Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Hebu fikiria kwamba, umepika chakula kizuri sana na unaamini mumeo mpenzi wako akirudi kutoka kazini na kula chakula hicho atafurahi, hata kama hatakwambia, ‘asante.' Lakini mume huyo anaporudi anajizungusha na hatimaye anasema kwamba, hatakula chakula. Unapomuuliza sababu anasema tu kwamba, ameshiba. Unapomuuliza amekula wapi, anaweza kujibu kiungwana kwa uongo kwamba, amekula chakula cha mchana saa mbaya, au alikuwa na ‘pati' ndogo pale kazini au chochote.
Mwingine hakujibu kiungwana kwa kiwango hicho, bali atafoka na kutoa kashfa. ‘unataka kujua nimekula wapi ili iweje?' anaweza pia kukuambia, ‘unafikiri ni wewe peke yako unayejua kupika?' Kuna majibu mengine, ambayo ni mabaya zaidi na yenye kukwaza zaidi ya hayo. Hebu niambie kama ni wewe unakumbana na kisirani hiki ungefanyaje?
Mwingine hakujibu kiungwana kwa kiwango hicho, bali atafoka na kutoa kashfa. ‘unataka kujua nimekula wapi ili iweje?' anaweza pia kukuambia, ‘unafikiri ni wewe peke yako unayejua kupika?' Kuna majibu mengine, ambayo ni mabaya zaidi na yenye kukwaza zaidi ya hayo. Hebu niambie kama ni wewe unakumbana na kisirani hiki ungefanyaje?