanaume wana roho mbaya kuliko wanawake :cool2:
 
Inategema na wanawake sio wote, kuna mwanamke mimi namjua analea mtoto wa mme wake kwa mapenzi zaidi, kuliko watoto zake wenyewe wa kuzaa na huyo mme wake.

Sio wanawake wote wana roho mbaya, matatizo sisi wanaume tunatazama upande mmoja tu, hatutazami upande wetu pia.


Usisahau kuna parcentage kubwa ya wanaume wana roho mbaya kuliko wanawake :cool2:

huwezi umiza kichwa sana kuwaza roho mbaya ya baba kama ile ya mama!..kumbuka mama ana muda mwingi wa kulea/kukaa na mtoto kuliko baba...so ni rahisi kuona effects zake (good/bad)
 
mimi nimelelewa na mama wa kambo karibia maisha yangu yote maana mama yangu alifariki tangu nikiwa darasa la kwanza lakini sijawahi kunyayasika kwa njia yoyote ile huyu mama amekuwa mtu mwenye upendo sana na nimejifunza mengi kutoka kwake na nitaendelea kumshukuru sana maisha yangu yote.

SIO MAMA WA KAMBO WOTE WANA ROHO MBAYA .

Ni kweli Zabibu sio mama wakambo wote wana roho mbaya. Hapa ile methali ya samaki mmoja akioza wote wameoza ndo inafanya kazi kwa mama wa kambo. Naijua familia moja ambayo mama alifariki. Mtoto wa mwisho wa huyu marehemu alikuwa darasa la sita. Baba( mume wa marehemu) alioa mke mwingine. Mama huyu mpya aliwajali sana watoto aliowakuta, ila watoto kwa kusikia kwamba wamama wakambo ni wabaya, wakawa hawamjali wala kumheshimu huyu mama mpya. Lakini mama huyu akaendeleza upendo wake na kupuuza visa anavyofanyiwa na watoto. Yule aliyekuwa darasa la sita akachipuka na kufaulu kwenda sekondari ambako alifaulu division I form four na kuendelea form five na hatimaye Chuo kikuu. Keshamaliza na amepata kazi nzuuri.

Pointi hapa ni kwamba kama yule mama aliyeolewa kwenye hii nyumba angekuwa na roho mbaya basi huyu mtoto aliyekuwa darasa la sita angenyanyasika na asingeenda kokote. Pia mara nyingi watoto ndo huanza chokochoko na mama wa kambo ambaye naye hurudisha mapigo. Inapotokea hivyo watu bila kujua chanzo huanza: 'Ooh! Mama mbaya, anatesa watoto'.
Kwenye mahusiano ya watoto na mama wa kambo yawapasa watoto wamheshimu kama mama yao, wasichukulie kwamba kwa kuwa ni mama wa kambo basi ni mtu mbaya.
 
Sio wamama wote Bagah ila asilimia kubwa roho zao ni mbaya sana...

Ukichukua wamama wa kambo 10 wawili kati yao ndio wana roho nzuri..
 
Sio wamama wote Bagah ila asilimia kubwa roho zao ni mbaya sana...

Ukichukua wamama wa kambo 10 wawili kati yao ndio wana roho nzuri..

habari yako shem wa ukweh!..
nakubaliana na ww kwa asilimia zote SL
 
ubaya mdogo hufuta wema uliokithiri..ni kawaida kwa binadamu kulaumu pale mambo yanapokwenda kombo au anapotendewa ndivyosivyo hata kama ni haki yake kutendewa hivyo...hivyo basi hata mtoto akilelewa na mama wa kambo akatendewa wema lakini ikitokea akafanyiwa sivyo wema woote husahaulika...
 
kwakweli msitukumbushe sie tulioteseka jamani,huwa sielewi ni nn hasa inakua ivo mana hatukuwa wakorofi wala nini
ila Mungu hulipa hapahapa duniani,now tuko ngangari kama "skype avosema"
 
kwakweli msitukumbushe sie tulioteseka jamani,huwa sielewi ni nn hasa inakua ivo mana hatukuwa wakorofi wala nini
ila Mungu hulipa hapahapa duniani,now tuko ngangari kama "skype avosema"

Kumbe tupo wengi tuliokulia ktk mikono ya chuma! Tujipe pole kwa mateso ila tujipongeze kwa kufuzu maana haikua kazi ndogo kuvumilia kichapo, matusi, kejeli, kulala au kushinda njaa, nk.
 
je baba wa mtoto nae ana nafasi gani katika hili sekeseke?

Baba wa mtoto akiwa karibu na mtoto wake na kumpenda kwa dhati atahakikisha huyo mama wa kambo hamnyanyasi mwanae.

Kwangu mtoto anatangulia kabla hata ya maslahi yangu. Asilani siwezi kuruhusu mtoto wangu kukosa furaha na amani kisa mama yake wa kambo.

Ndiyo maana ni vyema wazazi wakawafundisha watoto wao kutokukubali kunyanyaswa na yeyote yule. Mimi sioni ubaya wowote ule kumfundisha mtoto wako kuwa hakuna mwenye haki ya kumpiga, kwa mfano.

Na ikitokea kapigwa basi naye apigane. Heshima wakati mwingine ni lazima mtu uitafute la sivyo utafanywa mkeka.
 
Baba wa mtoto akiwa karibu na mtoto wake na kumpenda kwa dhati atahakikisha huyo mama wa kambo hamnyanyasi mwanae.

Kwangu mtoto anatangulia kabla hata ya maslahi yangu. Asilani siwezi kuruhusu mtoto wangu kukosa furaha na amani kisa mama yake wa kambo.

Ndiyo maana ni vyema wazazi wakawafundisha watoto wao kutokukubali kunyanyaswa na yeyote yule. Mimi sioni ubaya wowote ule kumfundisha mtoto wako kuwa hakuna mwenye haki ya kumpiga, kwa mfano.

Na ikitokea kapigwa basi naye apigane. Heshima wakati mwingine ni lazima mtu uitafute la sivyo utafanywa mkeka.

Ngoja niyapitie haya mafundisho huenda yakanisaidia mbeleni ktk kulea watoto, I highly appreciated this useful piece of advice.
 
Baba wa mtoto akiwa karibu na mtoto wake na kumpenda kwa dhati atahakikisha huyo mama wa kambo hamnyanyasi mwanae.

Kwangu mtoto anatangulia kabla hata ya maslahi yangu. Asilani siwezi kuruhusu mtoto wangu kukosa furaha na amani kisa mama yake wa kambo.

Ndiyo maana ni vyema wazazi wakawafundisha watoto wao kutokukubali kunyanyaswa na yeyote yule. Mimi sioni ubaya wowote ule kumfundisha mtoto wako kuwa hakuna mwenye haki ya kumpiga, kwa mfano.

Na ikitokea kapigwa basi naye apigane. Heshima wakati mwingine ni lazima mtu uitafute la sivyo utafanywa mkeka.
Ni kweli NN, ukaribu wa baba kwa mtoto ndio kinga pekee inayoweza kumwepusha mtoto na manyanyaso/vipigo kutoka kwa mama wa kambo...


Ila cha kushangaza kuna wanaume wajinga sana, eti libaba linahama upande wa mwanae na kuwa upande wa mkewe, kila anachoambiwa na mtoto ni uongo na kila anachoambiwa na mkewe ni ukweli, mtoto anabaki peke yake, hana wa kumsapoti wala kumweleza shida zake...hapa atanyanyasika mpaka apate akili ya kiutu uzima aweze kujiokoa peke yake.


Mama wa kambo huwa wanapima upepo wa baba akikuta libaba lege lege basi huyo mtoto cha moto atakiona, ila kama baba anamsimamo na yuko upande wa mtoto kamwe hatathubutu kumnyanyasa... Mtoto anajenga kujiamini na ataishi kwa amani...
 
Ni kweli NN, ukaribu wa baba kwa mtoto ndio kinga pekee inayoweza kumwepusha mtoto na manyanyaso/vipigo kutoka kwa mama wa kambo...


Ila cha kushangaza kuna wanaume wajinga sana, eti libaba linahama upande wa mwanae na kuwa upande wa mkewe, kila anachoambiwa na mtoto ni uongo na kila anachoambiwa na mkewe ni ukweli, mtoto anabaki peke yake, hana wa kumsapoti wala kumweleza shida zake...hapa atanyanyasika mpaka apate akili ya kiutu uzima aweze kujiokoa peke yake.


Mama wa kambo huwa wanapima upepo wa baba akikuta libaba lege lege basi huyo mtoto cha moto atakiona, ila kama baba anamsimamo na yuko upande wa mtoto kamwe hatathubutu kumnyanyasa... Mtoto anajenga kujiamini na ataishi kwa amani...

inasikikitisha kuwa ulichokisema ni kweli kwa asilimia nyingi..........................!
ila wapo mama wa kambo wazuri sana tu...................hata hivyo huwa najiuliza.............mtoto ni mtoto lakini kinachomshinda mama kumpenda mtoto ambaye hajamzaa ni kitu gani.............!......ingekua vizuri kama tungepata wamama wakambo tukawasikia maelezo yao...................labda tungeelewa kiini cha roho zao mbaya...................!
 
Back
Top Bottom